< Torati 23 >

1 Asiingie mtu yeyote aliyehasiwa kwa kupondwa makende au kwa kukatwa uume wake katika kusanyiko la Bwana.
A geldyng whanne hise stoonys ben brokun, ethir kit awey, and his yerde is kit awei, schal not entre in to the chirche of the Lord.
2 Mtu yeyote ambaye amezaliwa kwenye ndoa isiyo halali au wazao wake wasiingie kwenye kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.
A child borun of hordom schal not entre in to the chirche of the Lord, `til to the tenthe generacioun.
3 Hapatakuwa na Mwamoni au Mmoabu au yeyote wa wazao wao atakayeruhusiwa kuingia katika kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.
Ammonytis and Moabitis, yhe aftir the tenthe generacioun, schulen not entre into the `chirche of the Lord with outen ende;
4 Kwa kuwa hawakuja kuwalaki wakiwa na mkate na maji mlipokuwa njiani mlipotoka Misri, tena walimwajiri Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori iliyoko Aramu-Naharaimu ili kuwalaani ninyi.
for thei nolden come to you with breed and watir in the weie, whanne ye yeden out of Egipt; and for thei hireden ayens thee Balaam, the sone of Beor, fro Mesopotanye of Sirye, that he schulde curse thee;
5 Hata hivyo, Bwana Mungu wenu hakumsikiliza Balaamu bali aligeuza laana kuwa baraka kwenu kwa sababu Bwana Mungu wenu anawapenda.
and thi Lord God nolde here Balaam, and God turnede `the cursyng of Balaam in to thi blessyng, for he louyde thee.
6 Msitafute mapatano ya urafiki nao maisha yenu yote.
Thou schalt not make pees with hem, nethir thou schalt seke goodis to hem, in alle the daies of thi lijf in to with outen ende.
7 Usimchukie Mwedomu, kwa kuwa yeye ni ndugu yako. Usimchukie Mmisri, kwa sababu uliishi kama mgeni katika nchi yake.
Thou schalt not `haue abhomynacioun of a man of Ydumye, for he is thi brothir, nethir of a man of Egipt, for thou were a comelyng in the lond of hym.
8 Kizazi cha tatu cha watoto watakaozaliwa nao wanaweza kuingia katika kusanyiko la Bwana.
Thei that ben borun of hem, schulen entre in the thridde generacioun in to the `chirche of the Lord.
9 Unapokuwa umepiga kambi dhidi ya adui zako, jitenge na kitu chochote kisicho safi.
Whanne thou schalt go out `in to batel ayens thin enemyes, thou schalt kepe thee fro al yuel thing.
10 Ikiwa mtu amechafuka kwa sababu ya kutokwa na shahawa usiku, inampasa atoke nje ya kambi na kukaa huko.
If a man is among you, which is defoulid in `sleep of nyyt, he schal go out of `the castels;
11 Lakini jioni ikikaribia ataoga, na baada ya jua kuzama ataingia tena kambini.
and he schal not turne ayen bifore that he be waischun in watir at euentid, and aftir the goyng doun of the sunne he schal go ayen in to the castels.
12 Tengeni mahali nje ya kambi ambapo mnaweza kwenda kujisaidia.
Thou schalt haue a place without the castels, to which thou schalt go out to nedeful thingis of kynde;
13 Kama sehemu ya vifaa vyenu kuweni na kitu cha kulimia, nanyi mnapojisaidia, chimba shimo na kisha funika kile kikutokacho.
and thou schalt bere a litil stake in the girdil; and whanne thou hast sete, thou schalt digge `bi cumpas, and `thou schalt hile with erthe thingis `defied out,
14 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu hutembea katika kambi yenu ili kuwalinda na kuwaweka adui zenu mikononi mwenu. Kambi yenu ni lazima iwe takatifu, ili asione kitu chochote miongoni mwenu kilicho kichafu akageuka na kuwaacha.
where thou art releuyd. For thi Lord God goeth in the myddis of castels, that he diliuere thee, and bitake thin enemyes to thee, that thi castels be hooli, and no thing of filthe appere in tho, lest he forsake thee.
15 Ikiwa mtumwa amekimbilia kwako, usimrudishe kwa bwana wake.
Thou schalt not bitake a seruaunt to his lord, which seruaunt fleeth to thee;
16 Mwache aishi miongoni mwenu mahali popote anapopapenda na katika mji wowote anaochagua. Usimwonee.
he schal dwelle with thee in the place that plesith hym, and he schal reste in oon of thi citees; and make thou not hym sori.
17 Asiwepo Mwisraeli mwanamke kahaba au mwanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
Noon hoore schal be of the douytris of Israel, nether a letchour of the sones of Israel.
18 Kamwe usilete mapato ya ukahaba ikiwa ni ya mwanamke au ni ya mwanaume katika nyumba ya Bwana Mungu wako kwa ajili ya nadhiri yoyote, kwa sababu Bwana Mungu wako anachukizwa na yote mawili.
Thou schalt not offre the hire of `an hoore hows, nether the prijs of a dogge, in the hows of thi Lord God, what euer thing it is that thou hast avowid; for euer eithir is abhomynacioun bifor thi Lord God.
19 Usimtoze ndugu yako riba, iwe ni fedha ama chakula ama kitu kingine chochote ambacho waweza kupata riba juu yake.
Thou schalt not leene to thi brothir to vsure money, neither fruytis,
20 Unaweza kumtoza mgeni riba, lakini siyo nduguyo Mwisraeli, ili kwamba Bwana Mungu wako akubariki katika kila kitu unachoweka mkono katika nchi unayoingia kuimiliki.
nethir ony othir thing, but to an alien. Forsothe thou schalt leene to thi brothir without vsure that that he nedith, that thi Lord God blesse thee in al thi werk, in the lond to which thou schalt entre to welde.
21 Ukiweka nadhiri kwa Bwana Mungu wako, usichelewe kuitimiza, kwa kuwa Bwana Mungu wako atakudai, nawe utakuwa na hatia ya dhambi.
Whanne thou makist auow to thi Lord God, thou schalt not tarie to yelde, for thi Lord God schal `requyre, ether axe, that; and if thou tariest, it schal be arretid to thee in to synne.
22 Lakini ukijizuia kuweka nadhiri, hutakuwa na hatia.
If thou `nylt bihete, thou schalt be with out synne.
23 Chochote kitakachotamkwa kwa midomo yako ni lazima uhakikishe umekifanya, kwa sababu uliweka nadhiri yako kwa hiari mbele za Bwana Mungu wako kwa kinywa chako mwenyewe.
Forsothe thou schalt kepe, and `do that that yede out onys of thi lippis, as thou bihiytist to thi Lord God, and hast spoke with thin owne wille and thi mouth.
24 Kama ukiingia katika shamba la mizabibu la jirani yako, unaweza kula zabibu kadiri utakavyo, lakini usiweke chochote kwenye kikapu chako.
If thou entrist in to the vynere of thi neiybore, ete thou grapis, as myche as plesith thee; but bere thou not out with thee.
25 Kama ukiingia katika shamba la nafaka la jirani yako, unaweza kukwanyua kwa mikono yako, lakini usikate kwa mundu nafaka iliyosimama.
If thou entrist in to `the corn of thi freend, thou schalt breke `eeris of corn, and frote togidere with `the hond; but thou schalt not repe with a sikil.

< Torati 23 >