< Torati 16 >
1 Shikeni mwezi wa Abibu, na kuiadhimisha Pasaka ya Bwana Mungu wenu, kwa sababu katika mwezi wa Abibu, Mungu aliwatoa Misri usiku.
“Observe the month of new grain, at the beginning of springtime, so that you may accomplish the Passover to the Lord your God. For in this month, the Lord your God led you away from Egypt in the night.
2 Mtatoa dhabihu ya Pasaka ya mnyama kwa Bwana Mungu wenu kutoka kundi lenu la mbuzi na kondoo au la ngʼombe, mahali pale ambapo Bwana atapachagua kama makao kwa ajili ya Jina lake.
And you shall immolate the Passover to the Lord your God, from sheep and from oxen, in the place which the Lord your God will choose, so that his name may dwell there.
3 Msile nyama hiyo pamoja na mikate iliyotiwa chachu, lakini kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu, mikate ya kujitesa, kwa sababu mliondoka Misri kwa haraka, ili kwamba siku zote za maisha yenu mpate kukumbuka wakati wenu wa kuondoka Misri.
You shall not eat it with leavened bread. For seven days you shall eat, without leaven, the bread of affliction. For you departed from Egypt in fear. So may you remember the day of your departure from Egypt, throughout all the days of your life.
4 Chachu isionekane katika mali zenu katika nchi yenu yote kwa siku saba. Nyama yoyote ya dhabihu mtakayotoa jioni ya siku ya kwanza isibakizwe mpaka asubuhi.
No leaven shall be present in all your confines for seven days. And by morning, there shall not remain any of the flesh which was immolated on the first day in the evening.
5 Kamwe msitoe dhabihu ya Pasaka katika mji wowote ambao Bwana Mungu wenu amewapa,
You cannot immolate the Passover in any of your cities, which the Lord your God will give to you, that you wish,
6 isipokuwa mahali atakapopachagua kama makao kwa ajili ya Jina lake. Hapo ndipo lazima mtoe dhabihu ya Pasaka jioni, jua litakapotua, iwe kumbukumbu yenu ya kutoka Misri.
but only in the place which the Lord your God will choose, so that his name may dwell there. You shall immolate the Passover in the evening, upon the setting of the sun, which is the time when you departed from Egypt.
7 Okeni na mle mahali pale ambapo Bwana Mungu wenu atakapopachagua, kisha asubuhi mrudi kwenye mahema yenu.
And you shall cook and eat it in the place which the Lord your God will choose, and, rising up in the morning, you shall go into your tent.
8 Kwa siku sita mtakula mikate isiyotiwa chachu na siku ya saba fanyeni kusanyiko kwa ajili ya Bwana Mungu wenu na msifanye kazi.
For six days, you shall eat unleavened bread. And on the seventh day, because it is the assembly of the Lord your God, you shall do no work.
9 Mhesabu majuma saba tangu wakati mnapoanza kuchukua mundu kuvuna nafaka.
You shall number for yourself seven weeks from that day, the day on which you put the sickle to the grain field.
10 Kisha msherehekee Sikukuu ya Majuma kwa Bwana Mungu wenu kwa kutoa sadaka ya hiari kwa kadiri ya baraka ambayo Bwana Mungu wenu amewapa.
And you shall celebrate the Feast of Weeks, to the Lord your God, with a voluntary oblation from your hand, which you shall offer according to the blessing of the Lord your God.
11 Shangilieni mbele za Bwana Mungu wenu mahali atakapopachagua kama makao ya Jina lake, ninyi, wana wenu na binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, Walawi walio katika miji yenu, na wageni, yatima na wajane waishio miongoni mwenu.
And you shall feast in the sight of the Lord your God: you, your son and your daughter, your man servant and your woman servant, and the Levite who is within your gates, and the new arrival as well as the orphan and the widow, who abide with you, in the place which the Lord your God will choose, so that his name may dwell there.
12 Kumbukeni kwamba mlikuwa watumwa kule Misri na mfuate amri hizi kwa uangalifu.
And you shall recall that you were a servant in Egypt. And you shall preserve and carry out the things that have been instructed.
13 Adhimisheni sikukuu ya vibanda kwa siku saba baada ya kukusanya mazao yenu ya nafaka na kukamua zabibu.
Likewise, you shall celebrate the Feast of Tabernacles for seven days, when you will have gathered your fruits from the orchard and the winepress.
14 Mfurahie sikukuu yenu, ninyi, wana wenu, binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, Walawi, wageni, yatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu.
And you shall feast at the time of your festival: you, your son and daughter, your man servant and woman servant, likewise the Levite and the new arrival, the orphan and the widow, who are within your gates.
15 Kwa siku saba mtaiadhimisha sikukuu ya Bwana Mungu wenu katika mahali atakapopachagua Bwana. Kwa kuwa Bwana Mungu wenu atawabariki katika mavuno yenu na katika kazi zote za mikono yenu na furaha yenu itakamilika.
For seven days you shall celebrate feasts to the Lord your God in the place which the Lord will choose. And the Lord your God will bless you in all your crops, and in every work of your hands. And you shall be joyful.
16 Wanaume wenu wote lazima wajitokeze mara tatu kwa mwaka mbele za Bwana Mungu wenu mahali atakapopachagua: kwa ajili ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma, na Sikukuu ya Vibanda. Hakuna mtu atakayejitokeza mbele za Bwana mikono mitupu:
Three times a year, all your males shall appear in the sight the Lord your God in the place which he will choose: at the Feast of Unleavened Bread, at the Feast of Weeks, and at the Feast of Tabernacles. No one shall appear before the Lord empty.
17 Kila mmoja wenu ni lazima alete zawadi kulingana na jinsi ambavyo Bwana Mungu wenu alivyowabariki.
But each one shall offer according to what he will have, according to the blessing of the Lord his God, which he will give to him.
18 Wateue waamuzi na maafisa kwa kila kabila lenu katika kila mji ambao Bwana Mungu wenu anawapa, nao watawaamua watu kwa usawa.
You shall appoint judges and magistrates at all your gates, which the Lord your God will give to you, throughout each of your tribes, so that they may judge the people with a just judgment,
19 Msipotoshe haki wala msifanye upendeleo. Msikubali rushwa kwa sababu rushwa hupofusha macho ya wenye busara na kugeuza maneno ya wenye haki.
and not so as to show favoritism to either side. You shall not accept a person’s reputation, nor gifts. For gifts blind the eyes of the wise and alter the words of the just.
20 Mfuate haki na haki peke yake, ili mweze kuishi na kuimiliki nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa.
You shall justly pursue what is just, so that you may live and possess the land, which the Lord your God will give to you.
21 Msisimamishe nguzo yoyote ya Ashera kando ya madhabahu mliyomjengea Bwana Mungu wenu,
You shall not plant a sacred grove, nor shall you plant any tree near the altar of the Lord your God;
22 wala msisimamishe jiwe la kuabudu, kwa maana Bwana Mungu wenu anavichukia vitu hivi.
you shall neither make nor set up for yourself a statue. These things the Lord your God hates.”