< Torati 21 >

1 Kama mtu akikutwa ameuawa, naye amelala kwenye shamba katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kuimiliki, wala haijulikani ni nani aliyemuua,
Jeśli w ziemi, którą PAN, twój Bóg, daje ci w posiadanie, zostanie znaleziony zabity człowiek leżący na polu, a nie wiadomo, kto go zabił;
2 wazee wenu na waamuzi watatoka na kupima umbali kutoka maiti alipolala mpaka kwenye miji ya jirani.
Wtedy twoi starsi i sędziowie wyjdą i zmierzą odległość do miast [leżących] dokoła zabitego.
3 Kisha wazee wa ule mji ulio karibu zaidi na yule maiti watamchukua mtamba ambaye hajapata kufanyishwa kazi na ambaye hajafungwa nira,
A starsi tego miasta, które leży najbliżej zabitego, wezmą jałówkę, której jeszcze nie użyto do pracy i która jeszcze nie ciągnęła w jarzmie;
4 na kumpeleka kwenye bonde ambalo halijapata kulimwa au kupandwa mazao na ambapo kuna chemchemi itiririkayo. Huko kwenye hilo bonde, wazee watamvunja yule mtamba shingo.
I zaprowadzą starsi tego miasta jałówkę do kamienistej doliny, gdzie nigdy nie uprawiano ani nie zasiewano, i tam utną kark jałówki w tej dolinie.
5 Makuhani, hao wana wa Lawi, watasogea mbele, kwa kuwa Bwana Mungu wenu, amewachagua kuhudumu na kutoa baraka katika jina la Bwana, na kuamua mashauri yote ya mabishano na mashambulio.
Potem przyjdą kapłani, synowie Lewiego, gdyż ich wybrał PAN, twój Bóg, aby mu służyli i aby błogosławili w imię PANA, a według ich uznania ma być rozstrzygnięty każdy spór i każde zranienie;
6 Ndipo wazee wote wa mji ulio karibu zaidi na huyo maiti watanawa mikono yao juu ya huyo mtamba ambaye shingo yake imevunjwa huko kwenye bonde,
I wszyscy starsi tego miasta, które leży najbliżej zabitego, umyją swoje ręce nad jałówką, którą ścięto w dolinie;
7 nao watatangaza: “Mikono yetu haikumwaga damu hii, wala macho yetu hayakuona likifanyika.
I oświadczą: Nasze ręce nie wylały tej krwi i nasze oczy [tego] nie widziały.
8 Ee Bwana, ukubali upatanisho kwa watu wako Israeli, ambao umewakomboa, wala usiwahesabie watu wako hatia ya damu ya mtu asiyekuwa na hatia.” Nayo damu iliyomwagika itakuwa imefanyiwa upatanisho.
PANIE, przyjmij przebłaganie za twój lud Izraela, który odkupiłeś, a nie poczytaj twemu ludowi Izraela niewinnej krwi. I będą oczyszczeni od tej krwi.
9 Hivyo mtakuwa mmejitakasa wenyewe kutoka hatia ya kumwaga damu isiyokuwa na hatia, kwa kuwa mmefanya lile lililo sawa mbele za macho ya Bwana.
W ten sposób usuniesz niewinną krew spośród siebie, gdy uczynisz to, co jest prawe w oczach PANA.
10 Mkienda vitani kupigana na adui zenu naye Bwana Mungu wenu akawatia adui mikononi mwenu, nanyi mkachukua mateka,
Gdy też wyruszysz na wojnę przeciwko swoim wrogom i PAN, twój Bóg, wyda ich w twoje ręce, i weźmiesz z nich jeńców;
11 kama ukiona miongoni mwa mateka mwanamke mzuri wa sura nawe wavutwa naye, waweza kumwoa akawa mke wako.
I zobaczysz wśród jeńców piękną kobietę, którą sobie upodobasz, i chciałbyś pojąć ją za żonę;
12 Mlete nyumbani mwako, anyoe nywele na kukata kucha zake,
Wtedy przyprowadzisz ją do swego domu, a ona ogoli swoją głowę i obetnie sobie paznokcie;
13 avue nguo alizokuwa amevaa alipotekwa. Baada ya kuishi nyumbani mwako na kumwombolezea baba yake na mama yake kwa mwezi mzima, ndipo utakapoweza kumwendea na kuwa mume wake naye atakuwa mke wako.
I złoży z siebie szatę, w której została pojmana, zostanie w twoim domu i będzie opłakiwać swego ojca i matkę przez cały miesiąc. Potem będziesz z nią obcował i będziesz jej mężem, a ona będzie twoją żoną.
14 Lakini kama hutaendelea kupendezwa naye, mwache aende popote anapotaka. Kamwe huwezi kumuuza au kumtendea kama mtumwa, kwa sababu utakuwa umemvunjia heshima.
A jeśli nie będzie ci się podobać, wtedy pozwolisz jej odejść, dokąd zechce; żadną miarą nie sprzedasz jej za pieniądze i nie będziesz nią kupczyć, gdyż ją poniżyłeś.
15 Kama mwanaume ana wake wawili, naye anampenda mmoja na mwingine hampendi na wote wawili wamemzalia wana wa kiume, lakini mwana mzaliwa wa kwanza ni wa yule mke asiyempenda,
Gdyby mężczyzna miał dwie żony, jedną kochaną, a drugą znienawidzoną, i one urodzą mu synów – kochana i znienawidzona – a pierworodny będzie synem znienawidzonej;
16 wakati anapotoa wosia wa mali yake kwa wanawe, kamwe asitoe haki za mzaliwa wa kwanza kwa mwana wa mke ampendaye kwa upendeleo, badala ya mzaliwa hasa wa kwanza, ambaye ni mwana wa mke ambaye hampendi.
To gdy będzie przydzielał dobra swoim synom w dziedzictwo, nie będzie mógł ustanowić pierworodnym syna kochanej przed pierworodnym synem znienawidzonej;
17 Ni lazima amkubali mwana wa mke asiyempenda kama mzaliwa wa kwanza kwa kumpa sehemu ya vile vyote alivyo navyo maradufu. Mwana huyo ni ishara ya kwanza ya nguvu za baba yake. Haki ya mzaliwa wa kwanza ni yake yeye.
Ale za pierworodnego uzna syna znienawidzonej, dając mu podwójną część wszystkiego, co ma, gdyż on [jest] początkiem jego siły, jemu przysługuje prawo pierworództwa.
18 Kama mtu ana mwana mkaidi na mwasi ambaye hamtii baba yake na mama yake, na hasikii wazazi wanapomrudi,
Jeśli ktoś ma syna upartego i krnąbrnego, który nie słucha ani głosu swojego ojca, ani głosu swojej matki, a choć go karcą, nie słucha ich;
19 baba yake na mama yake watamleta kwa wazee kwenye lango la mji wake.
Wtedy jego ojciec i matka wezmą go i przyprowadzą do starszych swego miasta i do bramy jego miejscowości;
20 Watawaambia wazee, “Huyu mwanetu ni mkaidi na mwasi. Hatutii sisi, yeye ni mpotovu na mlevi.”
I powiedzą do starszych miasta: Ten nasz syn jest uparty i krnąbrny, nie słucha naszego głosu, [jest] żarłokiem i pijakiem;
21 Kisha wanaume wote wa mjini mwake watampiga kwa mawe mpaka afe. Ndivyo imewapasa kuondoa maovu kati yenu. Israeli yote itasikia hili na kuogopa.
Wtedy wszyscy mężczyźni tego miasta ukamienują go na śmierć; w ten sposób usuniesz zło spośród siebie, a cały Izrael usłyszy o tym i będzie się bać.
22 Kama mtu ana hatia ya kosa linalompasa kuuawa naye akauawa, mwili wake utaangikwa mtini,
A jeśli ktoś popełni grzech zasługujący na śmierć i poniesie śmierć, a powiesisz go na drzewie;
23 kamwe msiuache mwili wake mtini usiku kucha. Hakikisheni mnauzika mwili wake siku ile ile, kwa sababu kila mtu anayeangikwa mtini yupo chini ya laana ya Mungu. Msiinajisi nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi wenu.
Jego trup nie pozostanie na drzewie przez noc, lecz musisz go pochować tego samego dnia, bo ten, kto wisi, [jest] przeklęty przez Boga. Nie będziesz plugawił twojej ziemi, którą PAN, twój Bóg, daje ci w dziedzictwo.

< Torati 21 >