< Torati 3 >

1 Kisha tukageuka tukakwea kufuata njia iliyoelekea Bashani, Ogu mfalme wa Bashani akaondoka na jeshi lake lote kupigana na sisi huko Edrei.
“And we turn and go up the way to Bashan, and Og king of Bashan comes out to meet us, he and all his people, to the battle [at] Edrei.
2 Bwana akaniambia, “Usimwogope kwa kuwa nimekwisha mkabidhi mikononi mwako pamoja na jeshi lake lote na nchi yake. Umfanyie sawasawa na ulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.”
And YHWH says to me, Do not fear him, for I have given him, and all his people, and his land into your hand, and you have done to him as you have done to Sihon king of the Amorite who is dwelling in Heshbon.
3 Hivyo Bwana Mungu wetu pia akamweka Ogu mfalme wa Bashani pamoja na jeshi lake lote mikononi mwetu. Tuliwaangamiza wote, hakubakia hata mmoja.
And our God YHWH indeed gives Og king of Bashan and all his people into our hands, and we strike him until there has been no remnant left to him;
4 Wakati huo tuliteka miji yake yote. Hakuna mji hata mmoja kati ya ile sitini ambao hatukuuteka, yaani eneo lote la Argobu, utawala wa Mfalme Ogu katika Bashani.
and we capture all his cities at that time; there has not been a city which we have not taken from them—sixty cities, all the region of Argob, the kingdom of Og in Bashan.
5 Miji yote hii ilijengewa ngome zenye kuta ndefu zenye malango na makomeo, pia kulikuwako na vijiji vingi ambavyo havikujengewa kuta.
All these [are] cities fortified with high walls, double gates, and bar, apart from very many cities of the open place;
6 Tuliwaangamiza kabisa, kama tulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Heshboni, tukiangamiza kila mji, yaani wanaume, wanawake na watoto.
and we devote them, as we have done to Sihon king of Heshbon, devoting [the] men, the women, and the infants of every city;
7 Lakini wanyama wote wa kufuga pamoja na nyara kutoka kwenye miji yao tulichukua vikawa vyetu.
and all the livestock, and the spoil of the cities, we have spoiled for ourselves.
8 Hivyo kwa wakati huo tukachukua kutoka kwa wafalme hawa wawili wa Waamori nchi ya mashariki ya Yordani, kutoka Bonde la Arnoni mpaka kufika kwenye Mlima Hermoni.
And at that time we take the land out of the hand of the two kings of the Amorite, which is beyond the Jordan, from the Brook of Arnon to Mount Hermon
9 (Wasidoni huuita mlima huo Sirioni, nao Waamori huuita Seniri.)
(Sidonians call Hermon Sirion, and the Amorites call it Senir),
10 Tuliteka miji yote kwenye uwanda wa juu, Gileadi yote, Bashani yote mpaka kufika Saleka na Edrei, miji ya utawala wa Ogu huko Bashani.
all the cities of the plain, and all Gilead, and all Bashan, as far as Salchah and Edrei, cities of the kingdom of Og in Bashan.
11 (Mfalme Ogu wa Bashani ndiye peke yake aliyesalia miongoni mwa mabaki ya Warefai. Kitanda chake kilikuwa cha chuma chenye urefu wa dhiraa tisa na upana wa dhiraa nne. Mpaka sasa kinaweza kuonekana katika mji wa Waamoni wa Raba.)
For only Og king of Bashan had been left of the remnant of the Rephaim; behold, his bedstead [is] a bedstead of iron. Is it not in Rabbath of the sons of Ammon? Its length [is] nine cubits and its breadth [is] four cubits, by the cubit of a man.
12 Katika nchi tuliyoiteka wakati ule, niliwapa kabila la Reubeni na Gadi eneo lililoko kaskazini la Aroeri kando ya Bonde la Arnoni, na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake.
And this land, [which] we had possessed at that time, from Aroer, which [is] by the Brook of Arnon, and the half of Mount Gilead and its cities, I have given to the Reubenite and to the Gadite;
13 Kisha nusu ya kabila la Manase niliwapa sehemu ya Gileadi iliyobaki pamoja na Bashani yote, ambayo ilikuwa utawala wa Ogu. (Eneo lote la Argobu katika Bashani lilikuwa linajulikana kama nchi ya Warefai.
and the rest of Gilead and all Bashan, the kingdom of Og, I have given to the half tribe of Manasseh; all the region of Argob, with all Bashan—it is called the land of [the] Rephaim.
14 Yairi, mzao wa kabila la Manase, alichukua eneo lote la nchi ya Argobu hadi kufikia mpaka wa Wageshuri na Wamaaka, ukaitwa kwa jina lake; kwa hiyo mpaka leo hii Bashani inaitwa Hawoth-Yairi.)
Jair son of Manasseh has taken all the region of Argob, as far as the border of Geshuri and Maachathi ([namely] Bashan), and calls them by his own name, Havoth-Jair, to this day.
15 Nikampa Makiri nchi ya Gileadi.
And I have given Gilead to Machir.
16 Lakini niliwapa Wareubeni na Wagadi eneo kuanzia Gileadi hadi Bonde la Arnoni (katikati ya bonde ulikuwa ndio mpaka), kuelekea mpaka Mto Yaboki, ambao ndio mpaka wa Waamoni.
And to the Reubenite and to the Gadite I have given from Gilead even to the Brook of Arnon, the middle of the valley and the border, even to the Brook of Jabbok, the border of the sons of Ammon,
17 Kwa upande wa magharibi mpaka wao ulikuwa Yordani katika Araba, toka ziwa Galilaya hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), kwenye miteremko ya Pisga upande wa mashariki.
and the plain, and the Jordan, and the border, from Chinnereth even to the Sea of the Plain (the Salt Sea), under the Springs of Pisgah, at the [sun]-rising.
18 Wakati huo nilikuamuru: “Bwana Mungu wako amekupa nchi hii uimiliki. Lakini ni lazima wanaume wenu wote wenye uwezo, wakiwa wamejiandaa tayari kwa vita, wavuke ngʼambo wakiwatangulia ndugu zako Waisraeli.
And at that time I command you, saying, Your God YHWH has given this land to you to possess it; you pass over armed before your brothers the sons of Israel, all the sons of might.
19 Lakini wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu (kwani najua mnayo mifugo mingi) wanaweza kukaa katika miji niliyowapa,
Only your wives, and your infants, and your livestock—I have known that you have much livestock—dwell in your cities which I have given to you,
20 mpaka hapo Bwana atakapowapa ndugu zenu kupumzika kama alivyowapa ninyi, wao pia wamiliki ile nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, ngʼambo ya Yordani. Baada ya hapo, kila mmoja wenu anaweza kurudi kwenye milki niliyowapa.”
until YHWH gives rest to your brothers like yourselves, and they also have possessed the land which your God YHWH is giving to them beyond the Jordan; then you have each turned back to his possession which I have given to you.
21 Wakati huo nilimwamuru Yoshua, “Umejionea kwa macho yako mwenyewe yale yote ambayo Bwana Mungu wenu amewafanyia wafalme hawa wawili. Bwana atazifanyia falme zote huko mnakokwenda vivyo hivyo.
And I have commanded Joshua at that time, saying, Your eyes are seeing all that which your God YHWH has done to these two kings—so YHWH does to all the kingdoms to where you are passing over;
22 Msiwaogope, Bwana Mungu wenu atapigana kwa ajili yenu.”
do not fear them, for your God YHWH—He is fighting for you.
23 Wakati huo nilimsihi Bwana:
And to YHWH I beg for grace at that time, saying,
24 “Ee Bwana Mwenyezi, umemwonyesha mtumishi wako ukuu wako na mkono wako wenye uweza. Kwa kuwa ni mungu yupi aliye mbinguni au duniani anayeweza kufanya kazi na matendo makuu kama ufanyayo wewe?
Lord YHWH, You have begun to show Your servant Your greatness and Your strong hand; for who [is] a god in the heavens or in earth who does according to Your works and according to Your might?
25 Acha niende nikaione hiyo nchi nzuri ngʼambo ya Yordani, ile nchi nzuri ya vilima na Lebanoni.”
Please let me pass over and see the good land which [is] beyond the Jordan, this good hill-country, and Lebanon.
26 Lakini kwa sababu yenu Bwana alinikasirikia na hakutaka kunisikiliza. Bwana aliniambia, “Hilo latosha; usiseme nami jambo hili tena.
And YHWH shows Himself angry with me for your sake, and has not listened to me, and YHWH says to me, Enough of you; do not add to speak to Me about this thing anymore;
27 Kwea juu ya kilele cha Pisga uangalie magharibi, kaskazini, kusini na mashariki. Iangalie hiyo nchi kwa macho yako, kwa vile wewe hutavuka Yordani.
go up [to] the top of Pisgah, and lift up your eyes westward, and northward, and southward, and eastward, and see with your eyes, for you do not pass over this Jordan;
28 Lakini mwagize Yoshua, mtie moyo na umtie nguvu, kwa kuwa yeye atawaongoza watu hawa hadi ngʼambo na kuwarithisha nchi utakayoiona.”
and charge Joshua, and strengthen him, and harden him, for he passes over before this people, and he causes them to inherit the land which you see.
29 Kwa hiyo tulikaa kwenye bonde karibu na Beth-Peori.
And we dwell in a valley opposite Beth-Peor.”

< Torati 3 >