< Torati 26 >

1 Mtakapokuwa mmeingia nchi ile ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi na mtakapokuwa mmeimiliki na kukaa ndani yake,
And whanne thou hast entrid in to the lond which thi Lord God schal yyue to thee to welde, and thou hast gete it, and hast dwellid therynne,
2 chukueni baadhi ya mavuno ya kwanza ya yale yote mtakayozalisha kutoka udongo wa nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa na mweke kwenye kapu. Kisha uende mahali ambapo Bwana Mungu wako atapachagua kuwa makao kwa ajili ya Jina lake
thou schalt take the firste fruytis of alle thi fruytis, and thou schalt putte in a panyere; and thou schalt go to the place which thi Lord God chees, that his name be inwardly clepid there.
3 na umwambie kuhani atakayekuwepo kwa wakati huo, “Ninatangaza leo kwa Bwana Mungu wako kwamba nimekuja katika nchi ambayo Bwana aliwaapia baba zetu kwamba atatupa.”
And thou schalt go to the preest, that schal be in tho daies, and thou schalt seie to hym, Y knowleche to dai bifor thi Lord God, that Y entride in to the lond, for which he swoor to oure fadris, that he schulde yyue it to vs.
4 Kuhani atapokea lile kapu mikononi mwako na kuliweka chini mbele ya madhabahu ya Bwana Mungu wako.
And the preest schal take the panyere of thin hond, and schal sette bifor the auter of thi Lord God.
5 Kisha utatangaza mbele za Bwana Mungu wako: “Baba yangu alikuwa Mwaramu aliyekuwa anatangatanga, akaenda Misri pamoja na watu wachache, akaishi huko hadi akawa taifa kubwa, lenye nguvu na watu wengi.
And thou schalt speke in the siyt of thi Lord God, Sirus pursuede my fadir, `which fadir yede doun in to Egipt, and was a pilgrym there in feweste noumbre; and he encreesside in to a greet folk, and strong, and of multitude without noumbre.
6 Lakini Wamisri walituonea na kututaabisha, wakitufanyisha kazi ngumu.
And Egipcians turmentiden vs, and pursueden, and puttiden greuouseste birthuns.
7 Kisha tulimlilia Bwana, Mungu wa baba zetu, naye Bwana akasikia sauti yetu na akaona huzuni yetu, taabu yetu na mateso yetu.
And we crieden to the Lord God of oure fadris, which herde vs, and bihelde oure mekenesse, and trauel, and angwischis;
8 Kwa hiyo Bwana akatutoa nchi ya Misri kwa mkono wenye nguvu na ulionyooshwa, pamoja na utisho mkuu, ishara za miujiza na maajabu.
and he ledde vs out of Egipt in myyti hond, and arm holdun forth, in grete drede, in myraclis, and grete wondris,
9 Akatuleta mahali hapa akatupa nchi hii, nchi inayotiririka maziwa na asali;
and ledde vs in to this place; and yaf to vs a lond flowynge with mylk and hony.
10 nami sasa ninaleta malimbuko ya ardhi ambayo wewe, Ee Bwana, umenipa.” Weka kapu mbele za Bwana Mungu wako na usujudu mbele zake.
And therfor Y offre now to thee the fyrste fruytis of the fruitis of the lond which the Lord yaf to me. And thou schalt leeue tho in the siyt of thi Lord God. And whanne thi Lord God is worchipid,
11 Kisha wewe pamoja na Walawi na wageni wote walioko miongoni mwenu mtafurahi katika vitu vyote vizuri ambavyo Bwana Mungu wenu amewapa pamoja na wa nyumbani mwenu.
thou schalt ete in alle the goodis whiche thi Lord God yaf to thee and to thin hows, thou, and the dekene, and the comelyng which is with thee.
12 Wakati utakapokuwa umeshatoa zaka zote za mazao yako katika mwaka wa tatu, ambao ni mwaka wa zaka, utampa Mlawi, mgeni, yatima na mjane, ili waweze kula katika miji yenu na kushiba.
Whanne thou hast fillid the tithe of alle thi fruytis, in the thridde yeer of tithis, thou schalt yyue to the dekene, and to the comelyng, and to the fadirles, ether modirles child, and to widewe, that thei ete with ynne thi yatis, and be fillid.
13 Kisha umwambie Bwana Mungu wako: “Nimeondoa katika nyumba yangu ile sehemu iliyowekwa wakfu na nimempa Mlawi, mgeni, yatima na mjane, kulingana na yote uliyoamuru. Sijazihalifu amri zako wala kusahau hata mojawapo.
And thou schalt speke in the siyt of thi Lord God, Y haue take awai that that is halewid of myn hows, and Y yaf it to the dekene, and to the comelyng, to the fadirles, ethir modirles child, and to the widewe, as thou comaundidist to me; Y passide not thi comaundementis, Y foryat not thin heest.
14 Sijala sehemu iliyowekwa wakfu wakati nilipokuwa nikiomboleza, wala sijaondoa mojawapo wakati nilipokuwa najisi, wala sijatoa sehemu yake yoyote kwa wafu. Nimemtii Bwana Mungu wangu; nimefanya kila kitu ulichoniamuru.
Y ete not of tho thingis in my morenyng, nether Y departide tho in ony vnclennesse, nethir Y spendide of tho ony thing in biriyng of deed body, `that is, in makynge feestis therof in biryynge of deed men. Y obeiede to the vois of my Lord God, and Y dide alle thingis as thou comaundidist to me.
15 Angalia chini kutoka mbinguni, maskani yako matakatifu, uwabariki watu wako Israeli pamoja na nchi uliyotupa kama ulivyoahidi kwa kiapo kwa baba zetu, nchi inayotiririka maziwa na asali.”
Bihold thou fro thi seyntuarie, fro the hiy dwellyng place of heuene, and blesse thou thi puple Israel, and the lond which thou hast youe to vs, as thou `hast swoore to oure fadris; the lond flowynge with mylk and hony.
16 Bwana Mungu wako anakuagiza leo kufuata amri hizi na sheria; zishike kwa bidii kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote.
To dai thi Lord God comaundide to thee, that thou do these comaundementis and domes, that thou kepe and fille of al thin herte, and of al thi soule.
17 Umetangaza leo kwamba Bwana ndiye Mungu wako na kwamba utafuata njia zake, kwamba utayashika maagizo yake, amri zake na sheria zake nawe utamtii.
Thou hast chose the Lord to day, that he be God to thee, and thou go in hise weies, and thou kepe hise cerymonyes, and heestis, and domes, and obeie to his comaundement.
18 Naye Bwana ametangaza leo kwamba ninyi ni taifa lake, hazina yake ya thamani kama alivyoahidi, ili kwamba mpate kuyashika maagizo yake yote.
Lo! the Lord chees thee to day, that thou be a special puple to hym, as he spak to thee, and that thou kepe alle hise comaundementis;
19 Ametangaza kwamba atawaweka juu kuliko mataifa mengine aliyoyafanya katika sifa, kuwa fahari na heshima, na kwamba mtakuwa taifa takatifu kwa Bwana Mungu wenu, kama alivyoahidi.
and he schal make thee hiyere than alle folkis, whiche he made in to his preisyng, and name, and glorie; that thou be an holi puple of thi Lord God, as he spak to thee.

< Torati 26 >