< Torati 20 >
1 Mtakapokwenda vitani kupigana na adui zenu na mkaona farasi na magari ya vita na jeshi kubwa kuliko lenu, msiwaogope, kwa sababu Bwana Mungu wenu aliyewatoa kutoka Misri, atakuwa pamoja nanyi.
for to come out: come to/for battle upon enemy your and to see: see horse and chariot people: soldiers many from you not to fear from them for LORD God your with you [the] to ascend: rise you from land: country/planet Egypt
2 Wakati mtakapokaribia kwenda vitani, kuhani atakuja mbele na kuhutubia jeshi.
and to be like/as to present: come you to(wards) [the] battle and to approach: approach [the] priest and to speak: speak to(wards) [the] people
3 Atasema: “Sikia, ee Israeli, leo unakwenda vitani kupigana na adui zako. Usife moyo wala usiogope, usitishwe wala usitiwe hofu mbele yao.
and to say to(wards) them to hear: hear Israel you(m. p.) approaching [the] day to/for battle upon enemy your not be tender heart your not to fear and not to hurry and not to tremble from face of their
4 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu ndiye huenda pamoja nanyi kuwapigania dhidi ya adui zenu na kuwapatia ushindi.”
for LORD God your [the] to go: went with you to/for to fight to/for you with enemy your to/for to save [obj] you
5 Maafisa wataliambia jeshi: “Je, kuna yeyote aliyejenga nyumba mpya ambayo haijawekwa wakfu? Yeye na arudi nyumbani, ama sivyo anaweza kufa vitani na mtu mwingine akaiweka wakfu.
and to speak: speak [the] official to(wards) [the] people to/for to say who? [the] man which to build house: home new and not to dedicate him to go: went and to return: return to/for house: home his lest to die in/on/with battle and man another to dedicate him
6 Je, kuna yeyote aliyepanda shamba la mizabibu na hajaanza kulifurahia? Yeye na arudi nyumbani, au sivyo anaweza kufa vitani na mtu mwingine akalifurahia.
and who? [the] man which to plant vineyard and not to profane/begin: fruit him to go: went and to return: return to/for house: home his lest to die in/on/with battle and man another to profane/begin: fruit him
7 Je, kuna yeyote aliyeposa mwanamke na hajamwoa? Yeye na arudi nyumbani, ama sivyo anaweza kufa vitani na mtu mwingine akamwoa.”
and who? [the] man which to betroth woman: wife and not to take: marry her to go: went and to return: return to/for house: home his lest to die in/on/with battle and man another to take: marry her
8 Kisha maafisa wataongeza haya, “Je, kuna mtu anayeogopa ama kufa moyo? Yeye na arudi nyumbani ili ndugu zake nao wasije wakafa moyo pia.”
and to add: again [the] official to/for to speak: speak to(wards) [the] people and to say who? [the] man [the] afraid and tender [the] heart to go: went and to return: return to/for house: home his and not to melt [obj] heart brother: compatriot his like/as heart his
9 Wakati maafisa watakapomaliza kuzungumza na jeshi, watawateua wakuu wa vikosi.
and to be like/as to end: finish [the] official to/for to speak: speak to(wards) [the] people and to reckon: overseer ruler army in/on/with head: leader [the] people
10 Wakati mtakapokwenda kushambulia mji, wapeni watu wake masharti ya amani.
for to present: come to(wards) city to/for to fight upon her and to call: call to to(wards) her to/for peace
11 Wakikubali na kuwafungulia malango yao, watu wake wote watawatumikia kwa kufanya kazi ngumu na watawatumikia.
and to be if peace to answer you and to open to/for you and to be all [the] people [the] to find in/on/with her to be to/for you to/for taskworker and to serve you
12 Ikiwa watakataa kufanya mapatano ya amani na wakiwaingiza katika vita, basi mtauzunguka mji huo kwa vita.
and if not to ally with you and to make with you battle and to confine upon her
13 Wakati Bwana Mungu wenu atakapouweka mji huo mkononi mwenu, waueni kwa upanga wanaume wote waliomo ndani yake.
and to give: give her LORD God your in/on/with hand: power your and to smite [obj] all male her to/for lip: edge sword
14 Kwa upande wa wanawake, watoto, mifugo na kila kitu kingine chochote ndani ya huo mji, mnaweza kuvichukua kama nyara kwa ajili yenu. Nanyi mnaweza kuzitumia hizo nyara ambazo Bwana Mungu wenu amewapa kutoka kwa adui zenu.
except [the] woman and [the] child and [the] animal and all which to be in/on/with city all spoil her to plunder to/for you and to eat [obj] spoil enemy your which to give: give LORD God your to/for you
15 Hivi ndivyo mtakavyofanya kwa miji yote ambayo iko mbali nanyi, ambayo haimilikiwi na mataifa ya karibu.
so to make: do to/for all [the] city [the] distant from you much which not from city [the] nation [the] these they(fem.)
16 Hata hivyo, katika miji ya mataifa ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi, msiache kitu chochote hai kinachopumua.
except from city [the] people [the] these which LORD God your to give: give to/for you inheritance not to live all breath
17 Waangamizeni kabisa Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi, kama Bwana Mungu wenu alivyowaamuru.
for to devote/destroy to devote/destroy them [the] Hittite and [the] Amorite [the] Canaanite and [the] Perizzite [the] Hivite and [the] Jebusite like/as as which to command you LORD God your
18 La sivyo, watawafundisha kufuata mambo yote ya machukizo wanayofanya wakiabudu miungu yao, nanyi mtatenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wenu.
because which not to learn: teach [obj] you to/for to make: do like/as all abomination their which to make: do to/for God their and to sin to/for LORD God your
19 Wakati mtakapouzunguka mji kwa vita kwa muda mrefu, mkipigana dhidi yake ili kuuteka, msiharibu miti yake kwa kuikata kwa shoka, kwa sababu mtaweza kula matunda yake. Hivyo msiikate. Je, miti hiyo ya mashambani ni watu, hata muizingire?
for to confine to(wards) city day many to/for to fight upon her to/for to capture her not to ruin [obj] tree her to/for to banish upon him axe for from him to eat and [obj] him not to cut: cut for man tree [the] land: country to/for to come (in): besiege from face: before your in/on/with siege
20 Hata hivyo, mnaweza kuikata miti ambayo sio miti ya matunda na kuitumia kujenga ngome, mpaka mji ulio katika vita na ninyi utakapoanguka.
except tree which to know for not tree food he/she/it [obj] him to ruin and to cut: cut and to build siege upon [the] city which he/she/it to make with you battle till to go down she