< Torati 28 >
1 Kama ukimtii Bwana Mungu wako kwa bidii na kufuata amri zake zote ninazokupa leo kwa bidii, Bwana Mungu wako atakuweka juu ya mataifa yote katika dunia.
Ako zbilja poslušaš glas Jahve, Boga svoga, držeći i vršeći sve njegove zapovijedi što ti ih danas naređujem, Jahve, Bog tvoj, uzvisit će te nad sve narode na zemlji.
2 Baraka hizi zote zitakuja juu yako na kukupata, kama ukimtii Bwana Mungu wako:
Svi ovi blagoslovi sići će na te i stići će te ako budeš slušao glas Jahve, Boga svoga.
3 Utabarikiwa mjini na utabarikiwa mashambani.
Blagoslovljen ćeš biti u gradu, blagoslovljen u polju.
4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na mazao ya nchi yako na wanyama wako wachanga wa kufugwa, yaani ndama wa makundi yako ya ngʼombe, na wana-kondoo wa makundi yako.
Blagoslovljen će biti plod utrobe tvoje, rod zemlje tvoje, plod blaga tvoga: mlad krava tvojih i prirast stada tvoga.
5 Kapu lako na vyombo vyako vya kukandia vitabarikiwa.
Blagoslovljen će biti tvoj koš i naćve tvoje.
6 Utabarikiwa uingiapo na utabarikiwa utokapo.
Blagoslovljen ćeš biti kad ulaziš, blagoslovljen kad izlaziš.
7 Bwana atasababisha adui wainukao dhidi yako kushindwa mbele yako. Watakujia kwa njia moja lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba.
Neprijatelje tvoje koji se dignu protiv tebe Jahve će položiti preda te potučene; jednim će putem izaći na te, a na sedam putova razbježat će se ispred tebe.
8 Bwana ataagiza baraka juu ya ghala zako na juu ya kila kitu utakachogusa kwa mkono wako. Bwana Mungu wako atakubariki katika nchi anayokupa.
Jahve će narediti da blagoslov bude s tobom u žitnicama tvojim i u svakom pothvatu ruke tvoje i blagoslivljat će te u zemlji koju ti Jahve, Bog tvoj, daje.
9 Bwana atakufanya kuwa taifa lake takatifu, kama alivyokuahidi kwa kiapo, kama ukishika maagizo ya Bwana Mungu wako na kwenda katika njia zake.
Jahve će od tebe učiniti narod sebi posvećen, kako ti se zakleo, ako budeš držao zapovijedi Jahve, Boga svoga, i hodio njegovim putovima.
10 Kisha mataifa yote ya dunia wataona kuwa unaitwa kwa jina la Bwana, nao watakuogopa.
Svi narodi zemlje vidjet će da je nada te zazvano ime Jahvino te će strahovati od tebe.
11 Bwana atakupa kustawi kwa wingi, katika tunda la uzao wa tumbo lako, katika wanyama wachanga wa mifugo yako na katika mazao ya ardhi yako, katika nchi aliyowaapia baba zako kuwapa.
Jahve će te obasuti obilnim dobrima: porodom utrobe tvoje, priraštajem blaga tvoga i rodom s tla tvoga u zemlji za koju se Jahve zakleo ocima tvojim da će ti je dati.
12 Bwana atafungua mbingu, ghala zake za baraka, kukupa mvua kwa majira yake na kubariki kazi zako zote za mikono yako. Utakopesha mataifa mengi lakini hutakopa kwa yeyote.
Jahve će ti otvoriti svoju bogatu riznicu - nebo - da daje kišu tvojoj zemlji u pravo vrijeme i blagoslovi svaki pothvat ruku tvojih. Mnogim ćeš narodima u zajam davati, a sam nećeš uzimati u zajam.
13 Bwana atakufanya kichwa, wala si mkia. Kama utazingatia maagizo ya Bwana Mungu wako ninayokupa siku hii ya leo na kuyafuata kwa bidii, daima utakuwa juu, kamwe hutakuwa chini.
Jahve će te držati na pročelju, a ne u začelju; uvijek ćeš biti na vrhu, nikad na dnu, ako budeš slušao zapovijedi Jahve, Boga svoga, što ti ih danas naređujem da ih držiš i vršiš.
14 Usihalifu amri zangu zozote ninazokupa leo, kwa kwenda kuume au kushoto, kwa kufuata miungu mingine na kuitumikia.
Ni od jedne riječi što vam je danas nalažem nemoj odstupati ni desno ni lijevo idući za drugim bogovima i iskazujući im štovanje.
15 Hata hivyo, kama hutamtii Bwana Mungu wako na kuzishika kwa bidii amri zake zote na maagizo ninayokupa leo, laana hizi zote zitakuja juu yako na kukupata:
Ali ako ne budeš slušao glasa Jahve, Boga svoga, ne držeći i ne vršeći svih njegovih zapovijedi i svih njegovih zakona što ti ih danas naređujem, sva će ova prokletstva doći na te i stići će te:
16 Utalaaniwa mjini na utalaaniwa mashambani.
Proklet ćeš biti u gradu, proklet u polju.
17 Kapu lako na chombo chako cha kukandia kitalaaniwa.
Proklet će biti koš tvoj i naćve tvoje.
18 Uzao wa tumbo lako utalaaniwa, mazao ya ardhi yako, ndama wa makundi yako ya ngʼombe na wana-kondoo wa makundi yako.
Proklet će biti plod utrobe tvoje i rod zemlje tvoje, mlad krava tvojih i priraštaj stada tvoga.
19 Utalaaniwa uingiapo na utokapo.
Proklet ćeš biti kad ulaziš, proklet kad izlaziš.
20 Bwana ataleta laana juu yako, fadhaa na kukaripiwa katika kila kitu unachokigusa kwa mkono wako, mpaka uwe umeharibiwa na kuangamizwa ghafula kwa ajili ya maovu uliyoyafanya kwa kumwacha yeye.
Jahve će na te puštati prokletstvo, zabunu i kletvu u svemu na što pružiš ruku svoju da uradiš, sve dok ne budeš satrt i brzo ne propadneš zbog zloće svojih djela kojima si me napustio.
21 Bwana atakupiga kwa magonjwa mpaka akuangamize kutoka nchi unayoingia kuimiliki.
Kugu će Jahve za te privezati dok te ne nestane sa zemlje u koju ideš da je zaposjedneš.
22 Bwana atakupiga kwa magonjwa ya kudhoofisha, kwa homa na kuwashwa, hari na kwa ukame, kutu na kuwa na uchungu ambavyo vitakupiga mpaka uangamie.
Jahve će te udariti sušicom, groznicom, upalom, žegom i sušom, medljikom i snijeti; to će te goniti dok te ne nestane.
23 Anga juu yako itakuwa shaba, na ardhi chini yako itakuwa chuma.
Nebesa nad tvojom glavom postat će mjedena, a tlo pod tvojim nogama postat će gvozdeno.
24 Bwana atafanya mvua ya nchi yako kuwa mavumbi na mchanga; vitakujia kutoka angani mpaka uangamie.
Kišu tvoje zemlje Jahve će pretvarati u pijesak i prašinu da na te pada s nebesa dok te ne uništi.
25 Bwana atakufanya ushindwe mbele ya adui zako. Utawajia kwa njia moja lakini utawakimbia mbele yao kwa njia saba, nawe utakuwa kitu cha kuchukiza kwa falme zote za dunia.
Jahve će od tebe učiniti pobijeđenoga pred tvojim neprijateljima; jednim ćeš putem prema njima izlaziti, a na sedam putova bježat ćeš ispred njih. Strašilo ćeš postati za sva zemaljska kraljevstva.
26 Mizoga yenu itakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi, wala hapatakuwepo mtu yeyote wa kuwafukuza.
I mrtvo tijelo tvoje postat će hranom svim pticama nebeskim i svoj zvjeradi zemaljskoj. Nikoga neće biti da ih plaši.
27 Bwana atakupiga kwa majipu ya Misri na kwa vidonda vitokavyo usaha na kuwashwa, ambako huwezi kuponywa.
Jahve će te udarati egipatskim prištevima, čirevima, krastama i svrabom, od kojih se nećeš moći izliječiti.
28 Bwana atakupiga kwa wazimu, upofu na kuchanganyikiwa kwa akili.
Jahve će te udarati bjesnilom, sljepoćom i ludilom;
29 Wakati wa adhuhuri utapapasapapasa huku na huko kama mtu kipofu katika giza. Hutafanikiwa katika lolote ufanyalo; siku baada ya siku utaonewa na kunyangʼanywa, wala hakuna yeyote atakayekuokoa.
u po bijela dana tumarat ćeš kao što tumara slijepac po mraku; nećeš imati uspjeha u svojim pothvatima; sve vrijeme svoje bit ćeš izrabljivan i pljačkan, a neće biti nikoga da te spasi.
30 Utaposa mke, lakini mtu mwingine atakutana naye kimwili. Utajenga nyumba, lakini hutaishi ndani yake. Utapanda shamba la mizabibu, lakini hutakula matunda yake.
Sa ženom ćeš se zaručivati, ali će je drugi posjedovati. Kuću ćeš graditi, ali u njoj nećeš stanovati. Vinograd ćeš zasađivati, ali ga nećeš brati.
31 Ngʼombe wako atachinjwa mbele ya macho yako lakini hutakula nyama yake. Punda wako atachukuliwa kwa nguvu kutoka kwako wala hatarudishwa. Kondoo wako watapewa adui zako, wala hakuna mtu yeyote wa kuwaokoa.
Tvoga će vola na tvoje oči zaklati, ali ti od njega nećeš jesti; tvoga će magarca ispred tebe otimati, ali ti ga neće vraćati; stado će tvoje neprijatelju tvome predavati, a neće biti nikoga da ti pritekne u pomoć.
32 Wanao na binti zako watatolewa kwa mataifa mengine, nawe utayachosha macho yako ukiwatazamia siku baada ya siku, hutakuwa na nguvu kuinua mkono.
Sinovi tvoji i kćeri tvoje bit će predavani drugome narodu. Oči će tvoje svaki dan kapati gledajući za njima, ali ruka tvoja neće moći ništa.
33 Taifa usilolijua watakula mazao ya nchi yako na taabu ya kazi yako, hutakuwa na chochote, bali kuonewa kikatili siku zako zote.
Narod koji i ne poznaješ jest će plod sa zemlje tvoje i svu muku tvoju, dok ćeš ti sve vrijeme svoje biti izrabljivan i gažen.
34 Vitu utakavyoviona kwa macho yako vitakufanya wazimu.
Ludovat ćeš od prizora što će ih oči tvoje gledati.
35 Bwana atayapiga magoti yako na miguu yako kwa majipu yenye maumivu makali yasiyoponyeka, yakienea kutoka nyayo za miguu yako hadi utosini.
Jahve će te udarati ljutim prištevima po koljenima i po stegnima - od stopala nogu tvojih do tjemena na glavi tvojoj - od kojih se nećeš moći izliječiti.
36 Bwana atakupeleka wewe na mfalme uliyemweka juu yako uende kwenye taifa ambalo hukulijua wewe wala baba zako. Huko utaabudu miungu mingine, miungu ya miti na mawe.
Jahve će odvesti i tebe i tvoga kralja, koga budeš postavio nad sobom, među narod nepoznat i tebi i tvojim ocima te ćeš ondje iskazivati štovanje drugim bogovima, drvenim i kamenim.
37 Utakuwa kitu cha kuchukiza, tena kitu cha kudharauliwa na kudhihakiwa kwa mataifa yote huko Bwana atakakokupeleka.
Bit ćeš na zgražanje, porugu i ruglo svim narodima među koje te Jahve odvede.
38 Utapanda mbegu nyingi katika shamba lakini utavuna haba, kwa sababu nzige watazila.
Mnogo ćeš sjemena bacati u polje, ali ćeš malo žeti jer će ti urod skakavci ogolijevati.
39 Utapanda mashamba ya mizabibu na kuyapalilia, lakini hutakunywa divai yake wala hutakusanya zabibu, kwa sababu wadudu watazila.
Vinograde ćeš saditi i obrađivati, ali vina nećeš piti niti ćeš što brati jer će ih crv izjedati.
40 Utakuwa na mizeituni katika nchi yako yote, lakini hutatumia hayo mafuta yake, kwa sababu zeituni zitapukutika.
Imat ćeš masline po svemu svome području, ali se uljem nećeš mazati jer će ti masline opadati.
41 Utakuwa na wana na binti lakini hawatakuwa nawe, kwa sababu watachukuliwa mateka.
Sinove ćeš i kćeri rađati, ali tvoji neće biti jer će u sužanjstvo odlaziti.
42 Makundi ya nzige yatavamia miti yako yote na mazao ya nchi yako.
Sva tvoja stabla i rod sa zemlje tvoje postat će plijenom kukaca.
43 Mgeni anayeishi miongoni mwako atainuka juu zaidi na zaidi kuliko wewe, lakini wewe utashuka chini zaidi na zaidi.
Došljak koji bude u sredini tvojoj uzdizat će se nada te, a ti ćeš padati sve niže i niže.
44 Yeye atakukopesha, lakini wewe hutamkopesha. Yeye atakuwa kichwa, lakini wewe utakuwa mkia.
On će uzaimati tebi, a ne ti njemu; on će biti glava, a ti rep.
45 Laana hizi zote zitakuja juu yako. Zitakufuatia na kukupata mpaka uangamizwe, kwa sababu hukumtii Bwana Mungu wako, na kuzishika amri zake na maagizo yake aliyokupa.
Sva će te ova prokletstva snalaziti, progoniti i doseći dok te ne unište, jer nisi slušao glasa Jahve, Boga svoga, ni držao zapovijedi njegovih i zakona njegovih koje ti je dao.
46 Zitakuwa ishara na ajabu kwako na kwa wazao wako milele.
Ona će služiti za čudesni znak na tebi i tvome potomstvu zauvijek.
47 Kwa sababu hukumtumikia Bwana Mungu wako kwa furaha na kwa moyo wakati wa kufanikiwa kwako,
Budući da nisi htio služiti Jahvi, Bogu svome, vesela i radosna srca zbog obilja svega,
48 kwa hiyo katika njaa na kiu, katika uchi na umaskini wa kutisha, utawatumikia adui ambao Bwana atawatuma dhidi yako. Yeye ataweka nira ya chuma shingoni mwako hadi amekwisha kukuangamiza.
služit ćeš neprijatelju svome, koga će Jahve poslati na te, u gladu i žeđi, golotinji i oskudici svakoj. Na tvoju će šiju navaljivati jaram od gvožđa dok te ne satre.
49 Bwana ataleta taifa dhidi yako kutoka mbali, kutoka miisho ya dunia, kama tai ashukiavyo mawindo chini, taifa ambalo hutaijua lugha yake,
Jahve će iz daljine, s kraja zemlje, dovesti na te narod koji će sletjeti kao orao. Bit će to narod kojemu jezika nećeš razumjeti;
50 taifa lenye uso mkali lisilojali wazee wala kuwahurumia vijana.
narod bezdušan, koji neće pokazivati obzira prema starima ni smilovanja prema mladima.
51 Watakula wadogo wa mifugo yako na mazao ya nchi yako mpaka umeangamia. Hawatakuachia nafaka, divai mpya au mafuta, wala ndama wowote wa kundi lako au wana-kondoo wa kundi lako mpaka umekuwa magofu.
On će ti jesti mlado od tvoga blaga i rod tvoje njive dok te ne uništi; neće ti ostavljati ni žita, ni vina, ni ulja, ni mlado od krave, ni priraštaj od stada, sve dok te ne upropasti.
52 Nao wataizingira miji yote katika nchi yako mpaka kuta ndefu za ngome ambazo unazitegemea zimeanguka. Watazingira miji yote katika nchi ambayo Bwana Mungu wako anakupa.
Opsjedat će te u svim tvojim gradovima širom zemlje tvoje dok ne obori visoke i utvrđene bedeme u koje si polagao nadu svoju; opsjednut će te u svim gradovima tvojim širom zemlje tvoje koju ti dadne Jahve, Bog tvoj.
53 Utakula uzao wa tumbo lako, nyama ya wana wako na binti zako ambao Bwana Mungu wako amekupa, kwa sababu ya mateso yale adui zako watakayokuletea wakati wa kukuzingira.
U tjeskobi i jadu, kojima će te neprijatelj tvoj pritisnuti, jest ćeš plod utrobe svoje - meso sinova svojih i kćeri svojih koje ti dadne Jahve, Bog tvoj.
54 Hata yule mtu muungwana sana na makini miongoni mwako hatakuwa na huruma kwa ndugu yake mwenyewe au kwa mke ampendaye au watoto wake waliosalia,
Čovjek najnježniji i najmekši u tebe zlobnim će okom gledati na vlastitog brata, ženu u svome naručju i djecu svoju što mu preostanu,
55 naye hatampa hata mmoja wao nyama ya watoto wake ambao anawala. Kwa kuwa hakuna kitu kingine kilichosalia kwake katika mazingirwa makali ambayo adui yako watakuletea kwa miji yako yote.
ne hoteći ni s jednim od njih dijeliti mesa sinova svojih koje bude jeo, jer zbog tjeskobe i jada, kojima će te neprijatelj tvoj pritiskati po svim gradovima tvojim, drugo mu neće preostajati.
56 Mwanamke ambaye ni muungwana sana na makini miongoni mwako, yaani ambaye ni makini sana na muungwana kiasi kwamba asingethubutu kugusa ardhi kwa wayo wa mguu wake, yeye atakuwa mchoyo kwa mume ampendaye na mwanawe mwenyewe au binti yake,
I žena najnježnija i najmekša što bude u tebe - toliko nježna i tankoćutna da se ne usuđuje spustiti stopala na zemlju - zlobnim će okom gledati na muža u svome naručju, i na sina svoga, i na kćer svoju,
57 kondoo wa nyuma kutoka kwenye tumbo lake na watoto anaowazaa. Kwa kuwa anakusudia kuwala kwa siri wakati wa kuzingirwa na katika taabu zile ambazo adui yako atazileta juu yako na miji yako.
i na posteljicu svoju što joj iziđe između nogu, i na djecu što ih ima roditi, jer će ih potajno jesti, oskudna u svemu, zbog nevolje i jada kojim će te neprijatelj tvoj pritisnuti po svim gradovima tvojim.
58 Kama hutafuata kwa bidii maneno yote ya sheria hii, ambayo yameandikwa katika kitabu hiki na kama hutalicha hili jina la fahari na la kutisha, yaani la Bwana Mungu wako,
Ako ne budeš držao i vršio riječi ovoga Zakona što su napisane u ovoj knjizi, ne poštujući ovo slavno i strašno Ime - Jahvu, Boga svoga -
59 Bwana ataleta mapigo ya kutisha juu yako na kwa wazao wako, maafa makali na ya kudumu, magonjwa mazito na ya kudumu.
Jahve će tebe i tvoje potomstvo teško ošinuti velikim i dugotrajnim bičevima, pogubnim i dugim bolestima.
60 Atakuletea juu yako magonjwa yote ya Misri yale uliyoyaogopa, nayo yataambatana nawe.
Pustit će na te sva zla egipatska kojih si se plašio, i ona će se prilijepiti za te.
61 Pia Bwana atakuletea kila aina ya ugonjwa na maafa ambayo hayakuandikwa humu katika kitabu hiki cha sheria, mpaka utakapokuwa umeangamizwa.
A i svaku drugu bolest i bič, koji nije naveden u knjizi ovoga Zakona, Jahve će na te puštati dok te ne uništi.
62 Ninyi ambao mlikuwa wengi kama nyota za angani mtaachwa wachache tu, kwa sababu hamkumtii Bwana Mungu wenu.
Ostat će vas samo malo, vas što brojni bijaste kao zvijezde nebeske, a sve zato što nisi slušao glasa Jahve, Boga svoga.
63 Kama ilivyompendeza Bwana kuwafanya ninyi mstawi na kuongezeka kwa idadi, ndivyo itakavyompendeza kuwaharibu na kuwaangamiza ninyi. Mtangʼolewa kutoka nchi mnayoiingia kuimiliki.
Kako se Jahve nad vama radovao usrećujući vas i množeći, tako će se Jahve radovati nad vama rušeći vas i uništavajući da se iskorijenite sa zemlje u koju idete da je zaposjednete.
64 Kisha Bwana atawatawanya miongoni mwa mataifa yote, kutoka mwisho mmoja wa dunia hadi mwingine. Huko mtaabudu miungu mingine, miungu ya miti na ya mawe, ambayo ninyi wala baba zenu hamkuijua.
Jahve će vas razbacati po svim narodima, s kraja na kraj zemlje; ondje ćeš iskazivati štovanje drugim bogovima: drvenim i kamenim - koji su bili nepoznati i tebi i tvojim ocima.
65 Miongoni mwa mataifa hayo hamtapata raha wala mahali pa kupumzisha wayo wa mguu wenu. Huko Bwana atawapa mahangaiko ya mawazo, macho yaliyochoka kwa kungojea na moyo uliokata tamaa.
Ali među tim narodima nećeš imati mira; ni tvome stopalu neće biti počivališta, nego će ti ondje Jahve dati srce uznemireno, oči utonule, dušu tjeskobnu.
66 Utaishi katika mahangaiko siku zote, ukiwa umejaa hofu usiku na mchana, wala hutakuwa kamwe na uhakika wa maisha yako.
Život tvoj visjet će o niti; bojat ćeš se i danju i noću i nećeš biti siguran za život svoj.
67 Wakati wa asubuhi utasema hivi, “Laiti ingekuwa jioni!” Jioni utasema, “Laiti ingekuwa asubuhi,” kwa sababu ya hofu ile itakayojaza moyo wako na vitu vile macho yako yatakavyoviona.
U strahu koji će ti stezati srce i od prizora što će ga oči tvoje gledati, jutrom ćeš govoriti: 'Oh, da je već večer!' a navečer ćeš govoriti: 'Oh, da je već jutro!'
68 Bwana atawarudisha tena Misri kwa meli, safari niliyosema kamwe hamngeenda tena. Huko mtajiuza ninyi wenyewe kwa adui zenu kama watumwa wa kiume na wa kike, lakini hakuna yeyote atakayewanunua.
U Egipat će te na galijama natrag odvesti Jahve putem za koji sam ti rekao da ga više ne smiješ vidjeti. Ondje ćete se vi sami prodavati svojim neprijateljima za robove i ropkinje, ali neće biti kupca.”