< Torati 18 >

1 Makuhani ambao ni Walawi, yaani kabila lote la Lawi, hawatakuwa na mgawo wala urithi pamoja na Israeli. Wataishi kwa sadaka zitolewazo kwa ajili ya Bwana za kuteketezwa kwa moto, kwa maana huo ndio urithi wao.
Preestis and dekenes, and alle men that ben of the same lynage, schulen `not haue part and eritage with the tother puple of Israel, for thei schulen ete the sacrifices of the Lord, and the offryngis of hym;
2 Hawatakuwa na urithi miongoni mwa ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.
and thei schulen not take ony othir thing of the possessioun of her britheren; for the Lord hym silf is the `eritage of hem, as he spak to hem.
3 Hili ndilo fungu la makuhani kutoka kwa watu watakaotoa dhabihu ya fahali au kondoo: mguu wa mbele, mataya na matumbo.
This schal be the doom of preestis of the puple, and of hem that offren sacrifices; whether `thei offren an oxe, ether a scheep, thei schulen yyue to the preest the schuldre, and the paunche, the firste fruytis of wheete,
4 Mtawapa malimbuko ya nafaka zenu, divai mpya, mafuta na sufu ya kwanza kutoka manyoya ya kondoo zenu,
and of wyn, and of oile, and a part of wollis of the scheryng of scheep.
5 kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewachagua pamoja na wazao wao kutoka makabila yenu kusimama na kuhudumu katika jina la Bwana siku zote.
For thi Lord God chees hym of alle thi lynagis, that he stonde and mynystre to `the name of the Lord, he and hise sones, with outen ende.
6 Ikiwa Mlawi atahama kutoka mmojawapo ya miji yenu popote katika Israeli ambapo anaishi, akaja kwa moyo wote mahali ambapo Bwana atapachagua,
If a dekene goith out of oon of thi citees of al Israel, in which he dwellith, `and wole come and desirith the place which the Lord chees,
7 anaweza akahudumu katika jina la Bwana Mungu wake kama Walawi wenzake wote wanaohudumu hapo mbele za Bwana.
he schal mynystre in the name of his Lord God as alle hise britheren dekenes, that schulen stonde in that tyme byfore the Lord.
8 Atashiriki sawa katika mafao yao, hata kama amepokea fedha kutoka mauzo ya mali ya jamaa yake.
He schal take the same part of meetis, `which and othere dekenes schulen take; outakun that that is due to hym in his citee, bi `successioun ethir eritage `of fadir.
9 Wakati mtakapoingia katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, msijifunze kuiga njia za machukizo za mataifa ya huko.
Whanne thou hast entrid in to the lond which thi Lord God schal yyue to thee, be thou war lest thou wole sue abhomynaciouns of tho folkis;
10 Asionekane mtu yeyote miongoni mwenu ampitishaye mwanawe au binti yake katika moto, atakayefanya uaguzi, ulozi, anayetabiri nyakati, anayejishughulisha na uchawi,
noon be foundun in thee that clensith his sone, ether his douytir, `and ledith bi the fier, ethir that axith questiouns of dyuynouris `that dyuynen aboute the auteris, and that taketh hede to dremes and chiteryng of bryddis; nethir ony wicche be,
11 wala arogaye kwa kupiga mafundo, wala mwaguzi au anayeabudu mizimu, wala awaombaye wafu.
nethir an enchauntere, `that is, that disseyueth mennus iyen that a thing seme that is not; nether a man take counsel at hem that han a feend spekynge `in the wombe, nether take counsel at false dyuynouris nethir seke of deed men the treuthe.
12 Mtu yeyote afanyaye mambo haya ni chukizo kwa Bwana, tena ni kwa sababu ya matendo haya ya kuchukiza wayafanyayo ndiyo maana Bwana Mungu wenu atayafukuza mataifa hayo mbele yenu.
For the Lord hath abhomynacioun of alle these thingis, and for siche wickidnessis he schal do awei hem in thin entryng.
13 Kamwe msilaumiwe mbele za Bwana Mungu wenu.
Thou schalt be perfit and without filthe, with thi Lord God.
14 Mataifa mtakayowafukuza husikiliza wale wafanyao ulozi na uaguzi. Lakini kwenu ninyi, Bwana Mungu wenu hajawaruhusu kufanya hivyo.
These hethen men, `the lond of whiche thou schalt welde, heren hem that worchen bi chiteryng of briddis, and false dyuynouris; forsothe thou art tauyt in other maner of thi Lord God.
15 Bwana Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu wenyewe. Msikilizeni yeye.
Thi Lord God schal reise a prophete of thi folk and of thi britheren as me, thou schalt here hym;
16 Kwa kuwa hivi ndivyo mlivyomwomba Bwana Mungu wenu kule Horebu siku ile ya kusanyiko, wakati mliposema, “Na tusiisikie sauti ya Bwana Mungu wetu, wala kuuona moto huu mkubwa tena, ama sivyo tutakufa.”
as thou axidist of thi Lord God in Oreb, whanne the cumpany was gaderid, and thou seidist, Y schal no more here the vois of my Lord God, and Y schal no more se `this grettiste fier, lest Y die.
17 Bwana akaniambia: “Wanachosema ni vyema.
And the Lord seide to me, Thei spaken wel alle thingis.
18 Nitawainulia nabii kama wewe kutoka miongoni mwa ndugu zao; nitaweka maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia kila kitu nitakachomwamuru.
Y schal reise to hem a prophete, lijk thee, of the myddis of her britheren, and Y schal putte my wordis in his mouth, and he schal speke to hem alle thingis, whiche I schal comaunde to him.
19 Kama mtu yeyote hatasikiliza maneno yangu ambayo huyo nabii atayasema kwa Jina langu, mimi mwenyewe nitamwajibisha.
Forsothe Y schal be vengere of `that man, that nyle here the wordis `of hym, whiche he schal speke in my name.
20 Lakini nabii ambaye atathubutu kusema kwa Jina langu kitu chochote ambacho sikumwamuru akiseme, au nabii ambaye husema kwa jina la miungu mingine ni lazima auawe.”
`Sotheli a prophete `schal be slayn, which is bischrewid with pride, and wole speke in my name tho thingis, whiche Y comaundide not to hym, that he schulde seie, ethir bi the name of alien goddis.
21 Mnaweza kuulizana wenyewe, “Tutawezaje kujua wakati ujumbe haukusemwa na Bwana?”
That if thou answerist bi pryuy thouyt, Hou may Y vndirstonde the word, which the Lord spak not? thou schalt haue this signe,
22 Ikiwa kile nabii anachotangaza kwa jina la Bwana hakikutokea au kutimia, huo ni ujumbe ambao Bwana hakusema. Nabii huyo amesema kwa ujuaji. Msimwogope huyo.
`The Lord spak not this thing which thilke prophete biforseid in the name of the Lord, `and it bifallith not, but `the prophete feynede bi the pride of his soule, and therfor thou schalt not drede hym.

< Torati 18 >