< Torati 24 >

1 Ikiwa mtu atamwoa mke na akamchukia kwa sababu ya kukosa adabu, naye akamwandikia hati ya talaka, akampa na kumfukuza kutoka nyumbani kwake,
When a man takes a wife, and marries her, then it shall be, if she finds no favor in his eyes, because he has found some unseemly thing in her, that he shall write her a bill of divorcement, and give it in her hand, and send her out of his house.
2 ikiwa baada ya kuondoka nyumbani kwake atakuwa mke wa mtu mwingine,
And when she has departed out of his house, she may go and be another man's.
3 ikiwa mume wake wa pili atachukizwa naye akamwandikia hati ya talaka, akampa na kumfukuza kutoka nyumbani kwake, au kama akifa,
And if the latter husband dislikes her, and writes her a bill of divorcement, and gives it in her hand, and sends her out of his house, or if the latter husband dies, who took her to be his wife,
4 basi yule mume wake wa kwanza, ambaye alimpa talaka, haruhusiwi kumwoa tena baada ya mwanamke huyo kuwa najisi. Hayo yatakuwa machukizo machoni pa Bwana. Usilete dhambi juu ya nchi ambayo Bwana Mungu wako anakupa kama urithi.
her former husband, who sent her away, may not take her again to be his wife after she is defiled. For that is abomination before Jehovah, and thou shall not cause the land to sin, which Jehovah thy God gives thee for an inheritance.
5 Kama mtu ameoa karibuni, kamwe asipelekwe vitani au kupewa wajibu mwingine wowote. Kwa mwaka mmoja atakuwa huru kubaki nyumbani ili amfurahishe mke aliyemwoa.
When a man takes a new wife, he shall not go out in the army, neither shall he be charged with any business. He shall be free at home one year, and shall cheer his wife whom he has taken.
6 Usitoe jozi ya mawe ya kusagia, hata ikiwa lile la juu, kuweka rehani kwa ajili ya deni, kwa sababu itakuwa ni kuweka uhai wa mtu kama dhamana.
No man shall take the mill or the upper millstone to pledge, for he takes life to pledge.
7 Kama mtu akikamatwa akiiba yeyote miongoni mwa ndugu zake wa Waisraeli na kumtenda kama mtumwa au akimuuza, mwizi huyo ni lazima auawe. Nawe utaondoa uovu kutoka miongoni mwenu.
If a man is found stealing any of his brothers of the sons of Israel, and he deals with him harshly, or sells him, then that thief shall die. So shall thou put away the evil from the midst of thee.
8 Pakitokea magonjwa ya ngozi ya kuambukiza, mwe waangalifu sana kufanya sawasawa na maagizo ya makuhani, ambao ni Walawi. Ni lazima mfuate kwa uangalifu yale niliyowaamuru.
Take heed in the disease of leprosy, that thou observe diligently, and do according to all that the priests the Levites shall teach you. As I commanded them, so ye shall observe to do.
9 Kumbukeni kile Bwana Mungu wenu alichomfanyia Miriamu njiani baada ya ninyi kutoka Misri.
Remember what Jehovah thy God did to Miriam by the way as ye came forth out of Egypt.
10 Unapomkopesha jirani yako chochote, usiingie nyumbani kwake kutwaa kile anachokitoa kama rehani.
When thou do lend thy neighbor any manner of loan, thou shall not go into his house to fetch his pledge.
11 Ukae nje na umwache huyo mtu uliyemkopesha akuletee hiyo rehani.
Thou shall stand outside, and the man to whom thou lend shall bring forth the pledge outside to thee.
12 Ikiwa mtu huyo ni maskini, usiende kulala ukiwa na hiyo rehani yake katika milki yako.
And if he is a poor man, thou shall not sleep with his pledge.
13 Rudisha vazi lake kabla ya machweo ya jua ili apate kulilalia. Kisha atakushukuru na kitaonekana kama kitendo cha haki mbele za Bwana Mungu wako.
Thou shall surely restore to him the pledge when the sun goes down, that he may sleep in his garment, and bless thee. And it shall be righteousness to thee before Jehovah thy God.
14 Usimwonee mtu maskini na mhitaji ambaye umemwajiri, akiwa ni nduguyo Mwisraeli au mgeni anayeishi katika mojawapo ya miji yenu.
Thou shall not oppress a hired servant who is poor and needy, whether he be of thy brothers, or of thy sojourners that are in thy land within thy gates.
15 Mlipe ujira wake kila siku kabla ya jua kutua, kwa sababu yeye ni maskini na anautegemea ujira huo. La sivyo, anaweza kumlilia Bwana dhidi yako, nawe ukapata hatia ya dhambi.
Thou shall give him his hire in his day, neither shall the sun go down upon it, for he is poor, and sets his heart upon it, lest he cry against thee to Jehovah, and it be sin to thee.
16 Baba wasiuawe kwa ajili ya watoto wao, wala watoto wasiuawe kwa ajili ya baba zao; kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe.
The fathers shall not be put to death for the sons, neither shall the sons be put to death for the fathers. Every man shall be put to death for his own sin.
17 Usipotoshe hukumu ya mgeni au yatima, au kuchukua vazi la mjane kama rehani.
Thou shall not distort the justice due to the sojourner, or to the fatherless, nor take the widow's raiment to pledge,
18 Kumbukeni kwamba mlikuwa watumwa huko Misri, naye Bwana Mungu wenu akawakomboa kutoka huko. Hii ndiyo sababu ninawaamuru kutenda hili.
but thou shall remember that thou were a bondman in Egypt, and Jehovah thy God redeemed thee from there. Therefore I command thee to do this thing.
19 Unapovuna shamba lako na ukasahau mganda, usirudi kuuchukua. Acha kwa ajili ya mgeni, yatima na mjane, ili Bwana Mungu wako aweze kukubariki wewe katika kazi zote za mikono yako.
When thou reap thy harvest in thy field, and have forgotten a sheaf in the field, thou shall not go again to fetch it. It shall be for the sojourner, for the fatherless, and for the widow, that Jehovah thy God may bless thee in all the work of thy hands.
20 Unapovuna zeituni kutoka miti yako, usirudie matawi mara ya pili. Acha kilichobaki kwa ajili ya mgeni, yatima na mjane.
When thou beat thine olive tree, thou shall not go over the boughs again. It shall be for the sojourner, for the fatherless, and for the widow.
21 Unapochuma zabibu katika shamba lako la mizabibu usirudie tena. Acha zinazobaki kwa ajili ya mgeni, yatima na mjane.
When thou gather of thy vineyard, thou shall not glean it behind thee. It shall be for the sojourner, for the fatherless, and for the widow.
22 Kumbuka kwamba mlikuwa watumwa katika nchi ya Misri. Ndiyo sababu ninawaamuru kufanya hili.
And thou shall remember that thou were a bondman in the land of Egypt. Therefore I command thee to do this thing.

< Torati 24 >