< Torati 21 >
1 Kama mtu akikutwa ameuawa, naye amelala kwenye shamba katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kuimiliki, wala haijulikani ni nani aliyemuua,
Če je nekdo najden ubit na polju, ki ti ga Gospod, tvoj Bog, daje v last, ležeč na polju in se ne ve kdo ga je umoril,
2 wazee wenu na waamuzi watatoka na kupima umbali kutoka maiti alipolala mpaka kwenye miji ya jirani.
potem bodo prišli tvoje starešine in tvoji sodniki in bodo izmerili [razdaljo] do mest, ki so naokoli tega, ki je umorjen.
3 Kisha wazee wa ule mji ulio karibu zaidi na yule maiti watamchukua mtamba ambaye hajapata kufanyishwa kazi na ambaye hajafungwa nira,
Zgodilo se bo, da mesto, ki je bliže umorjenemu človeku, celo starešine tega mesta bodo vzeli telico, s katero še niso delali in ki še ni vlekla jarma,
4 na kumpeleka kwenye bonde ambalo halijapata kulimwa au kupandwa mazao na ambapo kuna chemchemi itiririkayo. Huko kwenye hilo bonde, wazee watamvunja yule mtamba shingo.
in starešine tega mesta bodo telico privedli dol v valovito dolino, ki ni niti obdelana niti posejana in tam, v dolini, bodo telici zlomili vrat
5 Makuhani, hao wana wa Lawi, watasogea mbele, kwa kuwa Bwana Mungu wenu, amewachagua kuhudumu na kutoa baraka katika jina la Bwana, na kuamua mashauri yote ya mabishano na mashambulio.
in duhovniki, sinovi Lévijevcev, se bodo približali, kajti njih je Gospod, tvoj Bog, izbral, da mu služijo in da blagoslavljajo v Gospodovem imenu, in po njihovi besedi bo vsaka polemika in vsak udarec preizkušen
6 Ndipo wazee wote wa mji ulio karibu zaidi na huyo maiti watanawa mikono yao juu ya huyo mtamba ambaye shingo yake imevunjwa huko kwenye bonde,
in vse starešine tega mesta, ki je bliže umorjenemu človeku, si bodo roke umili nad telico, ki je obglavljena v dolini
7 nao watatangaza: “Mikono yetu haikumwaga damu hii, wala macho yetu hayakuona likifanyika.
in odgovorili bodo ter rekli: ›Naše roke niso prelile te krvi niti naše oči tega niso videle.
8 Ee Bwana, ukubali upatanisho kwa watu wako Israeli, ambao umewakomboa, wala usiwahesabie watu wako hatia ya damu ya mtu asiyekuwa na hatia.” Nayo damu iliyomwagika itakuwa imefanyiwa upatanisho.
Bodi usmiljen, oh Gospod, svojemu ljudstvu Izraelu, ki si ga odkupil in ne polagaj nedolžne krvi na svoje ljudstvo Izrael, ki je najbliže.‹ In kri jim bo odpuščena.
9 Hivyo mtakuwa mmejitakasa wenyewe kutoka hatia ya kumwaga damu isiyokuwa na hatia, kwa kuwa mmefanya lile lililo sawa mbele za macho ya Bwana.
Tako boš izmed sebe odvzel krivdo nedolžne krvi, ko boš storil to, kar je pravilno v Gospodovih očeh.
10 Mkienda vitani kupigana na adui zenu naye Bwana Mungu wenu akawatia adui mikononi mwenu, nanyi mkachukua mateka,
Ko greš naprej v vojno zoper svoje sovražnike in ti jih Gospod, tvoj Bog, izroči v tvoje roke in si jih zajel kot ujetnike
11 kama ukiona miongoni mwa mateka mwanamke mzuri wa sura nawe wavutwa naye, waweza kumwoa akawa mke wako.
in vidiš med ujetniki lepo žensko in imaš do nje poželenje, da bi jo imel za svojo ženo,
12 Mlete nyumbani mwako, anyoe nywele na kukata kucha zake,
potem jo boš privedel domov, v svojo hišo. Ona si bo obrila svojo glavo in postrigla svoje nohte
13 avue nguo alizokuwa amevaa alipotekwa. Baada ya kuishi nyumbani mwako na kumwombolezea baba yake na mama yake kwa mwezi mzima, ndipo utakapoweza kumwendea na kuwa mume wake naye atakuwa mke wako.
in iz sebe bo odložila oblačila svojega ujetništva in ostala bo v tvoji hiši in cel mesec bo objokovala svojega očeta in svojo mater. Potem boš šel noter k njej in boš njen soprog in ona bo tvoja žena.
14 Lakini kama hutaendelea kupendezwa naye, mwache aende popote anapotaka. Kamwe huwezi kumuuza au kumtendea kama mtumwa, kwa sababu utakuwa umemvunjia heshima.
In zgodilo se bo, če z njo ne boš imel veselja, potem jo boš pustil oditi kamor ona hoče. Toda, ker si jo ponižal, je nikakor ne boš prodal za denar, iz nje ne boš naredil trgovskega blaga.
15 Kama mwanaume ana wake wawili, naye anampenda mmoja na mwingine hampendi na wote wawili wamemzalia wana wa kiume, lakini mwana mzaliwa wa kwanza ni wa yule mke asiyempenda,
Če ima mož dve ženi, eno ljubljeno in drugo osovraženo in sta mu rodili otroke, obe, ljubljena in osovražena in če je prvorojenec od tiste, ki je bila osovražena,
16 wakati anapotoa wosia wa mali yake kwa wanawe, kamwe asitoe haki za mzaliwa wa kwanza kwa mwana wa mke ampendaye kwa upendeleo, badala ya mzaliwa hasa wa kwanza, ambaye ni mwana wa mke ambaye hampendi.
potem se bo zgodilo, ko daje svojim sinovom podedovati to, kar ima, da ne sme narediti sina ljubljene prvorojenca pred sinom osovražene, ki je zares prvorojenec,
17 Ni lazima amkubali mwana wa mke asiyempenda kama mzaliwa wa kwanza kwa kumpa sehemu ya vile vyote alivyo navyo maradufu. Mwana huyo ni ishara ya kwanza ya nguvu za baba yake. Haki ya mzaliwa wa kwanza ni yake yeye.
temveč bo sina osovražene priznal za prvorojenca s tem, da mu da dvojni delež od vsega, kar ima, kajti on je začetek njegove moči; pravica prvorojenca je njegova.
18 Kama mtu ana mwana mkaidi na mwasi ambaye hamtii baba yake na mama yake, na hasikii wazazi wanapomrudi,
Če ima človek trmoglavega in upornega sina, ki noče ubogati glasu svojega očeta ali glasu svoje matere in ko sta ga karala, da ju noče poslušati,
19 baba yake na mama yake watamleta kwa wazee kwenye lango la mji wake.
potem naj ga njegov oče in njegova mati primeta in ga privedeta k starešinam njegovega mesta in k velikim vratom njegovega kraja
20 Watawaambia wazee, “Huyu mwanetu ni mkaidi na mwasi. Hatutii sisi, yeye ni mpotovu na mlevi.”
in starešinam mesta bosta rekla: ›Ta najin sin je trmoglav in uporen, noče ubogati najinega glasu. Požeruh je in pijanec.‹
21 Kisha wanaume wote wa mjini mwake watampiga kwa mawe mpaka afe. Ndivyo imewapasa kuondoa maovu kati yenu. Israeli yote itasikia hili na kuogopa.
In vsi ljudje iz njegovega mesta ga bodo kamnali s kamni, da ta umre. Tako boš zlo odstranil proč izmed vas in ves Izrael bo slišal in se bal.
22 Kama mtu ana hatia ya kosa linalompasa kuuawa naye akauawa, mwili wake utaangikwa mtini,
Če je moški zagrešil greh, vreden smrti, in bo usmrčen in ga obesiš na drevo,
23 kamwe msiuache mwili wake mtini usiku kucha. Hakikisheni mnauzika mwili wake siku ile ile, kwa sababu kila mtu anayeangikwa mtini yupo chini ya laana ya Mungu. Msiinajisi nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi wenu.
naj njegovo truplo ne ostane vso noč na drevesu, temveč ga boš vsekakor tisti dan pokopal (kajti ta, ki je obešen, je preklet od Boga), da tvoja dežela, ki ti jo Gospod, tvoj Bog, daje za dediščino, ne bo omadeževana.