< Torati 24 >

1 Ikiwa mtu atamwoa mke na akamchukia kwa sababu ya kukosa adabu, naye akamwandikia hati ya talaka, akampa na kumfukuza kutoka nyumbani kwake,
Si un homme a pris une femme, et qu’il l’ait eue, et qu’elle n’ait pas trouvé grâce à ses yeux à cause de quelque défaut honteux, il écrira un acte de répudiation; il le mettra dans la main de cette femme, et il la renverra de sa maison.
2 ikiwa baada ya kuondoka nyumbani kwake atakuwa mke wa mtu mwingine,
Et lorsque, sortie, elle aura épousé un autre mari,
3 ikiwa mume wake wa pili atachukizwa naye akamwandikia hati ya talaka, akampa na kumfukuza kutoka nyumbani kwake, au kama akifa,
Et que celui-ci aussi conçoive de l’aversion pour elle, lui donne un acte de répudiation, et la renvoie de sa maison, ou bien meure,
4 basi yule mume wake wa kwanza, ambaye alimpa talaka, haruhusiwi kumwoa tena baada ya mwanamke huyo kuwa najisi. Hayo yatakuwa machukizo machoni pa Bwana. Usilete dhambi juu ya nchi ambayo Bwana Mungu wako anakupa kama urithi.
Le premier mari ne pourra pas la reprendre pour femme, parce quelle a été souillée, et qu’elle est devenue abominable devant le Seigneur: ne fais pas pécher la terre que le Seigneur ton Dieu t’a livrée pour la posséder.
5 Kama mtu ameoa karibuni, kamwe asipelekwe vitani au kupewa wajibu mwingine wowote. Kwa mwaka mmoja atakuwa huru kubaki nyumbani ili amfurahishe mke aliyemwoa.
Lorsqu’un homme aura pris une femme depuis peu, il n’ira point à la guerre, et aucune charge publique ne lui sera imposée, mais il s’occupera sans aucune faute dans sa maison, à se réjouir pendant une année avec sa femme.
6 Usitoe jozi ya mawe ya kusagia, hata ikiwa lile la juu, kuweka rehani kwa ajili ya deni, kwa sababu itakuwa ni kuweka uhai wa mtu kama dhamana.
Tu ne recevras point pour gage la meule de dessous et de dessus; parce que c’est l’âme de celui qui te l’offre.
7 Kama mtu akikamatwa akiiba yeyote miongoni mwa ndugu zake wa Waisraeli na kumtenda kama mtumwa au akimuuza, mwizi huyo ni lazima auawe. Nawe utaondoa uovu kutoka miongoni mwenu.
Si un homme est surpris embauchant son frère d’entre les enfants d’Israël, et que, celui-ci vendu, il ait reçu le prix, il sera mis à mort, et tu ôteras le mal d’au milieu de toi.
8 Pakitokea magonjwa ya ngozi ya kuambukiza, mwe waangalifu sana kufanya sawasawa na maagizo ya makuhani, ambao ni Walawi. Ni lazima mfuate kwa uangalifu yale niliyowaamuru.
Evite soigneusement de contracter la plaie de la lèpre; mais tu feras tout ce que t’enseigneront les prêtres de la race lévitique, selon que je leur ai prescrit, et accomplis-le exactement.
9 Kumbukeni kile Bwana Mungu wenu alichomfanyia Miriamu njiani baada ya ninyi kutoka Misri.
Souvenez-vous de ce qu’a fait le Seigneur votre Dieu à Marie dans le chemin, lorsque vous sortiez de l’Egypte.
10 Unapomkopesha jirani yako chochote, usiingie nyumbani kwake kutwaa kile anachokitoa kama rehani.
Lorsque tu redemanderas à ton prochain quelque chose, qu’il te doit, tu n’entreras point dans sa maison, pour emporter un gage,
11 Ukae nje na umwache huyo mtu uliyemkopesha akuletee hiyo rehani.
Mais tu te tiendras dehors, et c’est lui qui t’apportera ce qu’il aura.
12 Ikiwa mtu huyo ni maskini, usiende kulala ukiwa na hiyo rehani yake katika milki yako.
Que s’il est pauvre, le gage ne passera pas la nuit chez toi;
13 Rudisha vazi lake kabla ya machweo ya jua ili apate kulilalia. Kisha atakushukuru na kitaonekana kama kitendo cha haki mbele za Bwana Mungu wako.
Mais tu le lui rendras aussitôt avant le coucher du soleil, afin que dormant dans son vêtement, il te bénisse, et que tu aies pour toi la justice devant le Seigneur ton Dieu.
14 Usimwonee mtu maskini na mhitaji ambaye umemwajiri, akiwa ni nduguyo Mwisraeli au mgeni anayeishi katika mojawapo ya miji yenu.
Tu ne nieras point le salaire de l’indigent et du pauvre, qu’il soit ton frère, ou un étranger qui demeure avec toi dans ta terre et au dedans de tes portes;
15 Mlipe ujira wake kila siku kabla ya jua kutua, kwa sababu yeye ni maskini na anautegemea ujira huo. La sivyo, anaweza kumlilia Bwana dhidi yako, nawe ukapata hatia ya dhambi.
Mais tu lui rendras le jour même le prix de son travail avant le coucher du soleil, parce qu’il est pauvre, et que c’est par là qu’il sustente son âme, afin qu’il ne crie pas contre toi au Seigneur, et qu’il ne te soit pas imputé à péché.
16 Baba wasiuawe kwa ajili ya watoto wao, wala watoto wasiuawe kwa ajili ya baba zao; kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe.
Des pères ne seront pas mis à mort pour des enfants, ni des enfants pour des pères; mais chacun mourra pour son péché.
17 Usipotoshe hukumu ya mgeni au yatima, au kuchukua vazi la mjane kama rehani.
Tu ne pervertiras point le jugement d’un étranger et d’un orphelin; et tu n’ôteras point, pour gage, à la veuve son vêtement.
18 Kumbukeni kwamba mlikuwa watumwa huko Misri, naye Bwana Mungu wenu akawakomboa kutoka huko. Hii ndiyo sababu ninawaamuru kutenda hili.
Souviens-toi que tu as servi en Egypte, et que le Seigneur ton Dieu t’a retiré de là. C’est pourquoi voici ce que je t’ordonne de faire:
19 Unapovuna shamba lako na ukasahau mganda, usirudi kuuchukua. Acha kwa ajili ya mgeni, yatima na mjane, ili Bwana Mungu wako aweze kukubariki wewe katika kazi zote za mikono yako.
Quand tu moissonneras les grains dans ton champ, et que par oubli tu auras laissé une gerbe, tu ne retourneras point pour la prendre; mais tu la laisseras emporter par l’étranger, l’orphelin et la veuve, afin que le Seigneur ton Dieu te bénisse dans toutes les œuvres de tes mains.
20 Unapovuna zeituni kutoka miti yako, usirudie matawi mara ya pili. Acha kilichobaki kwa ajili ya mgeni, yatima na mjane.
Si tu recueilles les fruits des oliviers, tu ne retourneras point pour recueillir tout ce qui sera resté sur les arbres; mais tu le laisseras à l’étranger, à l’orphelin et à la veuve.
21 Unapochuma zabibu katika shamba lako la mizabibu usirudie tena. Acha zinazobaki kwa ajili ya mgeni, yatima na mjane.
Si tu vendanges ta vigne, tu ne recueilleras point les grappes de raisins restantes; mais qu’elles soient laissées pour l’usage de l’étranger, de l’orphelin et de la veuve.
22 Kumbuka kwamba mlikuwa watumwa katika nchi ya Misri. Ndiyo sababu ninawaamuru kufanya hili.
Souviens-toi que toi aussi, tu as servi en Egypte, et c’est pour cela que je t’ordonne de faire ces choses.

< Torati 24 >