< Torati 3 >

1 Kisha tukageuka tukakwea kufuata njia iliyoelekea Bashani, Ogu mfalme wa Bashani akaondoka na jeshi lake lote kupigana na sisi huko Edrei.
Тогава възвихме та отидохме към Васан; и васанският цар Ог излезе против нас, той и всичките му люде, на бой в Едраи.
2 Bwana akaniambia, “Usimwogope kwa kuwa nimekwisha mkabidhi mikononi mwako pamoja na jeshi lake lote na nchi yake. Umfanyie sawasawa na ulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.”
А Господ ми рече: Не бой се от него, защото предадох в ръката ти него, всичките му люде и земята му; ще му направиш както направи на аморейския цар Сион, който живееше в Есевон.
3 Hivyo Bwana Mungu wetu pia akamweka Ogu mfalme wa Bashani pamoja na jeshi lake lote mikononi mwetu. Tuliwaangamiza wote, hakubakia hata mmoja.
И така, Господ нашият Бог предаде в ръката ни и васанския цар Ог и всичките му люде; и поразихме го така, че не му оставихме никого да оцелее.
4 Wakati huo tuliteka miji yake yote. Hakuna mji hata mmoja kati ya ile sitini ambao hatukuuteka, yaani eneo lote la Argobu, utawala wa Mfalme Ogu katika Bashani.
В онова време превзехме всичките му градове; нямаше град, който не превзехме от тях; шестдесет града, цялата Арговска област, царството на Ога във Васан.
5 Miji yote hii ilijengewa ngome zenye kuta ndefu zenye malango na makomeo, pia kulikuwako na vijiji vingi ambavyo havikujengewa kuta.
Всичките тия градове бяха укрепени с високи стени, с порти и лостове; и освен тях имаше твърде много неукрепени градове.
6 Tuliwaangamiza kabisa, kama tulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Heshboni, tukiangamiza kila mji, yaani wanaume, wanawake na watoto.
Тях изтребихме, както сторихме на есевонския цар Сион; изтребихме всеки град, с мъжете, жените и децата.
7 Lakini wanyama wote wa kufuga pamoja na nyara kutoka kwenye miji yao tulichukua vikawa vyetu.
А всичкия добитък и користите на градовете разграбихме за себе си.
8 Hivyo kwa wakati huo tukachukua kutoka kwa wafalme hawa wawili wa Waamori nchi ya mashariki ya Yordani, kutoka Bonde la Arnoni mpaka kufika kwenye Mlima Hermoni.
Така, в онова време, взехме от ръцете на двамата аморейски царе земята, която оттатък Иордан, от потока Арнон до планината Ермон;
9 (Wasidoni huuita mlima huo Sirioni, nao Waamori huuita Seniri.)
(Ермон сидонците наричат Сирион, а аморейците го наричат Санир);
10 Tuliteka miji yote kwenye uwanda wa juu, Gileadi yote, Bashani yote mpaka kufika Saleka na Edrei, miji ya utawala wa Ogu huko Bashani.
всичките градове на поляната, целия Галаад и целия Васан, до Салха и Едраи, градове от царството на Ога във Васан,
11 (Mfalme Ogu wa Bashani ndiye peke yake aliyesalia miongoni mwa mabaki ya Warefai. Kitanda chake kilikuwa cha chuma chenye urefu wa dhiraa tisa na upana wa dhiraa nne. Mpaka sasa kinaweza kuonekana katika mji wa Waamoni wa Raba.)
(Защото само васанският цар Ог беше останал от оцелелите от исполините; ето, леглото му беше желязно легло; не е ли то в Рава на амонците? Дължината му беше девет лакътя, и широчината му четири лакътя, според лакътя на мъж.)
12 Katika nchi tuliyoiteka wakati ule, niliwapa kabila la Reubeni na Gadi eneo lililoko kaskazini la Aroeri kando ya Bonde la Arnoni, na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake.
И дадох на рувимците и на гадците земята, който превзехме в онова време, от Ароир, който е при потока Арнон и половината от планинските страни на Галаад с градовете му;
13 Kisha nusu ya kabila la Manase niliwapa sehemu ya Gileadi iliyobaki pamoja na Bashani yote, ambayo ilikuwa utawala wa Ogu. (Eneo lote la Argobu katika Bashani lilikuwa linajulikana kama nchi ya Warefai.
а остатъка на Галаад и целия Васан, царството на Ога, дадох на половината от манасиевото племе, цялата Арговска област, с целия Васан, който се нарича земя на исполините.
14 Yairi, mzao wa kabila la Manase, alichukua eneo lote la nchi ya Argobu hadi kufikia mpaka wa Wageshuri na Wamaaka, ukaitwa kwa jina lake; kwa hiyo mpaka leo hii Bashani inaitwa Hawoth-Yairi.)
Манасиевият потомец Яир взе цялата Арговска област до границите на гесурците и маахатците, и нарече земите по свое име Васан-авот-яир, както се наричат и до днес.
15 Nikampa Makiri nchi ya Gileadi.
А на Махира дадох Галаад.
16 Lakini niliwapa Wareubeni na Wagadi eneo kuanzia Gileadi hadi Bonde la Arnoni (katikati ya bonde ulikuwa ndio mpaka), kuelekea mpaka Mto Yaboki, ambao ndio mpaka wa Waamoni.
Но на рувимците и на гадците дадох от Галаад до потока Арнон, до средата на потока, за граница, и до потока Явок, границата на амонците,
17 Kwa upande wa magharibi mpaka wao ulikuwa Yordani katika Araba, toka ziwa Galilaya hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), kwenye miteremko ya Pisga upande wa mashariki.
и полето, и Иордан, който им е граница от Хинерот до морето в полето, то ест, Соленото море, под Асдот-фасга на изток.
18 Wakati huo nilikuamuru: “Bwana Mungu wako amekupa nchi hii uimiliki. Lakini ni lazima wanaume wenu wote wenye uwezo, wakiwa wamejiandaa tayari kwa vita, wavuke ngʼambo wakiwatangulia ndugu zako Waisraeli.
В онова време ви заповядах, казвайки: Господ вашият Бог ви даде тая земя да я притежавате; затова всички вие храбри мъже минете въоръжени пред братята си израилтяните.
19 Lakini wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu (kwani najua mnayo mifugo mingi) wanaweza kukaa katika miji niliyowapa,
Само жените ви, децата ви и добитъкът ви (защото зная, че имате много добитък) нека останат в градовете, които ви дадох,
20 mpaka hapo Bwana atakapowapa ndugu zenu kupumzika kama alivyowapa ninyi, wao pia wamiliki ile nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, ngʼambo ya Yordani. Baada ya hapo, kila mmoja wenu anaweza kurudi kwenye milki niliyowapa.”
догде Господ успокои братята ви както е успокоил и вас, и превземат и те земята, която Господ нашият Бог ще им даде оттатък Иордан; тогава да се върнете всеки в наследството, което ви дадох.
21 Wakati huo nilimwamuru Yoshua, “Umejionea kwa macho yako mwenyewe yale yote ambayo Bwana Mungu wenu amewafanyia wafalme hawa wawili. Bwana atazifanyia falme zote huko mnakokwenda vivyo hivyo.
В онова време заръчах на Исуса, като му казах: Очите ти видяха всичко що стори Господ вашият Бог на тия двама царе; така ще направи Господ и на всичките царства, към които преминаваш.
22 Msiwaogope, Bwana Mungu wenu atapigana kwa ajili yenu.”
Да се не боите от тях; защото Господ вашият Бог, Той воюва за вас.
23 Wakati huo nilimsihi Bwana:
В онова време се молих Господу, казвайки:
24 “Ee Bwana Mwenyezi, umemwonyesha mtumishi wako ukuu wako na mkono wako wenye uweza. Kwa kuwa ni mungu yupi aliye mbinguni au duniani anayeweza kufanya kazi na matendo makuu kama ufanyayo wewe?
Господи Иеова, Ти си почнал да показваш на слугата Си величието Си и крепката Си ръка; защото кой и тоя бог, на небето или на земята, който може да работи, както Ти работиш и според Твоите мощни дела?
25 Acha niende nikaione hiyo nchi nzuri ngʼambo ya Yordani, ile nchi nzuri ya vilima na Lebanoni.”
Нека премина, моля Ти се, и видя добрата земя оттатък Иордан, оная добра планинска страна и Ливан.
26 Lakini kwa sababu yenu Bwana alinikasirikia na hakutaka kunisikiliza. Bwana aliniambia, “Hilo latosha; usiseme nami jambo hili tena.
Но Господ понеже бе се разгневил на мене поради вас, не ме послуша; и Господ ми рече: Стига ти; да Ми не продумаш вече за това.
27 Kwea juu ya kilele cha Pisga uangalie magharibi, kaskazini, kusini na mashariki. Iangalie hiyo nchi kwa macho yako, kwa vile wewe hutavuka Yordani.
Възкачи се на върха на Фасга, и дигни очи към запад и север, към юг и изток, та гледай земята с очите си; защото няма да преминеш тоя Иордан.
28 Lakini mwagize Yoshua, mtie moyo na umtie nguvu, kwa kuwa yeye atawaongoza watu hawa hadi ngʼambo na kuwarithisha nchi utakayoiona.”
И заръчай на Исуса, насърчи го и укрепи го; защото той ще мине пред тия люде, и той ще им раздели за наследство земята, който ще видиш.
29 Kwa hiyo tulikaa kwenye bonde karibu na Beth-Peori.
И така, седяхме в долината срещу Вет-фегор.

< Torati 3 >