< Torati 15 >

1 Kila mwisho wa miaka saba ni lazima mfute madeni.
In the seuenthe yeer thou schalt make remyssioun,
2 Hivi ndivyo itakavyofanyika: Kila mkopeshaji atafuta mkopo aliomkopesha Mwisraeli mwenzake. Hatamtaka Mwisraeli mwenzake au ndugu yake amlipe hilo deni, kwa sababu wakati wa Bwana wa kufuta madeni umetangazwa.
that schal be fillid bi this ordre. To whom ony thing is `dettid, ethir owid of his freend, ether neiybore, and brother, he schal not mowe axe, for it is the yeer of remyssioun of the Lord.
3 Unaweza kudai malipo kwa mgeni, lakini lazima ufute kila deni ambalo unamdai ndugu yako.
Thou schalt axe of a pilgrym and comelyng; thou hast not power to axe of a citeseyn and neiybore;
4 Hata hivyo, hapatakuwepo maskini miongoni mwenu, kwa kuwa katika nchi Bwana Mungu wenu anayowapa kuimiliki kama urithi wenu, atawabariki sana,
and outerli a nedi man and begger schal not be among you, that thi Lord God blesse thee, in the lond which he schal yyue to thee in to the possessioun.
5 ikiwa tutamtii Bwana Mungu wenu kikamilifu na kuwa waangalifu kuyafuata maagizo haya yote ninayowapa leo.
If netheles thou schalt here the vois of thi Lord God, and schalt kepe alle thingis whiche he comaundide, and whiche Y comaunde to dai to thee, he schal blesse thee, as he bihiyte.
6 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu atawabariki kama alivyoahidi, nanyi mtawakopesha mataifa mengi lakini hamtakopa kwa yeyote. Mtatawala mataifa mengi lakini hakuna taifa litakalowatawala ninyi.
Thou schalt leene to many folkis, and thou schalt not take borewyng of ony man; thou schalt be lord of ful many naciouns, and no man schal be lord of thee.
7 Ikiwa kuna mtu maskini miongoni mwa ndugu zenu, katika mji wowote wa hiyo nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, msiwe na moyo mgumu wala usimfumbie mkono ndugu yako aliye maskini.
If oon of thi britheren that dwellen with ynne the yatis of thi citee, in the lond which thi Lord God schal yyue to thee, cometh to pouert, thou schalt not make hard thin herte, nether thou schalt `drawe to gydere the hond,
8 Afadhali fungua mikono yako na umkopeshe kwa hiari chochote anachohitaji.
but thou schalt opene it to the pore man, and thou schalt `yyue loone to which thou siest hym haue nede.
9 Jihadhari usijiwekee wazo hili ovu: “Mwaka wa saba, mwaka wa kufuta madeni umekaribia,” usije ukaonyesha nia mbaya kwa ndugu yako mhitaji na ukaacha kumpa chochote. Anaweza kumlalamikia Bwana dhidi yako nawe utakuwa umepatikana na hatia ya dhambi.
Be thou war lest perauenture wickid thouyt crepe priueli to thee, and thou seie in thin herte, The seuenthe yeer of remyssioun neiyeth; and thou turne awey the iyen fro thi pore brother, and thou nyle yyue to hym the loone that he axith; lest he crie ayens thee to the Lord, and it be maad to thee in to synne.
10 Mpe kwa ukarimu na ufanye hivyo bila kinyongo moyoni, ndipo kwa sababu ya hili Bwana Mungu wenu atakubariki katika kazi zako zote na kwa kila kitu utakachokiwekea mkono wako.
But thou schalt yyue to hym, and thou schalt `not do ony thing falsly in releuynge `hise nedis, that thi Lord God blesse thee in al tyme, and in alle thingis to whiche thou schalt sette to hond.
11 Siku zote watakuwepo watu maskini katika nchi. Kwa hiyo ninawaamuru mwe na mikono iliyokunjuliwa kuwaelekea ndugu zenu, kuwaelekea maskini na wahitaji katika nchi yenu.
Pore men schulen not faile in the lond of `thin habitacioun; therfor Y comaunde to thee, that thou opene the hond to thi brother nedi and pore, that lyuen with thee in the lond.
12 Kama Mwebrania mwenzako, mwanaume au mwanamke, akijiuza kwako na kukutumikia miaka sita, katika mwaka wa saba ni lazima umwache aende zake akiwa huru.
Whanne thi brothir an Ebrew man, ethir an Ebrew womman, is seeld to thee, and hath serued thee sixe yeer, in the seuenthe yeer thou schalt delyuere hym fre.
13 Nawe wakati utakapomwachia usimwache aende mikono mitupu.
And thou schalt not suffre hym go awey voide, to whom thou hast yyue fredom;
14 Mpe kwa uhuru kutoka zizi lako la kondoo na mbuzi, kutoka sakafu yako ya kupuria nafaka na kutoka mashinikizo yako ya kukamulia divai. Mpe kama vile ambavyo Bwana Mungu wako alivyokubariki.
but thou schalt yyue lijflode in the weye, of flockis, and of cornfloor, and of thi pressour, in whiche thi Lord God hath blessid thee.
15 Kumbukeni kuwa ninyi mlikuwa watumwa huko Misri naye Bwana Mungu wenu aliwakomboa. Ndiyo sababu nimewapa agizo hili leo.
Haue thou mynde that also thou seruedist in the lond of Egipt, and thi Lord God delyurede thee, `ether made thee free, and therfor Y comaunde now to thee.
16 Lakini mtumishi wako akikuambia, “Sitaki kukuacha,” kwa sababu anakupenda wewe na jamaa yako naye anaridhika nawe,
Forsothe if `the seruaunt seith, Y nyle go out, for he loueth thee, and thin hows, and feelith that it is wel to hym at thee, thou schalt take `a nal,
17 ndipo utachukua chuma kidogo utoboe sikio lake mpaka hicho chuma kiingie kwenye ubao wa mlango, naye atakuwa mtumishi wako wa maisha. Ufanye vivyo hivyo kwa mtumishi wa kike.
and thou schalt peerse his eere in the yate of thin hous, and he schal serue thee til in to the world, `that is til to the iubilee, ethir fiftithe yeer; also thou schalt do in lijk maner to the handmayde.
18 Usifikiri kuwa kuna ugumu kumwacha mtumishi wako huru, kwa sababu utumishi wake kwako kwa miaka hii sita umekuwa wa thamani mara mbili ya ujira wa mtumishi wa kuajiriwa. Naye Bwana Mungu wenu atakubarikia kwa kila kitu utakachofanya.
Thou schalt not turne awei fro hem thin iyen, whanne thou schalt delyure hem fre, for bi the hire of an hirid man thei serueden thee bi sixe yeer; that thi Lord God blesse thee, in alle the werkis whiche thou doist.
19 Wekeni wakfu kwa Bwana Mungu wenu kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa makundi yenu ya ngʼombe na ya mbuzi na kondoo. Maksai walio wazaliwa wa kwanza msiwafanyize kazi, wala msinyoe manyoya ya wazaliwa wa kwanza wa kondoo.
Of the first gendrid thingis that ben borun in thi droues, and scheep, what euer is of male kynde, thou schalt halewe to thi Lord God. Thou schalt not worche in the firste gendrid thing `of oxe, and thou schalt not clippe the firste gendrid thinges of scheep.
20 Kila mwaka ninyi na jamaa zenu mtapaswa kuwala mbele za Bwana Mungu wenu pale mahali atakapopachagua.
Thou schalt ete tho bi alle yeeris in the siyt of thi Lord God, thou, and thin hows, in the place `which the Lord chees.
21 Kama mnyama ana dosari, akiwa ni kilema au kipofu au kama ana kilema kibaya, kamwe usimtoe dhabihu kwa Bwana Mungu wenu.
Sotheli if it hath a wem, ethir is crokid, ethir is blynd, ethir is foul, ethir feble in ony part, it schal not be offrid to thi Lord God;
22 Itawapasa kumla ninyi wenyewe katika miji yenu. Wote wasio safi na walio safi kwa desturi za kiibada mwaweza kula kama vile mnavyokula paa au kulungu.
but thou schalt ete it with ynne the yatis of thi citee, bothe a cleene man and vncleene schulen ete tho in lijk maner, as a capret and an hert.
23 Lakini kamwe msinywe damu; imwageni ardhini kama maji.
Onely thou schalt kepe this, that thou ete not the blood of tho, but schede out as watir in to erthe.

< Torati 15 >