< Torati 23 >

1 Asiingie mtu yeyote aliyehasiwa kwa kupondwa makende au kwa kukatwa uume wake katika kusanyiko la Bwana.
An eunuch, whose testicles are broken or cut away, or yard cut off, shall not enter into the church of the Lord.
2 Mtu yeyote ambaye amezaliwa kwenye ndoa isiyo halali au wazao wake wasiingie kwenye kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.
A mamzer, that is to say, one born of a prostitute, shall not enter into the church of the Lord, until the tenth generation.
3 Hapatakuwa na Mwamoni au Mmoabu au yeyote wa wazao wao atakayeruhusiwa kuingia katika kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.
The Ammonite and the Moabite, even after the tenth generation shall not enter into the church of the Lord for ever:
4 Kwa kuwa hawakuja kuwalaki wakiwa na mkate na maji mlipokuwa njiani mlipotoka Misri, tena walimwajiri Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori iliyoko Aramu-Naharaimu ili kuwalaani ninyi.
Because they would not meet you with bread and water in the way, when you came out of Egypt: hand because they hired against thee Balaam, the son of Beer, from Mesopotamia in Syria, to curse thee.
5 Hata hivyo, Bwana Mungu wenu hakumsikiliza Balaamu bali aligeuza laana kuwa baraka kwenu kwa sababu Bwana Mungu wenu anawapenda.
And the Lord thy God would not hear Balaam, and he turned his cursing into thy blessing, because he loved thee.
6 Msitafute mapatano ya urafiki nao maisha yenu yote.
Thou shalt not make peace with them, neither shalt thou seek their prosperity all the days of thy life for ever.
7 Usimchukie Mwedomu, kwa kuwa yeye ni ndugu yako. Usimchukie Mmisri, kwa sababu uliishi kama mgeni katika nchi yake.
Thou shalt not abhor the Edomite, because he is thy brother: nor the Egyptian, because thou wast a stranger in his land.
8 Kizazi cha tatu cha watoto watakaozaliwa nao wanaweza kuingia katika kusanyiko la Bwana.
They that are born of them, in the third generation shall enter into the church of the Lord.
9 Unapokuwa umepiga kambi dhidi ya adui zako, jitenge na kitu chochote kisicho safi.
When thou goest out to war against thy enemies, thou shalt keep thyself from every evil thing.
10 Ikiwa mtu amechafuka kwa sababu ya kutokwa na shahawa usiku, inampasa atoke nje ya kambi na kukaa huko.
If there be among you any man, that is defiled in a dream by night, he shall go forth out of the camp.
11 Lakini jioni ikikaribia ataoga, na baada ya jua kuzama ataingia tena kambini.
And shall not return, before he be washed with water in the evening: and after sunset he shall return into the camp.
12 Tengeni mahali nje ya kambi ambapo mnaweza kwenda kujisaidia.
Thou shalt have a place without the camp, to which thou mayst go for the necessities of nature,
13 Kama sehemu ya vifaa vyenu kuweni na kitu cha kulimia, nanyi mnapojisaidia, chimba shimo na kisha funika kile kikutokacho.
Carrying a paddle at thy girdle. And when thou sittest down, thou shalt dig round about, and with the earth that is dug up thou shalt cover
14 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu hutembea katika kambi yenu ili kuwalinda na kuwaweka adui zenu mikononi mwenu. Kambi yenu ni lazima iwe takatifu, ili asione kitu chochote miongoni mwenu kilicho kichafu akageuka na kuwaacha.
That which thou art eased of: (for the Lord thy God walketh in the midst of thy camp, to deliver thee, and to give up thy enemies to thee: ) and let thy camp be holy, and let no uncleanness appear therein, lest he go away from thee.
15 Ikiwa mtumwa amekimbilia kwako, usimrudishe kwa bwana wake.
Thou shalt not deliver to his master the servant that is fled to thee.
16 Mwache aishi miongoni mwenu mahali popote anapopapenda na katika mji wowote anaochagua. Usimwonee.
He shall dwell with thee ill the place that shall please him, and shall rest, in one of thy cities: give him no trouble.
17 Asiwepo Mwisraeli mwanamke kahaba au mwanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
There shall be no whore among the daughters of Israel, nor whoremonger among the sons of Israel.
18 Kamwe usilete mapato ya ukahaba ikiwa ni ya mwanamke au ni ya mwanaume katika nyumba ya Bwana Mungu wako kwa ajili ya nadhiri yoyote, kwa sababu Bwana Mungu wako anachukizwa na yote mawili.
Thou shalt not offer the hire of a strumpet, nor the price of a dog, in the house of the Lord thy God, whatsoever it be that thou hast vowed: because both these are an abomination to the Lord thy God.
19 Usimtoze ndugu yako riba, iwe ni fedha ama chakula ama kitu kingine chochote ambacho waweza kupata riba juu yake.
Thou shalt not lend to thy brother money to usury, nor corn, nor any other thing:
20 Unaweza kumtoza mgeni riba, lakini siyo nduguyo Mwisraeli, ili kwamba Bwana Mungu wako akubariki katika kila kitu unachoweka mkono katika nchi unayoingia kuimiliki.
But to the stranger. To thy brother thou shalt lend that which he wanteth, without usury: that the Lord thy God may bless thee in all thy works in the land, which thou shalt go in to possess.
21 Ukiweka nadhiri kwa Bwana Mungu wako, usichelewe kuitimiza, kwa kuwa Bwana Mungu wako atakudai, nawe utakuwa na hatia ya dhambi.
When thou hast made a vow to the Lord thy God, thou shalt not delay to pay it: because the Lord thy God will require it. And if thou delay, it shall be imputed to thee for a sin.
22 Lakini ukijizuia kuweka nadhiri, hutakuwa na hatia.
If thou wilt not promise, thou shalt be without sin.
23 Chochote kitakachotamkwa kwa midomo yako ni lazima uhakikishe umekifanya, kwa sababu uliweka nadhiri yako kwa hiari mbele za Bwana Mungu wako kwa kinywa chako mwenyewe.
But that which is once gone out of thy lips, thou shalt observe, and shalt do as thou hast promised to the Lord thy God, and hast spoken with thy own will and with thy own mouth.
24 Kama ukiingia katika shamba la mizabibu la jirani yako, unaweza kula zabibu kadiri utakavyo, lakini usiweke chochote kwenye kikapu chako.
Going into thy neighbour’s vineyard, thou mayst eat as many grapes as thou pleasest: but must carry none out with thee:
25 Kama ukiingia katika shamba la nafaka la jirani yako, unaweza kukwanyua kwa mikono yako, lakini usikate kwa mundu nafaka iliyosimama.
If thou go into thy friend’s corn, thou mayst break the ears, and rub them in thy hand: but not reap them with a sickle.

< Torati 23 >