< Torati 25 >
1 Watu wanapokuwa na ugomvi, wapeleke mahakamani na waamuzi wataamua shauri hilo; watawaachia wasio na kosa na kuwahukumu wenye hatia.
When there ariseth a controversy between men, and they come nigh unto judgment, and judgment is granted them, then shall they justify the righteous man, and condemn the lawless.
2 Kama mtu mwenye hatia anastahili kuchapwa, mwamuzi atamwamuru alale chini ili achapwe mbele yake idadi ya viboko kulingana na kosa lake,
And it shall be—if the lawless man be, worthy of stripes, then shall the judge cause him to lie down and be beaten before him, according to the measure of his lawlessness, by number:
3 lakini kamwe asichapwe zaidi ya viboko arobaini. Ikiwa atachapwa zaidi ya viboko arobaini, nduguyo atadhalilika machoni pako.
forty stripes, may he give him not going beyond, —lest, if he do go beyond to smite him above these, with many stripes, then should thy brother be of no account in thine eyes.
4 Usimfunge maksai kinywa anapopura nafaka.
Thou shalt not muzzle an ox when he is treading out the corn.
5 Ikiwa ndugu wanaishi pamoja na mmoja wao akafa bila kuacha mwana, kamwe mjane wake asiolewe nje ya jamaa hiyo. Ndugu wa mumewe atamchukua, amwoe na kutimiza wajibu wa shemeji kwake.
When brethren dwell together, and one of them dieth, having, no son, the wife of the dead shall not marry outside to a stranger, —her husband’s brother, shall go in unto her, and take her unto him to wife and do for her as a husband’s brother.
6 Mwana wa kwanza atakayemzaa atapewa jina la ndugu aliyekufa ili jina lake lisifutike katika Israeli.
And it shall be, that, the firstborn which she beareth, shall succeed in the name of his brother who is dead, —so shall his name not be wiped out from Israel.
7 Hata hivyo, ikiwa ndugu huyo wa mume hataki kuoa huyo mke wa nduguye, mjane atawaendea wazee kwenye lango la mji na kusema, “Ndugu wa mume wangu anakataa kuendeleza jina la nduguye katika Israeli. Hataki kutimiza wajibu wa shemeji kwangu.”
But, if the man like not to take his sister-in-law, then shall his sister-in-law go up unto the gate, unto the elders, and say—My husband’s brother hath refused, to raise up unto his brother a name in Israel, he is not willing to do as a husband’s brother unto me.
8 Ndipo wazee wa mji wake watamwita na kuzungumza naye. Kama atashikilia kukataa akisema, “Sitaki kumwoa,”
Then shall the elders of his city call him and speak unto him, —and he shall stand and say, I like not to take her.
9 mjane wa nduguye atamwendea mbele ya wazee, atamvua kiatu kimoja na kumtemea mate usoni, na kusema, “Hivi ndivyo ambavyo hufanywa kwa mtu ambaye atakataa kuendeleza jamaa ya ndugu yake.”
Then shall his brother’s wife come near unto him in the presence of the elders, and draw his shoe from off his foot, and spit in his face, —and respond and say, Thus shall it be done unto the man who will not build up the house of his brother.
10 Jamaa ya mtu huyo itafahamika katika Israeli kama Jamaa ya Aliyevuliwa Kiatu.
And his name shall be called in Israel, —The house of him who had his shoe drawn off.
11 Ikiwa watu wawili wanapigana na mke wa mmoja wao akaja kumwokoa mumewe na yule anayemshambulia, naye mke huyo akifika na kumkamata sehemu za siri,
When men strive together one with another, and the wife of the one draweth near to deliver her husband out of the hand of him that smiteth him, —and she putteth forth her hand, and seizeth him by his parts of shame,
12 huyo mwanamke utamkata mkono wake. Usimhurumie.
then shalt thou cut off her hand, thine eye shall not pity.
13 Usiwe na mawe ya kupimia ya aina mbili katika mkoba wako, moja zito na jingine jepesi.
Thou shalt not have in thy bag divers weights, —a great and a small.
14 Usiwe na vipimo viwili tofauti katika nyumba yako, kimoja kikubwa, kingine kidogo.
Thou shalt not have in thy house divers measures, —a great and a small.
15 Ni lazima uwe na uzito na vipimo sahihi na vya haki, ili upate kuishi maisha marefu katika nchi anayokupa Bwana Mungu wako.
A weight full and just, shalt thou have, a measure full and just, shalt thou have, —that thy days may be prolonged upon the soil which Yahweh thy God is giving unto thee.
16 Kwa maana Bwana Mungu wako humchukia yeyote ambaye hufanya mambo kama haya, yeyote anayetenda kwa udanganyifu.
For an abomination unto Yahweh thy God, is every one that doeth these things, —every one that doeth unjustly.
17 Kumbuka kile Waamaleki walichowatendea mlipokuwa njiani mkitoka Misri.
Remember that which Amalek did unto thee by the way when ye came forth out of Egypt;
18 Wakati mlipokuwa mmechoka na kuishiwa nguvu kwa safari yenu, wakawapiga wale wote waliokuja nyuma. Waamaleki hawakumwogopa Mungu.
how he encountered thee by the way and cut off in thy rear all the worn-out behind thee, thou thyself, being weary and worn, —how he feared not God.
19 Bwana Mungu wako atakapokupa pumziko mbali na adui zako wote wanaokuzunguka katika nchi akupayo kuimiliki kuwa urithi, utafutilia mbali kumbukumbu lote la Waamaleki chini ya mbingu. Usisahau!
Therefore shall it be when Yahweh thy God hath given thee rest from all thine enemies round about in the land which Yahweh thy God is giving unto thee for an inheritance to possess it, then shalt thou wipe out the remembrance of Amalek from under the heavens, —thou shalt not forget.