< Torati 2 >

1 Kisha tukageuka nyuma na kusafiri kuelekea jangwani kwa njia inayoelekea Bahari ya Shamu, kama Bwana alivyonielekeza. Kwa muda mrefu tulitembea kuzunguka vilima katika nchi ya Seiri.
Then we turned, and took our journey into the wilderness by the way of the Red sea, as the LORD spoke to me: and we compassed mount Seir many days.
2 Kisha Bwana akaniambia,
And the LORD spoke to me, saying,
3 “Umetembea kuzunguka hii nchi ya vilima kwa muda wa kutosha; sasa geukia kaskazini.
Ye have compassed this mountain long enough: turn you northward.
4 Wape watu maagizo haya: ‘Mko karibu kupita katikati ya nchi ya ndugu zako ambao ni wazao wa Esau, ambao wanaishi Seiri. Watawaogopa, lakini mwe waangalifu.
And command thou the people, saying, Ye [are] to pass through the border of your brethren the children of Esau, who dwell in Seir; and they will be afraid of you: therefore take ye good heed to yourselves:
5 Msiwachokoze kwa vita kwa maana sitawapa ninyi sehemu yoyote ya nchi yao, hata sehemu ya kutosha kuweka wayo wenu juu yake. Nimempa Esau nchi ya vilima ya Seiri kama yake mwenyewe.
Meddle not with them; for I will not give you of their land, no, not so much as a foot-breadth; because I have given mount Seir to Esau [for] a possession.
6 Mtawalipa fedha kwa chakula mtakachokula na maji mtakayokunywa.’”
Ye shall buy food of them for money, that ye may eat; and ye shall also buy water of them for money, that ye may drink.
7 Bwana Mungu wenu amewabariki kwa kazi yote ya mikono yenu. Amewalinda katika safari yenu katikati ya jangwa hili kubwa. Kwa miaka hii arobaini Bwana Mungu wenu amekuwa pamoja nanyi, na hamkupungukiwa na kitu chochote.
For the LORD thy God hath blessed thee in all the works of thy hand: he knoweth thy walking through this great wilderness: these forty years the LORD thy God [hath been] with thee: thou hast lacked nothing.
8 Basi tulipita kwa ndugu zetu wazao wa Esau ambao wanaishi Seiri. Tuligeuka kutoka njia ya Araba ambayo inatokea Elathi na Esion-Geberi, tukasafiri kufuata njia ya jangwa la Moabu.
And when we passed by from our brethren the children of Esau, who dwelt in Seir, through the way of the plain from Elath, and from Ezion-gaber, we turned and passed by the way of the wilderness of Moab.
9 Kisha Bwana akaniambia, “Usiwasumbue Wamoabu kwa vita, kwa kuwa sitawapa sehemu yoyote ya nchi yao. Nimetoa nchi ya Ari kwa wazao wa Loti kama milki yao.”
And the LORD said to me, Distress not the Moabites, neither contend with them in battle: for I will not give thee of their land [for] a possession; because I have given Ar to the children of Lot [for] a possession.
10 (Waemi walikuwa wakiishi huko hapo zamani, watu wenye nguvu na wengi, warefu kama Waanaki.
(The Emims dwelt in it in times past, a people great, and many, and tall as the Anakims;
11 Kama walivyokuwa Waanaki, hao pia walikuwa kama Warefai, lakini Wamoabu waliwaita Waemi.
Who also were accounted giants, as the Anakims; but the Moabites call them Emims.
12 Wahori waliishi Seiri, lakini wazao wa Esau waliwafukuza. Waliwaangamiza Wahori na kukaa mahali pao, kama Waisraeli walivyofanya katika nchi ambayo Bwana aliwapa kama milki yao.)
The Horims also dwelt formerly in Seir, but the children of Esau succeeded them, when they had destroyed them from before them, and dwelt in their stead; as Israel did to the land of his possession, which the LORD gave to them.)
13 Bwana akasema, “Sasa ondokeni mvuke Bonde la Zeredi.” Hivyo tukavuka bonde.
Now rise, [said I], and pass over the brook Zered: and we went over the brook Zered.
14 Miaka thelathini na minane ilipita tangu wakati tulipoondoka Kadesh-Barnea mpaka tulipovuka Bonde la Zeredi. Kwa wakati huo kile kizazi chote cha wanaume kuanzia wale wawezao kwenda vitani kilikuwa kimekufa, kama Bwana alivyokuwa amewaapia.
And the space in which we came from Kadesh-barnea, until we passed the brook Zered, [was] thirty and eight years; until all the generation of the men of war were wasted from among the host, as the LORD swore to them.
15 Mkono wa Bwana uliwakabili hadi alipowaangamiza wote huko kambini.
For indeed the hand of the LORD was against them, to destroy them from among the host, until they were consumed.
16 Ikawa baada ya mtu wa mwisho kuanzia wale wawezao kwenda vitani kufa,
So it came to pass, when all the men of war were consumed and dead from among the people,
17 Bwana akaniambia,
That the LORD spoke to me, saying,
18 “Leo utapita katika nchi ya Moabu huko Ari.
Thou art to pass over through Ar, the coast of Moab, this day:
19 Utakapokuja kwa Waamoni, msiwasumbue wala kuwachokoza kwa vita, kwa kuwa sitawapa ardhi yoyote iliyo ya Waamoni kuwa milki yenu. Nimeitoa kama milki ya wazao wa Loti.”
And [when] thou comest nigh over against the children of Ammon, distress them not, nor meddle with them: for I will not give thee of the land of the children of Ammon [any] possession; because I have given it to the children of Lot [for] a possession.
20 (Hiyo pia ilidhaniwa kuwa nchi ya Warefai waliokuwa wakiishi huko, lakini Waamoni waliwaita Wazamzumi.
(That also was accounted a land of giants: giants dwelt in it in old time; and the Ammonites call them Zamzummims;
21 Walikuwa watu wenye nguvu na wengi, warefu kama Waanaki. Bwana akawaangamiza kutoka mbele ya Waamoni, ambao waliwafukuza na kukaa mahali pao.
A people great, and many, and tall as the Anakims; but the LORD destroyed them before them; and they succeeded them, and dwelt in their stead:
22 Bwana alikuwa amefanya vivyo hivyo kwa wazao wa Esau, ambao waliishi Seiri, wakati alipowaangamiza Wahori watoke mbele yao. Waliwafukuza na wao wakaishi mahali pao mpaka leo.
As he did to the children of Esau, who dwelt in Seir, when he destroyed the Horims from before them; and they succeeded them, and dwelt in their stead even to this day:
23 Nao Waavi ambao waliishi katika vijiji mpaka Gaza, Wakaftori waliokuja kutoka Kaftori waliwaangamiza na kukaa mahali pao.)
And the Avims who dwelt in Hazerim [even] to Azzah, the Caphtorims, who came forth from Caphtor, destroyed them, and dwelt in their stead.)
24 “Ondoka sasa na uvuke Bonde la Arnoni. Tazama, nimemweka mikononi mwako Sihoni Mwamori, mfalme wa Heshboni na nchi yake. Anza kuimiliki nchi hiyo na umwingize katika vita.
Arise ye, take your journey, and pass over the river Arnon: behold, I have given into thy hand Sihon the Amorite, king of Heshbon, and his land: begin to possess [it], and contend with him in battle.
25 Siku hii ya leo nitaanza kuwatia hofu na woga mataifa yote chini ya mbingu wawaogope ninyi. Watakaposikia taarifa zenu, watatetemeka na kufadhaika kwa sababu yenu.”
This day will I begin to put the dread of thee and the fear of thee upon the nations [that are] under the whole heaven, who shall hear report of thee, and shall tremble, and be in anguish because of thee.
26 Kutoka jangwa la Kedemothi nilituma wajumbe wenye maneno ya amani kwa Sihoni mfalme wa Heshboni kusema,
And I sent messengers from the wilderness of Kedemoth to Sihon king of Heshbon with words of peace, saying,
27 “Turuhusu tupite katika nchi yako. Tutapita katika barabara kuu, hatutageuka kuume wala kushoto.
Let me pass through thy land: I will go along by the highway, I will neither turn to the right hand nor to the left.
28 Tuuzie chakula tule na maji tunywe kwa thamani yake katika fedha. Turuhusu tu tupite kwa miguu,
Thou shalt sell me food for money, that I may eat; and give me water for money, that I may drink: only I will pass through on my feet;
29 kama wazao wa Esau ambao wanaishi Seiri na Wamoabu ambao wanaishi Ari walivyotufanyia, mpaka tuvuke Yordani kuingia nchi ambayo Bwana Mungu wetu anatupatia.”
(As the children of Esau who dwell in Seir, and the Moabites who dwell in Ar, did to me; ) until I shall pass over Jordan into the land which the LORD our God giveth us.
30 Lakini Sihoni mfalme wa Heshboni alikataa kuturuhusu kupita. Kwa kuwa Bwana Mungu wako alikuwa ameifanya roho yake kuwa ngumu na moyo wake kuwa mkaidi ili amweke kwenye mikono yenu, kama alivyofanya sasa.
But Sihon king of Heshbon would not let us pass by him: for the LORD thy God hardened his spirit, and made his heart obstinate, that he might deliver him into thy hand, as [appeareth] this day.
31 Bwana akaniambia, “Tazama, nimeanza kuwapa Mfalme Sihoni na nchi yake kwako. Sasa anzeni kuishinda na kuimiliki nchi yake.”
And the LORD said to me, Behold, I have begun to give Sihon and his land before thee: begin to possess, that thou mayest inherit his land.
32 Wakati Sihoni pamoja na jeshi lake lote walipokuja kukutana nasi katika vita huko Yahazi,
Then Sihon came out against us, he and all his people, to fight at Jahaz.
33 Bwana Mungu wetu alimweka mikononi mwetu, nasi tukamwangamiza pamoja na wanawe na jeshi lake lote.
And the LORD our God delivered him before us; and we smote him, and his sons, and all his people.
34 Kwa wakati ule tuliteka miji yake yote na kuiangamiza kabisa: wanaume, wanawake na watoto. Hatukumwacha yeyote.
And we took all his cities at that time, and utterly destroyed the men, and the women, and the little ones of every city, we left none to remain.
35 Lakini mifugo na nyara tulizoziteka kutoka ile miji tulijichukulia wenyewe.
Only the cattle we took for a prey to ourselves, and the spoil of the cities which we took.
36 Kutoka Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kutoka mji ulio ndani ya bonde, hata mpaka Gileadi, hapakuwa na mji hata mmoja uliokuwa na nguvu kutushinda. Bwana Mungu wetu alitupa yote.
From Aroer, which [is] by the brink of the river of Arnon, and [from] the city that [is] by the river, even to Gilead, there was not one city too strong for us: the LORD our God delivered all to us:
37 Lakini kulingana na amri ya Bwana Mungu wetu, hamkujiingiza katika nchi yoyote ya Waamoni, wala katika sehemu yoyote iliyo kandokando ya Mto Yaboki, wala katika miji iliyoko katika vilima.
Only to the land of the children of Ammon thou camest not, [nor] to any place of the river Jabbok, nor to the cities on the mountains, nor to whatever the LORD our God forbad us.

< Torati 2 >