< Torati 15 >
1 Kila mwisho wa miaka saba ni lazima mfute madeni.
“At the end of seven years you make a release,
2 Hivi ndivyo itakavyofanyika: Kila mkopeshaji atafuta mkopo aliomkopesha Mwisraeli mwenzake. Hatamtaka Mwisraeli mwenzake au ndugu yake amlipe hilo deni, kwa sababu wakati wa Bwana wa kufuta madeni umetangazwa.
and this [is] the matter of the release: every owner of a loan [is] to release his hand which he lifts up against his neighbor, he does not exact of his neighbor and of his brother, but has proclaimed a release to YHWH;
3 Unaweza kudai malipo kwa mgeni, lakini lazima ufute kila deni ambalo unamdai ndugu yako.
of the stranger you may exact, but that which is yours with your brother your hand releases,
4 Hata hivyo, hapatakuwepo maskini miongoni mwenu, kwa kuwa katika nchi Bwana Mungu wenu anayowapa kuimiliki kama urithi wenu, atawabariki sana,
except there is an end [when] no poor [are] with you; for YHWH greatly blesses you in the land which your God YHWH is giving to you [for] an inheritance to possess it,
5 ikiwa tutamtii Bwana Mungu wenu kikamilifu na kuwa waangalifu kuyafuata maagizo haya yote ninayowapa leo.
only if you listen diligently to the voice of your God YHWH, to observe to do all this command which I am commanding you today.
6 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu atawabariki kama alivyoahidi, nanyi mtawakopesha mataifa mengi lakini hamtakopa kwa yeyote. Mtatawala mataifa mengi lakini hakuna taifa litakalowatawala ninyi.
For your God YHWH has blessed you as He has spoken to you; and you have lent [to] many nations, but you have not borrowed; and you have ruled over many nations, but they do not rule over you.
7 Ikiwa kuna mtu maskini miongoni mwa ndugu zenu, katika mji wowote wa hiyo nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, msiwe na moyo mgumu wala usimfumbie mkono ndugu yako aliye maskini.
When there is with you any poor of one of your brothers, in one of your cities, in your land which your God YHWH is giving to you, you do not harden your heart, nor shut your hand from your needy brother;
8 Afadhali fungua mikono yako na umkopeshe kwa hiari chochote anachohitaji.
for you certainly open your hand to him, and certainly lend him sufficiency for his lack which he lacks.
9 Jihadhari usijiwekee wazo hili ovu: “Mwaka wa saba, mwaka wa kufuta madeni umekaribia,” usije ukaonyesha nia mbaya kwa ndugu yako mhitaji na ukaacha kumpa chochote. Anaweza kumlalamikia Bwana dhidi yako nawe utakuwa umepatikana na hatia ya dhambi.
Take heed to yourself lest there be a worthless word in your heart, saying, The seventh year [is] near, the year of release; and your eye is evil against your needy brother, and you do not give to him, and he has called to YHWH concerning you, and it has been sin in you;
10 Mpe kwa ukarimu na ufanye hivyo bila kinyongo moyoni, ndipo kwa sababu ya hili Bwana Mungu wenu atakubariki katika kazi zako zote na kwa kila kitu utakachokiwekea mkono wako.
you certainly give to him, and your heart is not sad in your giving to him, for because of this thing your God YHWH blesses you in all your works and in every putting forth of your hand;
11 Siku zote watakuwepo watu maskini katika nchi. Kwa hiyo ninawaamuru mwe na mikono iliyokunjuliwa kuwaelekea ndugu zenu, kuwaelekea maskini na wahitaji katika nchi yenu.
because the poor does not cease out of the land, therefore I am commanding you, saying, You certainly open your hand to your brother, to your poor and to your needy one in your land.
12 Kama Mwebrania mwenzako, mwanaume au mwanamke, akijiuza kwako na kukutumikia miaka sita, katika mwaka wa saba ni lazima umwache aende zake akiwa huru.
When your brother is sold to you, a Hebrew or a Hebrewess, and he has served you [for] six years, then in the seventh year you send him away free from you.
13 Nawe wakati utakapomwachia usimwache aende mikono mitupu.
And when you send him away free from you, you do not send him away empty;
14 Mpe kwa uhuru kutoka zizi lako la kondoo na mbuzi, kutoka sakafu yako ya kupuria nafaka na kutoka mashinikizo yako ya kukamulia divai. Mpe kama vile ambavyo Bwana Mungu wako alivyokubariki.
you certainly adorn him from your flock, and from your threshing-floor, and from your wine-vat; you give to him [from] that which your God YHWH has blessed you [with],
15 Kumbukeni kuwa ninyi mlikuwa watumwa huko Misri naye Bwana Mungu wenu aliwakomboa. Ndiyo sababu nimewapa agizo hili leo.
and you have remembered that you have been a servant in the land of Egypt, and your God YHWH ransoms you; therefore I am commanding you this thing today.
16 Lakini mtumishi wako akikuambia, “Sitaki kukuacha,” kwa sababu anakupenda wewe na jamaa yako naye anaridhika nawe,
And it has been, when he says to you, I do not go out from you, because he has loved you and your house, because [it is] good for him with you,
17 ndipo utachukua chuma kidogo utoboe sikio lake mpaka hicho chuma kiingie kwenye ubao wa mlango, naye atakuwa mtumishi wako wa maisha. Ufanye vivyo hivyo kwa mtumishi wa kike.
then you have taken the awl, and have put [it] through his ear, and through the door, and he has been a perpetual servant to you; and you also do so to your handmaid.
18 Usifikiri kuwa kuna ugumu kumwacha mtumishi wako huru, kwa sababu utumishi wake kwako kwa miaka hii sita umekuwa wa thamani mara mbili ya ujira wa mtumishi wa kuajiriwa. Naye Bwana Mungu wenu atakubarikia kwa kila kitu utakachofanya.
It is not hard in your eyes in your sending him away free from you; for [his worth has been] double the hire of a hired worker [when] he has served you six years; and your God YHWH has blessed you in all that you do.
19 Wekeni wakfu kwa Bwana Mungu wenu kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa makundi yenu ya ngʼombe na ya mbuzi na kondoo. Maksai walio wazaliwa wa kwanza msiwafanyize kazi, wala msinyoe manyoya ya wazaliwa wa kwanza wa kondoo.
Every firstling that is born in your herd and in your flock—you sanctify the male to your God YHWH; you do not work with the firstling of your ox, nor shear the firstling of your flock;
20 Kila mwaka ninyi na jamaa zenu mtapaswa kuwala mbele za Bwana Mungu wenu pale mahali atakapopachagua.
you eat it before your God YHWH year by year, in the place which YHWH chooses, you and your house.
21 Kama mnyama ana dosari, akiwa ni kilema au kipofu au kama ana kilema kibaya, kamwe usimtoe dhabihu kwa Bwana Mungu wenu.
And when there is a blemish in it, [or it is] lame or blind, [or has] any evil blemish, you do not sacrifice it to your God YHWH;
22 Itawapasa kumla ninyi wenyewe katika miji yenu. Wote wasio safi na walio safi kwa desturi za kiibada mwaweza kula kama vile mnavyokula paa au kulungu.
you eat it within your gates, the unclean and the clean alike, as the roe and as the deer.
23 Lakini kamwe msinywe damu; imwageni ardhini kama maji.
Only, you do not eat its blood—you pour it on the earth as water.”