< Torati 18 >

1 Makuhani ambao ni Walawi, yaani kabila lote la Lawi, hawatakuwa na mgawo wala urithi pamoja na Israeli. Wataishi kwa sadaka zitolewazo kwa ajili ya Bwana za kuteketezwa kwa moto, kwa maana huo ndio urithi wao.
The priests the Levites, even all the tribe of Levi, shall have no portion nor inheritance with Israel; they shall eat the offerings of the LORD made by fire, and His inheritance.
2 Hawatakuwa na urithi miongoni mwa ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.
And they shall have no inheritance among their brethren; the LORD is their inheritance, as He hath spoken unto them.
3 Hili ndilo fungu la makuhani kutoka kwa watu watakaotoa dhabihu ya fahali au kondoo: mguu wa mbele, mataya na matumbo.
And this shall be the priests' due from the people, from them that offer a sacrifice, whether it be ox or sheep, that they shall give unto the priest the shoulder, and the two cheeks, and the maw.
4 Mtawapa malimbuko ya nafaka zenu, divai mpya, mafuta na sufu ya kwanza kutoka manyoya ya kondoo zenu,
The first-fruits of thy corn, of thy wine, and of thine oil, and the first of the fleece of thy sheep, shalt thou give him.
5 kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewachagua pamoja na wazao wao kutoka makabila yenu kusimama na kuhudumu katika jina la Bwana siku zote.
For the LORD thy God hath chosen him out of all thy tribes, to stand to minister in the name of the LORD, him and his sons for ever.
6 Ikiwa Mlawi atahama kutoka mmojawapo ya miji yenu popote katika Israeli ambapo anaishi, akaja kwa moyo wote mahali ambapo Bwana atapachagua,
And if a Levite come from any of thy gates out of all Israel, where he sojourneth, and come with all the desire of his soul unto the place which the LORD shall choose;
7 anaweza akahudumu katika jina la Bwana Mungu wake kama Walawi wenzake wote wanaohudumu hapo mbele za Bwana.
then he shall minister in the name of the LORD his God, as all his brethren the Levites do, who stand there before the LORD.
8 Atashiriki sawa katika mafao yao, hata kama amepokea fedha kutoka mauzo ya mali ya jamaa yake.
They shall have like portions to eat, beside that which is his due according to the fathers' houses.
9 Wakati mtakapoingia katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, msijifunze kuiga njia za machukizo za mataifa ya huko.
When thou art come into the land which the LORD thy God giveth thee, thou shalt not learn to do after the abominations of those nations.
10 Asionekane mtu yeyote miongoni mwenu ampitishaye mwanawe au binti yake katika moto, atakayefanya uaguzi, ulozi, anayetabiri nyakati, anayejishughulisha na uchawi,
There shall not be found among you any one that maketh his son or his daughter to pass through the fire, one that useth divination, a soothsayer, or an enchanter, or a sorcerer,
11 wala arogaye kwa kupiga mafundo, wala mwaguzi au anayeabudu mizimu, wala awaombaye wafu.
or a charmer, or one that consulteth a ghost or a familiar spirit, or a necromancer.
12 Mtu yeyote afanyaye mambo haya ni chukizo kwa Bwana, tena ni kwa sababu ya matendo haya ya kuchukiza wayafanyayo ndiyo maana Bwana Mungu wenu atayafukuza mataifa hayo mbele yenu.
For whosoever doeth these things is an abomination unto the LORD; and because of these abominations the LORD thy God is driving them out from before thee.
13 Kamwe msilaumiwe mbele za Bwana Mungu wenu.
Thou shalt be whole-hearted with the LORD thy God.
14 Mataifa mtakayowafukuza husikiliza wale wafanyao ulozi na uaguzi. Lakini kwenu ninyi, Bwana Mungu wenu hajawaruhusu kufanya hivyo.
For these nations, that thou art to dispossess, hearken unto soothsayers, and unto diviners; but as for thee, the LORD thy God hath not suffered thee so to do.
15 Bwana Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu wenyewe. Msikilizeni yeye.
A prophet will the LORD thy God raise up unto thee, from the midst of thee, of thy brethren, like unto me; unto him ye shall hearken;
16 Kwa kuwa hivi ndivyo mlivyomwomba Bwana Mungu wenu kule Horebu siku ile ya kusanyiko, wakati mliposema, “Na tusiisikie sauti ya Bwana Mungu wetu, wala kuuona moto huu mkubwa tena, ama sivyo tutakufa.”
according to all that thou didst desire of the LORD thy God in Horeb in the day of the assembly, saying: 'Let me not hear again the voice of the LORD my God, neither let me see this great fire any more, that I die not.'
17 Bwana akaniambia: “Wanachosema ni vyema.
And the LORD said unto me: 'They have well said that which they have spoken.
18 Nitawainulia nabii kama wewe kutoka miongoni mwa ndugu zao; nitaweka maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia kila kitu nitakachomwamuru.
I will raise them up a prophet from among their brethren, like unto thee; and I will put My words in his mouth, and he shall speak unto them all that I shall command him.
19 Kama mtu yeyote hatasikiliza maneno yangu ambayo huyo nabii atayasema kwa Jina langu, mimi mwenyewe nitamwajibisha.
And it shall come to pass, that whosoever will not hearken unto My words which he shall speak in My name, I will require it of him.
20 Lakini nabii ambaye atathubutu kusema kwa Jina langu kitu chochote ambacho sikumwamuru akiseme, au nabii ambaye husema kwa jina la miungu mingine ni lazima auawe.”
But the prophet, that shall speak a word presumptuously in My name, which I have not commanded him to speak, or that shall speak in the name of other gods, that same prophet shall die.'
21 Mnaweza kuulizana wenyewe, “Tutawezaje kujua wakati ujumbe haukusemwa na Bwana?”
And if thou say in thy heart: 'How shall we know the word which the LORD hath not spoken?'
22 Ikiwa kile nabii anachotangaza kwa jina la Bwana hakikutokea au kutimia, huo ni ujumbe ambao Bwana hakusema. Nabii huyo amesema kwa ujuaji. Msimwogope huyo.
When a prophet speaketh in the name of the LORD, if the thing follow not, nor come to pass, that is the thing which the LORD hath not spoken; the prophet hath spoken it presumptuously, thou shalt not be afraid of him.

< Torati 18 >