< Torati 21 >

1 Kama mtu akikutwa ameuawa, naye amelala kwenye shamba katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kuimiliki, wala haijulikani ni nani aliyemuua,
If a man is found slain in the land which Jehovah thy God gives thee to possess it, lying in the field, and it not be known who has smitten him,
2 wazee wenu na waamuzi watatoka na kupima umbali kutoka maiti alipolala mpaka kwenye miji ya jirani.
then thy elders and thy judges shall come forth. And they shall measure to the cities which are round about him who is slain,
3 Kisha wazee wa ule mji ulio karibu zaidi na yule maiti watamchukua mtamba ambaye hajapata kufanyishwa kazi na ambaye hajafungwa nira,
and it shall be, that the city which is nearest to the slain man, even the elders of that city shall take a heifer of the herd, which has not been worked with, and which has not drawn in the yoke,
4 na kumpeleka kwenye bonde ambalo halijapata kulimwa au kupandwa mazao na ambapo kuna chemchemi itiririkayo. Huko kwenye hilo bonde, wazee watamvunja yule mtamba shingo.
and the elders of that city shall bring down the heifer to a valley with running water, which is neither plowed nor sown, and shall break the heifer's neck there in the valley.
5 Makuhani, hao wana wa Lawi, watasogea mbele, kwa kuwa Bwana Mungu wenu, amewachagua kuhudumu na kutoa baraka katika jina la Bwana, na kuamua mashauri yote ya mabishano na mashambulio.
And the priests the sons of Levi shall come near, for Jehovah thy God has chosen them to minister to him, and to bless in the name of Jehovah, and according to their word shall every controversy and every stroke be.
6 Ndipo wazee wote wa mji ulio karibu zaidi na huyo maiti watanawa mikono yao juu ya huyo mtamba ambaye shingo yake imevunjwa huko kwenye bonde,
And all the elders of that city, who are nearest to the slain man, shall wash their hands over the heifer whose neck was broken in the valley,
7 nao watatangaza: “Mikono yetu haikumwaga damu hii, wala macho yetu hayakuona likifanyika.
and they shall answer and say, Our hands have not shed this blood, neither have our eyes seen it.
8 Ee Bwana, ukubali upatanisho kwa watu wako Israeli, ambao umewakomboa, wala usiwahesabie watu wako hatia ya damu ya mtu asiyekuwa na hatia.” Nayo damu iliyomwagika itakuwa imefanyiwa upatanisho.
Forgive, O Jehovah, thy people Israel whom thou have redeemed, and allow no innocent blood to remain in the midst of thy people Israel. And the blood shall be forgiven them.
9 Hivyo mtakuwa mmejitakasa wenyewe kutoka hatia ya kumwaga damu isiyokuwa na hatia, kwa kuwa mmefanya lile lililo sawa mbele za macho ya Bwana.
So shall thou put away the innocent blood from the midst of thee when thou shall do that which is right in the eyes of Jehovah.
10 Mkienda vitani kupigana na adui zenu naye Bwana Mungu wenu akawatia adui mikononi mwenu, nanyi mkachukua mateka,
When thou go forth to battle against thine enemies, and Jehovah thy God delivers them into thy hands, and thou carry them away captive,
11 kama ukiona miongoni mwa mateka mwanamke mzuri wa sura nawe wavutwa naye, waweza kumwoa akawa mke wako.
and see among the captives a beautiful woman, and thou have a desire for her, and would take her to thee to wife,
12 Mlete nyumbani mwako, anyoe nywele na kukata kucha zake,
then thou shall bring her home to thy house. And she shall shave her head, and pare her nails,
13 avue nguo alizokuwa amevaa alipotekwa. Baada ya kuishi nyumbani mwako na kumwombolezea baba yake na mama yake kwa mwezi mzima, ndipo utakapoweza kumwendea na kuwa mume wake naye atakuwa mke wako.
and she shall put the raiment of her captivity from off her, and shall remain in thy house, and bewail her father and her mother a full month. And after that thou shall go in to her, and be her husband, and she shall be thy wife.
14 Lakini kama hutaendelea kupendezwa naye, mwache aende popote anapotaka. Kamwe huwezi kumuuza au kumtendea kama mtumwa, kwa sababu utakuwa umemvunjia heshima.
And it shall be, if thou have no delight in her, then thou shall let her go where she will, but thou shall not sell her at all for money. Thou shall not deal with her harshly, because thou have humbled her.
15 Kama mwanaume ana wake wawili, naye anampenda mmoja na mwingine hampendi na wote wawili wamemzalia wana wa kiume, lakini mwana mzaliwa wa kwanza ni wa yule mke asiyempenda,
If a man has two wives, the one beloved, and the other regarded inferior, and they have borne him sons, both the beloved and the one regarded inferior, and if the firstborn son be hers who was regarded inferior,
16 wakati anapotoa wosia wa mali yake kwa wanawe, kamwe asitoe haki za mzaliwa wa kwanza kwa mwana wa mke ampendaye kwa upendeleo, badala ya mzaliwa hasa wa kwanza, ambaye ni mwana wa mke ambaye hampendi.
then it shall be, in the day that he causes his sons to inherit that which he has, that he may not make the son of the beloved the firstborn before the son of the one regarded inferior, who is the firstborn.
17 Ni lazima amkubali mwana wa mke asiyempenda kama mzaliwa wa kwanza kwa kumpa sehemu ya vile vyote alivyo navyo maradufu. Mwana huyo ni ishara ya kwanza ya nguvu za baba yake. Haki ya mzaliwa wa kwanza ni yake yeye.
But he shall acknowledge the firstborn, the son of the one regarded inferior, by giving him a double portion of all that he has, for he is the beginning of his strength. The right of the firstborn is his.
18 Kama mtu ana mwana mkaidi na mwasi ambaye hamtii baba yake na mama yake, na hasikii wazazi wanapomrudi,
If a man has a stubborn and rebellious son, who will not obey the voice of his father, or the voice of his mother, and, though they chasten him, will not hearken to them,
19 baba yake na mama yake watamleta kwa wazee kwenye lango la mji wake.
then his father and his mother shall lay hold on him, and bring him out to the elders of his city, and to the gate of his place.
20 Watawaambia wazee, “Huyu mwanetu ni mkaidi na mwasi. Hatutii sisi, yeye ni mpotovu na mlevi.”
And they shall say to the elders of his city, This our son is stubborn and rebellious, he will not obey our voice. He is a glutton, and a drunkard.
21 Kisha wanaume wote wa mjini mwake watampiga kwa mawe mpaka afe. Ndivyo imewapasa kuondoa maovu kati yenu. Israeli yote itasikia hili na kuogopa.
And all the men of his city shall stone him to death with stones. So thou shall put away the evil from the midst of thee, and all Israel shall hear, and fear.
22 Kama mtu ana hatia ya kosa linalompasa kuuawa naye akauawa, mwili wake utaangikwa mtini,
And if a man has committed a sin worthy of death, and he be put to death, and thou hang him on a tree,
23 kamwe msiuache mwili wake mtini usiku kucha. Hakikisheni mnauzika mwili wake siku ile ile, kwa sababu kila mtu anayeangikwa mtini yupo chini ya laana ya Mungu. Msiinajisi nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi wenu.
his body shall not remain all night upon the tree, but thou shall surely bury him the same day, for he who is hanged is accursed of God, that thou not defile thy land which Jehovah thy God gives thee for an inheritance.

< Torati 21 >