< Torati 26 >
1 Mtakapokuwa mmeingia nchi ile ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi na mtakapokuwa mmeimiliki na kukaa ndani yake,
Lorsque tu seras entré dans la terre que le Seigneur ton Dieu va le donner pour la posséder, que tu l’auras conquise et que tu auras habité en elle,
2 chukueni baadhi ya mavuno ya kwanza ya yale yote mtakayozalisha kutoka udongo wa nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa na mweke kwenye kapu. Kisha uende mahali ambapo Bwana Mungu wako atapachagua kuwa makao kwa ajili ya Jina lake
Tu prendras les prémices de tous tes fruits, tu les mettras dans la corbeille, et tu iras au lieu que le Seigneur ton Dieu aura choisi, afin que son nom y soit invoqué,
3 na umwambie kuhani atakayekuwepo kwa wakati huo, “Ninatangaza leo kwa Bwana Mungu wako kwamba nimekuja katika nchi ambayo Bwana aliwaapia baba zetu kwamba atatupa.”
Et tu t’approcheras du prêtre qu’il y aura en ces jours-là, et tu lui diras: Je déclare hautement aujourd’hui, en présence du Seigneur ton Dieu, que je suis entré dans la terre, au sujet de laquelle il a juré à nos pères qu’il nous la donnerait.
4 Kuhani atapokea lile kapu mikononi mwako na kuliweka chini mbele ya madhabahu ya Bwana Mungu wako.
Alors le prêtre prenant la corbeille de ta main, la déposera devant l’autel du Seigneur ton Dieu,
5 Kisha utatangaza mbele za Bwana Mungu wako: “Baba yangu alikuwa Mwaramu aliyekuwa anatangatanga, akaenda Misri pamoja na watu wachache, akaishi huko hadi akawa taifa kubwa, lenye nguvu na watu wengi.
Et tu diras en présence du Seigneur ton Dieu: Un Syrien poursuivait mon père, qui descendit en Egypte, et là, il séjourna avec un très petit nombre d’hommes; mais il forma une nation grande, forte et nombreuse à l’infini.
6 Lakini Wamisri walituonea na kututaabisha, wakitufanyisha kazi ngumu.
Mais les Egyptiens nous affligèrent et nous persécutèrent, nous imposant des fardeaux très lourds,
7 Kisha tulimlilia Bwana, Mungu wa baba zetu, naye Bwana akasikia sauti yetu na akaona huzuni yetu, taabu yetu na mateso yetu.
Alors nous criâmes au Seigneur le Dieu de nos pères, qui nous exauça, et regarda notre humiliation, notre labeur, et notre angoisse;
8 Kwa hiyo Bwana akatutoa nchi ya Misri kwa mkono wenye nguvu na ulionyooshwa, pamoja na utisho mkuu, ishara za miujiza na maajabu.
Et il nous retira de l’Egypte par une main forte et un bras étendu, par une grande terreur, des signes et des prodiges;
9 Akatuleta mahali hapa akatupa nchi hii, nchi inayotiririka maziwa na asali;
Puis il nous a introduits en ce lieu et nous a livré cette terre, où coulent du lait et du miel.
10 nami sasa ninaleta malimbuko ya ardhi ambayo wewe, Ee Bwana, umenipa.” Weka kapu mbele za Bwana Mungu wako na usujudu mbele zake.
Et c’est pour cela que maintenant j’offre les prémices des fruits de la terre, que le Seigneur m’a donnée. Et tu les laisseras en la présence du Seigneur ton Dieu, et adore le Seigneur ton Dieu.
11 Kisha wewe pamoja na Walawi na wageni wote walioko miongoni mwenu mtafurahi katika vitu vyote vizuri ambavyo Bwana Mungu wenu amewapa pamoja na wa nyumbani mwenu.
Et tu feras un festin de tous les biens que le Seigneur ton Dieu t’aura donnés, à toi et à ta maison, toi et le Lévite et l’étranger qui est avec toi.
12 Wakati utakapokuwa umeshatoa zaka zote za mazao yako katika mwaka wa tatu, ambao ni mwaka wa zaka, utampa Mlawi, mgeni, yatima na mjane, ili waweze kula katika miji yenu na kushiba.
Quand tu auras accompli la dîme de tous tes fruits, à la troisième année des décimes, tu les donneras au Lévite, à l’étranger, à l’orphelin et à la veuve, afin qu’ils les mangent au dedans de tes portes, et qu’ils soient rassasiés;
13 Kisha umwambie Bwana Mungu wako: “Nimeondoa katika nyumba yangu ile sehemu iliyowekwa wakfu na nimempa Mlawi, mgeni, yatima na mjane, kulingana na yote uliyoamuru. Sijazihalifu amri zako wala kusahau hata mojawapo.
Et tu diras en la présence du Seigneur ton Dieu: J’ai ôté de ma maison ce qui était consacré, et je l’ai donné au Lévite, à l’étranger, à l’orphelin et à la veuve, comme vous m’avez ordonné; je n’ai pas négligé vos commandements, et n’ai pas oublié votre ordre.
14 Sijala sehemu iliyowekwa wakfu wakati nilipokuwa nikiomboleza, wala sijaondoa mojawapo wakati nilipokuwa najisi, wala sijatoa sehemu yake yoyote kwa wafu. Nimemtii Bwana Mungu wangu; nimefanya kila kitu ulichoniamuru.
Je n’ai pas mangé de ces choses pendant mon deuil, je ne les ai mises à part pour aucun usage profane, et je n’en ai rien employé dans les funérailles. J’ai obéi à la voix du Seigneur mon Dieu et j’ai fait toutes choses, comme vous m’avez ordonné.
15 Angalia chini kutoka mbinguni, maskani yako matakatifu, uwabariki watu wako Israeli pamoja na nchi uliyotupa kama ulivyoahidi kwa kiapo kwa baba zetu, nchi inayotiririka maziwa na asali.”
Regardez de votre sanctuaire, du haut des cieux, votre demeure, et bénissez votre peuple d’Israël, et la terre que vous nous avez donnée, comme vous avez juré à nos pères, terre où coulent du lait et du miel.
16 Bwana Mungu wako anakuagiza leo kufuata amri hizi na sheria; zishike kwa bidii kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote.
Aujourd’hui le Seigneur ton Dieu t’a ordonné d’exécuter ces commandements et ces ordonnances, de les garder et de les accomplir de tout ton cœur et de toute ton âme.
17 Umetangaza leo kwamba Bwana ndiye Mungu wako na kwamba utafuata njia zake, kwamba utayashika maagizo yake, amri zake na sheria zake nawe utamtii.
Tu as choisi aujourd’hui le Seigneur, afin qu’il soit ton Dieu, afin que tu marches dans ses voies, et que tu gardes ses cérémonies, ses commandements et ses ordonnances, et que tu obéisses à son ordre;
18 Naye Bwana ametangaza leo kwamba ninyi ni taifa lake, hazina yake ya thamani kama alivyoahidi, ili kwamba mpate kuyashika maagizo yake yote.
Et le Seigneur t’a choisi aujourd’hui, afin que tu sois son peuple particulier, comme il t’a dit, et que tu gardes tous ses préceptes,
19 Ametangaza kwamba atawaweka juu kuliko mataifa mengine aliyoyafanya katika sifa, kuwa fahari na heshima, na kwamba mtakuwa taifa takatifu kwa Bwana Mungu wenu, kama alivyoahidi.
Et qu’il t’élève au-dessus de toutes les nations qu’il a créées pour sa louange, son nom et sa gloire; afin que tu sois le peuple saint du Seigneur ton Dieu, comme il a dit.