< Torati 12 >
1 Hizi ndizo amri na sheria ambazo ni lazima mwe waangalifu kuzifuata katika nchi ambayo Bwana, Mungu wa baba zenu, amewapa kumiliki, kwa muda wote mtakaoishi katika nchi.
And these [are] the ordinances and the judgments, which ye shall observe to do in the land, which the Lord God of your fathers gives you for an inheritance, all the days which ye live upon the land.
2 Haribuni kabisa kila mahali pao pa kuabudia kwenye milima mirefu, vilima na chini ya kila mti mkubwa ambamo mataifa haya mnayokwenda kuchukua ardhi yao huabudia miungu yao.
Ye shall utterly destroy all the places in which they served their gods, whose [land] ye inherit, on the high mountains and on the hills, and under the thick tree.
3 Bomoeni madhabahu zao, vunjeni yale mawe wanayoabudu, chomeni moto nguzo zao za Ashera; katilieni mbali sanamu za miungu yao na mfute majina yao mahali hapo.
And ye shall destroy their altars, and break in pieces their pillars, and ye shall cut down their groves, and ye shall burn with fire the graven images of their gods, and ye shall abolish their name out of that place.
4 Kamwe msimwabudu Bwana Mungu wenu kama wanavyoabudu wao.
Ye shall not do so to the Lord your God.
5 Bali mtatafuta mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua katika makabila yenu yote ili aliweke jina lake huko kuwa makao yake. Mahali hapo ndipo iwapasapo kwenda;
But in the place which the Lord thy God shall choose in one of your cities to name his name there, and to be called upon, ye shall even seek [him] out and go thither.
6 hapo ndipo mtakapoleta sadaka zenu za kuteketezwa na dhabihu, zaka zenu na changizo zenu, kile ulichoweka nadhiri kutoa, sadaka zenu za hiari na malimbuko ya makundi yenu ya ngʼombe pamoja na mbuzi na kondoo.
And ye shall carry thither your whole-burnt-offerings, and your sacrifices, and your first-fruits, and your vowed-offerings, and your freewill-offerings, and your offerings of thanksgiving, the first-born of your herds, and of your flocks.
7 Hapo, katika uwepo wa Bwana Mungu wenu, ninyi pamoja na jamaa zenu, mtakula na kufurahia kila kitu ambacho mmegusa kwa mikono yenu, kwa sababu Bwana Mungu wenu amewabariki.
And ye shall eat there before the Lord your God, and ye shall rejoice in all the things on which ye shall lay your hand, ye and your houses, as the Lord your God has blessed you.
8 Msifanye kama tunavyofanya hapa leo, kila mtu anavyopenda mwenyewe,
Ye shall not do altogether as we do here to-day, every man that which is pleasing in his own sight.
9 kwa kuwa bado hamjafikia mahali pa mapumziko na urithi ambao Bwana Mungu wenu anawapa.
For hitherto ye have not arrived at the rest and the inheritance, which the Lord our God gives you.
10 Lakini mtavuka Yordani na kuishi katika nchi Bwana Mungu wenu anayowapa kama urithi, naye atawapa pumziko kutokana na adui zenu wote wanaowazunguka ili ninyi mpate kuishi kwa salama.
And ye shall go over Jordan, and shall dwell in the land, which the Lord our God takes as an inheritance for you; and he shall give you rest from all your enemies round about, and ye shall dwell safely.
11 Kisha kuhusu mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua kuwa mahali pa makao ya Jina lake, hapo ndipo inapowapasa kuleta kila kitu ninachowaamuru: sadaka zenu za kuteketezwa na dhabihu, zaka zenu na changizo, pamoja na vitu vyote vyenye thamani ambavyo mmeweka nadhiri kumtolea Bwana.
And there shall be a place which the Lord thy God shall choose for his name to be called there, thither shall ye bring all things that I order you to-day; your whole-burnt-offerings, and your sacrifices, and your tithes, and the first-fruits of your hands, and every choice gift of yours, whatsoever ye shall vow to the Lord your God.
12 Hapo furahini mbele za Bwana Mungu wenu, ninyi, wana wenu na binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, pamoja na Walawi kutoka miji yenu ambao hawana mgawo wala urithi wao wenyewe.
And ye shall rejoice before the Lord your God, ye and your sons, and your daughters, and your men-servants and your maid-servants, and the Levite that is at your gates; because he has no portion or inheritance with you.
13 Kuweni waangalifu, msitoe dhabihu zenu za kuteketezwa mahali popote mnapopapenda.
Take heed to thyself that thou offer not thy whole-burnt-offerings in any place which thou shalt see;
14 Mtazitoa tu mahali pale ambapo Bwana atachagua katika mojawapo ya makabila yenu, nanyi hapo zingatieni kila jambo ninalowaamuru.
save in the place which the Lord thy God shall choose, in one of thy tribes, there shall ye offer your whole-burnt-offerings, and there shalt thou do all things whatsoever I charge thee this day.
15 Hata hivyo, mnaweza kuwachinja wanyama wenu katika miji yenu yoyote ile na kula nyama nyingi mpendavyo kama vile mmemchinja paa au kulungu, kulingana na baraka mtakazojaliwa na Bwana Mungu wenu. Watu walio najisi au walio safi wanaweza kula.
But thou shalt kill according to all thy desire, and shalt eat flesh according to the blessing of the Lord thy God, which he has given thee in every city; the unclean that is within thee and the clean shall eat it on equal terms, as the doe or the stag.
16 Lakini kamwe usinywe damu; imwage juu ya ardhi kama maji.
Only ye shall not eat the blood; ye shall pour it out on the ground as water.
17 Hamruhusiwi kula katika miji yenu zaka yenu ya nafaka, ya divai mpya na ya mafuta, au mzaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ngʼombe na makundi yenu ya mbuzi na kondoo, wala chochote ambacho mmeweka nadhiri kukitoa, au sadaka zako za hiari, wala matoleo maalum.
Thou shalt not be able to eat in thy cities the tithe of thy corn, and of thy wine, and of thine oil, the first-born of thine herd and of thy flock, and all [your] vows as many as ye shall have vowed, and your thank-offerings, and the first-fruits of thine hands.
18 Badala yake, mtakula vitu hivyo katika uwepo wa Bwana Mungu wenu mahali ambapo Bwana Mungu wenu atapachagua: wewe, wana wako na binti zako, watumishi wako wa kiume na wa kike, na Walawi kutoka miji yenu. Mnatakiwa mfurahi mbele za Bwana Mungu wenu kwa kula kitu mtakachoweka mikono yenu.
But before the Lord thy God thou shalt eat it, in the place which the Lord thy God shall choose for himself, thou, and thy son, and thy daughter, thy man-servant, and thy maid-servant, and the stranger that is within thy gates; and thou shalt rejoice before the Lord thy God, on whatsoever thou shalt lay thine hand.
19 Mwe waangalifu msiwapuuze Walawi kwa muda wote mnaoishi katika nchi yenu.
Take heed to thyself that thou do not desert the Levite all the time that thou livest upon the earth.
20 Bwana Mungu wenu atakapokuwa ameongeza nchi yenu kama alivyowaahidi, nanyi mkitamani nyama na mkisema, “Ningependa nyama,” hapo unaweza kula nyingi upendavyo.
And if the Lord thy God shall enlarge thy borders, as he said to thee, and thou shalt say, I will eat flesh; if thy soul should desire to eat flesh, thou shalt eat flesh according to all the desire of thy soul.
21 Kama mahali ambapo Bwana Mungu wenu atapachagua kuweka Jina lake ni mbali sana kutoka kwenu, unaweza kuchinja wanyama kutoka makundi yenu ya ngʼombe, ya mbuzi na ya kondoo ambayo Bwana amewapa, kama nilivyokuamuru, na mkiwa katika miji yenu wenyewe mnaweza kula nyingi mtakavyo.
And if the place be far from thee, which the Lord thy God shall choose for himself, that his name be called upon it, then thou shalt kill of thy herd and of thy flock which God shall have given thee, even as I commanded thee, and thou shalt eat in thy cities according to the desire of thy soul.
22 Mle kama vile mngekula paa na kulungu. Wote walio najisi kiibada na walio safi mwaweza kula.
As the doe and the stag are eaten, so shalt thou eat it; the unclean in thee and the clean shall eat it in like manner.
23 Lakini hakikisheni kwamba hamkunywa damu, kwa sababu damu ni uhai, kamwe msile uhai pamoja na nyama.
Take diligent heed that thou eat no blood, for blood [is] the life of it; the life shall not be eaten with the flesh.
24 Hamruhusiwi kamwe kunywa damu; imwageni juu ya ardhi kama maji.
Ye shall not eat [it]; ye shall pour it out on the ground as water.
25 Msinywe damu, ili mweze kufanikiwa ninyi pamoja na watoto wenu baada yenu, kwa sababu mtakuwa mkifanya lililo haki machoni pa Bwana.
Thou shalt not eat it, that it may be well with thee and with thy sons after thee, if thou shalt do that which is good and pleasing before the Lord thy God.
26 Lakini vichukueni vitu vyenu vilivyowekwa wakfu pamoja na vile mlivyoweka nadhiri, mwende mahali pale Bwana atakapopachagua.
But thou shalt take thy holy things, if thou hast any, and thy vowed-offerings, and come to the place which the Lord thy God shall choose to have his name named upon it.
27 Leteni sadaka zenu za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana Mungu wenu, vyote nyama na damu. Damu ya dhabihu zenu lazima imiminwe kando ya madhabahu ya Bwana Mungu wenu, lakini nyama mnaweza kula.
And thou shalt sacrifice thy whole-burnt-offerings, thou shalt offer the flesh upon the altar of the Lord thy God; but the blood of thy sacrifices thou shalt pour out at the foot of the altar of the Lord thy God, but the flesh thou shalt eat.
28 Mwe waangalifu kutii masharti haya yote ninayowapa, ili kwamba siku zote mweze kufanikiwa, ninyi pamoja na watoto wenu baada yenu, kwa sababu mtakuwa mkifanya lililo jema na sahihi mbele za macho ya Bwana Mungu wenu.
Beware and hearken, and thou shalt do all the commands which I charge thee, that it may be well with thee and with thy sons for ever, if thou shalt do that which is pleasing and good before the Lord thy God.
29 Bwana Mungu wenu atayakatilia mbali mbele yenu mataifa ambayo punde kidogo mtayavamia na kuyaondoa. Lakini mtakapokuwa mmeyafukuza na kuishi katika nchi yao,
And if the Lord thy God shall utterly destroy the nations, to whom thou goest in thither to inherit their land, from before thee, and thou shalt inherit it, and dwell in their land;
30 na baada ya kuangamizwa mbele yenu, mwe waangalifu msijiingize katika tanzi kwa kuuliza habari za miungu yao, mkisema, “Je, mataifa haya hutumikiaje miungu yao? Nasi tutafanya vivyo hivyo.”
take heed to thyself that thou seek not to follow them after they are destroyed before thee, saying, How do these nations act towards their gods? I will do likewise.
31 Kamwe msimwabudu Bwana Mungu wenu kwa njia wanayoabudu miungu yao, kwa sababu katika kuabudu miungu yao, wanafanya aina zote za machukizo anayoyachukia Bwana. Hata huwateketeza wana wao na binti zao kwa moto kama kafara kwa miungu yao.
Thou shalt not do so to thy God; for they have sacrificed to their gods the abominations of the Lord which he hates, for they burn their sons and their daughters in fire to their gods.
32 Angalieni kwamba mnafanya yote niliyowaamuru; msiongeze kitu wala msipunguze kitu.
Every word that I command you this day, it shalt thou observe to do: thou shalt not add to it, nor diminish from it.