< Torati 12 >

1 Hizi ndizo amri na sheria ambazo ni lazima mwe waangalifu kuzifuata katika nchi ambayo Bwana, Mungu wa baba zenu, amewapa kumiliki, kwa muda wote mtakaoishi katika nchi.
Estas son las leyes y las decisiones que deben tomar con cuidado en la tierra que el Señor, el Dios de sus padres, les ha dado para que sea su herencia todos los días de su vida en la tierra.
2 Haribuni kabisa kila mahali pao pa kuabudia kwenye milima mirefu, vilima na chini ya kila mti mkubwa ambamo mataifa haya mnayokwenda kuchukua ardhi yao huabudia miungu yao.
Destruirán por completo en todos aquellos lugares donde las naciones, a quienes ustedes van expulsar, adoran a sus dioses, en las montañas altas y las colinas y debajo de cada árbol frondoso:
3 Bomoeni madhabahu zao, vunjeni yale mawe wanayoabudu, chomeni moto nguzo zao za Ashera; katilieni mbali sanamu za miungu yao na mfute majina yao mahali hapo.
Sus altares y sus pilares serán derribados, y sus árboles sagrados serán quemados con fuego, y las imágenes de sus dioses serán derribadas; Deben borrar sus nombres de ese lugar.
4 Kamwe msimwabudu Bwana Mungu wenu kama wanavyoabudu wao.
No deben adorar al Señor su Dios de esta manera.
5 Bali mtatafuta mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua katika makabila yenu yote ili aliweke jina lake huko kuwa makao yake. Mahali hapo ndipo iwapasapo kwenda;
Pero vuelvan sus corazones al lugar que será escogido por el Señor su Dios, entre sus tribus, para poner su nombre allí y ustedes podrán ir adorarlo;
6 hapo ndipo mtakapoleta sadaka zenu za kuteketezwa na dhabihu, zaka zenu na changizo zenu, kile ulichoweka nadhiri kutoa, sadaka zenu za hiari na malimbuko ya makundi yenu ya ngʼombe pamoja na mbuzi na kondoo.
Y allí tienes que llevar sus ofrendas quemadas y otras ofrendas, y la décima parte de sus bienes, y las ofrendas para ser levantadas al Señor, y las ofrendas de sus juramentos, y las que ofreces libremente por el impulso de sus corazones y los primeros nacimientos entre sus vacas y sus ovejas;
7 Hapo, katika uwepo wa Bwana Mungu wenu, ninyi pamoja na jamaa zenu, mtakula na kufurahia kila kitu ambacho mmegusa kwa mikono yenu, kwa sababu Bwana Mungu wenu amewabariki.
Allí, ustedes y todas sus familias deben hacer una fiesta delante del Señor su Dios, con gozo en todo lo que pones, porque el Señor les ha dado su bendición.
8 Msifanye kama tunavyofanya hapa leo, kila mtu anavyopenda mwenyewe,
No deben hacer las cosas de la manera en que ahora las hacemos aquí, cada hombre como le parezca correcto:
9 kwa kuwa bado hamjafikia mahali pa mapumziko na urithi ambao Bwana Mungu wenu anawapa.
Porque no han venido al descanso ni a la herencia que el Señor su Dios les está dando.
10 Lakini mtavuka Yordani na kuishi katika nchi Bwana Mungu wenu anayowapa kama urithi, naye atawapa pumziko kutokana na adui zenu wote wanaowazunguka ili ninyi mpate kuishi kwa salama.
Pero cuando hayan cruzado el Jordán y estén viviendo en la tierra que el Señor su Dios les está dando como su herencia, y cuando los haya librado de todos los que luchan contra ustedes, y ustedes estén viviendo allí a salvo;
11 Kisha kuhusu mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua kuwa mahali pa makao ya Jina lake, hapo ndipo inapowapasa kuleta kila kitu ninachowaamuru: sadaka zenu za kuteketezwa na dhabihu, zaka zenu na changizo, pamoja na vitu vyote vyenye thamani ambavyo mmeweka nadhiri kumtolea Bwana.
Entonces habrá un lugar escogido por el Señor su Dios como lugar de descanso para su nombre, y allí ofrecerán todas las cosas que les he ordenado: sus ofrendas quemadas y sacrificios, y la décima parte de sus bienes, y las ofrendas para ser levantadas, y las ofrendas de sus juramentos que hacen al Señor;
12 Hapo furahini mbele za Bwana Mungu wenu, ninyi, wana wenu na binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, pamoja na Walawi kutoka miji yenu ambao hawana mgawo wala urithi wao wenyewe.
Y te alegrarás delante del Señor su Dios, ustedes y sus hijos y sus hijas, y sus siervos y sus siervas, y el levita que está entre ustedes en su casa, porque no tiene parte ni herencia entre ustedes.
13 Kuweni waangalifu, msitoe dhabihu zenu za kuteketezwa mahali popote mnapopapenda.
Tengan cuidado de no hacer sus ofrendas quemadas en cualquier lugar que vean:
14 Mtazitoa tu mahali pale ambapo Bwana atachagua katika mojawapo ya makabila yenu, nanyi hapo zingatieni kila jambo ninalowaamuru.
Pero en el lugar señalado por el Señor en una de tus tribus, que se ofrezcan sus ofrendas quemadas, y haz lo que te he ordenado que hagas.
15 Hata hivyo, mnaweza kuwachinja wanyama wenu katika miji yenu yoyote ile na kula nyama nyingi mpendavyo kama vile mmemchinja paa au kulungu, kulingana na baraka mtakazojaliwa na Bwana Mungu wenu. Watu walio najisi au walio safi wanaweza kula.
Solo pueden matar animales, como la gacela y él ciervo, para tu alimento en cualquiera de tus pueblos, según el deseo de tu alma, de acuerdo con la bendición del Señor tu Dios que él les ha dado. Él impuro y él limpio lo comerá.
16 Lakini kamwe usinywe damu; imwage juu ya ardhi kama maji.
Pero no pueden tomar la sangre como alimento, se debe drenar en la tierra como el agua.
17 Hamruhusiwi kula katika miji yenu zaka yenu ya nafaka, ya divai mpya na ya mafuta, au mzaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ngʼombe na makundi yenu ya mbuzi na kondoo, wala chochote ambacho mmeweka nadhiri kukitoa, au sadaka zako za hiari, wala matoleo maalum.
En tus ciudades no debes tomar como alimento la décima parte de tu grano, o de tu vino o tu aceite, o los primeros nacimientos de tu ganado o de tus rebaños, o cualquier cosa ofrecida bajo un juramento, o libremente ofrecido al Señor, o dado como ofrenda mecida;
18 Badala yake, mtakula vitu hivyo katika uwepo wa Bwana Mungu wenu mahali ambapo Bwana Mungu wenu atapachagua: wewe, wana wako na binti zako, watumishi wako wa kiume na wa kike, na Walawi kutoka miji yenu. Mnatakiwa mfurahi mbele za Bwana Mungu wenu kwa kula kitu mtakachoweka mikono yenu.
Pero comerán su alimento delante del Señor tu Dios en el lugar de su elección, donde podrán alegrarse delante de él, con su hijo y su hija, y su sirviente y su sierva, y el levita quien vive entre ustedes: y tendrán gozo delante del Señor su Dios por todo lo que pone en su mano.
19 Mwe waangalifu msiwapuuze Walawi kwa muda wote mnaoishi katika nchi yenu.
Asegúrense de no dejar de cuidar al levita mientras vivas en tu tierra.
20 Bwana Mungu wenu atakapokuwa ameongeza nchi yenu kama alivyowaahidi, nanyi mkitamani nyama na mkisema, “Ningependa nyama,” hapo unaweza kula nyingi upendavyo.
Cuando el Señor tu Dios amplíe el límite de tu tierra, como él ha dicho, y ustedes digan: Tomaré carne por mi comida, porque la deseo; entonces pueden comer cualquier carne que deseen.
21 Kama mahali ambapo Bwana Mungu wenu atapachagua kuweka Jina lake ni mbali sana kutoka kwenu, unaweza kuchinja wanyama kutoka makundi yenu ya ngʼombe, ya mbuzi na ya kondoo ambayo Bwana amewapa, kama nilivyokuamuru, na mkiwa katika miji yenu wenyewe mnaweza kula nyingi mtakavyo.
Si el lugar señalado por el Señor tu Dios como lugar de descanso para su nombre está lejos de ustedes, entonces podrás matar de tu ganado y de tus rebaños que el Señor les ha dado, como he dicho, y Coman en los pueblos donde están viviendo todo lo que desee su corazón.
22 Mle kama vile mngekula paa na kulungu. Wote walio najisi kiibada na walio safi mwaweza kula.
Será tu comida, como la gacela y el ciervo; él impuro y limpio podrán comer de ello.
23 Lakini hakikisheni kwamba hamkunywa damu, kwa sababu damu ni uhai, kamwe msile uhai pamoja na nyama.
Pero mira que no tomes la sangre para comer; porque la sangre es la vida; y no podrás hacer uso de la vida como alimento con la carne.
24 Hamruhusiwi kamwe kunywa damu; imwageni juu ya ardhi kama maji.
No la comerás como alimento, sino que lo derramarás en la tierra como el agua.
25 Msinywe damu, ili mweze kufanikiwa ninyi pamoja na watoto wenu baada yenu, kwa sababu mtakuwa mkifanya lililo haki machoni pa Bwana.
No la tomes por comida; para que les vaya bien a ti y a tus hijos después de ustedes, mientras hacen lo correcto ante los ojos del Señor.
26 Lakini vichukueni vitu vyenu vilivyowekwa wakfu pamoja na vile mlivyoweka nadhiri, mwende mahali pale Bwana atakapopachagua.
Pero las cosas santas que tienes, y las ofrendas de tus juramentos, deben llevarlas al lugar que será escogido por el Señor:
27 Leteni sadaka zenu za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana Mungu wenu, vyote nyama na damu. Damu ya dhabihu zenu lazima imiminwe kando ya madhabahu ya Bwana Mungu wenu, lakini nyama mnaweza kula.
Ofrecerán la carne y la sangre de tus holocaustos sobre el altar del Señor tu Dios; y la sangre de sus ofrendas será derramada sobre el altar del Señor tu Dios, y podrás comer la carne.
28 Mwe waangalifu kutii masharti haya yote ninayowapa, ili kwamba siku zote mweze kufanikiwa, ninyi pamoja na watoto wenu baada yenu, kwa sababu mtakuwa mkifanya lililo jema na sahihi mbele za macho ya Bwana Mungu wenu.
Toma nota de todas estas órdenes que te estoy dando y presten atención a ellas, para que te vaya bien a ti y a tus hijos después de ustedes, mientras hacen lo que es bueno y correcto a los ojos del Señor su Dios.
29 Bwana Mungu wenu atayakatilia mbali mbele yenu mataifa ambayo punde kidogo mtayavamia na kuyaondoa. Lakini mtakapokuwa mmeyafukuza na kuishi katika nchi yao,
Cuando el pueblo de la tierra a la que se dirigen haya sido destruida por el Señor tu Dios, y hayan tomado su tierra y estén viviendo en ella;
30 na baada ya kuangamizwa mbele yenu, mwe waangalifu msijiingize katika tanzi kwa kuuliza habari za miungu yao, mkisema, “Je, mataifa haya hutumikiaje miungu yao? Nasi tutafanya vivyo hivyo.”
Después de su destrucción, cuídate de no seguir sus caminos y de no pensar en sus dioses, diciendo: Cómo adoraron estas naciones a sus dioses Haré lo que ellos hicieron.
31 Kamwe msimwabudu Bwana Mungu wenu kwa njia wanayoabudu miungu yao, kwa sababu katika kuabudu miungu yao, wanafanya aina zote za machukizo anayoyachukia Bwana. Hata huwateketeza wana wao na binti zao kwa moto kama kafara kwa miungu yao.
No hagan esto al Señor tu Dios: porque todo lo que es repugnante para el Señor y odiado por él, lo han hecho en honor de sus dioses: incluso quemando a sus hijos e hijas en el fuego a sus dioses.
32 Angalieni kwamba mnafanya yote niliyowaamuru; msiongeze kitu wala msipunguze kitu.
Deben guardar con cuidado todas las palabras que les doy, sin agregar nada y sin quitarle nada.

< Torati 12 >