< Torati 23 >
1 Asiingie mtu yeyote aliyehasiwa kwa kupondwa makende au kwa kukatwa uume wake katika kusanyiko la Bwana.
He that is fractured or mutilated in his private parts shall not enter into the assembly of the Lord.
2 Mtu yeyote ambaye amezaliwa kwenye ndoa isiyo halali au wazao wake wasiingie kwenye kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.
[One born] of a harlot shall not enter into the assembly of the Lord.
3 Hapatakuwa na Mwamoni au Mmoabu au yeyote wa wazao wao atakayeruhusiwa kuingia katika kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.
The Ammanite and Moabite shall not enter into the assembly of the Lord, even until the tenth generation he shall not enter into the assembly of the Lord, even for ever:
4 Kwa kuwa hawakuja kuwalaki wakiwa na mkate na maji mlipokuwa njiani mlipotoka Misri, tena walimwajiri Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori iliyoko Aramu-Naharaimu ili kuwalaani ninyi.
because they met you not with bread and water by the way, when you went out of Egypt; and because they hired against you Balaam the son of Beor of Mesopotamia to curse you.
5 Hata hivyo, Bwana Mungu wenu hakumsikiliza Balaamu bali aligeuza laana kuwa baraka kwenu kwa sababu Bwana Mungu wenu anawapenda.
But the Lord your God would not listen to Balaam; and the Lord your God changed the curses into blessings, because the Lord your God loved you.
6 Msitafute mapatano ya urafiki nao maisha yenu yote.
You shall not speak peaceably or profitably to them all your days for ever.
7 Usimchukie Mwedomu, kwa kuwa yeye ni ndugu yako. Usimchukie Mmisri, kwa sababu uliishi kama mgeni katika nchi yake.
You shall not abhor an Edomite, because he is your brother; you shall not abhor an Egyptian, because you were a stranger in his land.
8 Kizazi cha tatu cha watoto watakaozaliwa nao wanaweza kuingia katika kusanyiko la Bwana.
If sons be born to them, in the third generation they shall enter into the assembly of the Lord.
9 Unapokuwa umepiga kambi dhidi ya adui zako, jitenge na kitu chochote kisicho safi.
And if you should go forth to engage with your enemies, then you shall keep you from every wicked thing.
10 Ikiwa mtu amechafuka kwa sababu ya kutokwa na shahawa usiku, inampasa atoke nje ya kambi na kukaa huko.
If there should be in you a man who is not clean by reason of his issue by night, then he shall go forth out of the camp, and he shall not enter into the camp.
11 Lakini jioni ikikaribia ataoga, na baada ya jua kuzama ataingia tena kambini.
And it shall come to pass towards evening he shall wash his body with water, and when the sun has gone down, he shall go into the camp.
12 Tengeni mahali nje ya kambi ambapo mnaweza kwenda kujisaidia.
And you shall have a place outside of the camp, and you shall go out there,
13 Kama sehemu ya vifaa vyenu kuweni na kitu cha kulimia, nanyi mnapojisaidia, chimba shimo na kisha funika kile kikutokacho.
and you shall have a trowel on your girdle; and it shall come to pass when you would relieve yourself abroad, that you shall dig with it, and shall bring back the earth and cover your nuisance.
14 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu hutembea katika kambi yenu ili kuwalinda na kuwaweka adui zenu mikononi mwenu. Kambi yenu ni lazima iwe takatifu, ili asione kitu chochote miongoni mwenu kilicho kichafu akageuka na kuwaacha.
Because the Lord your God walks in your camp to deliver you, and to give up your enemy before your face; and your camp shall be holy, and there shall not appear in you a disgraceful thing, and [so] he shall turn away from you.
15 Ikiwa mtumwa amekimbilia kwako, usimrudishe kwa bwana wake.
You shall not deliver a servant to his master, who [coming] from his master attaches himself to you.
16 Mwache aishi miongoni mwenu mahali popote anapopapenda na katika mji wowote anaochagua. Usimwonee.
He shall dwell with you, he shall dwell amongst you where he shall please; you shall not afflict him.
17 Asiwepo Mwisraeli mwanamke kahaba au mwanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
There shall not be a harlot of the daughters of Israel, and there shall not be a fornicator of the sons of Israel; there shall not be an idolatress of the daughters of Israel, and there shall not be an initiated person of the sons of Israel.
18 Kamwe usilete mapato ya ukahaba ikiwa ni ya mwanamke au ni ya mwanaume katika nyumba ya Bwana Mungu wako kwa ajili ya nadhiri yoyote, kwa sababu Bwana Mungu wako anachukizwa na yote mawili.
You shall not bring the hire of a harlot, nor the price of a dog into the house of the Lord your God, for any vow; because even both are an abomination to the Lord your God.
19 Usimtoze ndugu yako riba, iwe ni fedha ama chakula ama kitu kingine chochote ambacho waweza kupata riba juu yake.
You shall not lend to your brother on usury of silver, or usury of meat, or usury of any thing which you may lend out.
20 Unaweza kumtoza mgeni riba, lakini siyo nduguyo Mwisraeli, ili kwamba Bwana Mungu wako akubariki katika kila kitu unachoweka mkono katika nchi unayoingia kuimiliki.
You may lend on usury to a stranger, but to your brother you shall not lend on usury; that the Lord your God may bless you in all your works upon the land, into which you are entering to inherit it.
21 Ukiweka nadhiri kwa Bwana Mungu wako, usichelewe kuitimiza, kwa kuwa Bwana Mungu wako atakudai, nawe utakuwa na hatia ya dhambi.
And if you will vow a vow to the Lord your God, you shall not delay to pay it; for the Lord your God will surely require it of you, and [otherwise] it shall be sin in you.
22 Lakini ukijizuia kuweka nadhiri, hutakuwa na hatia.
But if you should be unwilling to vow, it is not sin in you.
23 Chochote kitakachotamkwa kwa midomo yako ni lazima uhakikishe umekifanya, kwa sababu uliweka nadhiri yako kwa hiari mbele za Bwana Mungu wako kwa kinywa chako mwenyewe.
You shall observe the words that proceed from between your lips; and as you have vowed a gift to the Lord God, [so] shall you do that which you have spoken with your mouth.
24 Kama ukiingia katika shamba la mizabibu la jirani yako, unaweza kula zabibu kadiri utakavyo, lakini usiweke chochote kwenye kikapu chako.
And if you should go into the corn field of your neighbour, then you may gather the ears with your hands; but you shall not put the sickle to your neighbour's corn.
25 Kama ukiingia katika shamba la nafaka la jirani yako, unaweza kukwanyua kwa mikono yako, lakini usikate kwa mundu nafaka iliyosimama.
And if you should go into the vineyard of your neighbour, you shall eat grapes sufficient to satisfy your desire; but you may not put them into a vessel.