< Torati 14 >

1 Ninyi ni watoto wa Bwana Mungu wenu. Msijichanje ama kujinyoa upara kwenye paji la uso kwa ajili ya aliyekufa,
Vous êtes les enfants de Yahweh, votre Dieu. Vous ne vous ferez point d’incision et vous ne vous tondrez point une place entre les yeux pour un mort.
2 kwa maana ninyi ni taifa takatifu kwa Bwana Mungu wenu. Bwana amewachagua ninyi kuwa taifa la kipekee kutoka mataifa yote juu ya uso wa dunia, mwe tunu yake.
Car tu es un peuple saint à Yahweh, ton Dieu; et Yahweh t’a choisi pour lui être un peuple particulier entre tous les peuples qui sont sur la face de la terre.
3 Msile kitu chochote ambacho ni machukizo.
Tu ne mangeras aucune chose abominable.
4 Hawa ndio wanyama mtakaokula: ngʼombe, kondoo, mbuzi,
Voici les animaux dont vous mangerez: le bœuf, la brebis et la chèvre;
5 kulungu, paa, kongoni, paa mweupe, mbuzi-mwitu, pofu na kondoo wa mlimani.
le cerf, la gazelle et le daim; le bouquetin, l’antilope, le bœuf sauvage et la chèvre sauvage.
6 Mnaweza kumla mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika mara mbili, pia yule anayecheua.
Vous mangerez de tout animal qui a la corne divisée et le pied fourchu, et qui rumine.
7 Hata hivyo, miongoni mwa wale wanaocheua au wale walio na kwato zilizogawanyika kamwe msile ngamia, sungura na pelele. Iwapo wanacheua, lakini hawana kwato zilizogawanyika; ni najisi kwenu kwa taratibu za kiibada.
Mais vous ne mangerez pas de ceux qui ruminent seulement, ou qui ont seulement la corne divisée et le pied fourchu; tels sont le chameau, le lièvre et le lapin, qui ruminent, mais qui n’ont pas la corne divisée: ils seront impurs pour vous;
8 Nguruwe pia ni najisi; ingawa ana kwato zilizogawanyika, hacheui. Msile nyama yake wala kugusa mzoga wake.
tel est encore le porc, qui a la corne divisée, mais qui ne rumine pas: il sera impur pour vous. Vous ne mangerez pas de leur chair, et vous ne toucherez pas leurs corps morts.
9 Katika viumbe hai vyote viishivyo kwenye maji, mnaweza kula yeyote aliye na mapezi na magamba.
Voici les animaux que vous mangerez parmi tous ceux qui sont dans les eaux: vous mangerez de tout ce qui a nageoires et écailles;
10 Lakini chochote kisicho na mapezi na magamba msile; kwenu ni najisi.
mais tout ce qui n’a pas nageoires et écailles, vous ne le mangerez pas: ce sera impur pour vous.
11 Mnaweza kula ndege yeyote aliye safi.
Vous mangerez tout oiseau pur.
12 Lakini wafuatao msiwale: tai, furukombe, kipungu,
Voici ceux dont vous ne mangerez pas: l’aigle, l’orfraie et le vautour;
13 kengewa mwekundu, kengewa mweusi, mwewe wa aina yoyote,
le faucon, le milan et toute espèce d’autours;
14 kunguru wa aina yoyote,
toute espèce de corbeaux;
15 mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga wa aina yoyote,
l’autruche, le hibou, la mouette et toute espèce d’éperviers;
16 bundi, mumbi, bundi mkubwa,
le chat-huant, l’ibis et la chouette;
17 mwari, nderi, mnandi,
le pélican, le cormoran et le plongeon;
18 korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
la cigogne et toute espèce de hérons; la huppe et la chauve-souris.
19 Wadudu wote warukao kwa makundi ni najisi kwenu, msiwale.
Vous regarderez comme impur tout insecte ailé: on n’en mangera pas.
20 Lakini viumbe vyote vyenye mabawa vilivyo safi mwaweza kula.
Vous mangerez tout oiseau pur.
21 Msile kitu chochote mtakachokuta kimekufa. Mnaweza kumpa mgeni yeyote anayeishi katika mojawapo ya miji yenu, naye anaweza kula au mnaweza kumuuzia mtu wa nchi nyingine. Lakini ninyi ni watu watakatifu kwa Bwana Mungu wenu. Msitokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
Vous ne mangerez d’aucune bête morte. Tu la donneras à l’étranger qui est dans tes portes, pour qu’il la mange, ou tu la vendras à un étranger; car tu es un peuple saint à Yahweh, ton Dieu. Tu ne feras pas cuire un chevreau dans le lait de sa mère.
22 Hakikisheni mmetenga sehemu ya kumi ya mazao yote ya mashamba yenu kila mwaka.
Tu lèveras la dîme de tout le produit de tes semailles, de ce que ton champ rapportera chaque année.
23 Mtakula zaka za nafaka yenu, divai mpya, mafuta na wazaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ngʼombe na ya kondoo na mbuzi mbele za Bwana Mungu wenu pale mahali atakapopachagua kama maskani kwa ajili ya Jina lake, ili kwamba mpate kujifunza kumheshimu Bwana Mungu wenu daima.
Et tu mangeras devant Yahweh, ton Dieu, dans le lieu qu’il aura choisi pour y faire habiter son nom, la dîme de ton blé, de ton vin nouveau et de ton huile, ainsi que les premiers-nés de tes bœufs et de tes brebis, afin que tu apprennes à craindre Yahweh, ton Dieu, à jamais.
24 Lakini ikiwa mahali pale ni mbali sana nanyi mmebarikiwa na Bwana Mungu wenu na hamwezi kubeba zaka yenu (kwa sababu mahali pale Bwana atakapopachagua kuliweka Jina lake ni mbali sana),
Mais si le chemin est trop long pour toi, et que tu ne puisses l’ y transporter, parce que le lieu que Yahweh choisira pour y faire habiter son nom sera trop loin de toi, lorsque Yahweh, ton Dieu, t’aura béni:
25 basi badilisheni zaka yenu kuwa fedha, mkaichukue hiyo fedha mwende nayo mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua.
tu échangeras ta dîme pour de l’argent et, ayant serré l’argent dans ta main, tu iras au lieu que Yahweh, ton Dieu, aura choisi.
26 Tumieni hiyo fedha kununua chochote ukitakacho: ngʼombe, kondoo, divai au kinywaji chochote chenye chachu au chochote mnachotaka. Kisha ninyi na wa nyumbani mwenu mtaila mbele za Bwana Mungu wenu na kufurahi.
Là, tu achèteras avec l’argent tout ce que désirera ton âme, des bœufs, des brebis, du vin, des liqueurs fermentées, tout ce que demandera ton âme, et tu mangeras là devant Yahweh, ton Dieu, et tu te réjouiras, toi et ta maison.
27 Msiache kuwajali Walawi waishio katika miji yenu, kwa kuwa hao hawana shamba wala urithi wao wenyewe.
Tu ne délaisseras pas le Lévite qui sera dans tes portes, car il n’a ni part ni héritage avec toi.
28 Mwishoni mwa kila mwaka wa tatu, leteni zaka zote za mazao ya miaka ile na uyahifadhi kwenye miji yenu,
À la fin de chaque troisième année, tu mettras à part toute la dîme de tes produits de cette année-là, et tu la déposeras dans tes portes.
29 ili Walawi (ambao hawana mashamba wala urithi wao wenyewe) na wageni, yatima na wajane wanaoishi kwenye miji yenu wapate kuja kula na kushiba, ili Bwana Mungu wenu apate kuwabariki ninyi katika kazi zote za mikono yenu.
Alors viendra le Lévite, qui n’a ni part ni héritage avec toi, ainsi que l’étranger, l’orphelin et la veuve, qui seront dans tes portes, et ils mangeront et se rassasieront, afin que Yahweh, ton Dieu, te bénisse dans toutes les œuvres que tu entreprendras de tes mains.

< Torati 14 >