< Torati 3 >

1 Kisha tukageuka tukakwea kufuata njia iliyoelekea Bashani, Ogu mfalme wa Bashani akaondoka na jeshi lake lote kupigana na sisi huko Edrei.
Potom obrátivše se, táhli jsme cestou k Bázan. I vytáhl Og, král Bázan, proti nám, on i všecken lid jeho k bitvě do Edrei.
2 Bwana akaniambia, “Usimwogope kwa kuwa nimekwisha mkabidhi mikononi mwako pamoja na jeshi lake lote na nchi yake. Umfanyie sawasawa na ulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.”
I řekl mi Hospodin: Neboj se ho, nebo v ruce tvé dal jsem jej, i všecken lid jeho i zemi jeho, a učiníš jemu tak, jako jsi učinil Seonovi, králi Amorejskému, kterýž bydlil v Ezebon.
3 Hivyo Bwana Mungu wetu pia akamweka Ogu mfalme wa Bashani pamoja na jeshi lake lote mikononi mwetu. Tuliwaangamiza wote, hakubakia hata mmoja.
Dal tedy Hospodin Bůh náš v ruce naše i Oga, krále Bázan, a všecken lid jeho, i porazili jsme jej, tak že jsme nepozůstavili po něm žádného živého.
4 Wakati huo tuliteka miji yake yote. Hakuna mji hata mmoja kati ya ile sitini ambao hatukuuteka, yaani eneo lote la Argobu, utawala wa Mfalme Ogu katika Bashani.
Dobyli jsme také téhož času všech měst jeho; nebylo města, kteréhož bychom jim neodjali, šedesáte měst, všecku krajinu Argob, království Oga v Bázan.
5 Miji yote hii ilijengewa ngome zenye kuta ndefu zenye malango na makomeo, pia kulikuwako na vijiji vingi ambavyo havikujengewa kuta.
Všecka ta města byla ohražená zdmi vysokými, branami a závorami, kromě měst otevřených, jichž bylo velmi mnoho.
6 Tuliwaangamiza kabisa, kama tulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Heshboni, tukiangamiza kila mji, yaani wanaume, wanawake na watoto.
A vyplénili jsme je, jako jsme učinili Seonovi, králi Ezebon, vyhladivše všecka města, muže, ženy i dítky.
7 Lakini wanyama wote wa kufuga pamoja na nyara kutoka kwenye miji yao tulichukua vikawa vyetu.
Všecka pak hovada a kořisti měst rozebrali jsme sobě.
8 Hivyo kwa wakati huo tukachukua kutoka kwa wafalme hawa wawili wa Waamori nchi ya mashariki ya Yordani, kutoka Bonde la Arnoni mpaka kufika kwenye Mlima Hermoni.
Vzali jsme také téhož času zemi z ruky dvou králů Amorejských, kteráž byla před Jordánem, od potoku Arnon až k hoře Hermon,
9 (Wasidoni huuita mlima huo Sirioni, nao Waamori huuita Seniri.)
(Sidonští říkají Hermonu Sarion, a Amorejští říkají jemu Sanir),
10 Tuliteka miji yote kwenye uwanda wa juu, Gileadi yote, Bashani yote mpaka kufika Saleka na Edrei, miji ya utawala wa Ogu huko Bashani.
Všecka města v kraji, a všecken Galád, a všecken Bázan až do Sálecha a Edrei, kteráž byla města království Og v Bázan.
11 (Mfalme Ogu wa Bashani ndiye peke yake aliyesalia miongoni mwa mabaki ya Warefai. Kitanda chake kilikuwa cha chuma chenye urefu wa dhiraa tisa na upana wa dhiraa nne. Mpaka sasa kinaweza kuonekana katika mji wa Waamoni wa Raba.)
Sám toliko Og, král v Bázan, z jiných obrů byl pozůstal. Aj, lůže jeho, lůže železné, ještě zůstává v Rabbat synů Ammon, devíti loktů zdýlí, a čtyř loket zšíří, jakž jest loket muže.
12 Katika nchi tuliyoiteka wakati ule, niliwapa kabila la Reubeni na Gadi eneo lililoko kaskazini la Aroeri kando ya Bonde la Arnoni, na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake.
Když tedy zemi tu obdrželi jsme dědičně toho času, krajinu od Aroer, jenž jest při potoku Arnon, a polovici hory Galád i města její, dal jsem pokolení Ruben a Gád.
13 Kisha nusu ya kabila la Manase niliwapa sehemu ya Gileadi iliyobaki pamoja na Bashani yote, ambayo ilikuwa utawala wa Ogu. (Eneo lote la Argobu katika Bashani lilikuwa linajulikana kama nchi ya Warefai.
Ostatek pak Galád a všecku zemi Bázan, království Oga, dal jsem polovici pokolení Manassesova, totiž všecku krajinu Argob, všecku Bázan, kteráž sloula země obrů.
14 Yairi, mzao wa kabila la Manase, alichukua eneo lote la nchi ya Argobu hadi kufikia mpaka wa Wageshuri na Wamaaka, ukaitwa kwa jina lake; kwa hiyo mpaka leo hii Bashani inaitwa Hawoth-Yairi.)
Jair, syn Manasse, vzal všecku krajinu Argob, až ku pomezí Gessuri a Machati; pročež nazval zemi Bázan od jména svého Havot Jair až do dnešního dne.
15 Nikampa Makiri nchi ya Gileadi.
Machirovi pak dal jsem Galád.
16 Lakini niliwapa Wareubeni na Wagadi eneo kuanzia Gileadi hadi Bonde la Arnoni (katikati ya bonde ulikuwa ndio mpaka), kuelekea mpaka Mto Yaboki, ambao ndio mpaka wa Waamoni.
A Rubenovu a Gádovu pokolení dal jsem krajinu od Galád až ku potoku Arnon, polovici potoka s pomezím až ku potoku Jabok, kdež jsou hranice synů Ammonitských,
17 Kwa upande wa magharibi mpaka wao ulikuwa Yordani katika Araba, toka ziwa Galilaya hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), kwenye miteremko ya Pisga upande wa mashariki.
A roviny tyto i Jordán s pomezím od Ceneret až k moři pustému, jenž jest moře slané, ležící pod horou Fazga k východu.
18 Wakati huo nilikuamuru: “Bwana Mungu wako amekupa nchi hii uimiliki. Lakini ni lazima wanaume wenu wote wenye uwezo, wakiwa wamejiandaa tayari kwa vita, wavuke ngʼambo wakiwatangulia ndugu zako Waisraeli.
A přikázal jsem vám toho času, řka: Hospodin Bůh váš dal vám zemi tuto, abyste ji dědičně obdrželi; vezmouce odění na sebe, půjdete před bratřími vašimi, syny Izraelskými, kteřížkoli silní jste.
19 Lakini wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu (kwani najua mnayo mifugo mingi) wanaweza kukaa katika miji niliyowapa,
Toliko ženy vaše a dítky vaše, a dobytek váš, (nebo vím, že mnoho dobytka máte, ) zůstanou v městech vašich, kteráž jsem dal vám,
20 mpaka hapo Bwana atakapowapa ndugu zenu kupumzika kama alivyowapa ninyi, wao pia wamiliki ile nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, ngʼambo ya Yordani. Baada ya hapo, kila mmoja wenu anaweza kurudi kwenye milki niliyowapa.”
Dokudž by nedal odpočinutí Hospodin bratřím vašim jako i vám, aby i oni dědičně obdrželi zemi, kterouž Hospodin Bůh váš dává jim za Jordánem; tedy navrátíte se jeden každý k dědictví svému, kteréž jsem dal vám.
21 Wakati huo nilimwamuru Yoshua, “Umejionea kwa macho yako mwenyewe yale yote ambayo Bwana Mungu wenu amewafanyia wafalme hawa wawili. Bwana atazifanyia falme zote huko mnakokwenda vivyo hivyo.
Také i Jozue přikázal jsem toho času, řka: Oči tvé vidí všecko, co učinil Hospodin Bůh váš těm dvěma králům; takť učiní Hospodin všechněm královstvím, do kterýchž ty půjdeš.
22 Msiwaogope, Bwana Mungu wenu atapigana kwa ajili yenu.”
Nebojtež se jich, nebo Hospodin Bůh váš, onť jest, kterýž bojuje za vás.
23 Wakati huo nilimsihi Bwana:
A tehdáž prosil jsem Hospodina, řka:
24 “Ee Bwana Mwenyezi, umemwonyesha mtumishi wako ukuu wako na mkono wako wenye uweza. Kwa kuwa ni mungu yupi aliye mbinguni au duniani anayeweza kufanya kazi na matendo makuu kama ufanyayo wewe?
Panovníče Hospodine, ty jsi počal ukazovati služebníku svému velikost svou a ruku svou přesilnou; nebo kdo jest Bůh silný na nebi aneb na zemi, ješto by činiti mohl skutky podobné tvým, a moci podobné tobě?
25 Acha niende nikaione hiyo nchi nzuri ngʼambo ya Yordani, ile nchi nzuri ya vilima na Lebanoni.”
Prosím, nechť vejdu a uzřím zemi tu výbornou, kteráž jest za Jordánem, horu tu výbornou i Libán.
26 Lakini kwa sababu yenu Bwana alinikasirikia na hakutaka kunisikiliza. Bwana aliniambia, “Hilo latosha; usiseme nami jambo hili tena.
Pohnul se pak Hospodin na mne pro vás a neuslyšel mne, ale řekl mi: Dosti máš, nemluv více o to se mnou.
27 Kwea juu ya kilele cha Pisga uangalie magharibi, kaskazini, kusini na mashariki. Iangalie hiyo nchi kwa macho yako, kwa vile wewe hutavuka Yordani.
Vstup na vrch hory Fazga, a pozdvihna očí svých k západu a k půlnoci, ku poledni i k východu, hleď očima svýma; nebo nepřejdeš Jordánu tohoto.
28 Lakini mwagize Yoshua, mtie moyo na umtie nguvu, kwa kuwa yeye atawaongoza watu hawa hadi ngʼambo na kuwarithisha nchi utakayoiona.”
Ale přikaž Jozue, a posilň ho, i potvrď ho; nebo půjde před lidem tímto, a on uvede jim v dědictví zemi, kterouž uzříš.
29 Kwa hiyo tulikaa kwenye bonde karibu na Beth-Peori.
I zůstali jsme v údolí naproti Betfegor.

< Torati 3 >