< Torati 18 >
1 Makuhani ambao ni Walawi, yaani kabila lote la Lawi, hawatakuwa na mgawo wala urithi pamoja na Israeli. Wataishi kwa sadaka zitolewazo kwa ajili ya Bwana za kuteketezwa kwa moto, kwa maana huo ndio urithi wao.
Os sacerdotes e os levitas - toda a tribo de Levi - não terão parte nem herança com Israel. Eles comerão as ofertas de Yahweh feitas pelo fogo e sua porção.
2 Hawatakuwa na urithi miongoni mwa ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.
Eles não terão herança entre seus irmãos. Iavé é sua herança, como ele lhes falou.
3 Hili ndilo fungu la makuhani kutoka kwa watu watakaotoa dhabihu ya fahali au kondoo: mguu wa mbele, mataya na matumbo.
Isto será devido pelo povo, por aqueles que oferecem um sacrifício, seja boi ou ovelha, que darão ao sacerdote: o ombro, as duas bochechas e as partes internas.
4 Mtawapa malimbuko ya nafaka zenu, divai mpya, mafuta na sufu ya kwanza kutoka manyoya ya kondoo zenu,
Você lhe dará as primeiras frutas de seu grão, de seu novo vinho e de seu óleo, e a primeira do velo de suas ovelhas.
5 kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewachagua pamoja na wazao wao kutoka makabila yenu kusimama na kuhudumu katika jina la Bwana siku zote.
Pois Javé, vosso Deus, o escolheu dentre todas as vossas tribos para ficar em nome de Javé, ele e seus filhos para sempre.
6 Ikiwa Mlawi atahama kutoka mmojawapo ya miji yenu popote katika Israeli ambapo anaishi, akaja kwa moyo wote mahali ambapo Bwana atapachagua,
Se um levita vier de algum de seus portões de todo Israel onde vive, e vier com todo o desejo de sua alma para o lugar que Javé escolher,
7 anaweza akahudumu katika jina la Bwana Mungu wake kama Walawi wenzake wote wanaohudumu hapo mbele za Bwana.
então ele ministrará em nome de Javé seu Deus, como fazem todos os seus irmãos levitas, que estão ali diante de Javé.
8 Atashiriki sawa katika mafao yao, hata kama amepokea fedha kutoka mauzo ya mali ya jamaa yake.
eles terão como que porções para comer, além do que provém da venda de seus bens familiares.
9 Wakati mtakapoingia katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, msijifunze kuiga njia za machukizo za mataifa ya huko.
Quando tiverdes entrado na terra que Iavé vosso Deus vos dá, não aprendereis a imitar as abominações dessas nações.
10 Asionekane mtu yeyote miongoni mwenu ampitishaye mwanawe au binti yake katika moto, atakayefanya uaguzi, ulozi, anayetabiri nyakati, anayejishughulisha na uchawi,
Não será encontrado com você ninguém que faça seu filho ou sua filha passar pelo fogo, alguém que use adivinhação, alguém que conte fortunas, ou um encantador, ou um feiticeiro,
11 wala arogaye kwa kupiga mafundo, wala mwaguzi au anayeabudu mizimu, wala awaombaye wafu.
ou um encantador, ou alguém que consulte um espírito familiar, ou um feiticeiro, ou um necromante.
12 Mtu yeyote afanyaye mambo haya ni chukizo kwa Bwana, tena ni kwa sababu ya matendo haya ya kuchukiza wayafanyayo ndiyo maana Bwana Mungu wenu atayafukuza mataifa hayo mbele yenu.
Para quem faz estas coisas é uma abominação para Javé. Por causa destas abominações, Yahweh seu Deus as expulsa de diante de você.
13 Kamwe msilaumiwe mbele za Bwana Mungu wenu.
Você será irrepreensível com Iavé seu Deus.
14 Mataifa mtakayowafukuza husikiliza wale wafanyao ulozi na uaguzi. Lakini kwenu ninyi, Bwana Mungu wenu hajawaruhusu kufanya hivyo.
Para estas nações, que vós despojareis, escutai aqueles que praticam a feitiçaria e os adivinhadores; mas quanto a vós, Yavé vosso Deus não permitiu que o fizésseis.
15 Bwana Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu wenyewe. Msikilizeni yeye.
Javé, vosso Deus, vos levantará um profeta dentre vós, de vossos irmãos, como eu. Vocês o escutarão.
16 Kwa kuwa hivi ndivyo mlivyomwomba Bwana Mungu wenu kule Horebu siku ile ya kusanyiko, wakati mliposema, “Na tusiisikie sauti ya Bwana Mungu wetu, wala kuuona moto huu mkubwa tena, ama sivyo tutakufa.”
Isto é de acordo com tudo o que você desejou de Javé seu Deus em Horeb no dia da assembléia, dizendo: “Não me deixe ouvir novamente a voz de Javé meu Deus, nem me deixe ver mais este grande fogo, que eu não morra”.
17 Bwana akaniambia: “Wanachosema ni vyema.
Yahweh me disse: “Eles disseram bem o que falaram”.
18 Nitawainulia nabii kama wewe kutoka miongoni mwa ndugu zao; nitaweka maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia kila kitu nitakachomwamuru.
Eu os criarei um profeta entre seus irmãos, como você”. Colocarei minhas palavras em sua boca, e ele lhes falará tudo o que eu lhe ordenar”.
19 Kama mtu yeyote hatasikiliza maneno yangu ambayo huyo nabii atayasema kwa Jina langu, mimi mwenyewe nitamwajibisha.
Acontecerá que, quem não escutar minhas palavras que ele falará em meu nome, eu as exigirei dele.
20 Lakini nabii ambaye atathubutu kusema kwa Jina langu kitu chochote ambacho sikumwamuru akiseme, au nabii ambaye husema kwa jina la miungu mingine ni lazima auawe.”
Mas o profeta que falar uma palavra presunçosamente em meu nome, que eu não lhe ordenei que falasse, ou que falar em nome de outros deuses, esse mesmo profeta morrerá”.
21 Mnaweza kuulizana wenyewe, “Tutawezaje kujua wakati ujumbe haukusemwa na Bwana?”
Você pode dizer em seu coração: “Como devemos saber a palavra que Javé não falou?
22 Ikiwa kile nabii anachotangaza kwa jina la Bwana hakikutokea au kutimia, huo ni ujumbe ambao Bwana hakusema. Nabii huyo amesema kwa ujuaji. Msimwogope huyo.
Quando um profeta fala em nome de Iavé, se a coisa não se segue, nem acontece, é a coisa que Iavé não falou. O profeta falou-a presunçosamente. Você não deve ter medo dele.