< Torati 19 >
1 Wakati Bwana Mungu wenu atakapokuwa amewaangamiza mataifa ambayo nchi yao anawapa ninyi, wakati mtakapokuwa mmewafukuza na kuishi katika miji yao na nyumba zao,
“When the Lord your God will have destroyed the nations, whose land he will deliver to you, and when you possess it and live in its cities and buildings,
2 ndipo mtenge miji mitatu iliyopo katikati ya nchi kwa ajili yenu, katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kuimiliki.
you shall separate for yourselves three cities in the midst of the land, which the Lord will give to you as a possession,
3 Jengeni barabara katika miji hiyo na kuigawa mara tatu, nchi anayowapa Bwana Mungu wenu kama urithi, ili kwamba yeyote amuuaye mtu aweze kukimbilia humo.
paving the road carefully. And you shall divide the entire province of your land equally into three parts, so that he who is forced to flee because of manslaughter may have a place nearby to which he may be able to escape.
4 Hii ndiyo kanuni kuhusu mtu amuuaye mwingine na kukimbilia humo kuokoa maisha yake, yaani, yeye amuuaye jirani yake bila kukusudia, wala hakumchukia kabla ya hapo.
This shall be the law of the killer who flees, whose life is to be saved. Whoever strikes down his neighbor unwillingly, and who has been proven to have had no hatred against him yesterday and the day before,
5 Kwa mfano, mtu aweza kwenda msituni na jirani yake kukata miti, naye anapozungusha shoka kuangusha mti, shoka linaweza kuchomoka kutoka kwenye mpini na kumpiga jirani yake na kumuua. Yule mtu anaweza kukimbilia katika mmojawapo ya miji hii na kuokoa maisha yake.
such that he had gone with him into the forest simply to cut wood, and in cutting down the tree, the axe slipped from his hand, or the iron slipped from the handle, and it struck his friend and killed him: he shall flee to one of the cities stated above, and he shall live.
6 Kama sivyo, mlipiza kisasi cha damu anaweza kumfuatilia kwa hasira kali, naye akamkamata na kumuua kama umbali ni mrefu sana hata ingawa hastahili kifo, kwa sababu amemuua jirani yake bila kukusudia.
Otherwise, perhaps the near relative of him whose blood was shed, impelled by his grief, might pursue and apprehend him, unless the way is too long, and he might strike down the life of him who is not guilty unto death, since he had demonstrated that he had no prior hatred against him who was slain.
7 Hii ndiyo sababu nimewaagiza ninyi kutenga miji mitatu ya makimbilio kwa ajili yenu.
For this reason, I instruct you to separate three cities at equal distance from one another.
8 Kama Bwana Mungu wenu akipanua nchi yenu, kama alivyoahidi kwa kiapo kwa baba zenu na kuwapa nchi yote aliyowaahidi,
And when the Lord your God will have enlarged your borders, just as he swore to your fathers, and when he will have given to you all the land that he has promised to them,
9 kwa sababu mmefuata kwa uangalifu sheria zote ninazowaamuru leo, kumpenda Bwana Mungu wenu na kuenenda siku zote katika njia zake, ndipo mtenge miji mingine, mitatu zaidi.
(but this is only so if you will keep his commandments and do the things which I instruct to you this day, so that you love the Lord your God, and walk in his ways at all times) you shall add for yourselves three other cities, and so you shall double the number of the three cities stated above.
10 Fanyeni hivi ili damu isiyo na hatia isimwagwe katika nchi yenu, ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi wenu, ili kwamba msije mkawa na hatia ya kumwaga damu.
So may innocent blood not be shed in the midst of the land which the Lord your God will give you to possess, lest you be guilty of blood.
11 Lakini kama mtu anamchukia ndugu yake, akamvizia, akamshambulia na kumuua, kisha akakimbilia katika mmojawapo ya miji hii,
But if anyone, having hatred for his neighbor, will have lain in ambush for his life, and, rising up, will have struck him, and he will have died, and if he will have fled to one of the cities stated above,
12 wazee wa mji wake watatuma ujumbe kwake, kumleta kutoka mji ule na kumkabidhi mlipiza kisasi cha damu kumuua.
the elders of his city shall send, and they shall take him from the place of refuge, and they shall deliver him into the hand of the relative of him whose blood was shed, and he shall die.
13 Msimwonee huruma. Lazima mwondoe katika Israeli hatia ya umwagaji damu isiyo na hatia ili kwamba mpate kufanikiwa.
You shall not take pity on him, and so shall you take away the blood of the innocent from Israel, so that it may be well with you.
14 Usisogeze jiwe la mpaka wa jirani yako ambao uliwekwa na wale waliokutangulia katika urithi upokeao katika nchi Bwana Mungu wako anayowapa kuimiliki.
You shall not take up or move the landmark of your neighbor, which those before you have placed, in your possession that the Lord your God will give to you, in the land you will receive to possess.
15 Shahidi mmoja hatoshi kumtia hatiani mtu kwa uhalifu au kosa lolote ambalo anaweza kuwa amelitenda. Lazima shauri lolote lithibitishwe kwa ushuhuda wa mashahidi wawili au watatu.
One witness shall not stand against another, no matter what the sin or outrage may be. For every word shall stand by the mouth of two or three witnesses.
16 Kama shahidi mwenye nia ya kumdhuru mwingine akisimama kumshtaki mtu kwa uhalifu,
If a lying witness will have stood against a man, accusing him of a transgression,
17 watu wawili wanaohusika katika mabishano lazima wasimame mbele za Bwana na mbele ya makuhani na waamuzi ambao wako kazini wakati huo.
both of those whose case it is shall stand before the Lord in the sight of the priests and the judges who shall be in those days.
18 Waamuzi lazima wafanye uchunguzi kwa makini na shahidi akionekana kuwa ni mwongo, akitoa ushuhuda wa uongo dhidi ya ndugu yake,
And when, after a very diligent examination, they will have found that the false witness had told a lie against his brother,
19 basi mtende kama alivyotaka kumtendea ndugu yake. Ni lazima mwondoe uovu miongoni mwenu.
they shall render to him just as he intended to do to his brother. And so shall you take away the evil from your midst.
20 Watu watakaosalia watasikia hili na kuogopa, uovu kama huo kamwe hautatendeka tena miongoni mwenu.
Then the others, upon hearing this, will be afraid, and they will by no means dare to do such things.
21 Msionyeshe huruma, uhai kwa uhai, jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu.
You shall not take pity on him. Instead, you shall require a life for a life, an eye for an eye, a tooth for a tooth, a hand for a hand, a foot for a foot.”