< Torati 26 >
1 Mtakapokuwa mmeingia nchi ile ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi na mtakapokuwa mmeimiliki na kukaa ndani yake,
Now when you have come into the land which the Lord is giving you for your heritage, and you have made it yours and are living in it;
2 chukueni baadhi ya mavuno ya kwanza ya yale yote mtakayozalisha kutoka udongo wa nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa na mweke kwenye kapu. Kisha uende mahali ambapo Bwana Mungu wako atapachagua kuwa makao kwa ajili ya Jina lake
You are to take a part of the first-fruits of the earth, which you get from the land which the Lord your God is giving you, and put it in a basket, and go to the place marked out by the Lord your God, as the resting-place of his name.
3 na umwambie kuhani atakayekuwepo kwa wakati huo, “Ninatangaza leo kwa Bwana Mungu wako kwamba nimekuja katika nchi ambayo Bwana aliwaapia baba zetu kwamba atatupa.”
And you are to come to him who is priest at that time, and say to him, I give witness today before the Lord your God, that I have come into the land which the Lord made an oath to our fathers to give us.
4 Kuhani atapokea lile kapu mikononi mwako na kuliweka chini mbele ya madhabahu ya Bwana Mungu wako.
Then the priest will take the basket from your hand and put it down in front of the altar of the Lord your God.
5 Kisha utatangaza mbele za Bwana Mungu wako: “Baba yangu alikuwa Mwaramu aliyekuwa anatangatanga, akaenda Misri pamoja na watu wachache, akaishi huko hadi akawa taifa kubwa, lenye nguvu na watu wengi.
And these are the words which you will say before the Lord your God: My father was a wandering Aramaean, and he went down with a small number of people into Egypt; there he became a great and strong nation:
6 Lakini Wamisri walituonea na kututaabisha, wakitufanyisha kazi ngumu.
And the Egyptians were cruel to us, crushing us under a hard yoke:
7 Kisha tulimlilia Bwana, Mungu wa baba zetu, naye Bwana akasikia sauti yetu na akaona huzuni yetu, taabu yetu na mateso yetu.
And our cry went up to the Lord, the God of our fathers, and the Lord's ear was open to the voice of our cry, and his eyes took note of our grief and the crushing weight of our work:
8 Kwa hiyo Bwana akatutoa nchi ya Misri kwa mkono wenye nguvu na ulionyooshwa, pamoja na utisho mkuu, ishara za miujiza na maajabu.
And the Lord took us out of Egypt with a strong hand and a stretched-out arm, with works of power and signs and wonders:
9 Akatuleta mahali hapa akatupa nchi hii, nchi inayotiririka maziwa na asali;
And he has been our guide to this place, and has given us this land, a land flowing with milk and honey.
10 nami sasa ninaleta malimbuko ya ardhi ambayo wewe, Ee Bwana, umenipa.” Weka kapu mbele za Bwana Mungu wako na usujudu mbele zake.
So now, I have come here with the first of the fruits of the earth which you, O Lord, have given me. Then you will put it down before the Lord your God and give him worship:
11 Kisha wewe pamoja na Walawi na wageni wote walioko miongoni mwenu mtafurahi katika vitu vyote vizuri ambavyo Bwana Mungu wenu amewapa pamoja na wa nyumbani mwenu.
And you will have joy in every good thing which the Lord your God has given to you and to your family; and the Levite, and the man from a strange land who is with you, will take part in your joy.
12 Wakati utakapokuwa umeshatoa zaka zote za mazao yako katika mwaka wa tatu, ambao ni mwaka wa zaka, utampa Mlawi, mgeni, yatima na mjane, ili waweze kula katika miji yenu na kushiba.
When you have taken out a tenth from the tenth of all your produce in the third year, which is the year when this has to be done, give it to the Levite, and the man from a strange land, and the child without a father, and the widow, so that they may have food in your towns and be full;
13 Kisha umwambie Bwana Mungu wako: “Nimeondoa katika nyumba yangu ile sehemu iliyowekwa wakfu na nimempa Mlawi, mgeni, yatima na mjane, kulingana na yote uliyoamuru. Sijazihalifu amri zako wala kusahau hata mojawapo.
And say before the Lord your God, I have taken all the holy things out of my house and have given them to the Levite, and the man from a strange land, and him who has no father, and the widow, as you have given me orders: I have kept in mind all your orders, in nothing have I gone against them:
14 Sijala sehemu iliyowekwa wakfu wakati nilipokuwa nikiomboleza, wala sijaondoa mojawapo wakati nilipokuwa najisi, wala sijatoa sehemu yake yoyote kwa wafu. Nimemtii Bwana Mungu wangu; nimefanya kila kitu ulichoniamuru.
No part of these things has been used for food in a time of weeping, or put away when I was unclean, or given for the dead: I have given ear to the voice of the Lord my God, and have done all you have given me orders to do.
15 Angalia chini kutoka mbinguni, maskani yako matakatifu, uwabariki watu wako Israeli pamoja na nchi uliyotupa kama ulivyoahidi kwa kiapo kwa baba zetu, nchi inayotiririka maziwa na asali.”
So, looking down from your holy place in heaven, send your blessing on your people Israel and on the land which you have given us, as you said in your oath to our fathers, a land flowing with milk and honey.
16 Bwana Mungu wako anakuagiza leo kufuata amri hizi na sheria; zishike kwa bidii kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote.
Today the Lord your God gives you orders to keep all these laws and decisions: so then keep and do them with all your heart and all your soul.
17 Umetangaza leo kwamba Bwana ndiye Mungu wako na kwamba utafuata njia zake, kwamba utayashika maagizo yake, amri zake na sheria zake nawe utamtii.
Today you have given witness that the Lord is your God, and that you will go in his ways and keep his laws and his orders and his decisions and give ear to his voice:
18 Naye Bwana ametangaza leo kwamba ninyi ni taifa lake, hazina yake ya thamani kama alivyoahidi, ili kwamba mpate kuyashika maagizo yake yote.
And the Lord has made it clear this day that you are a special people to him, as he gave you his word; and that you are to keep all his orders;
19 Ametangaza kwamba atawaweka juu kuliko mataifa mengine aliyoyafanya katika sifa, kuwa fahari na heshima, na kwamba mtakuwa taifa takatifu kwa Bwana Mungu wenu, kama alivyoahidi.
And that he will make you high over all the nations he has made, in praise, in name, and in honour, and that you are to be a holy people to the Lord your God as he has said.