< Torati 24 >
1 Ikiwa mtu atamwoa mke na akamchukia kwa sababu ya kukosa adabu, naye akamwandikia hati ya talaka, akampa na kumfukuza kutoka nyumbani kwake,
Un homme prend une femme et devient son mari, mais il arrive qu'elle n'entre pas en grâce auprès de lui, parce qu'il a découvert en elle quelque chose de repoussant, il écrit pour elle une lettre de divorce, la lui remet en main et la renvoie de sa maison;
2 ikiwa baada ya kuondoka nyumbani kwake atakuwa mke wa mtu mwingine,
elle quitte sa maison et part; puis elle devient la femme d'un autre mari;
3 ikiwa mume wake wa pili atachukizwa naye akamwandikia hati ya talaka, akampa na kumfukuza kutoka nyumbani kwake, au kama akifa,
ce dernier mari la prend en haine, et écrit pour elle une lettre de divorce, et la lui remet en main et la renvoie de sa maison; ou bien l'homme qui l'avait épousée en dernier lieu, vient à mourir;
4 basi yule mume wake wa kwanza, ambaye alimpa talaka, haruhusiwi kumwoa tena baada ya mwanamke huyo kuwa najisi. Hayo yatakuwa machukizo machoni pa Bwana. Usilete dhambi juu ya nchi ambayo Bwana Mungu wako anakupa kama urithi.
dans ce cas le premier mari qui l'a répudiée, ne pourra la reprendre pour femme après qu'elle se sera souillée, car c'est l'abomination de l'Éternel, et tu ne dois pas entacher de péché le pays que l'Éternel, ton Dieu, te donne en propriété.
5 Kama mtu ameoa karibuni, kamwe asipelekwe vitani au kupewa wajibu mwingine wowote. Kwa mwaka mmoja atakuwa huru kubaki nyumbani ili amfurahishe mke aliyemwoa.
Un nouveau marié ne fera point la campagne avec l'armée; on ne lui imposera aucune charge quelconque; il sera exempté pendant un an pour sa maison, afin qu'il puisse réjouir la femme qu'il a épousée.
6 Usitoe jozi ya mawe ya kusagia, hata ikiwa lile la juu, kuweka rehani kwa ajili ya deni, kwa sababu itakuwa ni kuweka uhai wa mtu kama dhamana.
L'on ne se nantira pas du moulin et de la meule; car ce serait se nantir de la vie même.
7 Kama mtu akikamatwa akiiba yeyote miongoni mwa ndugu zake wa Waisraeli na kumtenda kama mtumwa au akimuuza, mwizi huyo ni lazima auawe. Nawe utaondoa uovu kutoka miongoni mwenu.
Si quelqu'un est surpris volant un homme, l'un de ses frères, l'un des enfants d'Israël, et l'employant comme esclave et le vendant, ce voleur-là mourra. Ote ainsi le mal du milieu de toi.
8 Pakitokea magonjwa ya ngozi ya kuambukiza, mwe waangalifu sana kufanya sawasawa na maagizo ya makuhani, ambao ni Walawi. Ni lazima mfuate kwa uangalifu yale niliyowaamuru.
Prends garde à l'affection de la lèpre, afin d'être bien attentif à faire tout ce que vous enjoindront les Prêtres, les Lévites. Ayez soin de vous conformer à ce que je leur ai prescrit.
9 Kumbukeni kile Bwana Mungu wenu alichomfanyia Miriamu njiani baada ya ninyi kutoka Misri.
Rappelle-toi ce que l'Éternel, ton Dieu, a fait à Marie, pendant la route lors de votre sortie de l'Egypte.
10 Unapomkopesha jirani yako chochote, usiingie nyumbani kwake kutwaa kile anachokitoa kama rehani.
Lorsque tu feras à ton frère un prêt quelconque, tu n'entreras point dans sa maison, pour t'y saisir d'un gage;
11 Ukae nje na umwache huyo mtu uliyemkopesha akuletee hiyo rehani.
tu resteras dehors, et celui à qui tu fais le prêt, t'apportera le gage dehors.
12 Ikiwa mtu huyo ni maskini, usiende kulala ukiwa na hiyo rehani yake katika milki yako.
Et si c'est un homme pauvre, tu ne te coucheras pas ayant encore son gage.
13 Rudisha vazi lake kabla ya machweo ya jua ili apate kulilalia. Kisha atakushukuru na kitaonekana kama kitendo cha haki mbele za Bwana Mungu wako.
Tu lui rendras le gage au coucher du soleil, afin qu'il ait son manteau pour se coucher, et qu'il te bénisse; et cela te sera compté comme justice devant l'Éternel, ton Dieu.
14 Usimwonee mtu maskini na mhitaji ambaye umemwajiri, akiwa ni nduguyo Mwisraeli au mgeni anayeishi katika mojawapo ya miji yenu.
Ne frustre pas le mercenaire pauvre et indigent, d'entre tes frères ou les étrangers qui seront dans ton pays, dans tes Portes.
15 Mlipe ujira wake kila siku kabla ya jua kutua, kwa sababu yeye ni maskini na anautegemea ujira huo. La sivyo, anaweza kumlilia Bwana dhidi yako, nawe ukapata hatia ya dhambi.
Donne-lui son salaire à son jour, et que le soleil ne se couche pas sans qu'il l'ait; car il est pauvre, et c'est le souhait de son âme, de peur qu'il ne réclame contre toi auprès de l'Éternel, et que tu ne te charges d'un péché.
16 Baba wasiuawe kwa ajili ya watoto wao, wala watoto wasiuawe kwa ajili ya baba zao; kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe.
Les pères ne seront pas mis à mort pour les fils, ni les fils pour les pères: chacun sera mis à mort pour son propre péché.
17 Usipotoshe hukumu ya mgeni au yatima, au kuchukua vazi la mjane kama rehani.
Ne fais pas céder le droit de l'étranger, ni de l'orphelin, et ne prends pas en gage la robe de la veuve,
18 Kumbukeni kwamba mlikuwa watumwa huko Misri, naye Bwana Mungu wenu akawakomboa kutoka huko. Hii ndiyo sababu ninawaamuru kutenda hili.
te souvenant que tu as été esclave en Egypte, et que l'Éternel, ton Dieu, t'en a racheté; c'est pourquoi je t'enjoins d'accomplir ce précepte.
19 Unapovuna shamba lako na ukasahau mganda, usirudi kuuchukua. Acha kwa ajili ya mgeni, yatima na mjane, ili Bwana Mungu wako aweze kukubariki wewe katika kazi zote za mikono yako.
Lorsque tu moissonneras tes blés dans ton champ, si tu oublies une gerbe au champ, ne reviens pas la prendre; qu'elle soit pour étranger, l'orphelin et la veuve, afin que l'Éternel, ton Dieu, te bénisse dans tout le travail de tes mains.
20 Unapovuna zeituni kutoka miti yako, usirudie matawi mara ya pili. Acha kilichobaki kwa ajili ya mgeni, yatima na mjane.
Lorsque tu secoueras tes oliviers, ne fais pas après toi fouiller dans les rameaux; que ce soit pour l'étranger, l'orphelin et la veuve.
21 Unapochuma zabibu katika shamba lako la mizabibu usirudie tena. Acha zinazobaki kwa ajili ya mgeni, yatima na mjane.
Lorsque tu vendangeras ta vigne, tu ne grappilleras pas derrière toi; que ce soit pour l'étranger, l'orphelin et la veuve:
22 Kumbuka kwamba mlikuwa watumwa katika nchi ya Misri. Ndiyo sababu ninawaamuru kufanya hili.
souviens-toi que tu as été esclave dans le pays d'Egypte; c'est pourquoi je t'enjoins d'accomplir ce précepte.