< Torati 23 >
1 Asiingie mtu yeyote aliyehasiwa kwa kupondwa makende au kwa kukatwa uume wake katika kusanyiko la Bwana.
L'homme qu'on a fait eunuque ou qui l'est devenu par mutilation, n'entrera pas dans l'Eglise du Seigneur.
2 Mtu yeyote ambaye amezaliwa kwenye ndoa isiyo halali au wazao wake wasiingie kwenye kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.
Le fils de prostituée n'entrera pas dans l'Eglise du Seigneur.
3 Hapatakuwa na Mwamoni au Mmoabu au yeyote wa wazao wao atakayeruhusiwa kuingia katika kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.
L'Ammonite, le Moabite n'entreront pas dans l'Eglise du Seigneur jusqu'à la dernière génération; qu'ils n'y entrent point, qu'ils n'y entrent jamais;
4 Kwa kuwa hawakuja kuwalaki wakiwa na mkate na maji mlipokuwa njiani mlipotoka Misri, tena walimwajiri Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori iliyoko Aramu-Naharaimu ili kuwalaani ninyi.
Car ils ne sont point venus à votre rencontre avec des vivres et de l'eau lorsque vous arriviez d'Egypte, et ils avaient convoqué a prix d'argent, de la Mésopotamie, Balaam, fils de Béor, afin qu'il vous maudît.
5 Hata hivyo, Bwana Mungu wenu hakumsikiliza Balaamu bali aligeuza laana kuwa baraka kwenu kwa sababu Bwana Mungu wenu anawapenda.
Et le Seigneur ton Dieu ne fit pas à la volonté de Balaam, et le Seigneur ton Dieu changea en bénédictions les malédictions, parce que le Seigneur ton Dieu t'aime.
6 Msitafute mapatano ya urafiki nao maisha yenu yote.
Tu ne leur diras jamais de paroles pacifiques ou conciliantes, tant que tu existeras.
7 Usimchukie Mwedomu, kwa kuwa yeye ni ndugu yako. Usimchukie Mmisri, kwa sababu uliishi kama mgeni katika nchi yake.
Tu n'auras point en abomination l'Iduméen, car il est ton frère; ni l'Egyptien, car tu as été passager en sa contrée.
8 Kizazi cha tatu cha watoto watakaozaliwa nao wanaweza kuingia katika kusanyiko la Bwana.
Leurs fils, s'il s'en établit parmi vous, entreront à la troisième génération dans l'Eglise du Seigneur.
9 Unapokuwa umepiga kambi dhidi ya adui zako, jitenge na kitu chochote kisicho safi.
Garde-toi de toute action mauvaise, lorsque tu iras en guerre contre les ennemis.
10 Ikiwa mtu amechafuka kwa sababu ya kutokwa na shahawa usiku, inampasa atoke nje ya kambi na kukaa huko.
S'il se trouve parmi vous un homme qu'une pollution de nuit aura rendu impur, il sortira du camp sans y rentrer.
11 Lakini jioni ikikaribia ataoga, na baada ya jua kuzama ataingia tena kambini.
Et, sur le soir, il lavera son corps avec de l'eau, et après le soleil couche il rentrera au camp.
12 Tengeni mahali nje ya kambi ambapo mnaweza kwenda kujisaidia.
Il y aura un lieu indiqué hors du camp, où l'on ira lorsque l'on aura besoin hors du camp.
13 Kama sehemu ya vifaa vyenu kuweni na kitu cha kulimia, nanyi mnapojisaidia, chimba shimo na kisha funika kile kikutokacho.
Tu auras un piquet passé dans la ceinture, et, lorsque tu te seras accroupi hors du camp, tu creuseras avec ce piquet, puis, ramenant la terre, tu cacheras ton impureté.
14 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu hutembea katika kambi yenu ili kuwalinda na kuwaweka adui zenu mikononi mwenu. Kambi yenu ni lazima iwe takatifu, ili asione kitu chochote miongoni mwenu kilicho kichafu akageuka na kuwaacha.
Car le Seigneur ton Dieu viendra dans le camp pour te favoriser et te livrer ton ennemi; ton camp sera donc saint; qu'il n'y paraisse pas de souillure, qu'on la rejette au loin.
15 Ikiwa mtumwa amekimbilia kwako, usimrudishe kwa bwana wake.
Tu ne livreras pas, à son maître étranger, l'esclave qui s'échappant se sera attaché à toi.
16 Mwache aishi miongoni mwenu mahali popote anapopapenda na katika mji wowote anaochagua. Usimwonee.
Il demeurera avec toi, et il demeurera parmi vous, où il lui sera agréable; garde-toi de l'opprimer.
17 Asiwepo Mwisraeli mwanamke kahaba au mwanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
Il n'y aura pas de fille d'Israël qui se prostitue; ni de fils d'Israël qui fréquente des prostituées. Il n'y aura point d'initiée parmi les jeunes filles, ni d'initié parmi les fils d'Israël;
18 Kamwe usilete mapato ya ukahaba ikiwa ni ya mwanamke au ni ya mwanaume katika nyumba ya Bwana Mungu wako kwa ajili ya nadhiri yoyote, kwa sababu Bwana Mungu wako anachukizwa na yote mawili.
N'offre pas dans la maison du Seigneur le salaire de la prostituée ni le prix d'un chien; l'un et l'autre sont en abomination au Seigneur.
19 Usimtoze ndugu yako riba, iwe ni fedha ama chakula ama kitu kingine chochote ambacho waweza kupata riba juu yake.
Tu ne prendras à ton frère aucun intérêt, ni pour de l'argent, ni pour des vivres, ni pour quoi que ce soit que tu lui aurais prêté.
20 Unaweza kumtoza mgeni riba, lakini siyo nduguyo Mwisraeli, ili kwamba Bwana Mungu wako akubariki katika kila kitu unachoweka mkono katika nchi unayoingia kuimiliki.
Tu prêteras à intérêt aux étrangers, mais non à ton frère, afin que le Seigneur ton Dieu te bénisse en tous tes travaux, sur la terre où tu entres pour qu'elle soit ton héritage.
21 Ukiweka nadhiri kwa Bwana Mungu wako, usichelewe kuitimiza, kwa kuwa Bwana Mungu wako atakudai, nawe utakuwa na hatia ya dhambi.
Si tu as fait un vœu au Seigneur, tu ne mettras pas de retard à l'accomplir, car le Seigneur ton Dieu le réclamerait de toi, et il te serait imputé à péché.
22 Lakini ukijizuia kuweka nadhiri, hutakuwa na hatia.
Mais si tu n'avais pas entendu faire de vœu, il n'y aurait pas en toi de péché.
23 Chochote kitakachotamkwa kwa midomo yako ni lazima uhakikishe umekifanya, kwa sababu uliweka nadhiri yako kwa hiari mbele za Bwana Mungu wako kwa kinywa chako mwenyewe.
Tout ce qui sera sorti de tes lèvres, tu l'observeras; tu feras au Seigneur ton Dieu le prescrit qu'aura promis ta bouche, comme tu l'auras voué.
24 Kama ukiingia katika shamba la mizabibu la jirani yako, unaweza kula zabibu kadiri utakavyo, lakini usiweke chochote kwenye kikapu chako.
Si tu entres dans la moisson de ton prochain, il t'est permis de cueillir à la main un épi, mais ne va pas mettre la faux dans la moisson de ton prochain.
25 Kama ukiingia katika shamba la nafaka la jirani yako, unaweza kukwanyua kwa mikono yako, lakini usikate kwa mundu nafaka iliyosimama.
Si tu entres dans la vigne de ton prochain, il t'est permis de manger une grappe assez grosse pour que ton âme en soit rassasiée, mais ne va pas mettre du raisin dans un panier.