< Torati 2 >

1 Kisha tukageuka nyuma na kusafiri kuelekea jangwani kwa njia inayoelekea Bahari ya Shamu, kama Bwana alivyonielekeza. Kwa muda mrefu tulitembea kuzunguka vilima katika nchi ya Seiri.
Akhirnya kita kembali ke padang gurun lewat jalan yang menuju ke Teluk Akaba, seperti yang diperintahkan TUHAN. Lama kita mengembara di daerah pegunungan Edom.
2 Kisha Bwana akaniambia,
Lalu TUHAN berkata kepada saya
3 “Umetembea kuzunguka hii nchi ya vilima kwa muda wa kutosha; sasa geukia kaskazini.
bahwa sudah cukup lama kita mengembara di daerah itu. Jadi kita harus pergi ke utara.
4 Wape watu maagizo haya: ‘Mko karibu kupita katikati ya nchi ya ndugu zako ambao ni wazao wa Esau, ambao wanaishi Seiri. Watawaogopa, lakini mwe waangalifu.
Kemudian TUHAN menyuruh saya memberi petunjuk-petunjuk ini kepadamu, 'Tidak lama lagi kamu akan memasuki negeri Edom, daerah saudara-saudaramu, keturunan Esau. Mereka akan takut kepadamu,
5 Msiwachokoze kwa vita kwa maana sitawapa ninyi sehemu yoyote ya nchi yao, hata sehemu ya kutosha kuweka wayo wenu juu yake. Nimempa Esau nchi ya vilima ya Seiri kama yake mwenyewe.
tetapi kamu tak boleh menyerang mereka, sebab dari tanah mereka sedikit pun tak akan Kuberikan kepadamu, karena daerah Edom sudah Kuberikan kepada keturunan Esau.
6 Mtawalipa fedha kwa chakula mtakachokula na maji mtakayokunywa.’”
Kamu boleh membeli makanan dan minuman dari mereka.'
7 Bwana Mungu wenu amewabariki kwa kazi yote ya mikono yenu. Amewalinda katika safari yenu katikati ya jangwa hili kubwa. Kwa miaka hii arobaini Bwana Mungu wenu amekuwa pamoja nanyi, na hamkupungukiwa na kitu chochote.
Ingatlah bagaimana TUHAN Allahmu telah memberkati kamu dalam segala yang kamu lakukan. Ia memelihara kamu selama kamu mengembara di padang gurun yang luas ini. Ia melindungi kamu selama empat puluh tahun ini dan memberi segala yang kamu perlukan.
8 Basi tulipita kwa ndugu zetu wazao wa Esau ambao wanaishi Seiri. Tuligeuka kutoka njia ya Araba ambayo inatokea Elathi na Esion-Geberi, tukasafiri kufuata njia ya jangwa la Moabu.
Kemudian kita berjalan terus, meninggalkan jalan yang melalui kota-kota Elat dan Ezion-Geber menuju ke Laut Mati, lalu belok ke timur laut menuju Gurun Moab.
9 Kisha Bwana akaniambia, “Usiwasumbue Wamoabu kwa vita, kwa kuwa sitawapa sehemu yoyote ya nchi yao. Nimetoa nchi ya Ari kwa wazao wa Loti kama milki yao.”
TUHAN berkata kepada saya, 'Orang Moab, keturunan Lot, tak boleh kamu ganggu. Jangan juga menyerang mereka. Negeri Ar telah Kuberikan kepada mereka dan dari tanah mereka sedikit pun tak akan Kuberikan kepadamu.'"
10 (Waemi walikuwa wakiishi huko hapo zamani, watu wenye nguvu na wengi, warefu kama Waanaki.
(Dahulu Ar didiami oleh orang Emim. Mereka besar perawakannya, sama dengan orang Enak, juga bangsa raksasa.
11 Kama walivyokuwa Waanaki, hao pia walikuwa kama Warefai, lakini Wamoabu waliwaita Waemi.
Seperti orang Enak, mereka juga disebut orang Refaim, akan tetapi orang Moab menamakan mereka orang Emim.
12 Wahori waliishi Seiri, lakini wazao wa Esau waliwafukuza. Waliwaangamiza Wahori na kukaa mahali pao, kama Waisraeli walivyofanya katika nchi ambayo Bwana aliwapa kama milki yao.)
Dahulu orang Hori tinggal di Edom, tetapi diusir dan dimusnahkan oleh keturunan Esau, yang kemudian menduduki tanah mereka; begitu juga bangsa Israel di kemudian hari mengusir musuh-musuhnya dari tanah yang diberikan TUHAN kepada mereka.)
13 Bwana akasema, “Sasa ondokeni mvuke Bonde la Zeredi.” Hivyo tukavuka bonde.
"Kemudian kita menyeberangi Sungai Zered seperti yang diperintahkan TUHAN kepada kita.
14 Miaka thelathini na minane ilipita tangu wakati tulipoondoka Kadesh-Barnea mpaka tulipovuka Bonde la Zeredi. Kwa wakati huo kile kizazi chote cha wanaume kuanzia wale wawezao kwenda vitani kilikuwa kimekufa, kama Bwana alivyokuwa amewaapia.
Itu terjadi tiga puluh delapan tahun sesudah kita meninggalkan Kades-Barnea. Semua prajurit dari angkatan itu sudah mati seperti yang dikatakan TUHAN.
15 Mkono wa Bwana uliwakabili hadi alipowaangamiza wote huko kambini.
TUHAN terus-menerus melawan mereka sampai akhirnya mereka semua binasa.
16 Ikawa baada ya mtu wa mwisho kuanzia wale wawezao kwenda vitani kufa,
Sesudah mereka semua mati,
17 Bwana akaniambia,
TUHAN berkata kepada kita,
18 “Leo utapita katika nchi ya Moabu huko Ari.
'Hari ini kamu melalui daerah Moab, lewat negeri Ar.
19 Utakapokuja kwa Waamoni, msiwasumbue wala kuwachokoza kwa vita, kwa kuwa sitawapa ardhi yoyote iliyo ya Waamoni kuwa milki yenu. Nimeitoa kama milki ya wazao wa Loti.”
Maka kamu sampai ke dekat tanah orang Amon, keturunan Lot. Janganlah mengganggu atau menyerang mereka, sebab dari tanah yang sudah Kuberikan kepada mereka, sedikit pun tak ada yang akan Kuberikan kepadamu.'"
20 (Hiyo pia ilidhaniwa kuwa nchi ya Warefai waliokuwa wakiishi huko, lakini Waamoni waliwaita Wazamzumi.
(Daerah itu juga terkenal sebagai negeri Refaim, nama bangsa yang dahulu tinggal di situ; oleh orang Amon mereka dinamakan orang Zamzumim.
21 Walikuwa watu wenye nguvu na wengi, warefu kama Waanaki. Bwana akawaangamiza kutoka mbele ya Waamoni, ambao waliwafukuza na kukaa mahali pao.
Seperti orang Enak, mereka juga besar perawakannya. Mereka sangat kuat, dan jumlahnya banyak. Tetapi TUHAN membinasakan mereka, sehingga orang Amon merebut tanah itu, lalu berdiam di situ.
22 Bwana alikuwa amefanya vivyo hivyo kwa wazao wa Esau, ambao waliishi Seiri, wakati alipowaangamiza Wahori watoke mbele yao. Waliwafukuza na wao wakaishi mahali pao mpaka leo.
Begitu juga dilakukan TUHAN untuk orang Edom, keturunan Esau, yang mendiami daerah pegunungan Edom. TUHAN membinasakan orang Hori, sehingga orang Edom merebut tanah itu dan mendudukinya, lalu menetap di situ sampai sekarang.
23 Nao Waavi ambao waliishi katika vijiji mpaka Gaza, Wakaftori waliokuja kutoka Kaftori waliwaangamiza na kukaa mahali pao.)
Tanah di sepanjang pantai Laut Tengah diduduki orang-orang dari pulau Kreta. Mereka telah membinasakan orang Awi, penduduk asli tanah itu, lalu menduduki daerah itu sampai ke selatan sejauh kota Gaza.)
24 “Ondoka sasa na uvuke Bonde la Arnoni. Tazama, nimemweka mikononi mwako Sihoni Mwamori, mfalme wa Heshboni na nchi yake. Anza kuimiliki nchi hiyo na umwingize katika vita.
"Sesudah kita melewati daerah Moab, TUHAN berkata kepada kita, 'Pergilah sekarang menyeberangi Sungai Arnon. Aku akan menyerahkan kepadamu Sihon, raja Amori yang memerintah di Hesybon, bersama-sama dengan negerinya. Seranglah dia, lalu dudukilah tanahnya.
25 Siku hii ya leo nitaanza kuwatia hofu na woga mataifa yote chini ya mbingu wawaogope ninyi. Watakaposikia taarifa zenu, watatetemeka na kufadhaika kwa sababu yenu.”
Mulai hari ini Aku akan membuat kamu ditakuti bangsa-bangsa di mana saja. Setiap orang akan gemetar ketakutan bila mendengar tentang kamu.'"
26 Kutoka jangwa la Kedemothi nilituma wajumbe wenye maneno ya amani kwa Sihoni mfalme wa Heshboni kusema,
"Kemudian saya mengirim beberapa utusan dari padang gurun Kedemot kepada Raja Sihon dari Hesybon untuk menyampaikan usul perdamaian ini:
27 “Turuhusu tupite katika nchi yako. Tutapita katika barabara kuu, hatutageuka kuume wala kushoto.
'Izinkan kami melalui negeri Tuanku. Kami akan berjalan terus dan tidak menyimpang dari jalan raya.
28 Tuuzie chakula tule na maji tunywe kwa thamani yake katika fedha. Turuhusu tu tupite kwa miguu,
Kami akan membayar makanan yang kami makan dan air yang kami minum. Kami hanya perlu melalui negeri ini,
29 kama wazao wa Esau ambao wanaishi Seiri na Wamoabu ambao wanaishi Ari walivyotufanyia, mpaka tuvuke Yordani kuingia nchi ambayo Bwana Mungu wetu anatupatia.”
sampai kami menyeberangi Sungai Yordan untuk masuk ke negeri yang diberikan TUHAN Allah kami kepada kami. Keturunan Esau yang tinggal di Edom dan orang Moab yang tinggal di Ar juga sudah mengizinkan kami melalui daerah mereka.'
30 Lakini Sihoni mfalme wa Heshboni alikataa kuturuhusu kupita. Kwa kuwa Bwana Mungu wako alikuwa ameifanya roho yake kuwa ngumu na moyo wake kuwa mkaidi ili amweke kwenye mikono yenu, kama alivyofanya sasa.
Tetapi Raja Sihon tidak mengizinkan kita melalui negerinya itu. TUHAN Allahmu membuat dia keras kepala dan nekat supaya kita dapat mengalahkan dia. Daerahnya masih kita duduki sampai sekarang.
31 Bwana akaniambia, “Tazama, nimeanza kuwapa Mfalme Sihoni na nchi yake kwako. Sasa anzeni kuishinda na kuimiliki nchi yake.”
Kemudian TUHAN berkata kepada saya, 'Raja Sihon dan negerinya Kuserahkan kepadamu; ambillah dan dudukilah negeri itu.'
32 Wakati Sihoni pamoja na jeshi lake lote walipokuja kukutana nasi katika vita huko Yahazi,
Maka datanglah Sihon dengan seluruh pasukannya untuk memerangi kita dekat kota Yahas.
33 Bwana Mungu wetu alimweka mikononi mwetu, nasi tukamwangamiza pamoja na wanawe na jeshi lake lote.
Tetapi TUHAN Allah kita menyerahkan dia kepada kita, lalu kita mengalahkan dia beserta anak-anaknya dan seluruh tentaranya.
34 Kwa wakati ule tuliteka miji yake yote na kuiangamiza kabisa: wanaume, wanawake na watoto. Hatukumwacha yeyote.
Pada waktu itu juga kita rebut dan hancurkan setiap kota, dan bunuh seluruh penduduknya, laki-laki, perempuan, dan anak-anak. Tak ada yang dibiarkan hidup.
35 Lakini mifugo na nyara tulizoziteka kutoka ile miji tulijichukulia wenyewe.
Ternak mereka kita ambil dan kota-kotanya kita rampasi.
36 Kutoka Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kutoka mji ulio ndani ya bonde, hata mpaka Gileadi, hapakuwa na mji hata mmoja uliokuwa na nguvu kutushinda. Bwana Mungu wetu alitupa yote.
Dengan pertolongan TUHAN Allah kita, kita dapat merebut semua kota itu, mulai dari Aroer, di ujung Lembah Arnon, dan kota di tengah lembah itu, sampai ke daerah Gilead. Tak ada kota yang temboknya terlalu kuat bagi kita.
37 Lakini kulingana na amri ya Bwana Mungu wetu, hamkujiingiza katika nchi yoyote ya Waamoni, wala katika sehemu yoyote iliyo kandokando ya Mto Yaboki, wala katika miji iliyoko katika vilima.
Tetapi kita tidak mendekati daerah orang Amon atau tepi Sungai Yabok atau kota-kota di daerah pegunungan atau tempat lain mana pun yang dilarang TUHAN Allah kita."

< Torati 2 >