< Torati 20 >

1 Mtakapokwenda vitani kupigana na adui zenu na mkaona farasi na magari ya vita na jeshi kubwa kuliko lenu, msiwaogope, kwa sababu Bwana Mungu wenu aliyewatoa kutoka Misri, atakuwa pamoja nanyi.
“When you go out to battle against your enemy, and have seen horse and chariot—a people more numerous than you—you are not afraid of them, for your God YHWH [is] with you, who is bringing you up out of the land of Egypt;
2 Wakati mtakapokaribia kwenda vitani, kuhani atakuja mbele na kuhutubia jeshi.
and it has been, in your drawing near to the battle, that the priest has come near, and spoken to the people,
3 Atasema: “Sikia, ee Israeli, leo unakwenda vitani kupigana na adui zako. Usife moyo wala usiogope, usitishwe wala usitiwe hofu mbele yao.
and said to them, Hear, O Israel: You are drawing near today to battle against your enemies, do not let your hearts be tender, do not fear, nor make haste, nor be terrified at their presence,
4 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu ndiye huenda pamoja nanyi kuwapigania dhidi ya adui zenu na kuwapatia ushindi.”
for your God YHWH [is] He who is going with you, to fight for you with your enemies—to save you.
5 Maafisa wataliambia jeshi: “Je, kuna yeyote aliyejenga nyumba mpya ambayo haijawekwa wakfu? Yeye na arudi nyumbani, ama sivyo anaweza kufa vitani na mtu mwingine akaiweka wakfu.
And the authorities have spoken to the people, saying, Who [is] the man that has built a new house and has not dedicated it? Let him go and return to his house, lest he die in battle and another man dedicate it.
6 Je, kuna yeyote aliyepanda shamba la mizabibu na hajaanza kulifurahia? Yeye na arudi nyumbani, au sivyo anaweza kufa vitani na mtu mwingine akalifurahia.
And who [is] the man that has planted a vineyard and has not made it common? Let him go and return to his house, lest he die in battle, and another man make it common.
7 Je, kuna yeyote aliyeposa mwanamke na hajamwoa? Yeye na arudi nyumbani, ama sivyo anaweza kufa vitani na mtu mwingine akamwoa.”
And who [is] the man that has betrothed a woman and has not taken her? Let him go and return to his house, lest he die in battle, and another man take her.
8 Kisha maafisa wataongeza haya, “Je, kuna mtu anayeogopa ama kufa moyo? Yeye na arudi nyumbani ili ndugu zake nao wasije wakafa moyo pia.”
And the authorities have added to speak to the people and said, Who [is] the man that is afraid and tender of heart? Let him go and return to his house, and the heart of his brothers does not melt like his heart.
9 Wakati maafisa watakapomaliza kuzungumza na jeshi, watawateua wakuu wa vikosi.
And it has come to pass, as the authorities finish to speak to the people, that they have appointed princes of the hosts at the head of the people.
10 Wakati mtakapokwenda kushambulia mji, wapeni watu wake masharti ya amani.
When you draw near to a city to fight against it, then you have called to it for peace,
11 Wakikubali na kuwafungulia malango yao, watu wake wote watawatumikia kwa kufanya kazi ngumu na watawatumikia.
and it has been, if it answers you [with] peace, and has opened to you, then it has come to pass, all the people who are found in it are for tributaries to you, and have served you.
12 Ikiwa watakataa kufanya mapatano ya amani na wakiwaingiza katika vita, basi mtauzunguka mji huo kwa vita.
And if it does not make peace with you, and has made war with you, then you have laid siege against it,
13 Wakati Bwana Mungu wenu atakapouweka mji huo mkononi mwenu, waueni kwa upanga wanaume wote waliomo ndani yake.
and your God YHWH has given it into your hand, and you have struck every male of it by the mouth of the sword.
14 Kwa upande wa wanawake, watoto, mifugo na kila kitu kingine chochote ndani ya huo mji, mnaweza kuvichukua kama nyara kwa ajili yenu. Nanyi mnaweza kuzitumia hizo nyara ambazo Bwana Mungu wenu amewapa kutoka kwa adui zenu.
Only, the women, and the infants, and the livestock, and all that is in the city, all its spoil, you seize for yourself, and you have eaten the spoil of your enemies which your God YHWH has given to you.
15 Hivi ndivyo mtakavyofanya kwa miji yote ambayo iko mbali nanyi, ambayo haimilikiwi na mataifa ya karibu.
So you do to all the cities which are very far off from you, which are not of the cities of these nations.
16 Hata hivyo, katika miji ya mataifa ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi, msiache kitu chochote hai kinachopumua.
Only, of the cities of these peoples which your God YHWH is giving to you [for] an inheritance, you do not keep alive any [that are] breathing;
17 Waangamizeni kabisa Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi, kama Bwana Mungu wenu alivyowaamuru.
for you certainly devote the Hittite, and the Amorite, the Canaanite, and the Perizzite, the Hivite, and the Jebusite, as your God YHWH has commanded you,
18 La sivyo, watawafundisha kufuata mambo yote ya machukizo wanayofanya wakiabudu miungu yao, nanyi mtatenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wenu.
so that they do not teach you to do according to all their abominations which they have done for their gods, and you have sinned against your God YHWH.
19 Wakati mtakapouzunguka mji kwa vita kwa muda mrefu, mkipigana dhidi yake ili kuuteka, msiharibu miti yake kwa kuikata kwa shoka, kwa sababu mtaweza kula matunda yake. Hivyo msiikate. Je, miti hiyo ya mashambani ni watu, hata muizingire?
When you lay siege to a city [for] many days to fight against it, to capture it, you do not destroy its trees to force an axe against them, for you eat of them, and you do not cut them down—for the tree of the field [is] man’s—to go in at your presence in the siege.
20 Hata hivyo, mnaweza kuikata miti ambayo sio miti ya matunda na kuitumia kujenga ngome, mpaka mji ulio katika vita na ninyi utakapoanguka.
Only, the tree of which you know that it [is] not a fruit-tree, you destroy it, and have cut [it] down, and have built a bulwark against the city which is making war with you until you have subdued it.”

< Torati 20 >