< Torati 14 >

1 Ninyi ni watoto wa Bwana Mungu wenu. Msijichanje ama kujinyoa upara kwenye paji la uso kwa ajili ya aliyekufa,
Soyez les enfants du Seigneur votre Dieu: vous ne vous ferez point d’incisions; et vous ne couperez point vos cheveux à cause d’un mort,
2 kwa maana ninyi ni taifa takatifu kwa Bwana Mungu wenu. Bwana amewachagua ninyi kuwa taifa la kipekee kutoka mataifa yote juu ya uso wa dunia, mwe tunu yake.
Parce que tu es un peuple consacré au Seigneur ton Dieu; et il t’a choisi, afin que tu sois son peuple particulier entre toutes les nations qui sont sur la terre.
3 Msile kitu chochote ambacho ni machukizo.
Ne mangez pas ce qui est impur.
4 Hawa ndio wanyama mtakaokula: ngʼombe, kondoo, mbuzi,
Voici les animaux que vous devez manger: le bœuf, la brebis, la chèvre,
5 kulungu, paa, kongoni, paa mweupe, mbuzi-mwitu, pofu na kondoo wa mlimani.
Le cerf, et la chèvre sauvage, le bubale, le tragélaphe, le pygargue, l’oryx, la girafe.
6 Mnaweza kumla mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika mara mbili, pia yule anayecheua.
Tout animal qui a l’ongle fendu en deux et qui rumine, vous en mangerez.
7 Hata hivyo, miongoni mwa wale wanaocheua au wale walio na kwato zilizogawanyika kamwe msile ngamia, sungura na pelele. Iwapo wanacheua, lakini hawana kwato zilizogawanyika; ni najisi kwenu kwa taratibu za kiibada.
Mais pour ceux qui ruminent, et qui n’ont pas l’ongle fendu, comme le chameau, le lièvre, le chœrogrylle, vous ne devez pas en manger: parce que ces animaux ruminent, mais qu’ils n’ont pas l’ongle fendu, ils seront impurs pour vous.
8 Nguruwe pia ni najisi; ingawa ana kwato zilizogawanyika, hacheui. Msile nyama yake wala kugusa mzoga wake.
Le pourceau aussi, puisqu’il a l’ongle fendu, mais qu’il ne rumine point, sera impur; vous ne mangerez point de leur chair, et vous ne toucherez point leurs corps morts.
9 Katika viumbe hai vyote viishivyo kwenye maji, mnaweza kula yeyote aliye na mapezi na magamba.
Voici les bêtes que vous mangerez entre toutes celles qui vivent dans les eaux: celles qui ont des nageoires et des écailles, mangez-les;
10 Lakini chochote kisicho na mapezi na magamba msile; kwenu ni najisi.
Celles qui sont sans nageoires et sans écailles, ne les mangez point, parce qu’elles sont impures.
11 Mnaweza kula ndege yeyote aliye safi.
Mangez tous les oiseaux purs.
12 Lakini wafuatao msiwale: tai, furukombe, kipungu,
Ne mangez point les impurs: c’est-à-dire l’aigle, le griffon et l’aigle de mer,
13 kengewa mwekundu, kengewa mweusi, mwewe wa aina yoyote,
L’ixion, le vautour et le milan, selon son espèce;
14 kunguru wa aina yoyote,
Tout ce qui est de l’espèce du corbeau;
15 mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga wa aina yoyote,
L’autruche, le hibou, le larus et l’épervier, selon son espèce;
16 bundi, mumbi, bundi mkubwa,
Le héron, le cygne, l’ibis,
17 mwari, nderi, mnandi,
Le plongeon, le porphyrion, la chouette,
18 korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
L’onocrotale et le pluvier, chacun dans son espèce; la huppe aussi et la chauve-souris.
19 Wadudu wote warukao kwa makundi ni najisi kwenu, msiwale.
Et tout ce qui rampe sur la terre et qui a des ailes, sera impur, et ne se mangera pas.
20 Lakini viumbe vyote vyenye mabawa vilivyo safi mwaweza kula.
Mangez tout ce qui est pur.
21 Msile kitu chochote mtakachokuta kimekufa. Mnaweza kumpa mgeni yeyote anayeishi katika mojawapo ya miji yenu, naye anaweza kula au mnaweza kumuuzia mtu wa nchi nyingine. Lakini ninyi ni watu watakatifu kwa Bwana Mungu wenu. Msitokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
Quant à tout animal qui est crevé, n’en mangez point; donne-le à l’étranger qui est au-dedans de tes portes, afin qu’il en mange, ou vends-lui, parce que toi, tu es le peuple saint du Seigneur ton Dieu. Tu ne feras point cuire un chevreau dans le lait de sa mère.
22 Hakikisheni mmetenga sehemu ya kumi ya mazao yote ya mashamba yenu kila mwaka.
Tu sépareras la dixième partie de tous les fruits qui naissent dans la terre tous les ans;
23 Mtakula zaka za nafaka yenu, divai mpya, mafuta na wazaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ngʼombe na ya kondoo na mbuzi mbele za Bwana Mungu wenu pale mahali atakapopachagua kama maskani kwa ajili ya Jina lake, ili kwamba mpate kujifunza kumheshimu Bwana Mungu wenu daima.
Et tu en mangeras en la présence du Seigneur ton Dieu, au lieu qu’il aura choisi, afin que son nom y soit invoqué, le dixième de ton blé, de ton vin, de ton huile, et les premiers-nés de ton gros bétail et de tes brebis; afin que tu apprennes à craindre le Seigneur ton Dieu en tout temps.
24 Lakini ikiwa mahali pale ni mbali sana nanyi mmebarikiwa na Bwana Mungu wenu na hamwezi kubeba zaka yenu (kwa sababu mahali pale Bwana atakapopachagua kuliweka Jina lake ni mbali sana),
Mais lorsque le chemin sera trop long jusqu’au lieu qu’aura choisi le Seigneur ton Dieu, et lorsqu’il t’aura béni, et que tu ne pourras pas lui apporter toutes ces offrandes,
25 basi badilisheni zaka yenu kuwa fedha, mkaichukue hiyo fedha mwende nayo mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua.
Tu vendras tout, tu en feras de l’argent, puis tu le porteras en ta main, et tu partiras pour le lieu qu’aura choisi le Seigneur ton Dieu;
26 Tumieni hiyo fedha kununua chochote ukitakacho: ngʼombe, kondoo, divai au kinywaji chochote chenye chachu au chochote mnachotaka. Kisha ninyi na wa nyumbani mwenu mtaila mbele za Bwana Mungu wenu na kufurahi.
Tu achèteras avec ce même argent tout ce qui te plaira, soit en gros bétail, soit en brebis, du vin aussi et de la cervoise, et tout ce que désire ton âme; et tu mangeras devant le Seigneur ton Dieu, et tu feras un festin, toi et ta maison;
27 Msiache kuwajali Walawi waishio katika miji yenu, kwa kuwa hao hawana shamba wala urithi wao wenyewe.
Et le Lévite qui est au-dedans de tes portes, garde-toi de l’abandonner, parce qu’il n’a pas d’autre part dans ta sion.
28 Mwishoni mwa kila mwaka wa tatu, leteni zaka zote za mazao ya miaka ile na uyahifadhi kwenye miji yenu,
À la troisième année, tu sépareras une autre dîme de tout ce qui te vient en ce temps, et tu la réserveras au-dedans de tes portes.
29 ili Walawi (ambao hawana mashamba wala urithi wao wenyewe) na wageni, yatima na wajane wanaoishi kwenye miji yenu wapate kuja kula na kushiba, ili Bwana Mungu wenu apate kuwabariki ninyi katika kazi zote za mikono yenu.
Et il viendra, le Lévite qui n’a point de part ni de possession avec toi, ainsi que l’étranger, l’orphelin et la veuve qui sont au dedans de tes portes, et ils mangeront et se rassasieront, afin que le Seigneur ton Dieu te bénisse dans tous les ouvrages de tes mains que tu feras.

< Torati 14 >