< Torati 27 >
1 Mose na wazee wa Israeli wakawaagiza watu: “Yashikeni maagizo haya yote ninayowaagiza leo.
OR Mosè, con gli Anziani d'Israele, comandò e disse al popolo: Osservate tutti i comandamenti i quali oggi vi do.
2 Mtakapokuwa mmevuka Mto Yordani na kuingia katika nchi awapayo Bwana Mungu wenu, msimamishe mawe makubwa na mkayatie lipu.
E nel giorno che sarete passati il Giordano, [per entrar] nel paese che il Signore Iddio vostro vi dà, rizzati delle grandi pietre, e smaltale con calcina.
3 Andikeni juu yake maneno yote ya sheria hii wakati mtakapokuwa mmevuka na kuingia katika nchi awapayo Bwana Mungu wenu, nchi itiririkayo maziwa na asali, kama vile Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaahidi.
E scrivi sopra esse tutte le parole di questa Legge, dopo che tu sarai passato, per entrar nel paese che il Signore Iddio tuo ti dà, paese stillante latte e miele; siccome il Signore Iddio de' tuoi padri te ne ha parlato.
4 Mtakapokuwa mmevuka Yordani, simamisheni mawe haya juu ya Mlima Ebali, kama ninavyowaagiza leo, mkayatie lipu.
Quando adunque sarete passati il Giordano, rizzatevi queste pietre, le quali oggi vi comando, nel monte di Ebal; e smaltatele con calcina.
5 Huko mjengeeni Bwana Mungu wenu madhabahu, madhabahu ya mawe. Msitumie kifaa chochote cha chuma juu yake.
Edifica ancora quivi un altare al Signore Iddio tuo, un altar di pietre; non far passare ferro sopra esse.
6 Jengeni madhabahu ya Bwana Mungu wenu kwa mawe ya shambani, na mtoe sadaka za kuteketezwa juu yake kwa Bwana Mungu wenu.
Edifica l'altare del Signore Iddio tuo di pietre intiere; e offerisci sopra esso olocausti al Signore Iddio tuo.
7 Toeni sadaka za amani juu yake, mkizila na kufurahia mbele za Bwana Mungu wenu.
Sacrifica ancora quivi sacrificii da render grazie; e mangia, e rallegrati davanti al Signore Iddio tuo.
8 Nanyi mtaandika maneno yote ya sheria hii kwa wazi sana juu ya mawe haya ambayo mmesimamisha.”
E scrivi sopra quelle pietre tutte le parole di questa Legge chiaramente e bene.
9 Kisha Mose na makuhani, ambao ni Walawi, wakawaambia Israeli wote, “Nyamaza ee Israeli, sikiliza! Sasa umekuwa taifa la Bwana Mungu wako.
Mosè ancora, co' sacerdoti Leviti, parlò a tutto Israele, dicendo: Attendi, e ascolta, Israele: Oggi tu sei divenuto popolo del Signore Iddio tuo.
10 Mtii Bwana Mungu wako, na kufuata amri zake na maagizo ninayokupa leo.”
Ubbidisci adunque alla voce del Signore Iddio tuo, e metti in opera i suoi comandamenti, e i suoi statuti, i quali oggi ti do.
11 Siku ile ile Mose akawaagiza watu:
Mosè ancora in quello stesso giorno comandò, e disse al popolo:
12 Mtakapovuka Mto Yordani, makabila haya yatasimama juu ya Mlima Gerizimu kubariki watu: Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Yosefu na Benyamini.
Gli uni [d'infra voi] stieno sopra il monte di Gherizim, per benedire il popolo quando sarete passati il Giordano; [cioè, le tribù di] Simeone, [di] Levi, [di] Giuda, [d]'Issacar, [di] Giuseppe, e [di] Beniamino;
13 Makabila haya yatasimama juu ya Mlima Ebali kwa kutamka laana: Reubeni, Gadi, Asheri, Zabuloni, Dani na Naftali.
e gli altri stieno sopra il monte di Ebal, per [pronunziar] la maledizione; [cioè, le tribù di] Ruben, [di] Gad, [di] Aser, [di] Zabulon, [di] Dan, e [di] Neftali.
14 Nao Walawi watawasomea watu wote wa Israeli kwa sauti kubwa:
E parlino i Leviti, e dicano ad alta voce a tutti gl'Israeliti:
15 “Alaaniwe mtu afanyaye sanamu ya kuchonga au mwenye kusubu sanamu, kitu ambacho ni chukizo kwa Bwana, kazi ya mikono ya fundi stadi, na kuisimamisha kwa siri.”
Maledetto [sia] l'uomo che avrà fatta scultura, o statua di getto, [che è] cosa abbominevole al Signore, opera di man di artefice, e l'avrà riposta in luogo occulto. — E risponda tutto il popolo, e dica: Amen.
16 “Alaaniwe mtu amdharauye baba yake na mama yake.”
Maledetto [sia] chi sprezza suo padre o sua madre. — E dica tutto il popolo: Amen.
17 “Alaaniwe mtu asogezaye jiwe la mpaka wa jirani yake.”
Maledetto [sia] chi muove i termini del suo prossimo. — E tutto il popolo dica: Amen.
18 “Alaaniwe mtu ampotoshaye kipofu njiani.”
Maledetto [sia] chi trasvia il cieco. — E tutto il popolo dica: Amen.
19 “Alaaniwe mtu apotoshaye haki ya mgeni, yatima au mjane.”
Maledetto [sia] chi pervertisce la ragione del forestiere, dell'orfano, e della vedova. — E tutto il popolo dica: Amen.
20 “Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mke wa baba yake, kwa maana anadharau malazi ya baba yake.”
Maledetto [sia] chi giace con la moglie di suo padre; perciocchè egli scopre il lembo di suo padre. — E tutto il popolo dica: Amen.
21 “Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mnyama yeyote.”
Maledetto [sia] chi si congiugne con alcuna bestia. — E tutto il popolo dica: Amen.
22 “Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na dada yake, binti wa baba yake au binti wa mama yake.”
Maledetto [sia] chi giace con la sua sorella, figliuola di suo padre, o figliuola di sua madre. — E tutto il popolo dica: Amen.
23 “Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mama mkwe wake.”
Maledetto [sia] chi giace con la sua suocera. — E tutto il popolo dica: Amen.
24 “Alaaniwe mtu amuuaye jirani yake kwa siri.”
Maledetto [sia] chi uccide il suo prossimo in occulto. — E tutto il popolo dica: Amen.
25 “Alaaniwe mtu apokeaye rushwa ili kumuua mtu asiye na hatia.”
Maledetto [sia] chi prende presente, per far morir l'innocente. — E tutto il popolo dica: Amen.
26 “Alaaniwe mtu yule ambaye hatashikilia maneno ya sheria hii kwa kuyatekeleza.”
Maledetto [sia] chi non avrà attenute le parole di questa Legge, per metterle in opera. — E tutto il popolo dica: Amen.