< Torati 12 >
1 Hizi ndizo amri na sheria ambazo ni lazima mwe waangalifu kuzifuata katika nchi ambayo Bwana, Mungu wa baba zenu, amewapa kumiliki, kwa muda wote mtakaoishi katika nchi.
These are the statutes and the decrees that you will keep in the land that Yahweh, the God of your fathers, has given you to possess, all the days that you live on the earth.
2 Haribuni kabisa kila mahali pao pa kuabudia kwenye milima mirefu, vilima na chini ya kila mti mkubwa ambamo mataifa haya mnayokwenda kuchukua ardhi yao huabudia miungu yao.
You will surely destroy all the places where the nations that you will dispossess worshiped their gods, on the high mountains, on the hills, and under every green tree.
3 Bomoeni madhabahu zao, vunjeni yale mawe wanayoabudu, chomeni moto nguzo zao za Ashera; katilieni mbali sanamu za miungu yao na mfute majina yao mahali hapo.
You must break down their altars, dash in pieces their stone pillars, and burn their Asherah poles. You must cut down the carved figures of their gods and destroy their name out of that place.
4 Kamwe msimwabudu Bwana Mungu wenu kama wanavyoabudu wao.
You will not worship Yahweh your God like that.
5 Bali mtatafuta mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua katika makabila yenu yote ili aliweke jina lake huko kuwa makao yake. Mahali hapo ndipo iwapasapo kwenda;
But to the place that Yahweh your God will choose out of all your tribes to put his name, that will be the place where he lives, and it is there that you will go.
6 hapo ndipo mtakapoleta sadaka zenu za kuteketezwa na dhabihu, zaka zenu na changizo zenu, kile ulichoweka nadhiri kutoa, sadaka zenu za hiari na malimbuko ya makundi yenu ya ngʼombe pamoja na mbuzi na kondoo.
It is there that you will bring your burnt offerings, your sacrifices, your tithes, and the offerings presented by your hand, your offerings for vows, your freewill offerings, and the firstborn of your herds and flocks.
7 Hapo, katika uwepo wa Bwana Mungu wenu, ninyi pamoja na jamaa zenu, mtakula na kufurahia kila kitu ambacho mmegusa kwa mikono yenu, kwa sababu Bwana Mungu wenu amewabariki.
It is there that you will eat before Yahweh your God and rejoice about everything that you have put your hand to, you and your households, where Yahweh your God has blessed you.
8 Msifanye kama tunavyofanya hapa leo, kila mtu anavyopenda mwenyewe,
You will not do all the things that we are doing here today; now everyone is doing whatever is right in his own eyes;
9 kwa kuwa bado hamjafikia mahali pa mapumziko na urithi ambao Bwana Mungu wenu anawapa.
for you have not yet come to the rest, to the inheritance that Yahweh your God is giving you.
10 Lakini mtavuka Yordani na kuishi katika nchi Bwana Mungu wenu anayowapa kama urithi, naye atawapa pumziko kutokana na adui zenu wote wanaowazunguka ili ninyi mpate kuishi kwa salama.
But when you go over the Jordan and live in the land that Yahweh your God is causing you to inherit, and he will give you rest from all your enemies round about, so that you live in safety.
11 Kisha kuhusu mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua kuwa mahali pa makao ya Jina lake, hapo ndipo inapowapasa kuleta kila kitu ninachowaamuru: sadaka zenu za kuteketezwa na dhabihu, zaka zenu na changizo, pamoja na vitu vyote vyenye thamani ambavyo mmeweka nadhiri kumtolea Bwana.
Then to the place where Yahweh your God will choose to cause his name to live there—there you will bring everything I command you: your burnt offerings, your sacrifices, your tithes, and the offerings presented by your hand, and all your choice offerings for vows that you will vow to Yahweh.
12 Hapo furahini mbele za Bwana Mungu wenu, ninyi, wana wenu na binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, pamoja na Walawi kutoka miji yenu ambao hawana mgawo wala urithi wao wenyewe.
You will rejoice before Yahweh your God—you, your sons, your daughters, your male servants, your female servants, and the Levites who are within your gate, because he has no portion or inheritance among you.
13 Kuweni waangalifu, msitoe dhabihu zenu za kuteketezwa mahali popote mnapopapenda.
Pay attention to yourself that you do not offer your burnt offerings at every place that you see;
14 Mtazitoa tu mahali pale ambapo Bwana atachagua katika mojawapo ya makabila yenu, nanyi hapo zingatieni kila jambo ninalowaamuru.
but it is at the place that Yahweh will choose among one of your tribes that you will offer your burnt offerings, and there you will do everything that I command you.
15 Hata hivyo, mnaweza kuwachinja wanyama wenu katika miji yenu yoyote ile na kula nyama nyingi mpendavyo kama vile mmemchinja paa au kulungu, kulingana na baraka mtakazojaliwa na Bwana Mungu wenu. Watu walio najisi au walio safi wanaweza kula.
However, you may kill and eat animals within all your gates, as you wish, receiving the blessing of Yahweh your God for all that he has given you; the unclean and the clean persons both may eat of it, animals such as the gazelle and the deer.
16 Lakini kamwe usinywe damu; imwage juu ya ardhi kama maji.
But you will not eat the blood; you will pour it out on the earth like water.
17 Hamruhusiwi kula katika miji yenu zaka yenu ya nafaka, ya divai mpya na ya mafuta, au mzaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ngʼombe na makundi yenu ya mbuzi na kondoo, wala chochote ambacho mmeweka nadhiri kukitoa, au sadaka zako za hiari, wala matoleo maalum.
You may not eat within your gates from the tithe of your grain, your new wine, your oil, or the firstborn of your herd or flock; and you may not eat any of the meat you sacrifice along with any of your vows that you make, nor that of your freewill offerings, nor that of the offering you present with your hand.
18 Badala yake, mtakula vitu hivyo katika uwepo wa Bwana Mungu wenu mahali ambapo Bwana Mungu wenu atapachagua: wewe, wana wako na binti zako, watumishi wako wa kiume na wa kike, na Walawi kutoka miji yenu. Mnatakiwa mfurahi mbele za Bwana Mungu wenu kwa kula kitu mtakachoweka mikono yenu.
Instead, you will eat them before Yahweh your God in the place that Yahweh your God will choose—you, your son, your daughter, your male servant, your female servant, and the Levite who is within your gates; you will rejoice before Yahweh your God about everything to which you put your hand.
19 Mwe waangalifu msiwapuuze Walawi kwa muda wote mnaoishi katika nchi yenu.
Pay attention to yourself so that you do not forsake the Levite as long as you live on your land.
20 Bwana Mungu wenu atakapokuwa ameongeza nchi yenu kama alivyowaahidi, nanyi mkitamani nyama na mkisema, “Ningependa nyama,” hapo unaweza kula nyingi upendavyo.
When Yahweh your God enlarges your borders, as he has promised you, and you say, 'I will eat flesh,' because of your desire to eat meat, you may eat meat, as your soul desires.
21 Kama mahali ambapo Bwana Mungu wenu atapachagua kuweka Jina lake ni mbali sana kutoka kwenu, unaweza kuchinja wanyama kutoka makundi yenu ya ngʼombe, ya mbuzi na ya kondoo ambayo Bwana amewapa, kama nilivyokuamuru, na mkiwa katika miji yenu wenyewe mnaweza kula nyingi mtakavyo.
If the place that Yahweh your God chooses to put his name is too far from you, then you will kill some of your herd and your flock that Yahweh has given you, as I have commanded you; you may eat within your gates, as your soul desires.
22 Mle kama vile mngekula paa na kulungu. Wote walio najisi kiibada na walio safi mwaweza kula.
Like the gazelle and the deer are eaten, so you will eat of it; the unclean and the clean persons may eat of it alike.
23 Lakini hakikisheni kwamba hamkunywa damu, kwa sababu damu ni uhai, kamwe msile uhai pamoja na nyama.
Only be sure that you do not consume the blood, for the blood is the life; you will not eat the life with the meat.
24 Hamruhusiwi kamwe kunywa damu; imwageni juu ya ardhi kama maji.
You will not eat it; you will pour it out on the earth like water.
25 Msinywe damu, ili mweze kufanikiwa ninyi pamoja na watoto wenu baada yenu, kwa sababu mtakuwa mkifanya lililo haki machoni pa Bwana.
You will not eat it, so that it may go well with you, and with your children after you, when you will do what is right in the eyes of Yahweh.
26 Lakini vichukueni vitu vyenu vilivyowekwa wakfu pamoja na vile mlivyoweka nadhiri, mwende mahali pale Bwana atakapopachagua.
But the things that belong to Yahweh that you have and the offerings for your vows—you will take these and go to the place that Yahweh chooses.
27 Leteni sadaka zenu za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana Mungu wenu, vyote nyama na damu. Damu ya dhabihu zenu lazima imiminwe kando ya madhabahu ya Bwana Mungu wenu, lakini nyama mnaweza kula.
There you will offer your burnt offerings, the meat and the blood, on the altar of Yahweh your God; the blood of your sacrifices will be poured out on the altar of Yahweh your God, and you will eat the flesh.
28 Mwe waangalifu kutii masharti haya yote ninayowapa, ili kwamba siku zote mweze kufanikiwa, ninyi pamoja na watoto wenu baada yenu, kwa sababu mtakuwa mkifanya lililo jema na sahihi mbele za macho ya Bwana Mungu wenu.
Observe and listen to all these words that I command you, that it may go well with you and with your children after you forever, when you do what is good and right in the eyes of Yahweh your God.
29 Bwana Mungu wenu atayakatilia mbali mbele yenu mataifa ambayo punde kidogo mtayavamia na kuyaondoa. Lakini mtakapokuwa mmeyafukuza na kuishi katika nchi yao,
When Yahweh your God cuts off the nations from before you, when you go in to dispossess them, and you dispossess them, and live in their land,
30 na baada ya kuangamizwa mbele yenu, mwe waangalifu msijiingize katika tanzi kwa kuuliza habari za miungu yao, mkisema, “Je, mataifa haya hutumikiaje miungu yao? Nasi tutafanya vivyo hivyo.”
pay attention to yourself that you are not trapped into following them, after they are destroyed from before you—trapped into investigating their gods, into asking, 'How do these nations worship their gods? I will do the same.'
31 Kamwe msimwabudu Bwana Mungu wenu kwa njia wanayoabudu miungu yao, kwa sababu katika kuabudu miungu yao, wanafanya aina zote za machukizo anayoyachukia Bwana. Hata huwateketeza wana wao na binti zao kwa moto kama kafara kwa miungu yao.
You must not worship Yahweh your God in that way, for everything that is an abomination to Yahweh, things that he hates—they have done these with their gods; they even burn their sons and their daughters in fire for their gods.
32 Angalieni kwamba mnafanya yote niliyowaamuru; msiongeze kitu wala msipunguze kitu.
Whatever I command you, observe it. Do not add to it or take away from it.