< Torati 28 >

1 Kama ukimtii Bwana Mungu wako kwa bidii na kufuata amri zake zote ninazokupa leo kwa bidii, Bwana Mungu wako atakuweka juu ya mataifa yote katika dunia.
«و اگر آواز یهوه خدای خود را به دقت بشنوی تا هوشیار شده، تمامی اوامر اورا که من امروز به تو امر می‌فرمایم بجا آوری، آنگاه یهوه خدایت تو را بر جمیع امتهای جهان بلند خواهد گردانید.۱
2 Baraka hizi zote zitakuja juu yako na kukupata, kama ukimtii Bwana Mungu wako:
و تمامی این برکتها به توخواهد رسید و تو را خواهد دریافت، اگر آوازیهوه خدای خود را بشنوی.۲
3 Utabarikiwa mjini na utabarikiwa mashambani.
در شهر، مبارک ودر صحرا، مبارک خواهی بود.۳
4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na mazao ya nchi yako na wanyama wako wachanga wa kufugwa, yaani ndama wa makundi yako ya ngʼombe, na wana-kondoo wa makundi yako.
میوه بطن تو ومیوه زمین تو و میوه بهایمت و بچه های گاو وبره های گله تو مبارک خواهند بود.۴
5 Kapu lako na vyombo vyako vya kukandia vitabarikiwa.
سبد و ظرف خمیر تو مبارک خواهد بود.۵
6 Utabarikiwa uingiapo na utabarikiwa utokapo.
وقت درآمدنت مبارک، و وقت بیرون رفتنت مبارک خواهی بود.۶
7 Bwana atasababisha adui wainukao dhidi yako kushindwa mbele yako. Watakujia kwa njia moja lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba.
«و خداوند دشمنانت را که با تو مقاومت نمایند، از حضور تو منهزم خواهد ساخت، ازیک راه بر تو خواهند آمد، و از هفت راه پیش توخواهند گریخت.۷
8 Bwana ataagiza baraka juu ya ghala zako na juu ya kila kitu utakachogusa kwa mkono wako. Bwana Mungu wako atakubariki katika nchi anayokupa.
خداوند در انبارهای تو و به هر‌چه دست خود را به آن دراز می‌کنی بر توبرکت خواهد فرمود، و تو را در زمینی که یهوه خدایت به تو می‌دهد، مبارک خواهد ساخت.۸
9 Bwana atakufanya kuwa taifa lake takatifu, kama alivyokuahidi kwa kiapo, kama ukishika maagizo ya Bwana Mungu wako na kwenda katika njia zake.
واگر اوامر یهوه خدای خود را نگاهداری، و درطریقهای او سلوک نمایی، خداوند تو را برای خود قوم مقدس خواهد گردانید، چنانکه برای تو قسم خورده است.۹
10 Kisha mataifa yote ya dunia wataona kuwa unaitwa kwa jina la Bwana, nao watakuogopa.
و جمیع امتهای زمین خواهند دید که نام خداوند بر تو خوانده شده است، و از تو خواهند ترسید.۱۰
11 Bwana atakupa kustawi kwa wingi, katika tunda la uzao wa tumbo lako, katika wanyama wachanga wa mifugo yako na katika mazao ya ardhi yako, katika nchi aliyowaapia baba zako kuwapa.
و خداوندتو را در میوه بطنت و ثمره بهایمت ومحصول زمینت، در زمینی که خداوند برای پدرانت قسم خورد که به تو بدهد، به نیکویی خواهد افزود.۱۱
12 Bwana atafungua mbingu, ghala zake za baraka, kukupa mvua kwa majira yake na kubariki kazi zako zote za mikono yako. Utakopesha mataifa mengi lakini hutakopa kwa yeyote.
و خداوند خزینه نیکوی خود، یعنی آسمان را برای تو خواهد گشود، تا باران زمین تو را در موسمش بباراند، و تو را درجمیع اعمال دستت مبارک سازد، و به امتهای بسیار قرض خواهی داد، و تو قرض نخواهی گرفت.۱۲
13 Bwana atakufanya kichwa, wala si mkia. Kama utazingatia maagizo ya Bwana Mungu wako ninayokupa siku hii ya leo na kuyafuata kwa bidii, daima utakuwa juu, kamwe hutakuwa chini.
و خداوند تو را سر خواهد ساخت نه دم، و بلند خواهی بود فقط نه پست، اگر اوامریهوه خدای خود را که من امروز به تو امرمی فرمایم بشنوی، و آنها را نگاه داشته، بجاآوری.۱۳
14 Usihalifu amri zangu zozote ninazokupa leo, kwa kwenda kuume au kushoto, kwa kufuata miungu mingine na kuitumikia.
و از همه سخنانی که من امروز به تو امرمی کنم به طرف راست یا چپ میل نکنی، تاخدایان غیر را پیروی نموده، آنها را عبادت کنی.۱۴
15 Hata hivyo, kama hutamtii Bwana Mungu wako na kuzishika kwa bidii amri zake zote na maagizo ninayokupa leo, laana hizi zote zitakuja juu yako na kukupata:
«و اما اگر آواز یهوه خدای خود را نشنوی تا هوشیار شده، همه اوامر و فرایض او را که من امروز به تو امر می‌فرمایم بجا آوری، آنگاه جمیع این لعنتها به تو خواهد رسید، و تو را خواهددریافت.۱۵
16 Utalaaniwa mjini na utalaaniwa mashambani.
در شهر ملعون، و در صحرا ملعون خواهی بود.۱۶
17 Kapu lako na chombo chako cha kukandia kitalaaniwa.
سبد و ظرف خمیر تو ملعون خواهد بود.۱۷
18 Uzao wa tumbo lako utalaaniwa, mazao ya ardhi yako, ndama wa makundi yako ya ngʼombe na wana-kondoo wa makundi yako.
میوه بطن تو و میوه زمین تو وبچه های گاو و بره های گله تو ملعون خواهد بود.۱۸
19 Utalaaniwa uingiapo na utokapo.
وقت درآمدنت ملعون، و وقت بیرون رفتنت ملعون خواهی بود.۱۹
20 Bwana ataleta laana juu yako, fadhaa na kukaripiwa katika kila kitu unachokigusa kwa mkono wako, mpaka uwe umeharibiwa na kuangamizwa ghafula kwa ajili ya maovu uliyoyafanya kwa kumwacha yeye.
و به هر‌چه دست خود رابرای عمل نمودن دراز می‌کنی خداوند بر تولعنت و اضطراب و سرزنش خواهد فرستاد تا به زودی هلاک و نابود شوی، به‌سبب بدی کارهایت که به آنها مرا ترک کرده‌ای،۲۰
21 Bwana atakupiga kwa magonjwa mpaka akuangamize kutoka nchi unayoingia kuimiliki.
خداوندوبا را بر تو ملصق خواهد ساخت، تا تو را اززمینی که برای تصرفش به آن داخل می‌شوی، هلاک سازد.۲۱
22 Bwana atakupiga kwa magonjwa ya kudhoofisha, kwa homa na kuwashwa, hari na kwa ukame, kutu na kuwa na uchungu ambavyo vitakupiga mpaka uangamie.
و خداوند تو را با سل و تب والتهاب و حرارت و شمشیر و باد سموم و یرقان خواهد زد، و تو را تعاقب خواهند نمود تا هلاک شوی.۲۲
23 Anga juu yako itakuwa shaba, na ardhi chini yako itakuwa chuma.
و فلک تو که بالای سر تو است مس خواهد شد، و زمینی که زیر تو است آهن.۲۳
24 Bwana atafanya mvua ya nchi yako kuwa mavumbi na mchanga; vitakujia kutoka angani mpaka uangamie.
وخداوند باران زمینت را گرد و غبار خواهدساخت، که از آسمان بر تو نازل شود تا هلاک شوی.۲۴
25 Bwana atakufanya ushindwe mbele ya adui zako. Utawajia kwa njia moja lakini utawakimbia mbele yao kwa njia saba, nawe utakuwa kitu cha kuchukiza kwa falme zote za dunia.
«و خداوند تو را پیش روی دشمنانت منهزم خواهد ساخت. از یک راه بر ایشان بیرون خواهی رفت، و از هفت راه از حضور ایشان خواهی گریخت، و در تمامی ممالک جهان به تلاطم خواهی افتاد.۲۵
26 Mizoga yenu itakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi, wala hapatakuwepo mtu yeyote wa kuwafukuza.
و بدن شما برای همه پرندگان هوا و بهایم زمین خوراک خواهد بود، وهیچ‌کس آنها را دور نخواهد کرد.۲۶
27 Bwana atakupiga kwa majipu ya Misri na kwa vidonda vitokavyo usaha na kuwashwa, ambako huwezi kuponywa.
خداوند تو را به دنبل مصر و خراج و جرب و خارشی که تواز آن شفا نتوانی یافت، مبتلا خواهد ساخت.۲۷
28 Bwana atakupiga kwa wazimu, upofu na kuchanganyikiwa kwa akili.
خداوند تو را به دیوانگی و نابینایی و پریشانی دل مبتلا خواهد ساخت.۲۸
29 Wakati wa adhuhuri utapapasapapasa huku na huko kama mtu kipofu katika giza. Hutafanikiwa katika lolote ufanyalo; siku baada ya siku utaonewa na kunyangʼanywa, wala hakuna yeyote atakayekuokoa.
و در وقت ظهر مثل کوری که در تاریکی لمس نماید کورانه راه خواهی رفت، و در راههای خود کامیاب نخواهی شد، بلکه در تمامی روزهایت مظلوم وغارت شده خواهی بود، و نجات‌دهنده‌ای نخواهد بود.۲۹
30 Utaposa mke, lakini mtu mwingine atakutana naye kimwili. Utajenga nyumba, lakini hutaishi ndani yake. Utapanda shamba la mizabibu, lakini hutakula matunda yake.
زنی را نامزد خواهی کرد ودیگری با او خواهد خوابید. خانه‌ای بنا خواهی کرد و در آن ساکن نخواهی شد. تاکستانی غرس خواهی نمود و میوه‌اش را نخواهی خورد.۳۰
31 Ngʼombe wako atachinjwa mbele ya macho yako lakini hutakula nyama yake. Punda wako atachukuliwa kwa nguvu kutoka kwako wala hatarudishwa. Kondoo wako watapewa adui zako, wala hakuna mtu yeyote wa kuwaokoa.
گاوت در نظرت کشته شود و از آن نخواهی خورد. الاغت پیش روی تو به غارت برده شود وباز به‌دست تو نخواهند آمد. گوسفند تو به دشمنت داده می‌شود و برای تو رهاکننده‌ای نخواهد بود.۳۱
32 Wanao na binti zako watatolewa kwa mataifa mengine, nawe utayachosha macho yako ukiwatazamia siku baada ya siku, hutakuwa na nguvu kuinua mkono.
پسران و دخترانت به امت دیگرداده می‌شوند، و چشمانت نگریسته از آرزوی ایشان تمامی روز کاهیده خواهد شد، و در دست تو هیچ قوه‌ای نخواهد بود.۳۲
33 Taifa usilolijua watakula mazao ya nchi yako na taabu ya kazi yako, hutakuwa na chochote, bali kuonewa kikatili siku zako zote.
میوه زمینت ومشقت تو را امتی که نشناخته‌ای، خواهند خورد، و همیشه فقط مظلوم و کوفته شده خواهی بود.۳۳
34 Vitu utakavyoviona kwa macho yako vitakufanya wazimu.
به حدی که از چیزهایی که چشمت می‌بیند، دیوانه خواهی شد.۳۴
35 Bwana atayapiga magoti yako na miguu yako kwa majipu yenye maumivu makali yasiyoponyeka, yakienea kutoka nyayo za miguu yako hadi utosini.
خداوند زانوها و ساقها واز کف پا تا فرق سر تو را به دنبل بد که از آن شفانتوانی یافت، مبتلا خواهد ساخت.۳۵
36 Bwana atakupeleka wewe na mfalme uliyemweka juu yako uende kwenye taifa ambalo hukulijua wewe wala baba zako. Huko utaabudu miungu mingine, miungu ya miti na mawe.
خداوند تورا و پادشاهی را که بر خود نصب می‌نمایی، بسوی امتی که تو و پدرانت نشناخته‌اید، خواهدبرد، و در آنجا خدایان غیر را از چوب و سنگ عبادت خواهی کرد.۳۶
37 Utakuwa kitu cha kuchukiza, tena kitu cha kudharauliwa na kudhihakiwa kwa mataifa yote huko Bwana atakakokupeleka.
و در میان تمامی امتهایی که خداوند شما را به آنجا خواهد برد، عبرت ومثل و سخریه خواهی شد.۳۷
38 Utapanda mbegu nyingi katika shamba lakini utavuna haba, kwa sababu nzige watazila.
«تخم بسیار به مزرعه خواهی برد، و اندکی جمع خواهی کرد چونکه ملخ آن را خواهدخورد.۳۸
39 Utapanda mashamba ya mizabibu na kuyapalilia, lakini hutakunywa divai yake wala hutakusanya zabibu, kwa sababu wadudu watazila.
تاکستانها غرس نموده، خدمت آنها راخواهی کرد، اما شراب را نخواهی نوشید و انگوررا نخواهی چید، زیرا کرم آن را خواهد خورد.۳۹
40 Utakuwa na mizeituni katika nchi yako yote, lakini hutatumia hayo mafuta yake, kwa sababu zeituni zitapukutika.
تو را در تمامی حدودت درختان زیتون خواهد بود، لکن خویشتن را به زیت تدهین نخواهی کرد، زیرا زیتون تو نارس ریخته خواهدشد.۴۰
41 Utakuwa na wana na binti lakini hawatakuwa nawe, kwa sababu watachukuliwa mateka.
پسران و دختران خواهی آورد، لیکن ازآن تو نخواهند بود، چونکه به اسیری خواهندرفت.۴۱
42 Makundi ya nzige yatavamia miti yako yote na mazao ya nchi yako.
تمامی درختانت و محصول زمینت راملخ به تصرف خواهد آورد.۴۲
43 Mgeni anayeishi miongoni mwako atainuka juu zaidi na zaidi kuliko wewe, lakini wewe utashuka chini zaidi na zaidi.
غریبی که در میان تو است بر تو به نهایت رفیع و برافراشته خواهدشد، و تو به نهایت پست و متنزل خواهی گردید.۴۳
44 Yeye atakukopesha, lakini wewe hutamkopesha. Yeye atakuwa kichwa, lakini wewe utakuwa mkia.
او به تو قرض خواهد داد و تو به او قرض نخواهی داد، او سر خواهد بود و تو دم خواهی بود.۴۴
45 Laana hizi zote zitakuja juu yako. Zitakufuatia na kukupata mpaka uangamizwe, kwa sababu hukumtii Bwana Mungu wako, na kuzishika amri zake na maagizo yake aliyokupa.
«و جمیع این لعنتها به تو خواهد رسید، وتو را تعاقب نموده، خواهد دریافت تا هلاک شوی، از این جهت که قول یهوه خدایت را گوش ندادی تا اوامر و فرایضی را که به تو امر فرموده بود، نگاه داری.۴۵
46 Zitakuwa ishara na ajabu kwako na kwa wazao wako milele.
و تو را و ذریت تو را تا به ابدآیت و شگفت خواهد بود.۴۶
47 Kwa sababu hukumtumikia Bwana Mungu wako kwa furaha na kwa moyo wakati wa kufanikiwa kwako,
«از این جهت که یهوه خدای خود را به شادمانی و خوشی دل برای فراوانی همه‌چیزعبادت ننمودی.۴۷
48 kwa hiyo katika njaa na kiu, katika uchi na umaskini wa kutisha, utawatumikia adui ambao Bwana atawatuma dhidi yako. Yeye ataweka nira ya chuma shingoni mwako hadi amekwisha kukuangamiza.
پس دشمنانت را که خداوندبر تو خواهد فرستاد در گرسنگی و تشنگی وبرهنگی و احتیاج همه‌چیز خدمت خواهی نمود، و یوغ آهنین بر گردنت خواهد گذاشت تا تورا هلاک سازد.۴۸
49 Bwana ataleta taifa dhidi yako kutoka mbali, kutoka miisho ya dunia, kama tai ashukiavyo mawindo chini, taifa ambalo hutaijua lugha yake,
و خداوند از دور، یعنی ازاقصای زمین، امتی را که مثل عقاب می‌پرد بر توخواهد آورد، امتی که زبانش را نخواهی فهمید.۴۹
50 taifa lenye uso mkali lisilojali wazee wala kuwahurumia vijana.
امتی مهیب صورت که طرف پیران را نگاه ندارد و بر جوانان ترحم ننماید.۵۰
51 Watakula wadogo wa mifugo yako na mazao ya nchi yako mpaka umeangamia. Hawatakuachia nafaka, divai mpya au mafuta, wala ndama wowote wa kundi lako au wana-kondoo wa kundi lako mpaka umekuwa magofu.
و نتایج بهایم و محصول زمینت را بخورد تا هلاک شوی. وبرای تو نیز غله و شیره و روغن و بچه های گاو وبره های گوسفند را باقی نگذارد تا تو را هلاک سازد.۵۱
52 Nao wataizingira miji yote katika nchi yako mpaka kuta ndefu za ngome ambazo unazitegemea zimeanguka. Watazingira miji yote katika nchi ambayo Bwana Mungu wako anakupa.
و تو را در تمامی دروازه هایت محاصره کند تا دیواره های بلند و حصین که بر آنها توکل داری در تمامی زمینت منهدم شود، و تو را درتمامی دروازه هایت، در تمامی زمینی که یهوه خدایت به تو می‌دهد، محاصره خواهد نمود.۵۲
53 Utakula uzao wa tumbo lako, nyama ya wana wako na binti zako ambao Bwana Mungu wako amekupa, kwa sababu ya mateso yale adui zako watakayokuletea wakati wa kukuzingira.
و میوه بطن خود، یعنی گوشت پسران ودخترانت را که یهوه خدایت به تو می‌دهد درمحاصره و تنگی که دشمنانت تو را به آن زبون خواهند ساخت، خواهی خورد.۵۳
54 Hata yule mtu muungwana sana na makini miongoni mwako hatakuwa na huruma kwa ndugu yake mwenyewe au kwa mke ampendaye au watoto wake waliosalia,
مردی که درمیان شما نرم و بسیار متنعم است، چشمش بربرادر خود و زن هم آغوش خویش و بقیه فرزندانش که باقی می‌مانند بد خواهد بود.۵۴
55 naye hatampa hata mmoja wao nyama ya watoto wake ambao anawala. Kwa kuwa hakuna kitu kingine kilichosalia kwake katika mazingirwa makali ambayo adui yako watakuletea kwa miji yako yote.
به حدی که به احدی از ایشان از گوشت پسران خودکه می‌خورد نخواهد داد زیرا که در محاصره وتنگی که دشمنانت تو را در تمامی دروازه هایت به آن زبون سازند، چیزی برای او باقی نخواهد ماند.۵۵
56 Mwanamke ambaye ni muungwana sana na makini miongoni mwako, yaani ambaye ni makini sana na muungwana kiasi kwamba asingethubutu kugusa ardhi kwa wayo wa mguu wake, yeye atakuwa mchoyo kwa mume ampendaye na mwanawe mwenyewe au binti yake,
و زنی که در میان شما نازک و متنعم است که به‌سبب تنعم و نازکی خود جرات نمی کرد که کف پای خود را به زمین بگذارد، چشم او بر شوهرهم آغوش خود و پسر و دخترخویش بد خواهدبود.۵۶
57 kondoo wa nyuma kutoka kwenye tumbo lake na watoto anaowazaa. Kwa kuwa anakusudia kuwala kwa siri wakati wa kuzingirwa na katika taabu zile ambazo adui yako atazileta juu yako na miji yako.
و بر مشیمه‌ای که از میان پایهای او درآیدو بر اولادی که بزاید زیرا که آنها را به‌سبب احتیاج همه‌چیز در محاصره و تنگی که دشمنانت در دروازه هایت به آن تو را زبون سازندبه پنهانی خواهد خورد.»۵۷
58 Kama hutafuata kwa bidii maneno yote ya sheria hii, ambayo yameandikwa katika kitabu hiki na kama hutalicha hili jina la fahari na la kutisha, yaani la Bwana Mungu wako,
اگر به عمل نمودن تمامی کلمات این شریعت که در این کتاب مکتوب است، هوشیارنشوی و از این نام مجید و مهیب، یعنی یهوه، خدایت، نترسی،۵۸
59 Bwana ataleta mapigo ya kutisha juu yako na kwa wazao wako, maafa makali na ya kudumu, magonjwa mazito na ya kudumu.
آنگاه خداوند بلایای تو وبلایای اولاد تو را عجیب خواهد ساخت، یعنی بلایای عظیم و مزمن و مرضهای سخت و مزمن.۵۹
60 Atakuletea juu yako magonjwa yote ya Misri yale uliyoyaogopa, nayo yataambatana nawe.
و تمامی بیماریهای مصر را که از آنهامی ترسیدی بر تو باز خواهد آورد و به تو خواهدچسبید.۶۰
61 Pia Bwana atakuletea kila aina ya ugonjwa na maafa ambayo hayakuandikwa humu katika kitabu hiki cha sheria, mpaka utakapokuwa umeangamizwa.
و نیز همه مرضها و همه بلایایی که درطومار این شریعت مکتوب نیست آنها را خداوندبر تو مستولی خواهد گردانید تا هلاک شوی.۶۱
62 Ninyi ambao mlikuwa wengi kama nyota za angani mtaachwa wachache tu, kwa sababu hamkumtii Bwana Mungu wenu.
وگروه قلیل خواهید ماند، برعکس آن که مثل ستارگان آسمان کثیر بودید، زیرا که آواز یهوه خدای خود را نشنیدید.۶۲
63 Kama ilivyompendeza Bwana kuwafanya ninyi mstawi na kuongezeka kwa idadi, ndivyo itakavyompendeza kuwaharibu na kuwaangamiza ninyi. Mtangʼolewa kutoka nchi mnayoiingia kuimiliki.
و واقع می‌شودچنانکه خداوند بر شما شادی نمود تا به شمااحسان کرده، شما را بیفزاید همچنین خداوند برشما شادی خواهد نمود تا شما را هلاک و نابودگرداند، و ریشه شما از زمینی که برای تصرفش در آن داخل می‌شوید کنده خواهد شد.۶۳
64 Kisha Bwana atawatawanya miongoni mwa mataifa yote, kutoka mwisho mmoja wa dunia hadi mwingine. Huko mtaabudu miungu mingine, miungu ya miti na ya mawe, ambayo ninyi wala baba zenu hamkuijua.
وخداوند تو را در میان جمیع امتها از کران زمین تاکران دیگرش پراکنده سازد و در آنجا خدایان غیر را از چوب و سنگ که تو و پدرانت نشناخته‌اید، عبادت خواهی کرد.۶۴
65 Miongoni mwa mataifa hayo hamtapata raha wala mahali pa kupumzisha wayo wa mguu wenu. Huko Bwana atawapa mahangaiko ya mawazo, macho yaliyochoka kwa kungojea na moyo uliokata tamaa.
و در میان این امتها استراحت نخواهی یافت و برای کف پایت آرامی نخواهد بود، و در آنجا یهوه تو را دل لرزان و کاهیدگی چشم و پژمردگی جان خواهدداد.۶۵
66 Utaishi katika mahangaiko siku zote, ukiwa umejaa hofu usiku na mchana, wala hutakuwa kamwe na uhakika wa maisha yako.
و جان تو پیش رویت معلق خواهد بود، وشب و روز ترسناک شده، به‌جان خود اطمینان نخواهی داشت.۶۶
67 Wakati wa asubuhi utasema hivi, “Laiti ingekuwa jioni!” Jioni utasema, “Laiti ingekuwa asubuhi,” kwa sababu ya hofu ile itakayojaza moyo wako na vitu vile macho yako yatakavyoviona.
بامدادان خواهی گفت: کاش که شام می‌بود، و شامگاهان خواهی گفت: کاش که صبح می‌بود، به‌سبب ترس دلت که به آن خواهی ترسید، و به‌سبب رویت چشمت که خواهی دید.۶۷
68 Bwana atawarudisha tena Misri kwa meli, safari niliyosema kamwe hamngeenda tena. Huko mtajiuza ninyi wenyewe kwa adui zenu kama watumwa wa kiume na wa kike, lakini hakuna yeyote atakayewanunua.
و خداوند تو را در کشتیها ازراهی که به تو گفتم آن را دیگر نخواهی دید به مصر باز خواهد آورد، و خود را در آنجا به دشمنان خویش برای غلامی و کنیزی خواهیدفروخت و مشتری نخواهد بود.»۶۸

< Torati 28 >