< Torati 10 >

1 Wakati ule Bwana aliniambia, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza uje kwangu juu mlimani. Pia utengeneze Sanduku la mbao.
In the same time the Lord said vnto me, Hewe thee two Tables of stone like vnto the first, and come vp vnto me into the Mount, and make thee an Arke of wood,
2 Nitaandika juu ya vibao maneno yaliyokuwa katika vile vibao vya kwanza, ambavyo ulivivunja. Kisha utaviweka ndani ya Sanduku.”
And I will write vpon the Tables ye wordes that were vpon the first Tables, which thou brakest, and thou shalt put them in the Arke.
3 Hivyo nikatengeneza Sanduku kwa mti wa mshita, nikachonga pia vibao vya mawe kama vile vya kwanza, kisha nikakwea mlimani nikiwa na vibao viwili mikononi mwangu.
And I made an Arke of Shittim wood, and hewed two Tables of stone like vnto the first, and went vp into the Mountaine, and the two Tables in mine hand.
4 Bwana akaandika juu ya hivi vibao kile alichokuwa amekiandika kabla, Amri Kumi alizokuwa amewatangazia juu mlimani, kutoka kwenye moto siku ile ya kusanyiko. Bwana akanikabidhi.
Then he wrote vpon the Tables according to the first writing (the tenne commandements, which the Lord spake vnto you in the Mount out of the middes of the fire, in the day of the assemblie) and the Lord gaue them vnto me.
5 Kisha nikashuka kutoka mlimani na kuweka vibao ndani ya Sanduku nililokuwa nimelitengeneza, kama Bwana alivyoniagiza, navyo viko huko sasa.
And I departed, and came downe from the Mount, and put the Tables in the Arke which I had made: and there they be, as the Lord commanded me.
6 (Waisraeli walisafiri kutoka visima vya Yaakani hadi Mosera. Huko Aroni alifariki na kuzikwa, naye Eleazari mwanawe akachukua nafasi yake kama kuhani.
And ye children of Israel tooke their iourney from Beeroth of the children of Iaakan to Mosera, where Aaron dyed, and was buried, and Eleazar his sonne became Priest in his steade.
7 Kutoka pale, walisafiri hadi Gudgoda wakaendelea mpaka Yotbatha, nchi yenye vijito vya maji.
From thence they departed vnto Gudgodah, and from Gudgodah to Iotbath a land of running waters.
8 Wakati huo Bwana aliteua kabila la Lawi kulibeba Sanduku la Agano la Bwana, kusimama mbele za Bwana ili kutoa huduma, na kutangaza baraka kwa Jina lake, kama wanavyofanya mpaka leo.
The same time ye Lord separated the tribe of Leui to beare the Arke of the couenant of the Lord, and to stand before ye Lord, to minister vnto him, and to blesse in his Name vnto this day.
9 Hiyo ndiyo sababu ya Walawi kutokuwa na sehemu wala urithi miongoni mwa ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama Bwana Mungu wao alivyowaambia.)
Wherefore Leui hath no part nor inheritance with his brethren: for the Lord is his inheritance, as the Lord thy God hath promised him.
10 Basi nilikaa mlimani kwa siku arobaini usiku na mchana, kama nilivyofanya mara ya kwanza, pia Bwana alinisikiliza hata wakati huu. Haikuwa nia yake kuwaangamiza.
And I taried in the mount, as at ye first time, fourtie dayes and fourtie nightes, and the Lord heard me at that time also, and the Lord would not destroy thee.
11 Bwana akaniambia, “Nenda, ukawaongoze watu katika njia yao ili kwamba waweze kuingia na kuimiliki nchi ile niliyowaapia baba zao kuwapa.”
But the Lord said vnto me, Arise, goe forth in the iourney before the people, that they may goe in and possesse the land, which I sware vnto their fathers to giue vnto them.
12 Na sasa, ee Israeli, Bwana Mungu wako anataka nini kwako ila kumcha Bwana Mungu wako, kwenda katika njia zake, kumpenda na kumtumikia Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote,
And nowe, Israel, what doth the Lord thy God require of thee, but to feare the Lord thy God, to walke in all his wayes, and to loue him, and to serue the Lord thy God, with all thine heart, and with all thy soule?
13 na kuyashika maagizo ya Bwana na amri zake ninazokupa leo kwa mafanikio yako mwenyewe?
That thou keepe the commandements of the Lord, and his ordinances, which I commaund thee this day, for thy wealth?
14 Mbingu, hata mbingu za juu sana, dunia na kila kitu kilichomo ndani yake, ni mali ya Bwana Mungu wako.
Beholde, heauen, and the heauen of heauens is the Lords thy God, and the earth, with all that therein is.
15 Hata hivyo Bwana alikuwa na shauku na baba zako, akawapenda na akawachagua ninyi, wazao wao, kuliko mataifa yote, kama ilivyo leo.
Notwithstanding, the Lord set his delite in thy fathers to loue them, and did choose their seede after them, euen you aboue all people, as appeareth this day.
16 Kwa hiyo tahirini mioyo yenu, na msiwe na shingo ngumu tena.
Circumcise therefore the foreskin of your heart, and harden your neckes no more.
17 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni Mungu wa miungu na Bwana wa mabwana, Mungu mkuu, mwenye uweza na wa kutisha, ambaye hana upendeleo na hapokei rushwa.
For the Lord your God is God of gods, and Lord of lordes, a great God, mightie and terrible, which accepteth no persons nor taketh reward:
18 Huwapigania yatima na wajane, humpenda mgeni, akimpa chakula na mavazi.
Who doeth right vnto the fatherlesse and widowe, and loueth the stranger, giuing him foode and rayment.
19 Nanyi wapendeni wageni, kwa kuwa ninyi wenyewe mlikuwa wageni huko Misri.
Loue ye therefore the stranger: for ye were strangers in the land of Egypt.
20 Mche Bwana Mungu wako na umtumikie yeye. Shikamana naye kwa uthabiti na kuapa kwa jina lake.
Thou shalt feare the Lord thy God: thou shalt serue him, and thou shalt cleaue vnto him, and shalt sweare by his Name.
21 Yeye ni sifa yako; yeye ni Mungu wako, ambaye alikutendea yale maajabu makubwa na ya kutisha uliyoyaona kwa macho yako mwenyewe.
He is thy praise, and hee is thy God, that hath done for thee these great and terrible things, which thine eyes haue seene.
22 Baba zako walioshuka kwenda Misri jumla yao walikuwa sabini, na sasa Bwana Mungu wako amekufanya wengi kama nyota za angani.
Thy fathers went downe into Egypt with seuentie persons, and now the Lord thy God hath made thee, as ye starres of ye heauen in multitude.

< Torati 10 >