< Torati 26 >

1 Mtakapokuwa mmeingia nchi ile ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi na mtakapokuwa mmeimiliki na kukaa ndani yake,
And it will be that you will go into the land which Yahweh God your [is] about to give to you an inheritance and you will take possession of it and you will dwell in it.
2 chukueni baadhi ya mavuno ya kwanza ya yale yote mtakayozalisha kutoka udongo wa nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa na mweke kwenye kapu. Kisha uende mahali ambapo Bwana Mungu wako atapachagua kuwa makao kwa ajili ya Jina lake
And you will take some of [the] first of - all [the] fruit of the ground which you will bring in from land your which Yahweh God your [is] about to give to you and you will put [it] in the basket and you will go to the place where he will choose Yahweh God your to cause to dwell name his there.
3 na umwambie kuhani atakayekuwepo kwa wakati huo, “Ninatangaza leo kwa Bwana Mungu wako kwamba nimekuja katika nchi ambayo Bwana aliwaapia baba zetu kwamba atatupa.”
And you will go to the priest who he will be in the days those and you will say to him I declare this day to Yahweh God your that I have come into the land which he swore Yahweh to ancestors our to give to us.
4 Kuhani atapokea lile kapu mikononi mwako na kuliweka chini mbele ya madhabahu ya Bwana Mungu wako.
And he will take the priest the basket from hand your and he will set down it before [the] altar of Yahweh God your.
5 Kisha utatangaza mbele za Bwana Mungu wako: “Baba yangu alikuwa Mwaramu aliyekuwa anatangatanga, akaenda Misri pamoja na watu wachache, akaishi huko hadi akawa taifa kubwa, lenye nguvu na watu wengi.
And you will answer and you will say before - Yahweh God your [was] an Aramean wandering ancestor my and he went down Egypt towards and he sojourned there men of fewness and he became there a nation great mighty and numerous.
6 Lakini Wamisri walituonea na kututaabisha, wakitufanyisha kazi ngumu.
And they did harm to us the Egyptians and they afflicted us and they put on us labor hard.
7 Kisha tulimlilia Bwana, Mungu wa baba zetu, naye Bwana akasikia sauti yetu na akaona huzuni yetu, taabu yetu na mateso yetu.
And we cried out to Yahweh [the] God of ancestors our and he heard Yahweh voice our and he saw affliction our and toil our and oppression our.
8 Kwa hiyo Bwana akatutoa nchi ya Misri kwa mkono wenye nguvu na ulionyooshwa, pamoja na utisho mkuu, ishara za miujiza na maajabu.
And he brought out us Yahweh from Egypt by a hand strong and by an arm outstretched and by terror great and by signs and by wonders.
9 Akatuleta mahali hapa akatupa nchi hii, nchi inayotiririka maziwa na asali;
And he brought us to the place this and he gave to us the land this a land flowing of milk and honey.
10 nami sasa ninaleta malimbuko ya ardhi ambayo wewe, Ee Bwana, umenipa.” Weka kapu mbele za Bwana Mungu wako na usujudu mbele zake.
And therefore here! I have brought [the] first of [the] fruit of the ground which you have given to me O Yahweh and you will set down it before Yahweh God your and you will bow down before Yahweh God your.
11 Kisha wewe pamoja na Walawi na wageni wote walioko miongoni mwenu mtafurahi katika vitu vyote vizuri ambavyo Bwana Mungu wenu amewapa pamoja na wa nyumbani mwenu.
And you will rejoice in all the good which he has given to you Yahweh God your and to household your you and the Levite and the sojourner who [is] in midst your.
12 Wakati utakapokuwa umeshatoa zaka zote za mazao yako katika mwaka wa tatu, ambao ni mwaka wa zaka, utampa Mlawi, mgeni, yatima na mjane, ili waweze kula katika miji yenu na kushiba.
If you will finish to tithe all [the] tithe of produce your in the year third [the] year of the tithe and you will give [it] to the Levite to the sojourner to the fatherless one and to the widow and they will eat in gates your and they will be satisfied.
13 Kisha umwambie Bwana Mungu wako: “Nimeondoa katika nyumba yangu ile sehemu iliyowekwa wakfu na nimempa Mlawi, mgeni, yatima na mjane, kulingana na yote uliyoamuru. Sijazihalifu amri zako wala kusahau hata mojawapo.
And you will say before Yahweh God your I have removed the holy thing from the house and also I have given it to the Levite and to the sojourner to the fatherless one and to the widow according to all commandment your which you have commanded me not I have transgressed any of commandments your and not I have forgotten [them].
14 Sijala sehemu iliyowekwa wakfu wakati nilipokuwa nikiomboleza, wala sijaondoa mojawapo wakati nilipokuwa najisi, wala sijatoa sehemu yake yoyote kwa wafu. Nimemtii Bwana Mungu wangu; nimefanya kila kitu ulichoniamuru.
Not I have eaten in mourning my any of it and not I have removed any of it unclean and not I have given any of it to [the] dead I have listened to [the] voice of Yahweh God my I have done according to all that you have commanded me.
15 Angalia chini kutoka mbinguni, maskani yako matakatifu, uwabariki watu wako Israeli pamoja na nchi uliyotupa kama ulivyoahidi kwa kiapo kwa baba zetu, nchi inayotiririka maziwa na asali.”
Look down! from [the] habitation of holiness your from the heavens and bless people your Israel and the land which you have given to us just as you swore to ancestors our a land flowing of milk and honey.
16 Bwana Mungu wako anakuagiza leo kufuata amri hizi na sheria; zishike kwa bidii kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote.
The day this Yahweh God your [is] commanding you to observe the statutes these and the judgments and you will take care and you will observe them with all heart your and with all being your.
17 Umetangaza leo kwamba Bwana ndiye Mungu wako na kwamba utafuata njia zake, kwamba utayashika maagizo yake, amri zake na sheria zake nawe utamtii.
Yahweh you have declared this day to become for you God and to walk in ways his and to keep statutes his and commandments his and judgments his and to listen to voice his.
18 Naye Bwana ametangaza leo kwamba ninyi ni taifa lake, hazina yake ya thamani kama alivyoahidi, ili kwamba mpate kuyashika maagizo yake yote.
And Yahweh he has declared you this day to become for him a people of possession just as he spoke to you and to keep all commandments his.
19 Ametangaza kwamba atawaweka juu kuliko mataifa mengine aliyoyafanya katika sifa, kuwa fahari na heshima, na kwamba mtakuwa taifa takatifu kwa Bwana Mungu wenu, kama alivyoahidi.
And to set you most high above all the nations which he has made for praise and for a name and for honor and to be you a people holy to Yahweh God your just as he spoke.

< Torati 26 >