< Torati 2 >

1 Kisha tukageuka nyuma na kusafiri kuelekea jangwani kwa njia inayoelekea Bahari ya Shamu, kama Bwana alivyonielekeza. Kwa muda mrefu tulitembea kuzunguka vilima katika nchi ya Seiri.
Alors nous retournâmes en arrière, et nous allâmes, au désert par le chemin de la mer Rouge, comme l'Eternel m'avait dit, et nous tournoyâmes longtemps près de la montagne de Séhir.
2 Kisha Bwana akaniambia,
Et l'Eternel parla à moi, en disant:
3 “Umetembea kuzunguka hii nchi ya vilima kwa muda wa kutosha; sasa geukia kaskazini.
Vous avez assez tournoyé près de cette montagne, tournez-vous vers le Septentrion.
4 Wape watu maagizo haya: ‘Mko karibu kupita katikati ya nchi ya ndugu zako ambao ni wazao wa Esau, ambao wanaishi Seiri. Watawaogopa, lakini mwe waangalifu.
Et commande au peuple, en disant: Vous allez passer la frontière de vos frères, les enfants d'Esaü qui demeurent en Séhir, et ils auront peur de vous, mais soyez bien sur vos gardes.
5 Msiwachokoze kwa vita kwa maana sitawapa ninyi sehemu yoyote ya nchi yao, hata sehemu ya kutosha kuweka wayo wenu juu yake. Nimempa Esau nchi ya vilima ya Seiri kama yake mwenyewe.
N'ayez point de démêlé avec eux; car je ne vous donnerai rien de leur pays, non pas même pour y pouvoir asseoir la plante du pied, parce que j'ai donné à Esaü la montagne de Séhir en héritage.
6 Mtawalipa fedha kwa chakula mtakachokula na maji mtakayokunywa.’”
Vous achèterez d'eux les vivres à prix d'argent, et vous en mangerez; vous achèterez aussi d'eux l'eau à prix d'argent, et vous en boirez.
7 Bwana Mungu wenu amewabariki kwa kazi yote ya mikono yenu. Amewalinda katika safari yenu katikati ya jangwa hili kubwa. Kwa miaka hii arobaini Bwana Mungu wenu amekuwa pamoja nanyi, na hamkupungukiwa na kitu chochote.
Car l'Eternel ton Dieu t'a béni dans tout le travail de tes mains; il a connu le chemin que tu as tenu dans ce grand désert, [et] l'Eternel ton Dieu a été avec toi pendant ces quarante ans, [et] rien ne t'a manqué.
8 Basi tulipita kwa ndugu zetu wazao wa Esau ambao wanaishi Seiri. Tuligeuka kutoka njia ya Araba ambayo inatokea Elathi na Esion-Geberi, tukasafiri kufuata njia ya jangwa la Moabu.
Or nous nous détournâmes de nos frères les enfants d'Esaü, qui demeuraient en Séhir, depuis le chemin de la campagne, depuis Elath, et depuis Hetsjonguéber; et [de là] nous nous détournâmes et nous passâmes par le chemin du désert de Moab.
9 Kisha Bwana akaniambia, “Usiwasumbue Wamoabu kwa vita, kwa kuwa sitawapa sehemu yoyote ya nchi yao. Nimetoa nchi ya Ari kwa wazao wa Loti kama milki yao.”
Et l'Eternel me dit: Ne traitez point les Moabites en ennemis, et n'entrez point en guerre avec eux; car je ne te donnerai rien de leur pays en héritage; parce que j'ai donné Har en héritage aux enfants de Lot.
10 (Waemi walikuwa wakiishi huko hapo zamani, watu wenye nguvu na wengi, warefu kama Waanaki.
Les Emins y habitaient auparavant; c'était un grand peuple, et en grand nombre, et de haute stature comme les Hanakins.
11 Kama walivyokuwa Waanaki, hao pia walikuwa kama Warefai, lakini Wamoabu waliwaita Waemi.
Et en effet ils ont été réputés pour Réphaïms comme les Hanakins, et les Moabites les appelaient Emins.
12 Wahori waliishi Seiri, lakini wazao wa Esau waliwafukuza. Waliwaangamiza Wahori na kukaa mahali pao, kama Waisraeli walivyofanya katika nchi ambayo Bwana aliwapa kama milki yao.)
Les Horiens demeuraient aussi auparavant en Séhir, mais les enfants d'Esaü les en dépossédèrent, et les détruisirent de devant eux, et ils y habitèrent en leur place, ainsi qu'a fait Israël dans le pays de son héritage que l'Eternel lui a donné.
13 Bwana akasema, “Sasa ondokeni mvuke Bonde la Zeredi.” Hivyo tukavuka bonde.
[Mais] maintenant levez-vous, et passez le torrent de Zéred; et nous passâmes le torrent de Zéred.
14 Miaka thelathini na minane ilipita tangu wakati tulipoondoka Kadesh-Barnea mpaka tulipovuka Bonde la Zeredi. Kwa wakati huo kile kizazi chote cha wanaume kuanzia wale wawezao kwenda vitani kilikuwa kimekufa, kama Bwana alivyokuwa amewaapia.
Or le temps que nous avons marché depuis Kadès-barné, jusqu'à ce que nous avons eu passé le torrent de Zéred, a été de trente et huit ans, jusqu'à ce que toute cette génération-là, [savoir] les gens de guerre, a été consumée du milieu du camp, comme l'Eternel le leur avait juré.
15 Mkono wa Bwana uliwakabili hadi alipowaangamiza wote huko kambini.
Aussi la main de l'Eternel a été contr'eux pour les détruire du milieu du camp, jusqu'à ce qu'il les ait consumés.
16 Ikawa baada ya mtu wa mwisho kuanzia wale wawezao kwenda vitani kufa,
Or il est arrivé qu'après que tous les hommes de guerre d'entre le peuple ont été consumés par la mort;
17 Bwana akaniambia,
L'Eternel m'a parlé et m'a dit:
18 “Leo utapita katika nchi ya Moabu huko Ari.
Tu vas passer aujourd'hui la frontière de Moab, [savoir] Har.
19 Utakapokuja kwa Waamoni, msiwasumbue wala kuwachokoza kwa vita, kwa kuwa sitawapa ardhi yoyote iliyo ya Waamoni kuwa milki yenu. Nimeitoa kama milki ya wazao wa Loti.”
Tu approcheras vis à vis des enfants de Hammon; tu ne les traiteras point en ennemis, et tu n'auras point de démêlé avec eux; car je ne te donnerai rien du pays des enfants de Hammon en héritage, parce que je l'ai donné en héritage aux enfants de Lot.
20 (Hiyo pia ilidhaniwa kuwa nchi ya Warefai waliokuwa wakiishi huko, lakini Waamoni waliwaita Wazamzumi.
Ce [pays] aussi a été réputé pays des Réphaïms; [car] les Réphaïms y habitaient auparavant, et les Hammonites les appelaient Zamzummins;
21 Walikuwa watu wenye nguvu na wengi, warefu kama Waanaki. Bwana akawaangamiza kutoka mbele ya Waamoni, ambao waliwafukuza na kukaa mahali pao.
Qui étaient un peuple grand et nombreux, et de haute stature comme les Hanakins, mais l'Eternel les fit détruire de devant eux, et ils les dépossédèrent, et [y] habitèrent en leur place.
22 Bwana alikuwa amefanya vivyo hivyo kwa wazao wa Esau, ambao waliishi Seiri, wakati alipowaangamiza Wahori watoke mbele yao. Waliwafukuza na wao wakaishi mahali pao mpaka leo.
Comme il avait fait aux enfants d'Esaü qui demeuraient en Séhir, quand il fit détruire les Horiens de devant eux; et ainsi ils les dépossédèrent, et y habitèrent en leur place jusqu'à ce jour.
23 Nao Waavi ambao waliishi katika vijiji mpaka Gaza, Wakaftori waliokuja kutoka Kaftori waliwaangamiza na kukaa mahali pao.)
Or quant aux Hauviens, qui demeuraient en Hatsérim, jusqu'à Gaza, ils furent détruits par les Caphtorins, qui étant sortis de Caphtor, vinrent demeurer en leur place.
24 “Ondoka sasa na uvuke Bonde la Arnoni. Tazama, nimemweka mikononi mwako Sihoni Mwamori, mfalme wa Heshboni na nchi yake. Anza kuimiliki nchi hiyo na umwingize katika vita.
[L'Eternel dit aussi]: Levez-vous, et partez, et passez le torrent d'Arnon; Regarde, j'ai livré entre tes mains Sihon, Roi de Hesbon Amorrhéen, avec son pays, commence d'en prendre possession, et fais-lui la guerre.
25 Siku hii ya leo nitaanza kuwatia hofu na woga mataifa yote chini ya mbingu wawaogope ninyi. Watakaposikia taarifa zenu, watatetemeka na kufadhaika kwa sababu yenu.”
Je commencerai aujourd'hui à jeter la frayeur et la peur de toi sur les peuples qui sont sous tous les cieux, car ayant ouï parler de toi ils trembleront, et seront en angoisse à cause de ta présence.
26 Kutoka jangwa la Kedemothi nilituma wajumbe wenye maneno ya amani kwa Sihoni mfalme wa Heshboni kusema,
Alors j'envoyai du désert de Kédémoth des messagers à Sihon, Roi de Hesbon, avec des paroles de paix, disant:
27 “Turuhusu tupite katika nchi yako. Tutapita katika barabara kuu, hatutageuka kuume wala kushoto.
Que je passe par ton pays et j'irai par le grand chemin, sans me détourner ni à droite ni à gauche.
28 Tuuzie chakula tule na maji tunywe kwa thamani yake katika fedha. Turuhusu tu tupite kwa miguu,
Tu me feras distribuer des vivres pour de l'argent, afin que je mange; tu me donneras de l'eau pour de l'argent, afin que je boive; seulement que j'y passe de mes pieds.
29 kama wazao wa Esau ambao wanaishi Seiri na Wamoabu ambao wanaishi Ari walivyotufanyia, mpaka tuvuke Yordani kuingia nchi ambayo Bwana Mungu wetu anatupatia.”
Ainsi que m'ont fait les enfants d'Esaü qui demeurent en Séhir, les Moabites qui demeurent à Har, jusqu'à ce que je passe le Jourdain pour entrer au pays que l'Eternel notre Dieu, nous donne.
30 Lakini Sihoni mfalme wa Heshboni alikataa kuturuhusu kupita. Kwa kuwa Bwana Mungu wako alikuwa ameifanya roho yake kuwa ngumu na moyo wake kuwa mkaidi ili amweke kwenye mikono yenu, kama alivyofanya sasa.
Mais Sihon, Roi de Hesbon, ne voulut point nous laisser passer par son pays, car l'Eternel ton Dieu avait endurci son esprit, et roidi son cœur, afin de le livrer entre tes mains, comme [il paraît] aujourd'hui.
31 Bwana akaniambia, “Tazama, nimeanza kuwapa Mfalme Sihoni na nchi yake kwako. Sasa anzeni kuishinda na kuimiliki nchi yake.”
Et l'Eternel me dit: Regarde, j'ai commencé de te livrer Sihon avec son pays; commence à posséder son pays, pour le tenir en héritage.
32 Wakati Sihoni pamoja na jeshi lake lote walipokuja kukutana nasi katika vita huko Yahazi,
Sihon donc sortit contre nous, lui et tout son peuple pour combattre en Jahats.
33 Bwana Mungu wetu alimweka mikononi mwetu, nasi tukamwangamiza pamoja na wanawe na jeshi lake lote.
Mais l'Eternel notre Dieu nous le livra, et nous le battîmes, lui, ses enfants, et tout son peuple.
34 Kwa wakati ule tuliteka miji yake yote na kuiangamiza kabisa: wanaume, wanawake na watoto. Hatukumwacha yeyote.
Et en ce temps-là nous prîmes toutes ses villes; et nous détruisîmes à la façon de l'interdit toutes les villes où étaient les hommes, les femmes, et les petits enfants, et nous n'y laissâmes personne de reste.
35 Lakini mifugo na nyara tulizoziteka kutoka ile miji tulijichukulia wenyewe.
Seulement nous pillâmes les bêtes pour nous, et le butin des villes que nous avions prises.
36 Kutoka Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kutoka mji ulio ndani ya bonde, hata mpaka Gileadi, hapakuwa na mji hata mmoja uliokuwa na nguvu kutushinda. Bwana Mungu wetu alitupa yote.
Depuis Haroher, qui est sur le bord du torrent d'Arnon, et la ville qui est dans le torrent, jusqu'en Galaad, il n'y eut pas une ville qui pût se garantir de nous; l'Eternel notre Dieu nous les livra toutes.
37 Lakini kulingana na amri ya Bwana Mungu wetu, hamkujiingiza katika nchi yoyote ya Waamoni, wala katika sehemu yoyote iliyo kandokando ya Mto Yaboki, wala katika miji iliyoko katika vilima.
Seulement tu ne t'es point approché du pays des enfants de Hammon, ni d'aucun endroit qui touche le torrent de Jabbok, ni des villes de la montagne, ni d'aucun [lieu] que l'Eternel notre Dieu nous eût défendu [de conquérir].

< Torati 2 >