< Torati 18 >
1 Makuhani ambao ni Walawi, yaani kabila lote la Lawi, hawatakuwa na mgawo wala urithi pamoja na Israeli. Wataishi kwa sadaka zitolewazo kwa ajili ya Bwana za kuteketezwa kwa moto, kwa maana huo ndio urithi wao.
The priests, who are Levites, and all the tribe of Levi, will have no portion nor inheritance with Israel; they must eat the offerings of Yahweh made by fire as their inheritance.
2 Hawatakuwa na urithi miongoni mwa ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.
They must have no inheritance among their brothers; Yahweh is their inheritance, as he said to them.
3 Hili ndilo fungu la makuhani kutoka kwa watu watakaotoa dhabihu ya fahali au kondoo: mguu wa mbele, mataya na matumbo.
This is the share given to the priests, given to them from the people who offer a sacrifice, whether it be an oxen or a sheep: the shoulder, the two cheeks, and the inner parts.
4 Mtawapa malimbuko ya nafaka zenu, divai mpya, mafuta na sufu ya kwanza kutoka manyoya ya kondoo zenu,
The firstfruits of your grain, of your new wine, and of your oil, and the first of the fleece of your sheep, you must give him.
5 kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewachagua pamoja na wazao wao kutoka makabila yenu kusimama na kuhudumu katika jina la Bwana siku zote.
For Yahweh your God has chosen him out of all your tribes to stand to serve in the name of Yahweh, him and his sons forever.
6 Ikiwa Mlawi atahama kutoka mmojawapo ya miji yenu popote katika Israeli ambapo anaishi, akaja kwa moyo wote mahali ambapo Bwana atapachagua,
If a Levite comes from any of your towns out of all Israel from where he is living, and desires with all his soul to come to the place Yahweh will choose,
7 anaweza akahudumu katika jina la Bwana Mungu wake kama Walawi wenzake wote wanaohudumu hapo mbele za Bwana.
then he must serve in the name of Yahweh his God as all his brothers the Levites do, who stand there before Yahweh.
8 Atashiriki sawa katika mafao yao, hata kama amepokea fedha kutoka mauzo ya mali ya jamaa yake.
They must have similar portions to eat, besides of what comes of the sale of his family's inheritance.
9 Wakati mtakapoingia katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, msijifunze kuiga njia za machukizo za mataifa ya huko.
When you have come into the land that Yahweh your God is giving you, you must not learn to observe the abominations of those nations.
10 Asionekane mtu yeyote miongoni mwenu ampitishaye mwanawe au binti yake katika moto, atakayefanya uaguzi, ulozi, anayetabiri nyakati, anayejishughulisha na uchawi,
There must not be found among you anyone who sacrifices his son or his daughter in the fire, anyone who uses divination or tells fortunes, or reads signs found in a cup, or engages in witchcraft,
11 wala arogaye kwa kupiga mafundo, wala mwaguzi au anayeabudu mizimu, wala awaombaye wafu.
any charmer, anyone who conjurs up spirits, or one who casts spells, or who talks with spirits of the dead.
12 Mtu yeyote afanyaye mambo haya ni chukizo kwa Bwana, tena ni kwa sababu ya matendo haya ya kuchukiza wayafanyayo ndiyo maana Bwana Mungu wenu atayafukuza mataifa hayo mbele yenu.
For whoever does these things is an abomination to Yahweh; it is because of these abominations that Yahweh your God is driving them out from before you.
13 Kamwe msilaumiwe mbele za Bwana Mungu wenu.
You must be blameless before Yahweh your God.
14 Mataifa mtakayowafukuza husikiliza wale wafanyao ulozi na uaguzi. Lakini kwenu ninyi, Bwana Mungu wenu hajawaruhusu kufanya hivyo.
For these nations that you will dispossess listen to those who practice sorcery and divination; but as for you, Yahweh your God has not allowed you to do so.
15 Bwana Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu wenyewe. Msikilizeni yeye.
Yahweh your God will raise up for you a prophet from among you, one of your brothers, like me. You must listen to him.
16 Kwa kuwa hivi ndivyo mlivyomwomba Bwana Mungu wenu kule Horebu siku ile ya kusanyiko, wakati mliposema, “Na tusiisikie sauti ya Bwana Mungu wetu, wala kuuona moto huu mkubwa tena, ama sivyo tutakufa.”
This is what you asked from Yahweh your God at Horeb on the day of the assembly, saying, 'Let us not hear again the voice of Yahweh our God, nor see this great fire anymore, or we will die.'
17 Bwana akaniambia: “Wanachosema ni vyema.
Yahweh said to me, 'What they have said is good.
18 Nitawainulia nabii kama wewe kutoka miongoni mwa ndugu zao; nitaweka maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia kila kitu nitakachomwamuru.
I will raise up a prophet for them from among their brothers, just like you. I will put my words in his mouth, and he will speak to them all that I command him.
19 Kama mtu yeyote hatasikiliza maneno yangu ambayo huyo nabii atayasema kwa Jina langu, mimi mwenyewe nitamwajibisha.
It will happen that if anyone does not listen to the words of mine that he speaks in my name, I will require it of him.
20 Lakini nabii ambaye atathubutu kusema kwa Jina langu kitu chochote ambacho sikumwamuru akiseme, au nabii ambaye husema kwa jina la miungu mingine ni lazima auawe.”
But the prophet who speaks a word arrogantly in my name, a word that I have not commanded him to speak, or who speaks in the name of other gods, that very prophet must die.'
21 Mnaweza kuulizana wenyewe, “Tutawezaje kujua wakati ujumbe haukusemwa na Bwana?”
This is what you must say in your heart: 'How will we recognize a message that Yahweh has not spoken?'
22 Ikiwa kile nabii anachotangaza kwa jina la Bwana hakikutokea au kutimia, huo ni ujumbe ambao Bwana hakusema. Nabii huyo amesema kwa ujuaji. Msimwogope huyo.
You will recognize a message that Yahweh has spoken when a prophet speaks in the name of Yahweh. If that thing does not occur nor happen, then that is something that Yahweh has not spoken and the prophet has spoken it arrogantly, and you must not be afraid of him.