< Torati 10 >

1 Wakati ule Bwana aliniambia, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza uje kwangu juu mlimani. Pia utengeneze Sanduku la mbao.
Naquela época Yahweh me disse: “Corte duas tábuas de pedra como a primeira, e venha até mim na montanha, e faça uma arca de madeira”.
2 Nitaandika juu ya vibao maneno yaliyokuwa katika vile vibao vya kwanza, ambavyo ulivivunja. Kisha utaviweka ndani ya Sanduku.”
Vou escrever nas tábuas as palavras que estavam nas primeiras tábuas que você quebrou, e você as colocará na arca”.
3 Hivyo nikatengeneza Sanduku kwa mti wa mshita, nikachonga pia vibao vya mawe kama vile vya kwanza, kisha nikakwea mlimani nikiwa na vibao viwili mikononi mwangu.
Então fiz uma arca de madeira de acácia, cortei duas tábuas de pedra como a primeira, e subi à montanha, tendo as duas tábuas na mão.
4 Bwana akaandika juu ya hivi vibao kile alichokuwa amekiandika kabla, Amri Kumi alizokuwa amewatangazia juu mlimani, kutoka kwenye moto siku ile ya kusanyiko. Bwana akanikabidhi.
Ele escreveu nas tábuas, de acordo com o primeiro escrito, os dez mandamentos, que Javé falou com você na montanha fora do meio do fogo no dia da assembléia; e Javé os deu a mim.
5 Kisha nikashuka kutoka mlimani na kuweka vibao ndani ya Sanduku nililokuwa nimelitengeneza, kama Bwana alivyoniagiza, navyo viko huko sasa.
Eu me virei e desci da montanha, e coloquei as tábuas na arca que eu tinha feito; e lá estão elas como Iavé me ordenou.
6 (Waisraeli walisafiri kutoka visima vya Yaakani hadi Mosera. Huko Aroni alifariki na kuzikwa, naye Eleazari mwanawe akachukua nafasi yake kama kuhani.
(As crianças de Israel viajaram de Beeroth Bene Jaakan para Moserah. Lá Arão morreu, e lá ele foi enterrado; e Eleazar, seu filho, ministrou no escritório do sacerdote em seu lugar.
7 Kutoka pale, walisafiri hadi Gudgoda wakaendelea mpaka Yotbatha, nchi yenye vijito vya maji.
De lá eles viajaram para Gudgodah; e de Gudgodah para Jotbathah, uma terra de riachos de água.
8 Wakati huo Bwana aliteua kabila la Lawi kulibeba Sanduku la Agano la Bwana, kusimama mbele za Bwana ili kutoa huduma, na kutangaza baraka kwa Jina lake, kama wanavyofanya mpaka leo.
Naquele tempo Yahweh separou a tribo de Levi para carregar a arca do pacto de Yahweh, para estar diante de Yahweh para ministrar a ele, e para abençoar em seu nome, até os dias de hoje.
9 Hiyo ndiyo sababu ya Walawi kutokuwa na sehemu wala urithi miongoni mwa ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama Bwana Mungu wao alivyowaambia.)
Portanto, Levi não tem parte nem herança com seus irmãos; Iavé é sua herança, segundo Iavé, seu Deus falou com ele).
10 Basi nilikaa mlimani kwa siku arobaini usiku na mchana, kama nilivyofanya mara ya kwanza, pia Bwana alinisikiliza hata wakati huu. Haikuwa nia yake kuwaangamiza.
Eu fiquei na montanha, como na primeira vez, quarenta dias e quarenta noites; e Javé também me escutou daquela vez. Yahweh não o destruiria.
11 Bwana akaniambia, “Nenda, ukawaongoze watu katika njia yao ili kwamba waweze kuingia na kuimiliki nchi ile niliyowaapia baba zao kuwapa.”
Javé me disse: “Levantem-se, façam sua viagem diante do povo; e eles entrarão e possuirão a terra que jurei a seus pais que lhes daria”.
12 Na sasa, ee Israeli, Bwana Mungu wako anataka nini kwako ila kumcha Bwana Mungu wako, kwenda katika njia zake, kumpenda na kumtumikia Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote,
Agora, Israel, o que o Senhor teu Deus exige de ti, mas temer o Senhor teu Deus, caminhar em todos os seus caminhos, amá-lo e servir o Senhor teu Deus com todo o teu coração e com toda a tua alma,
13 na kuyashika maagizo ya Bwana na amri zake ninazokupa leo kwa mafanikio yako mwenyewe?
para guardar os mandamentos e estatutos do Senhor, que eu te ordeno hoje para teu bem?
14 Mbingu, hata mbingu za juu sana, dunia na kila kitu kilichomo ndani yake, ni mali ya Bwana Mungu wako.
Eis que a Javé, vosso Deus, pertence ao céu, ao céu dos céus e à terra, com tudo o que nela existe.
15 Hata hivyo Bwana alikuwa na shauku na baba zako, akawapenda na akawachagua ninyi, wazao wao, kuliko mataifa yote, kama ilivyo leo.
Somente Javé teve o prazer de seus pais para amá-los, e ele escolheu seus descendentes depois deles, mesmo você acima de todos os povos, como é hoje.
16 Kwa hiyo tahirini mioyo yenu, na msiwe na shingo ngumu tena.
Circuncide, portanto, o prepúcio de seu coração, e não seja mais de pescoço duro.
17 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni Mungu wa miungu na Bwana wa mabwana, Mungu mkuu, mwenye uweza na wa kutisha, ambaye hana upendeleo na hapokei rushwa.
Para Javé, vosso Deus, ele é Deus dos deuses e Senhor dos senhores, o grande Deus, o poderoso e o incrível, que não respeita as pessoas nem aceita subornos.
18 Huwapigania yatima na wajane, humpenda mgeni, akimpa chakula na mavazi.
Ele faz justiça para os órfãos de pai e viúva e ama o estrangeiro ao dar-lhe comida e roupas.
19 Nanyi wapendeni wageni, kwa kuwa ninyi wenyewe mlikuwa wageni huko Misri.
Portanto, ama o estrangeiro, pois foram estrangeiros na terra do Egito.
20 Mche Bwana Mungu wako na umtumikie yeye. Shikamana naye kwa uthabiti na kuapa kwa jina lake.
Você temerá a Javé, seu Deus. Você o servirá. Apegar-te-ás a ele, e jurarás pelo seu nome.
21 Yeye ni sifa yako; yeye ni Mungu wako, ambaye alikutendea yale maajabu makubwa na ya kutisha uliyoyaona kwa macho yako mwenyewe.
Ele é vosso louvor, e ele é vosso Deus, que fez por vós estas grandes e espantosas coisas que vossos olhos viram.
22 Baba zako walioshuka kwenda Misri jumla yao walikuwa sabini, na sasa Bwana Mungu wako amekufanya wengi kama nyota za angani.
Seus pais desceram ao Egito com setenta pessoas; e agora Javé, vosso Deus, vos fez como as estrelas do céu para a multidão.

< Torati 10 >