< Torati 18 >
1 Makuhani ambao ni Walawi, yaani kabila lote la Lawi, hawatakuwa na mgawo wala urithi pamoja na Israeli. Wataishi kwa sadaka zitolewazo kwa ajili ya Bwana za kuteketezwa kwa moto, kwa maana huo ndio urithi wao.
The priests, the Levites, even the whole tribe of Levi, shall have no part nor inheritance with Israel; the burnt-offerings of the Lord [are] their inheritance, they shall eat them.
2 Hawatakuwa na urithi miongoni mwa ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.
And they shall have no inheritance among their brethren; the Lord himself [is] his portion, as he said to him.
3 Hili ndilo fungu la makuhani kutoka kwa watu watakaotoa dhabihu ya fahali au kondoo: mguu wa mbele, mataya na matumbo.
And this [is] the due of the priests in the things coming from the people from those who offer sacrifices, whether it be a calf or a sheep; and thou shalt give the shoulder to the priest, and the cheeks, and the great intestine:
4 Mtawapa malimbuko ya nafaka zenu, divai mpya, mafuta na sufu ya kwanza kutoka manyoya ya kondoo zenu,
and the first-fruits of thy corn, and of thy wine, and of thine oil; and thou shalt give to him the first-fruits of the fleeces of thy sheep:
5 kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewachagua pamoja na wazao wao kutoka makabila yenu kusimama na kuhudumu katika jina la Bwana siku zote.
because the Lord has chosen him out of all thy tribes, to stand before the Lord thy God, to minister and bless in his name, himself and his sons among the children of Israel.
6 Ikiwa Mlawi atahama kutoka mmojawapo ya miji yenu popote katika Israeli ambapo anaishi, akaja kwa moyo wote mahali ambapo Bwana atapachagua,
And if a Levite come from one of the cities of all the children of Israel, where he himself dwells, accordingly as his mind desires, to the place which he shall have chosen,
7 anaweza akahudumu katika jina la Bwana Mungu wake kama Walawi wenzake wote wanaohudumu hapo mbele za Bwana.
he shall minister to the name of the Lord his God, as all his brethren the Levites, who stand there present before the Lord thy God.
8 Atashiriki sawa katika mafao yao, hata kama amepokea fedha kutoka mauzo ya mali ya jamaa yake.
He shall eat an allotted portion, besides the sale of his hereditary property.
9 Wakati mtakapoingia katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, msijifunze kuiga njia za machukizo za mataifa ya huko.
And when thou shalt have entered into the land which the Lord thy God gives thee, thou shalt not learn to do according to the abominations of those nations.
10 Asionekane mtu yeyote miongoni mwenu ampitishaye mwanawe au binti yake katika moto, atakayefanya uaguzi, ulozi, anayetabiri nyakati, anayejishughulisha na uchawi,
There shall not be found in thee one who purges his son or his daughter with fire, one who uses divination, who deals with omens, and augury,
11 wala arogaye kwa kupiga mafundo, wala mwaguzi au anayeabudu mizimu, wala awaombaye wafu.
a sorcerer employing incantation, one who has in him a divining spirit, and observer of signs, questioning the dead.
12 Mtu yeyote afanyaye mambo haya ni chukizo kwa Bwana, tena ni kwa sababu ya matendo haya ya kuchukiza wayafanyayo ndiyo maana Bwana Mungu wenu atayafukuza mataifa hayo mbele yenu.
For every one that does these things is an abomination to the Lord thy God; for because of these abominations the Lord will destroy them from before thy face.
13 Kamwe msilaumiwe mbele za Bwana Mungu wenu.
Thou shalt be perfect before the Lord thy God.
14 Mataifa mtakayowafukuza husikiliza wale wafanyao ulozi na uaguzi. Lakini kwenu ninyi, Bwana Mungu wenu hajawaruhusu kufanya hivyo.
For all these nations whose [land] thou shalt inherit, they will listen to omens and divinations; but the Lord thy God has not permitted thee so [to do].
15 Bwana Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu wenyewe. Msikilizeni yeye.
The Lord thy God shall raise up to thee a prophet of thy brethren, like me; him shall ye hear:
16 Kwa kuwa hivi ndivyo mlivyomwomba Bwana Mungu wenu kule Horebu siku ile ya kusanyiko, wakati mliposema, “Na tusiisikie sauti ya Bwana Mungu wetu, wala kuuona moto huu mkubwa tena, ama sivyo tutakufa.”
according to all things which thou didst desire of the Lord thy God in Choreb in the day of the assembly, saying, We will not again hear the voice of the Lord thy God, and we will not any more see this great fire, and [so] we shall not die.
17 Bwana akaniambia: “Wanachosema ni vyema.
And the Lord said to me, They have spoken rightly all that they have said to thee.
18 Nitawainulia nabii kama wewe kutoka miongoni mwa ndugu zao; nitaweka maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia kila kitu nitakachomwamuru.
I will raise up to them a prophet of their brethren, like thee; and I will put my words in his mouth, and he shall speak to them as I shall command him.
19 Kama mtu yeyote hatasikiliza maneno yangu ambayo huyo nabii atayasema kwa Jina langu, mimi mwenyewe nitamwajibisha.
And whatever man shall not hearken to whatsoever words that prophet shall speak in my name, I will take vengeance on him.
20 Lakini nabii ambaye atathubutu kusema kwa Jina langu kitu chochote ambacho sikumwamuru akiseme, au nabii ambaye husema kwa jina la miungu mingine ni lazima auawe.”
But the prophet whosoever shall impiously speak in my name a word which I have not commanded him to speak, and whosoever shall speak in the name of other gods, that prophet shall die.
21 Mnaweza kuulizana wenyewe, “Tutawezaje kujua wakati ujumbe haukusemwa na Bwana?”
But if thou shalt say in thine heart, How shall we know the word which the Lord has not spoken?
22 Ikiwa kile nabii anachotangaza kwa jina la Bwana hakikutokea au kutimia, huo ni ujumbe ambao Bwana hakusema. Nabii huyo amesema kwa ujuaji. Msimwogope huyo.
Whatsoever words that prophet shall speak in the name of the Lord, and they shall not come true, and not come to pass, this [is] the thing which the Lord has not spoken; that prophet has spoken wickedly: ye shall not spare him.