< Torati 14 >
1 Ninyi ni watoto wa Bwana Mungu wenu. Msijichanje ama kujinyoa upara kwenye paji la uso kwa ajili ya aliyekufa,
Ye are the children of the Lord your God. Ye shall not cut yourselues, nor make you any baldnesse betweene your eyes for the dead.
2 kwa maana ninyi ni taifa takatifu kwa Bwana Mungu wenu. Bwana amewachagua ninyi kuwa taifa la kipekee kutoka mataifa yote juu ya uso wa dunia, mwe tunu yake.
For thou art an holy people vnto ye Lord thy God, and the Lord hath chosen thee to be a precious people vnto himselfe, aboue all the people that are vpon the earth.
3 Msile kitu chochote ambacho ni machukizo.
Thou shalt eate no maner of abomination.
4 Hawa ndio wanyama mtakaokula: ngʼombe, kondoo, mbuzi,
These are the beastes, which ye shall eate, the beefe, the sheepe, and the goate,
5 kulungu, paa, kongoni, paa mweupe, mbuzi-mwitu, pofu na kondoo wa mlimani.
The hart, and the roe buck, and the bugle, and the wilde goate, and the vnicorne, and the wilde oxe, and the chamois.
6 Mnaweza kumla mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika mara mbili, pia yule anayecheua.
And euery beast that parteth ye hoofe, and cleaueth the clift into two clawes, and is of the beasts that cheweth the cudde, that shall ye eate.
7 Hata hivyo, miongoni mwa wale wanaocheua au wale walio na kwato zilizogawanyika kamwe msile ngamia, sungura na pelele. Iwapo wanacheua, lakini hawana kwato zilizogawanyika; ni najisi kwenu kwa taratibu za kiibada.
But these ye shall not eate, of them that chew the cud, and of them that deuide and cleaue the hoofe onely: ye camell, nor the hare, nor the cony: for they chewe the cudde, but deuide not ye hoofe: therefore they shall be vncleane vnto you:
8 Nguruwe pia ni najisi; ingawa ana kwato zilizogawanyika, hacheui. Msile nyama yake wala kugusa mzoga wake.
Also the swine, because he deuideth the hoofe, and cheweth not the cud, shalbe vncleane vnto you: ye shall not eate of their flesh, nor touch their dead carkeises.
9 Katika viumbe hai vyote viishivyo kwenye maji, mnaweza kula yeyote aliye na mapezi na magamba.
These ye shall eate, of all that are in the waters: all that haue finnes and scales shall ye eate.
10 Lakini chochote kisicho na mapezi na magamba msile; kwenu ni najisi.
And whatsoeuer hath no finnes nor scales, ye shall not eate: it shall be vncleane vnto you.
11 Mnaweza kula ndege yeyote aliye safi.
Of all cleane birdes ye shall eate:
12 Lakini wafuatao msiwale: tai, furukombe, kipungu,
But these are they, whereof ye shall not eate: the eagle, nor the goshawke, nor the osprey,
13 kengewa mwekundu, kengewa mweusi, mwewe wa aina yoyote,
Nor the glead nor the kite, nor the vulture, after their kind,
14 kunguru wa aina yoyote,
Nor all kinde of rauens,
15 mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga wa aina yoyote,
Nor the ostrich, nor the nightcrow, nor the semeaw, nor the hawke after her kinde,
16 bundi, mumbi, bundi mkubwa,
Neither the litle owle, nor the great owle, nor the redshanke,
Nor the pellicane, nor the swanne, nor the cormorant:
18 korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
The storke also, and the heron in his kinde, nor the lapwing, nor the backe.
19 Wadudu wote warukao kwa makundi ni najisi kwenu, msiwale.
And euery creeping thing that flieth, shall be vncleane vnto you: it shall not be eaten.
20 Lakini viumbe vyote vyenye mabawa vilivyo safi mwaweza kula.
But of all cleane foules ye may eate.
21 Msile kitu chochote mtakachokuta kimekufa. Mnaweza kumpa mgeni yeyote anayeishi katika mojawapo ya miji yenu, naye anaweza kula au mnaweza kumuuzia mtu wa nchi nyingine. Lakini ninyi ni watu watakatifu kwa Bwana Mungu wenu. Msitokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
Ye shall eate of nothing that dieth alone, but thou shalt giue it vnto the stranger that is within thy gates, that he may eate it: or thou maiest sell it vnto a stranger: for thou art an holy people vnto the Lord thy God. Thou shalt not seethe a kid in his mothers milke.
22 Hakikisheni mmetenga sehemu ya kumi ya mazao yote ya mashamba yenu kila mwaka.
Thou shalt giue the tithe of all the increase of thy seede, that commeth foorth of the fielde yeere by yeere.
23 Mtakula zaka za nafaka yenu, divai mpya, mafuta na wazaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ngʼombe na ya kondoo na mbuzi mbele za Bwana Mungu wenu pale mahali atakapopachagua kama maskani kwa ajili ya Jina lake, ili kwamba mpate kujifunza kumheshimu Bwana Mungu wenu daima.
And thou shalt eate before the Lord thy God (in the place which he shall chose to cause his Name to dwell there) the tithe of thy corne, of thy wine, and of thine oyle, and the first borne of thy kine and of thy sheepe, that thou maiest learne to feare the Lord thy God alway.
24 Lakini ikiwa mahali pale ni mbali sana nanyi mmebarikiwa na Bwana Mungu wenu na hamwezi kubeba zaka yenu (kwa sababu mahali pale Bwana atakapopachagua kuliweka Jina lake ni mbali sana),
And if the way be too long for thee, so that thou art not able to cary it, because the place is farre from thee, where the Lord thy God shall chose to set his Name, when the Lord thy God shall blesse thee,
25 basi badilisheni zaka yenu kuwa fedha, mkaichukue hiyo fedha mwende nayo mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua.
Then shalt thou make it in money, and take the money in thine hand, and goe vnto the place which the Lord thy God shall chose.
26 Tumieni hiyo fedha kununua chochote ukitakacho: ngʼombe, kondoo, divai au kinywaji chochote chenye chachu au chochote mnachotaka. Kisha ninyi na wa nyumbani mwenu mtaila mbele za Bwana Mungu wenu na kufurahi.
And thou shalt bestowe the money for whatsoeuer thine heart desireth: whether it be oxe, or sheepe, or wine, or strong drinke, or whatsoeuer thine heart desireth: and shalt eate it there before the Lord thy God, and reioyce, both thou, and thine household.
27 Msiache kuwajali Walawi waishio katika miji yenu, kwa kuwa hao hawana shamba wala urithi wao wenyewe.
And the Leuite that is within thy gates, shalt thou not forsake: for he hath neither part nor inheritance with thee.
28 Mwishoni mwa kila mwaka wa tatu, leteni zaka zote za mazao ya miaka ile na uyahifadhi kwenye miji yenu,
At the end of three yeere thou shalt bring foorth all the tithes of thine increase of the same yeere, and lay it vp within thy gates.
29 ili Walawi (ambao hawana mashamba wala urithi wao wenyewe) na wageni, yatima na wajane wanaoishi kwenye miji yenu wapate kuja kula na kushiba, ili Bwana Mungu wenu apate kuwabariki ninyi katika kazi zote za mikono yenu.
Then ye Leuite shall come, because he hath no part nor inheritance with thee, and the stranger, and the fatherlesse, and the widowe, which are within thy gates, and shall eate, and be filled, that the Lord thy God may blesse thee in al the worke of thine hand which thou doest.