< Torati 1 >

1 Haya ni maneno Mose aliyoyasema kwa Israeli yote jangwani mashariki ya Yordani, ambayo iko Araba, inayokabiliana na Sufu, kati ya Parani na Tofeli, Labani, Haserothi na Dizahabu.
These ben the wordis whiche Moyses spak to al Israel ouer Jordan, in the wildirnesse of the feeld, ayens the reed see, bitwix Pharan and Tophel and Laban and Asseroth, where is ful myche gold,
2 (Ni mwendo wa siku kumi na moja kutoka Horebu kwa njia ya Mlima Seiri mpaka Kadesh-Barnea.)
by enleuene daies fro Oreb bi the weie of the hil of Seir, til to Cades Barne.
3 Katika mwaka wa arobaini, siku ya kwanza ya mwezi wa kumi na moja, Mose aliwatangazia Waisraeli yale yote Bwana aliyomwamuru kuwahusu.
In the fortithe yeer, in the enleuenth monethe, in the firste dai of the monethe, Moises spak to the sones of Israel alle thingis whiche the Lord commandide to hym that he schulde seie to hem,
4 Hii ilikuwa baada ya kumshinda Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala Heshboni, na pia huko Edrei alikuwa amemshinda Ogu mfalme wa Bashani, ambaye alitawala huko Ashtarothi.
after that he smoot Seon, kyng of Ammorreis, that dwellide in Esebon, and Og, the kyng of Basan, that dwelide in Asseroth and in Edray, ouer Jordan, in the lond of Moab.
5 Huko mashariki ya Yordani katika nchi ya Moabu, Mose alianza kuielezea sheria hii, akisema:
And Moyses bigan to declare the lawe, and to seie,
6 Bwana Mungu wetu alisema nasi huko Horebu, “Mmekaa vya kutosha katika mlima huu.
Oure Lord God spak to vs in Oreb, and seide, It suffisith to you that ye han dwellid in this hil;
7 Vunjeni kambi, msonge mbele kuelekea nchi ya vilima ya Waamori; nendeni kwa watu wote ambao ni majirani wa Araba, katika milima, upande wa magharibi chini ya vilima, katika Negebu na kandokando ya pwani, mpaka nchi ya Wakanaani hadi Lebanoni, na kufika mto mkubwa Frati.
turne ye ayen, and come ye to the hil of Amorreis, and to othere placis that ben next it; to places of feeldis, and of hillis, and to lowere places ayens the south, and bisidis the brenke of the see, to the lond of Cananeys, and of Liban, `til to the greet flood Eufrates.
8 Tazama, nimewapa ninyi nchi hii. Ingieni mkaimiliki nchi ambayo Bwana aliapa kuwa angaliwapa baba zenu, Abrahamu, Isaki na Yakobo, pamoja na vizazi vyao baada yao.”
Lo, `he seith, Y haue youe to you; entre ye, and `welde ye `that lond on which the Lord swoor to youre fadrys, Abraham, Ysaac, and Jacob, that he schulde yyue it to hem, and to her seed after hem.
9 Wakati ule niliwaambia, “Ninyi mmekuwa mzigo mzito sana kwangu kuwachukua peke yangu.
And Y seide to you in that time, Y may not aloone susteyne you, for youre Lord God hath multiplied you,
10 Bwana Mungu wenu ameongeza hesabu yenu, hivi kwamba leo ninyi ni wengi kama nyota za angani.
and ye ben ful many to dai, as the sterris of heuene;
11 Naye Bwana, Mungu wa baba zenu na awaongeze mara elfu na kuwabariki kama alivyoahidi!
the Lord God of youre fadris adde to this noumbre many thousyndis, and blesse you, as he spak.
12 Lakini mimi nitawezaje kubeba matatizo yenu, na mizigo yenu, na magomvi yenu peke yangu?
Y may not aloone susteyne youre causis, and birthun, and stryues; yyue ye of you men wise `in dyuyn thingis,
13 Chagueni baadhi ya watu wenye hekima, wenye ufahamu na wanaoheshimika kutoka kila kabila lenu, nami nitawaweka juu yenu.”
and witti `in mennus thingis worthi to be don, whose conuersacioun is preued in youre lynagis, that Y sette hem princes to you.
14 Mlinijibu, “Shauri ulilolitoa ni zuri.”
Thanne ye answeriden to me, The thing is good which thou wolt do.
15 Kwa hiyo niliwachukua wanaume viongozi wa makabila yenu, wenye hekima na wanaoheshimika, nami nikawateua wawe na mamlaka juu yenu kama majemadari wa maelfu, wa mamia, wa hamsini, na wa makumi, na kama maafisa wa makabila.
And Y took of youre lynagis men wise and noble, `in vertues and kyn; and Y ordeynede hem princis, tribunes, and centuryouns, and quynquagenaries, and denys, whiche schulden teche you all thingis.
16 Nami wakati ule nikawaagiza waamuzi wenu: Sikilizeni magomvi kati ya ndugu zenu na mwamue kwa haki, hata kama shauri ni kati ya ndugu wa Kiisraeli, au kati ya mmoja wa ndugu wa Kiisraeli na mgeni.
And Y comaundide to hem, and seide, Here ye hem, and deme ye that that is iust, whether he be a citeseyn, whether a pilgrym.
17 Msionyeshe upendeleo katika maamuzi; wasikilizeni wote sawasawa, wadogo kwa wakubwa. Msimwogope mtu yeyote, kwa kuwa hukumu ni ya Mungu. Mniletee mimi shauri lolote lililo gumu sana kwenu, nami nitalisikiliza.
No difference schal be of persones; ye schulen here so a litil man, `that is, pore, as a greet man, nether ye schulen take the persoone of ony man, for it is the doom of God. That if ony thing semeth hard to you, telle ye to me, and Y schal here.
18 Nami wakati ule niliwaambia kila kitu ambacho mngefanya.
And Y comaundide alle thingis whiche ye ouyten to do.
19 Kisha, kama Bwana Mungu wetu alivyotuamuru, tuliondoka kutoka Horebu na kwenda kuelekea nchi ya vilima ya Waamori, kupitia jangwa lile kubwa lote la kutisha, lile mliloliona, nasi tukafika Kadesh-Barnea.
Forsothe we yeden forth fro Oreb, and passiden bi a feerdful deseert, and grettiste wildirnesse, which ye sien, bi the weye of the hil of Ammorrey, as oure Lord God comaundide to vs. And whanne we hadden come in to Cades Barne,
20 Kisha niliwaambia, “Mmefika katika nchi ya vilima ya Waamori, ambayo Bwana Mungu wetu anatupa.
Y seide to you, Ye ben comen to the hil of Ammorrey, which youre Lord God schal yyue to you;
21 Tazama, Bwana Mungu wenu amewapa nchi. Pandeni mkaimiliki kama Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaambia. Msiogope, wala msikate tamaa.”
se thou the lond which thi Lord God schal yyue to thee; `stie thou, and welde it, as oure Lord God spak to thi fadris; `nyle thou drede, nether `drede thou in herte ony thing.
22 Ndipo ninyi nyote mkanijia na kusema, “Tupeleke watu watutangulie kuipeleleza nchi kwa ajili yetu, na kutuletea taarifa kuhusu njia tutakayopita, na miji tutakayoiendea.”
And alle ye neiyiden to me, and ye seiden, Sende we men, that schulen biholde the lond, and telle to vs bi what weye we owen stie, and to whiche citees we owen to go.
23 Wazo hilo lilionekana zuri kwangu; kwa hiyo niliwachagua watu wenu kumi na wawili, mwanaume mmoja kutoka kila kabila.
And whanne the word pleside to me, Y sente of you twelue men, of ech lynage oon.
24 Waliondoka na kukwea katika nchi ya vilima, wakafika katika Bonde la Eshkoli na kuipeleleza.
And whanne thei hadden go, and hadden stied in to the hilli places, thei camen `til to the valei of Clustre; and whanne thei hadden biholde the lond,
25 Wakachukua baadhi ya matunda ya nchi, wakatuletea na kutuarifu, “Ni nchi nzuri ambayo Bwana Mungu wetu anatupa.”
thei token of the fruytis therof, to schewe the plentee, and brouyten `to vs, and seiden, The lond is good which oure Lord God schal yyue to vs.
26 Lakini hamkuwa tayari kukwea, mkaasi dhidi ya amri ya Bwana Mungu wenu.
And ye `nolden stie, but ye weren vnbileueful to the word of oure Lord God.
27 Mkanungʼunika ndani ya mahema yenu na kusema, “Bwana anatuchukia, kwa hiyo alitutoa Misri ili kututia mikononi mwa Waamori kutuangamiza.
And ye grutchiden in youre tabernaclis, and ye seiden, The Lord hatith vs, and herfor he ledde vs out of the lond of Egipt, that he schulde bitake vs in the hond of Ammorey, and schulde do awei vs.
28 Twende wapi? Ndugu zetu wametufanya kufa moyo. Wanasema, ‘Watu wa huko wana nguvu zaidi na ni warefu kuliko sisi tulivyo; miji ni mikubwa, yenye kuta zilizofika juu angani. Zaidi ya hayo, tumewaona Waanaki huko.’”
Whidur schulen we stie? the messangeris maden aferd oure herte, and seiden, A grettiste multitude is, and largere in stature than we; the citees ben greete, and wallid `til to the heuene; we sien there the sones of Enachym, that is, giauntis.
29 Ndipo nikawaambia, “Msihofu, wala msiwaogope.
And Y seide to you, `Nyle ye drede `with ynne, nether `drede withoutforth; the Lord God hym silf,
30 Bwana Mungu wenu anayewatangulia, atawapigania, kama alivyofanya kwa ajili yenu huko Misri, mbele ya macho yenu hasa,
which is youre ledere, schal fiyte for you, as he dide in Egipt, while alle men sien.
31 na pia huko jangwani. Huko mliona jinsi Bwana Mungu wenu alivyowachukua, kama baba amchukuavyo mwanawe, katika njia yote mliyoiendea mpaka mkafika mahali hapa.”
And ye sien in the wildirnesse, thi Lord God bar thee, as a man is wont to bere his litil sone, in al the weie bi which ye yeden til ye camen to this place.
32 Pamoja na hili, hamkumtegemea Bwana Mungu wenu,
And sotheli nether so ye bileueden to youre Lord God, that yede bifor you in the weie,
33 ambaye aliwatangulia katika safari yenu, kwa moto usiku na kwa wingu mchana, kuwatafutia mahali penu pa kupiga kambi na kuwaonyesha njia mtakayoiendea.
and mesuride the place in which ye ouyten to sette tentis, and schewide in nyyt the weie to you bi fier, and in dai bi a piler of cloude.
34 Wakati Bwana aliposikia lile mlilosema, alikasirika, akaapa, akasema:
And whanne the Lord hadde herd the vois of youre wordis, he was wrooth,
35 “Hakuna mtu wa kizazi hiki kiovu atakayeona nchi nzuri niliyoapa kuwapa baba zenu,
and swoor, and seide, Noon of the men of this werste generacioun schal se the good lond, which Y bihiyte vndur an ooth to youre fadris,
36 isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune. Yeye ataiona, nami nitampa yeye na wazao wake nchi aliyoikanyaga kwa miguu, kwa sababu alimfuata Bwana kwa moyo wote.”
outakun Caleph, the sone of Jephone; for he schal se it, and Y schal yyue to hym the lond on which he trad, and to hise sones, for he suede the Lord.
37 Kwa sababu yenu Bwana pia alinikasirikia mimi, akasema, “Hutaingia hiyo nchi pia.
Nether the indignacioun ayens the puple is wondirful, sithen the Lord was wrooth also to me for you, and seide,
38 Lakini msaidizi wako, Yoshua mwana wa Nuni, ataingia. Mtie moyo, kwa sababu atawaongoza Waisraeli kuirithi hiyo nchi.
Nether thou schalt entre thidur, but Josue, the sone of Nun, thi mynystre, he schal entre for thee; excyte and strengthe thou him, and he schal departe the lond bi lot to Israel.
39 Wale watoto ambao mliwasema wangelichukuliwa mateka, yaani watoto wenu ambao bado hawajui jema na baya, wataingia katika nchi. Nitawapa hiyo nchi, nao wataimiliki.
Youre litle children, of whiche ye seiden, that thei schulden be led prisoneris, and the sones that kunnen not to dai the diuersite of good and of yuel, thei schulen entre; and Y schal yyue to hem the lond, and thei schulen welde it.
40 Bali ninyi geukeni, mwondoke kuelekea jangwani kwa kufuata njia ya Bahari ya Shamu.”
Sotheli turne ye ayen, and go ye in to the wildirnesse, bi the weie of the Reed See.
41 Ndipo mkanijibu, “Tumemtenda Bwana dhambi. Tutakwenda kupigana, kama Bwana Mungu wetu alivyotuamuru.” Hivyo kila mmoja wenu akachukua silaha zake, huku mkifikiri kuwa ni rahisi kukwea katika nchi ya vilima.
And ye answeriden to me, We synneden to the Lord; we schulen stie, and we schulen fiyte, as oure Lord God comaundide. And whanne ye weren arayed with armeris, and yeden `into the hil, the Lord seide to me,
42 Lakini Bwana aliniambia, “Waambie, ‘Msipande kupigana, kwa sababu sitakuwa pamoja nanyi. Mtashindwa na adui zenu.’”
Seie thou to hem, `Nyle ye stye, nether fiyte ye, for Y am not with you, lest ye fallen bifor youre enemyes.
43 Hivyo niliwaambia, lakini hamkutaka kusikia. Mliasi dhidi ya amri ya Bwana, na katika kiburi chenu mlienda katika nchi ya vilima.
Y spak, and ye herden not; but ye `weren aduersaries to the comaundement of the Lord, and bolnden with prijde, and stieden in to the hil.
44 Waamori ambao waliishi katika vilima hivyo waliinuka dhidi yenu, wakawafukuza kama kundi la nyuki wakiwapiga njia yote ya Seiri mpaka Horma.
Therfor Ammorrey yede out, that dwellide in the hillis, and he cam ayens you, and pursuede you, as bees ben wont to pursue, and killide fro Seir til Horma. And whanne ye turneden ayen,
45 Mlirudi na kulia mbele za Bwana, lakini Mungu hakusikiliza kilio chenu, wala hakuwajali.
and wepten bifor the Lord, he herde not you, nether wolde asente to youre vois;
46 Hivyo mlikaa Kadeshi kwa siku nyingi, kwa muda ule wote mliokaa huko.
therfor ye saten in Cades Barne bi myche tyme.

< Torati 1 >