< Torati 26 >

1 Mtakapokuwa mmeingia nchi ile ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi na mtakapokuwa mmeimiliki na kukaa ndani yake,
And it shall be, when thou hast come in to the land which the LORD thy God giveth thee [for] an inheritance, and possessest it, and dwellest therein;
2 chukueni baadhi ya mavuno ya kwanza ya yale yote mtakayozalisha kutoka udongo wa nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa na mweke kwenye kapu. Kisha uende mahali ambapo Bwana Mungu wako atapachagua kuwa makao kwa ajili ya Jina lake
That thou shalt take of the first of all the fruit of the earth, which thou shalt bring of thy land that the LORD thy God giveth thee, and shalt put [it] in a basket, and shalt go to the place which the LORD thy God shall choose to place his name there.
3 na umwambie kuhani atakayekuwepo kwa wakati huo, “Ninatangaza leo kwa Bwana Mungu wako kwamba nimekuja katika nchi ambayo Bwana aliwaapia baba zetu kwamba atatupa.”
And thou shalt go to the priest that shall be in those days, and say to him, I profess this day to the LORD thy God, that I have come to the country which the Lord swore to our fathers to give us.
4 Kuhani atapokea lile kapu mikononi mwako na kuliweka chini mbele ya madhabahu ya Bwana Mungu wako.
And the priest shall take the basket from thy hand, and set it down before the altar of the LORD thy God.
5 Kisha utatangaza mbele za Bwana Mungu wako: “Baba yangu alikuwa Mwaramu aliyekuwa anatangatanga, akaenda Misri pamoja na watu wachache, akaishi huko hadi akawa taifa kubwa, lenye nguvu na watu wengi.
And thou shalt speak and say before the LORD thy God, A Syrian ready to perish [was] my father, and he went down to Egypt, and sojourned there with a few, and became there a nation, great, mighty, and populous:
6 Lakini Wamisri walituonea na kututaabisha, wakitufanyisha kazi ngumu.
And the Egyptians ill-treated us, and afflicted us, and laid upon us hard bondage:
7 Kisha tulimlilia Bwana, Mungu wa baba zetu, naye Bwana akasikia sauti yetu na akaona huzuni yetu, taabu yetu na mateso yetu.
And when we cried to the LORD God of our fathers, the LORD heard our voice, and looked on our affliction, and our labor, and our oppression:
8 Kwa hiyo Bwana akatutoa nchi ya Misri kwa mkono wenye nguvu na ulionyooshwa, pamoja na utisho mkuu, ishara za miujiza na maajabu.
And the LORD brought us out of Egypt with a mighty hand, and with an out-stretched arm, and with great terribleness, and with signs, and with wonders;
9 Akatuleta mahali hapa akatupa nchi hii, nchi inayotiririka maziwa na asali;
And he hath brought us into this place, and hath given us this land, [even] a land that floweth with milk and honey.
10 nami sasa ninaleta malimbuko ya ardhi ambayo wewe, Ee Bwana, umenipa.” Weka kapu mbele za Bwana Mungu wako na usujudu mbele zake.
And now, behold, I have brought the first-fruits of the land, which thou, O LORD, hast given me: and thou shalt set it before the LORD thy God, and worship before the LORD thy God:
11 Kisha wewe pamoja na Walawi na wageni wote walioko miongoni mwenu mtafurahi katika vitu vyote vizuri ambavyo Bwana Mungu wenu amewapa pamoja na wa nyumbani mwenu.
And thou shalt rejoice in every good [thing] which the LORD thy God hath given to thee, and to thy house, thou, and the Levite, and the stranger that [is] among you.
12 Wakati utakapokuwa umeshatoa zaka zote za mazao yako katika mwaka wa tatu, ambao ni mwaka wa zaka, utampa Mlawi, mgeni, yatima na mjane, ili waweze kula katika miji yenu na kushiba.
When thou hast made an end of tithing all the tithes of thy increase the third year, [which is] the year of tithing, and hast given [it] to the Levite, the stranger, the fatherless, and the widow, that they may eat within thy gates, and be filled:
13 Kisha umwambie Bwana Mungu wako: “Nimeondoa katika nyumba yangu ile sehemu iliyowekwa wakfu na nimempa Mlawi, mgeni, yatima na mjane, kulingana na yote uliyoamuru. Sijazihalifu amri zako wala kusahau hata mojawapo.
Then thou shalt say before the LORD thy God, I have brought away the hallowed things out of [my] house, and also have given them to the Levite, and to the stranger, to the fatherless, and to the widow, according to all thy commandments which thou hast commanded me: I have not transgressed thy commandments, neither have I forgotten [them]:
14 Sijala sehemu iliyowekwa wakfu wakati nilipokuwa nikiomboleza, wala sijaondoa mojawapo wakati nilipokuwa najisi, wala sijatoa sehemu yake yoyote kwa wafu. Nimemtii Bwana Mungu wangu; nimefanya kila kitu ulichoniamuru.
I have not eaten of it in my mourning, neither have I taken away [aught] of it for [any] unclean [use], nor given [aught] of it for the dead: [but] I have hearkened to the voice of the LORD my God, [and] have done according to all that thou hast commanded me.
15 Angalia chini kutoka mbinguni, maskani yako matakatifu, uwabariki watu wako Israeli pamoja na nchi uliyotupa kama ulivyoahidi kwa kiapo kwa baba zetu, nchi inayotiririka maziwa na asali.”
Look down from thy holy habitation, from heaven, and bless thy people Israel, and the land which thou hast given us, as thou didst swear to our fathers, a land that floweth with milk and honey.
16 Bwana Mungu wako anakuagiza leo kufuata amri hizi na sheria; zishike kwa bidii kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote.
This day the LORD thy God hath commanded thee to perform these statutes and judgments: thou shalt therefore keep and do them with all thy heart, and with all thy soul.
17 Umetangaza leo kwamba Bwana ndiye Mungu wako na kwamba utafuata njia zake, kwamba utayashika maagizo yake, amri zake na sheria zake nawe utamtii.
Thou hast avouched the LORD this day to be thy God, and to walk in his ways, and to keep his statutes, and his commandments, and his judgments, and to hearken to his voice:
18 Naye Bwana ametangaza leo kwamba ninyi ni taifa lake, hazina yake ya thamani kama alivyoahidi, ili kwamba mpate kuyashika maagizo yake yote.
And the LORD hath avouched thee this day to be his peculiar people, as he hath promised thee, and that [thou] shouldst keep all his commandments;
19 Ametangaza kwamba atawaweka juu kuliko mataifa mengine aliyoyafanya katika sifa, kuwa fahari na heshima, na kwamba mtakuwa taifa takatifu kwa Bwana Mungu wenu, kama alivyoahidi.
And to make thee high above all nations which he hath made, in praise, and in name, and in honor; and that thou mayest be a holy people to the LORD thy God, as he hath spoken.

< Torati 26 >