< Torati 10 >

1 Wakati ule Bwana aliniambia, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza uje kwangu juu mlimani. Pia utengeneze Sanduku la mbao.
En ce temps-là le Seigneur me dit: Taille-toi deux tables de pierre, comme les premières étaient, et monte vers moi sur la montagne, et tu feras une arche de bois,
2 Nitaandika juu ya vibao maneno yaliyokuwa katika vile vibao vya kwanza, ambavyo ulivivunja. Kisha utaviweka ndani ya Sanduku.”
Et j’écrirai sur ces tables les paroles qui étaient sur celles que tu as déjà brisées, et tu les placeras dans l’arche.
3 Hivyo nikatengeneza Sanduku kwa mti wa mshita, nikachonga pia vibao vya mawe kama vile vya kwanza, kisha nikakwea mlimani nikiwa na vibao viwili mikononi mwangu.
Je fis donc une arche de bois de sétim. Et lorsque j’eus taillé deux tables de pierre comme les premières, je montai sur la montagne, les ayant en mes mains.
4 Bwana akaandika juu ya hivi vibao kile alichokuwa amekiandika kabla, Amri Kumi alizokuwa amewatangazia juu mlimani, kutoka kwenye moto siku ile ya kusanyiko. Bwana akanikabidhi.
Et le Seigneur écrivit sur ces tables, selon ce qu’il avait d’abord écrit, les dix paroles qu’il vous adressa sur la montagne, du milieu du feu, quand le peuple était assemblé, et il me les donna.
5 Kisha nikashuka kutoka mlimani na kuweka vibao ndani ya Sanduku nililokuwa nimelitengeneza, kama Bwana alivyoniagiza, navyo viko huko sasa.
Et revenu de la montagne, je descendis, et je plaçai les tables dans l’arche que j’avais faite; et elles y sont demeurées jusqu’ici, comme le Seigneur m’a commandé.
6 (Waisraeli walisafiri kutoka visima vya Yaakani hadi Mosera. Huko Aroni alifariki na kuzikwa, naye Eleazari mwanawe akachukua nafasi yake kama kuhani.
Or les enfants d’Israël transportèrent leur camp de Béroth des enfants de Jacan à Moséra, où mourut et fut enseveli Aaron, à la place duquel Eléazar, son fils, exerça les fonctions du sacerdoce.
7 Kutoka pale, walisafiri hadi Gudgoda wakaendelea mpaka Yotbatha, nchi yenye vijito vya maji.
De là ils vinrent à Gadgad, et partis de ce lieu, ils campèrent à Jétébatha, terre d’eaux et de torrents.
8 Wakati huo Bwana aliteua kabila la Lawi kulibeba Sanduku la Agano la Bwana, kusimama mbele za Bwana ili kutoa huduma, na kutangaza baraka kwa Jina lake, kama wanavyofanya mpaka leo.
En ce temps-là, le Seigneur sépara la tribu de Lévi, afin qu’elle portât l’arche d’alliance du Seigneur, qu’elle se tînt devant lui pour son ministère, et qu’elle bénît en son nom, comme elle a fait jusqu’au présent jour.
9 Hiyo ndiyo sababu ya Walawi kutokuwa na sehemu wala urithi miongoni mwa ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama Bwana Mungu wao alivyowaambia.)
À cause de cela Lévi n’a pas eu de part, ni de possession avec ses frères, parce que le Seigneur lui-même est sa possession, comme lui a promis le Seigneur ton Dieu.
10 Basi nilikaa mlimani kwa siku arobaini usiku na mchana, kama nilivyofanya mara ya kwanza, pia Bwana alinisikiliza hata wakati huu. Haikuwa nia yake kuwaangamiza.
Pour moi, je me tins sur la montagne comme auparavant, quarante jours et quarante nuits; et le Seigneur m’exauça encore cette fois, et il ne voulut pas te perdre.
11 Bwana akaniambia, “Nenda, ukawaongoze watu katika njia yao ili kwamba waweze kuingia na kuimiliki nchi ile niliyowaapia baba zao kuwapa.”
Il me dit ensuite: Va, et précède le peuple, afin qu’il entre, et qu’il possède la terre que j’ai juré à ses pères de leur donner.
12 Na sasa, ee Israeli, Bwana Mungu wako anataka nini kwako ila kumcha Bwana Mungu wako, kwenda katika njia zake, kumpenda na kumtumikia Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote,
Et maintenant, Israël, qu’est-ce que le Seigneur ton Dieu demande de toi, si ce n’est que tu craignes le Seigneur ton Dieu, que tu marches dans ses voies, que tu l’aimes, que tu serves le Seigneur ton Dieu en tout ton cœur et en toute ton âme;
13 na kuyashika maagizo ya Bwana na amri zake ninazokupa leo kwa mafanikio yako mwenyewe?
Et que tu gardes les commandements du Seigneur et ses cérémonies, que moi, je te prescris aujourd’hui, afin que bien t’arrive?
14 Mbingu, hata mbingu za juu sana, dunia na kila kitu kilichomo ndani yake, ni mali ya Bwana Mungu wako.
Voici, au Seigneur ton Dieu est le ciel, et le ciel du ciel, et la terre et tout ce qui est sur elle.
15 Hata hivyo Bwana alikuwa na shauku na baba zako, akawapenda na akawachagua ninyi, wazao wao, kuliko mataifa yote, kama ilivyo leo.
Et cependant le Seigneur s’est uni étroitement à tes pères, il les a aimés, et il a choisi leur postérité après eux, c’est-à-dire, vous, d’entre toutes les nations, comme il est entièrement prouvé aujourd’hui.
16 Kwa hiyo tahirini mioyo yenu, na msiwe na shingo ngumu tena.
Opérez donc la circoncision de votre cœur, et ne rendez plus votre cou inflexible,
17 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni Mungu wa miungu na Bwana wa mabwana, Mungu mkuu, mwenye uweza na wa kutisha, ambaye hana upendeleo na hapokei rushwa.
Parce que le Seigneur votre Dieu est lui-même le Dieu des dieux et le Seigneur des seigneurs, le Dieu grand, puissant et terrible, qui n’a point égard à la personne, ni aux présents.
18 Huwapigania yatima na wajane, humpenda mgeni, akimpa chakula na mavazi.
Il fait justice à l’orphelin et à la veuve, il aime l’étranger, et il lui donne la nourriture et le vêtement.
19 Nanyi wapendeni wageni, kwa kuwa ninyi wenyewe mlikuwa wageni huko Misri.
Vous donc aussi, aimez les étrangers, parce que vous-mêmes aussi, vous avez été étrangers dans la terre d’Egypte.
20 Mche Bwana Mungu wako na umtumikie yeye. Shikamana naye kwa uthabiti na kuapa kwa jina lake.
Tu craindras le Seigneur ton Dieu, et tu le serviras lui seul; tu t’attacheras à lui, et tu jureras par son nom.
21 Yeye ni sifa yako; yeye ni Mungu wako, ambaye alikutendea yale maajabu makubwa na ya kutisha uliyoyaona kwa macho yako mwenyewe.
C’est lui-même qui est ta gloire et ton Dieu; lui qui a fait pour toi ces merveilles grandes et terribles qu’ont vues tes yeux.
22 Baba zako walioshuka kwenda Misri jumla yao walikuwa sabini, na sasa Bwana Mungu wako amekufanya wengi kama nyota za angani.
C’est au nombre de soixante dix âmes que tes pères sont descendus en Egypte, et voilà que maintenant le Seigneur ton Dieu t’a multiplié comme les astres du ciel.

< Torati 10 >