< Torati 15 >

1 Kila mwisho wa miaka saba ni lazima mfute madeni.
At the terme of seuen yeeres thou shalt make a freedome.
2 Hivi ndivyo itakavyofanyika: Kila mkopeshaji atafuta mkopo aliomkopesha Mwisraeli mwenzake. Hatamtaka Mwisraeli mwenzake au ndugu yake amlipe hilo deni, kwa sababu wakati wa Bwana wa kufuta madeni umetangazwa.
And this is the maner of the freedome: euery creditour shall quite ye lone of his hand which he hath lent to his neighbour: he shall not aske it againe of his neighbour, nor of his brother: for the yeere of the Lords freedome is proclaimed.
3 Unaweza kudai malipo kwa mgeni, lakini lazima ufute kila deni ambalo unamdai ndugu yako.
Of a stranger thou mayest require it: but that which thou hast with thy brother, thine hand shall remit:
4 Hata hivyo, hapatakuwepo maskini miongoni mwenu, kwa kuwa katika nchi Bwana Mungu wenu anayowapa kuimiliki kama urithi wenu, atawabariki sana,
Saue when there shall be no poore with thee: for the Lord shall blesse thee in the land, which the Lord thy God giueth thee, for an inheritance to possesse it:
5 ikiwa tutamtii Bwana Mungu wenu kikamilifu na kuwa waangalifu kuyafuata maagizo haya yote ninayowapa leo.
So that thou hearken vnto the voyce of the Lord thy God to obserue and doe all these commandements, which I commande thee this day.
6 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu atawabariki kama alivyoahidi, nanyi mtawakopesha mataifa mengi lakini hamtakopa kwa yeyote. Mtatawala mataifa mengi lakini hakuna taifa litakalowatawala ninyi.
For the Lord thy God hath blessed thee, as he hath promised thee: and thou shalt lend vnto many nations, but thou thy selfe shalt not borow, and thou shalt reigne ouer many nations, and they shall not reigne ouer thee.
7 Ikiwa kuna mtu maskini miongoni mwa ndugu zenu, katika mji wowote wa hiyo nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, msiwe na moyo mgumu wala usimfumbie mkono ndugu yako aliye maskini.
If one of thy brethren with thee be poore within any of thy gates in thy land, which the Lord thy God giueth thee, thou shalt not harden thine heart, nor shut thine hand from thy poore brother:
8 Afadhali fungua mikono yako na umkopeshe kwa hiari chochote anachohitaji.
But thou shalt open thine hand vnto him, and shalt lend him sufficient for his neede which he hath.
9 Jihadhari usijiwekee wazo hili ovu: “Mwaka wa saba, mwaka wa kufuta madeni umekaribia,” usije ukaonyesha nia mbaya kwa ndugu yako mhitaji na ukaacha kumpa chochote. Anaweza kumlalamikia Bwana dhidi yako nawe utakuwa umepatikana na hatia ya dhambi.
Beware that there be not a wicked thought in thine heart, to say, The seuenth yeere, the yeere of freedome is at hand: therefore it grieueth thee to looke on thy poore brother, and thou giuest him nought, and he crie vnto the Lord against thee, so that sinne be in thee:
10 Mpe kwa ukarimu na ufanye hivyo bila kinyongo moyoni, ndipo kwa sababu ya hili Bwana Mungu wenu atakubariki katika kazi zako zote na kwa kila kitu utakachokiwekea mkono wako.
Thou shalt giue him, and let it not grieue thine heart to giue vnto him: for because of this the Lord thy God shall blesse thee in al thy works, and in all that thou puttest thine hand to.
11 Siku zote watakuwepo watu maskini katika nchi. Kwa hiyo ninawaamuru mwe na mikono iliyokunjuliwa kuwaelekea ndugu zenu, kuwaelekea maskini na wahitaji katika nchi yenu.
Because there shall be euer some poore in the land, therefore I command thee, saying, Thou shalt open thine hand vnto thy brother, to thy needie, and to thy poore in thy land.
12 Kama Mwebrania mwenzako, mwanaume au mwanamke, akijiuza kwako na kukutumikia miaka sita, katika mwaka wa saba ni lazima umwache aende zake akiwa huru.
If thy brother an Ebrewe sell himselfe to thee, or an Ebrewesse, and serue thee sixe yeere, euen in the seuenth yeere thou shalt let him goe free from thee:
13 Nawe wakati utakapomwachia usimwache aende mikono mitupu.
And when thou sendest him out free from thee, thou shalt not let him goe away emptie,
14 Mpe kwa uhuru kutoka zizi lako la kondoo na mbuzi, kutoka sakafu yako ya kupuria nafaka na kutoka mashinikizo yako ya kukamulia divai. Mpe kama vile ambavyo Bwana Mungu wako alivyokubariki.
But shalt giue him a liberall reward of thy sheepe, and of thy corne, and of thy wine: thou shalt giue him of that wherewith the Lord thy God hath blessed thee.
15 Kumbukeni kuwa ninyi mlikuwa watumwa huko Misri naye Bwana Mungu wenu aliwakomboa. Ndiyo sababu nimewapa agizo hili leo.
And remember that thou wast a seruant in the land of Egypt, and the Lord thy God deliuered thee: therefore I command thee this thing to day.
16 Lakini mtumishi wako akikuambia, “Sitaki kukuacha,” kwa sababu anakupenda wewe na jamaa yako naye anaridhika nawe,
And if he say vnto thee, I will not go away from thee, because he loueth thee and thine house, and because he is well with thee,
17 ndipo utachukua chuma kidogo utoboe sikio lake mpaka hicho chuma kiingie kwenye ubao wa mlango, naye atakuwa mtumishi wako wa maisha. Ufanye vivyo hivyo kwa mtumishi wa kike.
Then shalt thou take a naule, and perce his eare through against the doore, and he shall be thy seruant for euer: and vnto thy maid seruant thou shall doe likewise.
18 Usifikiri kuwa kuna ugumu kumwacha mtumishi wako huru, kwa sababu utumishi wake kwako kwa miaka hii sita umekuwa wa thamani mara mbili ya ujira wa mtumishi wa kuajiriwa. Naye Bwana Mungu wenu atakubarikia kwa kila kitu utakachofanya.
Let it not grieue thee, when thou lettest him goe out free from thee: for he hath serued thee sixe yeeres, which is the double worth of an hired seruant: and the Lord thy God shall blesse thee in all that thou doest.
19 Wekeni wakfu kwa Bwana Mungu wenu kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa makundi yenu ya ngʼombe na ya mbuzi na kondoo. Maksai walio wazaliwa wa kwanza msiwafanyize kazi, wala msinyoe manyoya ya wazaliwa wa kwanza wa kondoo.
All the first borne males that come of thy cattell, and of thy sheepe, thou shalt sanctifie vnto the Lord thy God. Thou shalt do no worke with thy first borne bullocke, nor sheare thy first borne sheepe.
20 Kila mwaka ninyi na jamaa zenu mtapaswa kuwala mbele za Bwana Mungu wenu pale mahali atakapopachagua.
Thou shalt eate it before the Lord thy God yeere by yeere, in the place which the Lord shall chose, both thou, and thine household.
21 Kama mnyama ana dosari, akiwa ni kilema au kipofu au kama ana kilema kibaya, kamwe usimtoe dhabihu kwa Bwana Mungu wenu.
But if there be any blemish therein, as if it be lame, or blind, or haue any euill fault, thou shalt not offer it vnto the Lord thy God,
22 Itawapasa kumla ninyi wenyewe katika miji yenu. Wote wasio safi na walio safi kwa desturi za kiibada mwaweza kula kama vile mnavyokula paa au kulungu.
But shalt eate it within thy gates: the vncleane, and the cleane shall eate it alike, as the roe bucke, and as the hart.
23 Lakini kamwe msinywe damu; imwageni ardhini kama maji.
Onely thou shalt not eate the blood thereof, but powre it vpon the ground as water.

< Torati 15 >