< Torati 15 >

1 Kila mwisho wa miaka saba ni lazima mfute madeni.
Hvert syvende Aar skal du holde Friaar.
2 Hivi ndivyo itakavyofanyika: Kila mkopeshaji atafuta mkopo aliomkopesha Mwisraeli mwenzake. Hatamtaka Mwisraeli mwenzake au ndugu yake amlipe hilo deni, kwa sababu wakati wa Bwana wa kufuta madeni umetangazwa.
Og Friaaret skal holdes saaledes: Enhver, der har en Fordring paa sin Næste, skal give Afkald derpaa; han maa ikke kræve sin Næste og sin Broder, naar et Friaar er udraabt for HERREN.
3 Unaweza kudai malipo kwa mgeni, lakini lazima ufute kila deni ambalo unamdai ndugu yako.
Udlændinge maa du kræve; men det, du har til gode hos din Broder, skal du give Afkald paa.
4 Hata hivyo, hapatakuwepo maskini miongoni mwenu, kwa kuwa katika nchi Bwana Mungu wenu anayowapa kuimiliki kama urithi wenu, atawabariki sana,
Dog, der bliver ingen fattige hos dig; thi HERREN din Gud vil rigeligt velsigne dig i det Land, HERREN din Gud vil give dig i Arv og Eje,
5 ikiwa tutamtii Bwana Mungu wenu kikamilifu na kuwa waangalifu kuyafuata maagizo haya yote ninayowapa leo.
hvis du blot vil adlyde HERREN din Guds Røst, saa du omhyggeligt handler efter alle disse Bud, som jeg i Dag paalægger dig.
6 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu atawabariki kama alivyoahidi, nanyi mtawakopesha mataifa mengi lakini hamtakopa kwa yeyote. Mtatawala mataifa mengi lakini hakuna taifa litakalowatawala ninyi.
Thi HERREN din Gud vil velsigne dig, som han lovede dig, og du skal laane ud til mange Folk, men selv skal du ikke laane; og du skal faa Magt over mange Folk, men de skal ikke faa Magt over dig.
7 Ikiwa kuna mtu maskini miongoni mwa ndugu zenu, katika mji wowote wa hiyo nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, msiwe na moyo mgumu wala usimfumbie mkono ndugu yako aliye maskini.
Naar der findes en fattig hos dig, en af dine Brødre inden dine Porte et steds i dit Land, som HERREN din Gud vil give dig, maa du ikke være haardhjertet og lukke din Haand for din fattige Broder;
8 Afadhali fungua mikono yako na umkopeshe kwa hiari chochote anachohitaji.
men du skal lukke din Haand op for ham og laane ham, hvad han savner og trænger til.
9 Jihadhari usijiwekee wazo hili ovu: “Mwaka wa saba, mwaka wa kufuta madeni umekaribia,” usije ukaonyesha nia mbaya kwa ndugu yako mhitaji na ukaacha kumpa chochote. Anaweza kumlalamikia Bwana dhidi yako nawe utakuwa umepatikana na hatia ya dhambi.
Vogt dig for, at ikke saadan nedrig Tanke kommer op i dig: »Der er ikke længe til det syvende Aar, Friaaret!« saa du ser med onde Øjne paa din fattige Broder og ikke giver ham noget; thi da vil han raabe til HERREN over dig, og du vil paadrage dig Synd.
10 Mpe kwa ukarimu na ufanye hivyo bila kinyongo moyoni, ndipo kwa sababu ya hili Bwana Mungu wenu atakubariki katika kazi zako zote na kwa kila kitu utakachokiwekea mkono wako.
Men du skal give ham villigt uden at være fortrydelig i dit Hjerte over at skulle give ham; thi for den Sags Skyld vil HERREN din Gud velsigne dig i alt dit Virke, i alt, hvad du tager dig for.
11 Siku zote watakuwepo watu maskini katika nchi. Kwa hiyo ninawaamuru mwe na mikono iliyokunjuliwa kuwaelekea ndugu zenu, kuwaelekea maskini na wahitaji katika nchi yenu.
Thi der vil aldrig mangle fattige i Landet; derfor byder jeg dig: Du skal villigt lukke din Haand op for din nødlidende og fattige Broder i dit Land.
12 Kama Mwebrania mwenzako, mwanaume au mwanamke, akijiuza kwako na kukutumikia miaka sita, katika mwaka wa saba ni lazima umwache aende zake akiwa huru.
Naar en af dine Brødre, en hebraisk Mand eller Kvinde, sælger sig til dig, skal han trælle for dig i seks Aar, men i det syvende skal du give ham fri.
13 Nawe wakati utakapomwachia usimwache aende mikono mitupu.
Og naar du giver ham fri, maa du ikke lade ham gaa med tomme Hænder;
14 Mpe kwa uhuru kutoka zizi lako la kondoo na mbuzi, kutoka sakafu yako ya kupuria nafaka na kutoka mashinikizo yako ya kukamulia divai. Mpe kama vile ambavyo Bwana Mungu wako alivyokubariki.
men du skal give ham rigeligt med af dit Smaakvæg og fra din Lo og din Perse; efter som HERREN din Gud velsigner dig, skal du give ham.
15 Kumbukeni kuwa ninyi mlikuwa watumwa huko Misri naye Bwana Mungu wenu aliwakomboa. Ndiyo sababu nimewapa agizo hili leo.
Du skal komme i Hu, at du selv var Træl i Ægypten, og at HERREN din Gud udløste dig; derfor byder jeg dig dette i Dag.
16 Lakini mtumishi wako akikuambia, “Sitaki kukuacha,” kwa sababu anakupenda wewe na jamaa yako naye anaridhika nawe,
Men hvis han siger til dig: »Jeg vil ikke forlade dig, thi jeg har faaet Kærlighed til dig og dit Hus og har det godt hos dig«,
17 ndipo utachukua chuma kidogo utoboe sikio lake mpaka hicho chuma kiingie kwenye ubao wa mlango, naye atakuwa mtumishi wako wa maisha. Ufanye vivyo hivyo kwa mtumishi wa kike.
saa skal du tage en Syl og stikke den igennem hans Øre ind i Døren, og saa skal han være din Træl for Livstid. Og paa samme Maade skal du bære dig ad med din Trælkvinde.
18 Usifikiri kuwa kuna ugumu kumwacha mtumishi wako huru, kwa sababu utumishi wake kwako kwa miaka hii sita umekuwa wa thamani mara mbili ya ujira wa mtumishi wa kuajiriwa. Naye Bwana Mungu wenu atakubarikia kwa kila kitu utakachofanya.
Du maa ikke være fortrydelig over at skulle give ham fri; thi han har ved sit Arbejde i de seks Aar ydet dig det dobbelte af en Daglejers Løn; og HERREN vil velsigne dig i alt, hvad du tager dig for.
19 Wekeni wakfu kwa Bwana Mungu wenu kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa makundi yenu ya ngʼombe na ya mbuzi na kondoo. Maksai walio wazaliwa wa kwanza msiwafanyize kazi, wala msinyoe manyoya ya wazaliwa wa kwanza wa kondoo.
Alle førstefødte Handyr, der fødes dig mellem dit Hornkvæg og Smaakvæg, skal du hellige HERREN din Gud; du maa hverken bruge det førstefødte af dine Okser til Arbejde eller klippe Ulden af det førstefødte af dine Faar.
20 Kila mwaka ninyi na jamaa zenu mtapaswa kuwala mbele za Bwana Mungu wenu pale mahali atakapopachagua.
For HERREN din Guds Aasyn skal du sammen med din Husstand fortære det Aar efter Aar paa det Sted, HERREN udvælger.
21 Kama mnyama ana dosari, akiwa ni kilema au kipofu au kama ana kilema kibaya, kamwe usimtoe dhabihu kwa Bwana Mungu wenu.
Men hvis de har en Lyde, hvis de er lamme eller blinde eller har en anden slem Lyde, maa du ikke ofre dem til HERREN din Gud.
22 Itawapasa kumla ninyi wenyewe katika miji yenu. Wote wasio safi na walio safi kwa desturi za kiibada mwaweza kula kama vile mnavyokula paa au kulungu.
Inden dine Port kan du, baade de rene og urene iblandt eder, fortære dem som Gazeller eller Hjorte.
23 Lakini kamwe msinywe damu; imwageni ardhini kama maji.
Kun Blodet maa du ikke nyde; det skal du lade løbe ud paa Jorden som Vand.

< Torati 15 >