< Torati 14 >

1 Ninyi ni watoto wa Bwana Mungu wenu. Msijichanje ama kujinyoa upara kwenye paji la uso kwa ajili ya aliyekufa,
You are the children of Yahweh your God. You shall not cut yourselves, nor make any baldness between your eyes for the dead.
2 kwa maana ninyi ni taifa takatifu kwa Bwana Mungu wenu. Bwana amewachagua ninyi kuwa taifa la kipekee kutoka mataifa yote juu ya uso wa dunia, mwe tunu yake.
For you are a holy people to Yahweh your God, and Yahweh has chosen you to be a people for his own possession, above all peoples who are on the face of the earth.
3 Msile kitu chochote ambacho ni machukizo.
You shall not eat any abominable thing.
4 Hawa ndio wanyama mtakaokula: ngʼombe, kondoo, mbuzi,
These are the animals which you may eat: the ox, the sheep, the goat,
5 kulungu, paa, kongoni, paa mweupe, mbuzi-mwitu, pofu na kondoo wa mlimani.
the deer, the gazelle, the roebuck, the wild goat, the ibex, the antelope, and the chamois.
6 Mnaweza kumla mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika mara mbili, pia yule anayecheua.
Every animal that parts the hoof, and has the hoof split in two and chews the cud, among the animals, you may eat.
7 Hata hivyo, miongoni mwa wale wanaocheua au wale walio na kwato zilizogawanyika kamwe msile ngamia, sungura na pelele. Iwapo wanacheua, lakini hawana kwato zilizogawanyika; ni najisi kwenu kwa taratibu za kiibada.
Nevertheless these you shall not eat of them that chew the cud, or of those who have the hoof split: the camel, the hare, and the rabbit. Because they chew the cud but don’t part the hoof, they are unclean to you.
8 Nguruwe pia ni najisi; ingawa ana kwato zilizogawanyika, hacheui. Msile nyama yake wala kugusa mzoga wake.
The pig, because it has a split hoof but doesn’t chew the cud, is unclean to you. You shall not eat their meat. You shall not touch their carcasses.
9 Katika viumbe hai vyote viishivyo kwenye maji, mnaweza kula yeyote aliye na mapezi na magamba.
These you may eat of all that are in the waters: you may eat whatever has fins and scales.
10 Lakini chochote kisicho na mapezi na magamba msile; kwenu ni najisi.
You shall not eat whatever doesn’t have fins and scales. It is unclean to you.
11 Mnaweza kula ndege yeyote aliye safi.
Of all clean birds you may eat.
12 Lakini wafuatao msiwale: tai, furukombe, kipungu,
But these are they of which you shall not eat: the eagle, the vulture, the osprey,
13 kengewa mwekundu, kengewa mweusi, mwewe wa aina yoyote,
the red kite, the falcon, the kite of any kind,
14 kunguru wa aina yoyote,
every raven of any kind,
15 mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga wa aina yoyote,
the ostrich, the owl, the seagull, the hawk of any kind,
16 bundi, mumbi, bundi mkubwa,
the little owl, the great owl, the horned owl,
17 mwari, nderi, mnandi,
the pelican, the vulture, the cormorant,
18 korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
the stork, the heron after its kind, the hoopoe, and the bat.
19 Wadudu wote warukao kwa makundi ni najisi kwenu, msiwale.
All winged creeping things are unclean to you. They shall not be eaten.
20 Lakini viumbe vyote vyenye mabawa vilivyo safi mwaweza kula.
Of all clean birds you may eat.
21 Msile kitu chochote mtakachokuta kimekufa. Mnaweza kumpa mgeni yeyote anayeishi katika mojawapo ya miji yenu, naye anaweza kula au mnaweza kumuuzia mtu wa nchi nyingine. Lakini ninyi ni watu watakatifu kwa Bwana Mungu wenu. Msitokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
You shall not eat of anything that dies of itself. You may give it to the foreigner living among you who is within your gates, that he may eat it; or you may sell it to a foreigner; for you are a holy people to Yahweh your God. You shall not boil a young goat in its mother’s milk.
22 Hakikisheni mmetenga sehemu ya kumi ya mazao yote ya mashamba yenu kila mwaka.
You shall surely tithe all the increase of your seed, that which comes out of the field year by year.
23 Mtakula zaka za nafaka yenu, divai mpya, mafuta na wazaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ngʼombe na ya kondoo na mbuzi mbele za Bwana Mungu wenu pale mahali atakapopachagua kama maskani kwa ajili ya Jina lake, ili kwamba mpate kujifunza kumheshimu Bwana Mungu wenu daima.
You shall eat before Yahweh your God, in the place which he chooses to cause his name to dwell, the tithe of your grain, of your new wine, and of your oil, and the firstborn of your herd and of your flock; that you may learn to fear Yahweh your God always.
24 Lakini ikiwa mahali pale ni mbali sana nanyi mmebarikiwa na Bwana Mungu wenu na hamwezi kubeba zaka yenu (kwa sababu mahali pale Bwana atakapopachagua kuliweka Jina lake ni mbali sana),
If the way is too long for you, so that you are not able to carry it because the place which Yahweh your God shall choose to set his name there is too far from you, when Yahweh your God blesses you,
25 basi badilisheni zaka yenu kuwa fedha, mkaichukue hiyo fedha mwende nayo mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua.
then you shall turn it into money, bind up the money in your hand, and shall go to the place which Yahweh your God shall choose.
26 Tumieni hiyo fedha kununua chochote ukitakacho: ngʼombe, kondoo, divai au kinywaji chochote chenye chachu au chochote mnachotaka. Kisha ninyi na wa nyumbani mwenu mtaila mbele za Bwana Mungu wenu na kufurahi.
You shall trade the money for whatever your soul desires: for cattle, or for sheep, or for wine, or for strong drink, or for whatever your soul asks of you. You shall eat there before Yahweh your God, and you shall rejoice, you and your household.
27 Msiache kuwajali Walawi waishio katika miji yenu, kwa kuwa hao hawana shamba wala urithi wao wenyewe.
You shall not forsake the Levite who is within your gates, for he has no portion nor inheritance with you.
28 Mwishoni mwa kila mwaka wa tatu, leteni zaka zote za mazao ya miaka ile na uyahifadhi kwenye miji yenu,
At the end of every three years you shall bring all the tithe of your increase in the same year, and shall store it within your gates.
29 ili Walawi (ambao hawana mashamba wala urithi wao wenyewe) na wageni, yatima na wajane wanaoishi kwenye miji yenu wapate kuja kula na kushiba, ili Bwana Mungu wenu apate kuwabariki ninyi katika kazi zote za mikono yenu.
The Levite, because he has no portion nor inheritance with you, as well as the foreigner living among you, the fatherless, and the widow who are within your gates shall come, and shall eat and be satisfied; that Yahweh your God may bless you in all the work of your hand which you do.

< Torati 14 >