< Torati 15 >
1 Kila mwisho wa miaka saba ni lazima mfute madeni.
Na završetku sedme godine opraštaj dugove.
2 Hivi ndivyo itakavyofanyika: Kila mkopeshaji atafuta mkopo aliomkopesha Mwisraeli mwenzake. Hatamtaka Mwisraeli mwenzake au ndugu yake amlipe hilo deni, kwa sababu wakati wa Bwana wa kufuta madeni umetangazwa.
Ovako neka bude opraštanje: neka svatko oprosti dužniku svoje potraživanje; neka ne utjeruje duga od svoga bližnjega ni od svoga brata kad se jednom proglasi Jahvino otpuštanje dugova.
3 Unaweza kudai malipo kwa mgeni, lakini lazima ufute kila deni ambalo unamdai ndugu yako.
Možeš tražiti od tuđina, ali ono što se tvoga nađe kod tvoga brata treba da otpustiš,
4 Hata hivyo, hapatakuwepo maskini miongoni mwenu, kwa kuwa katika nchi Bwana Mungu wenu anayowapa kuimiliki kama urithi wenu, atawabariki sana,
da ne bude siromaha kod tebe. TÓa Jahve će te obilno blagoslivljati u zemlji koju ti Jahve, Bog tvoj, daje u baštinu da je zaposjedneš,
5 ikiwa tutamtii Bwana Mungu wenu kikamilifu na kuwa waangalifu kuyafuata maagizo haya yote ninayowapa leo.
samo ako budeš dobro slušao glas Jahve, Boga svoga, držeći i vršeći sve ove zapovijedi što ti ih danas naređujem.
6 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu atawabariki kama alivyoahidi, nanyi mtawakopesha mataifa mengi lakini hamtakopa kwa yeyote. Mtatawala mataifa mengi lakini hakuna taifa litakalowatawala ninyi.
Jahve, Bog tvoj, blagoslivljat će te kako ti je obećao te ćeš moći zajmove davati mnogim narodima, a sam ih nećeš morati uzimati; i nad mnogim ćeš narodima vladati, dok oni nad tobom neće gospodariti.
7 Ikiwa kuna mtu maskini miongoni mwa ndugu zenu, katika mji wowote wa hiyo nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, msiwe na moyo mgumu wala usimfumbie mkono ndugu yako aliye maskini.
Nađe li se kod tebe kakav siromah, netko od tvoje braće u kojem god gradu u zemlji što ti je Jahve, Bog tvoj, dadne, ne budi tvrda srca niti zatvaraj svoje ruke prema svome siromašnome bratu,
8 Afadhali fungua mikono yako na umkopeshe kwa hiari chochote anachohitaji.
nego mu širom rastvori svoju ruku i spremno mu daj što mu nedostaje.
9 Jihadhari usijiwekee wazo hili ovu: “Mwaka wa saba, mwaka wa kufuta madeni umekaribia,” usije ukaonyesha nia mbaya kwa ndugu yako mhitaji na ukaacha kumpa chochote. Anaweza kumlalamikia Bwana dhidi yako nawe utakuwa umepatikana na hatia ya dhambi.
Čuvaj se da ti se u srcu ne porodi opaka misao te rekneš: 'Sedma se godina, godina otpuštanja dugova, već približuje' - i da prijekim okom pogledaš svoga siromašnog brata i ništa mu ne dadneš. On bi zazvao Jahvu protiv tebe i grijeh bi bio na tebi.
10 Mpe kwa ukarimu na ufanye hivyo bila kinyongo moyoni, ndipo kwa sababu ya hili Bwana Mungu wenu atakubariki katika kazi zako zote na kwa kila kitu utakachokiwekea mkono wako.
Daj mu rado, a ne da ti srce bude zlovoljno kad mu daješ, jer će te zbog toga blagoslivljati Jahve, Bog tvoj, u svakom poslu tvome i u svakom pothvatu ruku tvojih.
11 Siku zote watakuwepo watu maskini katika nchi. Kwa hiyo ninawaamuru mwe na mikono iliyokunjuliwa kuwaelekea ndugu zenu, kuwaelekea maskini na wahitaji katika nchi yenu.
Kako siromaha nikad neće nestati iz zemlje, zapovijedam ti: širom otvaraj svoju ruku svome bratu, svome siromahu i potrebitu u zemlji svojoj.
12 Kama Mwebrania mwenzako, mwanaume au mwanamke, akijiuza kwako na kukutumikia miaka sita, katika mwaka wa saba ni lazima umwache aende zake akiwa huru.
Ako se tebi proda brat tvoj - Hebrejac ili Hebrejka - neka ti služi šest godina, a sedme ga godine otpusti od sebe slobodna.
13 Nawe wakati utakapomwachia usimwache aende mikono mitupu.
Kad ga slobodna od sebe otpustiš, ne šalji ga praznih ruku.
14 Mpe kwa uhuru kutoka zizi lako la kondoo na mbuzi, kutoka sakafu yako ya kupuria nafaka na kutoka mashinikizo yako ya kukamulia divai. Mpe kama vile ambavyo Bwana Mungu wako alivyokubariki.
Daruj ga čime između stoke svoje, s gumna svoga i iz badnja svoga; čime te već Jahve, Bog tvoj, blagoslovio, od toga i njemu daj.
15 Kumbukeni kuwa ninyi mlikuwa watumwa huko Misri naye Bwana Mungu wenu aliwakomboa. Ndiyo sababu nimewapa agizo hili leo.
Sjećaj se kako si bio rob u zemlji egipatskoj i kako te Jahve, Bog tvoj, otkupio. Zato ti ovo zapovijedam danas.
16 Lakini mtumishi wako akikuambia, “Sitaki kukuacha,” kwa sababu anakupenda wewe na jamaa yako naye anaridhika nawe,
Ali ako ti on kaže: 'Neću da odlazim od tebe', jer voli tebe i dom tvoj i jer mu je kod tebe bilo dobro -
17 ndipo utachukua chuma kidogo utoboe sikio lake mpaka hicho chuma kiingie kwenye ubao wa mlango, naye atakuwa mtumishi wako wa maisha. Ufanye vivyo hivyo kwa mtumishi wa kike.
uzmi tada šilo i probuši mu uho na vratima, i neka ti bude robom zauvijek! Tako isto učini i sa svojom sluškinjom.
18 Usifikiri kuwa kuna ugumu kumwacha mtumishi wako huru, kwa sababu utumishi wake kwako kwa miaka hii sita umekuwa wa thamani mara mbili ya ujira wa mtumishi wa kuajiriwa. Naye Bwana Mungu wenu atakubarikia kwa kila kitu utakachofanya.
Kad ga budeš otpuštao od sebe slobodna, neka ti ne bude teško, jer je zavrijedio dvostruku najamničku plaću za šest godina što ti je služio. Zato će te Jahve, Bog tvoj, blagosloviti u svemu što budeš radio.
19 Wekeni wakfu kwa Bwana Mungu wenu kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa makundi yenu ya ngʼombe na ya mbuzi na kondoo. Maksai walio wazaliwa wa kwanza msiwafanyize kazi, wala msinyoe manyoya ya wazaliwa wa kwanza wa kondoo.
Sve muške prvine što ih omladi tvoja krupna i sitna stoka posveti Jahvi, Bogu svome! Stoga vola prvenca nemoj uprezati niti strići prvenca od svoje sitne stoke.
20 Kila mwaka ninyi na jamaa zenu mtapaswa kuwala mbele za Bwana Mungu wenu pale mahali atakapopachagua.
Blaguj ga ti i tvoj dom svake godine u nazočnosti Jahve, Boga svoga, u mjestu što ga odabere Jahve.
21 Kama mnyama ana dosari, akiwa ni kilema au kipofu au kama ana kilema kibaya, kamwe usimtoe dhabihu kwa Bwana Mungu wenu.
Ali ako bi imali kakvu manu, ako bi bili hromi ili slijepi ili imali kakvu god ružnu manu, nemoj ih žrtvovati Jahvi, Bogu svomu!
22 Itawapasa kumla ninyi wenyewe katika miji yenu. Wote wasio safi na walio safi kwa desturi za kiibada mwaweza kula kama vile mnavyokula paa au kulungu.
Pojedi ih u svojoj kući. I nečist i čist mogu ih jesti, kao srnu i jelena.
23 Lakini kamwe msinywe damu; imwageni ardhini kama maji.
Jedino krvi njihove ne smiješ jesti! Istoči je na zemlju kao vodu.